DOKEZO Waziri wa Elimu, huu mtindo wa Kubakiza watoto shuleni wakati wa likizo ni Sahihi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,373
Mheshimiwa Waziri,

Kumekuwa na mtindo wa wamiliki wa shule kuamua tu kwa utashi wao kubakiza watoto shuleni(madarasa ya mitihani) kwa kigezo kwamba wapate muda wa kumalizia mitaala tena bila kushirikisha wazazi huku wakiwa tayari wamepanga na gharama zao.

Hivi walimu wanashindwa vipi kumaliza mtaala kwenye muda uliopangwa?Kibaya zaidi wamekuwa wakiongeza gharama za ziada za Tuition fee na transport hasa kwa shule binafsi.

Sasa kama lengo la walimu ni kumaliza mtaala hili si jukumu lao,kwanini gharama zirudi kwa mzazi?

Je ni sahihi mtoto kusoma bila kupumzika?Kuna watoto wanasoma mbali na wazazi wanahitaji kuonana na wazazi wao ambao hawajawaona kwa muda mrefu,sasa kumshikilia mtoto shuleni muda mrefu kisaikolojia imekaaje?

Mimi binafsi naona shule zimeamua kubuni tu mradi wa kujipatia kipato kwa kigezo cha kumaliza mitaala.

Tayari kuna shule zimeshatoa taarifa kwamba darasa la nne hawatafunga shule ili waendelee kufundishwa,Je mmeruhusu?

Tunaomba hili suala lizuiliwe kisheria na sio kwa matamko ya kila mara maana nakumbuka mwaka Jana ulitoa tamko la kuzuia watoto kubakizwa shuleni ila naona linajirudia tena.

Pia soma: Waziri wa Elimu Prof. Mkenda, sisitiza umuhimu wa kutowabakiza watoto shule kipindi cha likizo

UPDATE:

Wizara imeitikia wito wa wadau, soma Serikali: Wanafunzi wasizuiwe kwenda likizo
 

Attachments

  • uendeshaji wa shule usiozingatia sheria-WADAU.pdf
    535.6 KB · Views: 5
Asante sana mdau kwa kuleta uzi huu. Kweli kabisa hii tabia imeanza shamiri mno kuna shule wao wameamua darasa la 4,6 na 7 jumamosi wawe shule na likizo kisingizio kuwa wanamitihani na garama wameongeza kama ulivyosema hapo juu.

Hawa watoto wanahitaji kupumzika nadhani mh Waziri nivizuri ukatusaidia toa muongozo kwenye hizi shule.

Huu ni uhuni wa kujiongezea mapato tu sababu hata ukifatilia unakuta walimu hawapo wote mara wanapeana zamu kwenda kifupi ni kuzuga tu hizo siku.
 
Ni mtindo wa kipuuzi uliojengeka na kuzoeleka. Inakuwa haina maana kuwa na likizo kwa mwanafunzi, huko ni kumchosha.

Unakuta wanafunzi wanafululiza kusoma mwaka mzima huku hakuna cha maana wanachofundishwa zaidi ya kukaririshwa kama kasuku.

Hawa ni watoto wadogo inawapasa kupumzika baada ya kusoma mada nyingi kwa muhula mzima.

Akili inatakiwa ipumue ili kupokea maarifa mapya
 
Mheshimiwa Waziri,

Kumekuwa na mtindo wa wamiliki wa shule kuamua tu kwa utashi wao kubakiza watoto shuleni(madarasa ya mitihani) kwa kigezo kwamba wapate muda wa kumalizia mitaala tena bila kushirikisha wazazi huku wakiwa tayari wamepanga na gharama zao...
Umeshajaribu kufanya uchunguzi kidogo kuona kuwa hao unaowashtakia sio wamiliki wa hizo shule...?
 
Asante sana mdau kwa kuleta uzi huu. Kweli kabisa hii tabia imeanza shamiri mno kuna shule wao wameamua darasa la 4,6 na 7 jumamosi wawe shule na likizo kisingizio kuwa wanamitihani na garama wameongeza kama ulivyosema hapo juu. Hawa watoto wanahitaji kupumzika nadhani mh Waziri nivizuri ukatusaidia toa muongozo kwenye hizi shule.Huu ni uhuni wa kujiongezea mapato tu sababu hata ukifatilia unakuta walimu hawapo wote mara wanapeana zamu kwenda kifupi ni kuzuga tu hizo siku.
Ni kweli kuna harufu ya utapeli tu,hapa Waziri anapaswa atoe tamko,hili ni dili la shule kujipatia hela za zaida,hapo bado wakifungua shule ada iko palepale
 
Ni mtindo wa kipuuzi uliojengeka na kuzoeleka. Inakuwa haina maana kuwa na likizo kwa mwanafunzi, huko ni kumchosha. Unakuta wanafunzi wanafululiza kusoma mwaka mzima huku hakuna cha maana wanachofundishwa zaidi ya kukaririshwa kama kasuku. Hawa ni watoto wadogo inawapasa kupumzika baada ya kusoma mada nyingi kwa muhula mzima. Akili inatakiwa ipumue ili kupokea maarifa mapya
Ni kweli watoto wanateseka,na mabegi ya sikuhizi yalivyojaa makaunta book,bado wanaamka asubuhi sana,halafu inafika likizo wanataka tena waendelee kwenda shuleni tena kwa gharama za mzazi,huu ujinga ufike mwisho
 
Ni wakati wa kubadili mfumo wa elimu, ikiwezekana siku za kwenda shule ziwe nne badala ya tano kwa wiki.

Ijumaa iwe ni siku ya michezo tu, pia masomo yawe kwa njia ya vitendo zaidi badala ya rote learning ambayo inadumaza watoto.
Tutoe maoni labda wataweka kwenye Sera mpya ya elimu inayokuja.
 
Back
Top Bottom