Pole, nina shaka kama kweli unaweza kupata mtu wa kuanzisha nae familia kupitia mitandao! Yawezekana wanaotafuta wachumba humu wana familia zao wanatafuta michepuko tu ndo maana unakuta wana ID zaidi ya hizo. Ila najiuliza kama kweli wewe huna tatizo coz kote huko ulikopita kuanzia shule ya msingi hadi hapo ulipofika, kanisani, kitaa hakuna mwanaume ambaye umewahi kuvutiwa naye, ukizingatia mwenendo wa maisha yako siyo wa kutilia shaka sasa iweje hata waamini wenzio kanisani wasivutiwe na wewe amabye hakika umelelewa kimaadili? kwanini wanaokuona wasikupendekezee watoto wao, kaka zao na hata marafiki zao? SIKUKATISHI TAMAA NA STYLE UNAYOTUMIA KUTAFUTA MCHUMBA ILA NASHAURI KAMA UTAMPATA HAPA JF JIPE MUDA WA KUMFAHAMU VIZURI..ANZISHA URAFIKI WA KAWAIDA, FAHAMU RAFIKI ZAKE, NDUGU, WAZAZI NA HATA WAFANYAKAZI WENZAKE KABLA YA KUMRUHUSU AINGIE BONDE LAKO LA UFA.