Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 33

Na Bishop Hiluka

Kwa kitambo fulani kulizuka ukimya, Carlos alikuwa akimtazama Kisu kwa makini wakati akijimiminia pombe kwenye bilauri na kugida kwa pupa huku akisisimkwa mwili.

Aliendelea kunywa ile pombe kwa kitambo kirefu akiwa kimya hadi alipoanza kuchangamka zaidi, ndipo Carlos akaamua kuvunja ukimya.

“Sasa, ni kama nilivyokudokeza jana usiku, huenda wiki hii tutakuwa na kazi moja nzito…” Carlos alisema na kuongeza.

Endelea...

“Kama unavyojua dili zangu, huwa sibahatishi katika mipango yangu, na katika matukio yote ya uhalifu niliyowahi kufanya hakuna hata moja lililofeli.”

Kisu alibetua kichwa kukubaliana naye huku akimsikiliza kwa makini zaidi.

“Ila ujue kuingia benki na kutoka na fedha ambazo si halali yenu inataka ujasiri usio wa kawaida. Nimekuchagua wewe kutokana na sifa yako ya ujasiri uliopitiliza, uhuni, wehu na ubabe ili tufanye kazi hiyo, lakini pia nikijua kuwa utaniletea vijana wawili mahiri zaidi wenye ujasiri kama ulivyo mwenyewe,” Carlos alisema akiwa amemkazia macho Kisu.

“Hili wala usikonde, kuna watu wawili kama nilivyokueleza jana kwenye simu, Kabwe na Liston,” Kisu alisema na kuongeza. “Listoni nadhani unamkumbuka, ni yule jamaa wa ile ishu ya tanzanite feki mlipompiga yule Mjerumani enzi zile…”

“Ee, huyo sawa,” Carlos alidakia.

“Basi huyo mwingine ndiyo balaa, hana spea kabisa,” Kisu alisema na kuongeza, “Ukiwataka hata sasa hivi naweza kuwapigia simu nikawaelekeza waje hapa.”

“Ngoja kwanza tuyajenge, tukishaelewana ndiyo uwaite,” Carlos akasema na kuongeza, “Kazi ya kwanza unayotakiwa kuifanya, itabidi ushughulikie bunduki na jinsi gani utaweza kupata sare ya mlinzi wa kampuni ya The Jacarandah Group.”

Kisu alibetua kichwa chake kukubali huku akiinua bilauri yake na kugida pombe yote iliyokuwemo kisha aliikita ile bilauri juu ya meza.

“Pia tunahitaji kupata gari kama lile la The Jacarandah Group kwa ajili ya kuchukulia fedha kutoka benki, halafu kazi yangu ni kuipata hundi ya kampuni ya The Jacarandah Group kwani nina uhakika wa kuipata wakati wowote kuanzia leo jioni, ninachosubiri kwa sasa ni kopi ya hundi yao yenye saini za wanaoidhinisha kutoa pesa benki,” Carlos aliendelea kumweleza Kisu.

* * * * *

Asubuhi na mapema ya saa kumi na mbili kwa mujibu wa saa ya ukutani, Mama Jasmine ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka na kupiga pasi nguo za mumewe Yusuf, kisha akazitundika kwenye henga ya nguo. Alichukua ndoo akawahi bombani na kukinga maji aliyokuwa akiyamimina kwenye dumu kubwa maarufu kama jaba.

Alipomaliza aliingia chumbani akasimama kando ya kitanda, akamtazama mumewe kwa makini. Yusuf alikuwa bado yupo kwenye lindi zito la usingizi, hajitambui na ilionesha kuwa ingemchukua muda mwingine mrefu kuzinduka.

Kando ya Yusuf alikuwa amelala Jasmine. Mama Jasmine alizitoa nguo zilizokuwa ndani ya tenga la nguo chafu na kuanza kuzikagua, kama ilivyokuwa desturi yake kabla hajazifua. Alikwenda nje akazifua chap chap na kuzianika kisha akarudi tena chumbani.

Pale kitandani Yusuf alikuwa bado kalala, alijipindua na kutafuna maneno ambayo hayakusikika akiwa bado yupo usingizini. Mama Jasmine alijenga picha akilini mwake, ingekuwaje iwapo ataamua kuachana na mumewe! Akajiuliza kwani ni mara ngapi mumkewe aliwahi kumkosea au kulala nje, hakuna, ndiyo kwanza imetokea.

Je, alikuwa na uhakika gani kuwa mumewe alilala na mwanamke na si kama alivyoelezwa na Yusuf mwenyewe kuwa alikuwa na marafiki zake? Na kama Yusuf yuko sahihi, je, hakuona kama alikuwa anamkosea heshima mumewe kwa kutomuamini? Maswali mengi yalianza kupita kichwa kwa Mama Jasmine pasipo majibu.

Alimtazama tena Yusuf pale kitandani alipolala akiwa hajitambui wala hajijui, “Hmm, isingekuwa ni mimi si angekesha na kulala huko nje kama bundi?” Mama Jasmine aliwaza huku akihisi huruma huku donge la fadhaa likianza kumkaba kooni.

Alionekana kuingiwa huruma moyoni, na mara kikohozi kidogo kilimtoka, na nyuma yake wimbi la machozi lilikuja mbio na kuyafanya macho yake yajenge malengelenge ya machozi.

Yusuf alijigeuza na kushtuka pale aliposikia kikohozi cha mkewe. Macho yake yalikuwa mekundu na yaliyovimba kidogo kutokana na usingizi aliokuwa nao. Uso wake na mgongoni alikuwa na alama za mistari zilizosababishwa na matandiko.

Alimtazama mkewe huku uchovu ukimuendesha kutokana na jinsi alivyoonekana. Alijiinua na kukaa kitandani, miguu ikiwa chini huku akifikicha macho na kupiga miayo. Mama Jasmine aliendelea kusimama akimtazama kwa makini, lakini alikwisha yafuta haraka machozi yaliyokuwa yakimlengalenga machoni, baada ya kugundua Yusuf ameamka.

Yusuf alimtazama mkewe kwa wasiwasi, hakujua nini kilichokuwa kikiendelea kichwani kwa mkewe isipokuwa alichojua ni kuwa siku iliyokuwa imepita ilikuwa ni ndefu sana kwao.

Pia hakujua ni kwa nini yote yale yalitokea kwa siku moja ingawa alichojua ni kwamba yalitokea na kuitikisa ndoa yao kiasi cha nyufa kuanza kuonekana. Yusuf aliinamisha kichwa chake chini akiyakwepa macho ya mkewe huku akiomba mtikisiko usiendelee maana hakuwa tayari kuhimili mitikisiko mingine.

Alitamani ugomvi wao ungekuwa ndoto, maana kama mkewe aangeendelea na msimamo wake kulikuwa na uwezekano wa kuzaliwa nyufa kubwa na hatimaye nyumba ingeanguka…

“Habari ya asubuhi?” sauti ya Mama Jasmine ilimshtua Yusuf na kumuondoa haraka kutoka kwenye yale mawazo, hakutegemea kama mkewe angemsalimia kwa upendo kiasi kile.

“Safi tu, wewe?” Yusuf alijibu huku akimtazama mkewe kwa wasiwasi lakini akajikuta akiachia tabasamu baada ya kuuona uso wa mkewe ukiwa ana tashwishwi.

“Mi mzima,” alijibu Mama Jasmine, kisha kikapita kimya kati yao.

“Kwa nini jana uliamua kulala pale nje au ndiyo ulisusa?” Mama Jasmine alimuuliza mumewe akimkazia macho usoni.

“Sikususa, au unadhani nilipenda kulala pale, si vile tu wewe uliniletea mapozi nikaona isiwe taabu, lakini nafikiri tumeshayamaliza, au siyo?” Yusuf alijibu huku akiitazama saa yake ya mkononi ambayo alilala nayo, kisha akashusha pumzi ndefu.

“Nilikaa pale kitandani wee kisha nikazima taa na kulala, baadaye niliposhtuka sikukuona, huruma ikaniingia juu yako. Nikatoka nikidhani umelala sebuleni lakini sikukukuta, nikaelekea uwani pia haukuwepo. Hapo hasira zikanipanda tena, nilipotoka barazani si nikakuta unaweweseka kama kifaranga kilichonyeshewa mvua. Nikakuamsha ukaamka ukaanza kupepesuka ukielekea ndani kama mlevi, kama ungejiona ungejicheka na kuona aibu,” Mama Jasmine alisema huku akitabasamu.

“Nashukuru sana, mke wangu, kwa kuonesha jinsi gani ulivyo na huruma wala huna kinyongo kabisa,” Yusuf alisema huku akijiweka sawa pale kitandani.

“Ni kweli, sina kinyongo na ni mwingi wa huruma, ila kiukweli jana hukunikera tu bali uliniumiza sana…” Mama Jasmine alisema huku akimtazama Yusuf kwa aibu.

“Aah, Mama Jasmine, si yamekwisha, sasa unataka kuyaanzisha tena?” Yusuf alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Ndiyo yamekwisha, ila tu nasema kuwa una bahati sana, kama jana ningekuacha ulale hapo halafu waje vibaka, sijui ungefanyaje,” Mama Jasmine alimwambia Yusuf huku akitabasamu.

“Jana au leo kabla hapajapambazuka?” Yusuf aliuliza mkewe huku akivuta picha, ingekuwaje endapo angevamiwa na vibaka!

“Kweli, ni leo,” Mama Jasmine alijisahihisha na kuendelea, “Siku nyingine rudia kususa halafu ulale tena hapo nje utaipata habari yake.”

Mama Jasmine alisema na kuanza kusogea kwenye meza ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda akitaka kuchukua kitambaa chake cha kufunika nywele, lakini kabla hajakichukua, Yusuf alimvuta na kumtupia kitandani, naye akajitupa juu yake. Mama Jasmine alilala chali.

Mambo kwa upande wa Yusuf yameanza kurudi kwenye mstari, je, atavihimili vishindo vya Jacky ili aendelee kuilinda ndoa yake au ndiyo ataharibu zaidi. Vipi kuhusu Jacky, Carlos na sasa Kisu, nini kipo nyuma yao? Jibu ni kuendelea kufuatilia simulizi hii ya kusisimua...
 
Wakuu, nawashukuru sana wote mlioguswa, kuniombea au kunitakia heri nipone haraka, sijaweza kuzisoma posti zenu zilizomo humu (nadhani nitazisoma taratibu nikipata muda), ila naamini wengi wenu mmeguswa. Bado sijaanza kwenda kazini lakini siwezi kuendelea kukaa nje ya jukwaa hili, acha tuendelee mdogo mdogo na simulizi yetu ya Kizungumkuti, kwani hata tatizo lililonipata (naamini kabisa) limekuwa kizungumkuti kama ilivyo stori hii...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole sana ndugu kwa yaliokukuta, na vilevile tunakudhukuru sana kwa kutujari.....may God bless you.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kizungumkuti! - 34

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Jana au leo kabla hapajapambazuka?” Yusuf aliuliza mkewe huku akivuta picha, ingekuwaje endapo angevamiwa na vibaka!

“Kweli, ni leo,” Mama Jasmine alijisahihisha na kuendelea, “Siku nyingine rudia kususa halafu ulale tena hapo nje utaipata habari yake.”

Mama Jasmine alisema na kuanza kusogea kwenye meza ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda akitaka kuchukua kitambaa chake cha kufunika nywele, lakini kabla hajakichukua, Yusuf alimvuta na kumtupia kitandani, naye akajitupa juu yake. Mama Jasmine alilala chali.

Endelea...

Kitendo kile kilimwamsha Jasmine, aliinuka akakaa kitako pale kitandani huku akiwatazama wazazi wake kwa macho ya udadisi. Mama Jasmine alimsukuma Yusuf na kuinuka haraka, akachukua mswaki wa Jasmine na kuutia dawa, kisha akamteremsha Jasmine kutoka pale kitandani.

“Haya, twende ukapige mswaki, mtoto mzuri,” Mama Jasmine alisema huku akimpiga ukope Yusuf, akatoka na Jasmine hadi uwani, akachukua kikombe na kuchota maji yaliyokuwa ndani ya jaba na kumpa.

“Haya, kaa hapa upige mswaki vizuri na ukimaliza lazima nikukague, usiondoke hadi nije, sawa?” Mama Jasmine alimwambia Jasmine huku akianza kupiga hatua kuingia ndani, alipofika mlangoni aligeuka kumtupia jicho na kumuona akianza kujishughulisha na meno yake.

Jasmine alikuwa amechuchumaa kwenye ukingo wa ukuta wa ule ua akajitahidi kuchokonoa mswaki wake huku na huko kinywani kwake, kwani alijua baada ya kumaliza kupiga mswaki kulikuwa na ukaguzi.

Mama Jasmine aliingia chumbani ambako alimkuta Yusuf akiwa bado anamsubiri kwa hamu, alikwenda kuketi kitandani kando ya Yusuf huku akimtazama kwa aibu na hapo Yusuf akamdaka na kumsukumia kitandani. Mama Jasmine alijiangusha chali huku akiitandaza mikono kama aliyekuwa akiwambwa msalabani.

Yusuf alikuja juu yake huku mikono yake akiitandaza kuishikilia mikono ya mkewe na nyuso zao zikatazamana kwa ukaribu. Mama Jasmine alifumba macho yake kuyakwepa macho ya Yusuf, na taratibu wakajikuta wakianza kuhamia katika dunia nyingine kabisa, dunia ya mahaba… kuanzia hapo hapakuwa na kitu kingine zaidi ya kupeana mahaba mazito mazito.

Walipomaliza Yusuf alijifunga taulo kisha wote walielekea bafuni kwa ajili ya kuoga. Walipotoka nje Mama Jasmine alimkuta Jasmine akiwa bado amekaa pale pale upenuni mwa ua wa ile nyumba alipomwacha akisubiri kukaguliwa.

“Umemaliza?” Mama Jasmine alimuuliza mwanawe huku akimkazia macho. Jasmine alikubali kwa kichwa huku akikenyua meno yake kumuonesha mama yake.

“Haya nenda kanisubiri ndani kwenye makochi, nikitoka kuoga nakuja kukukagua kama umesugua vizuri,” Mama Jasmine alimwambia Jasmine huku akichota maji kwenye lile jaba na kuyajaza kwenye ndoo ya kuogea, kisha akayapeleka bafuni ambako mumewe Yusuf alikuwa amesimama anasubiri. Mama Jasmine alioga haraka haraka na kutoka akimwacha Yusuf anaendelea kuoga taratibu, yeye alikuwa akimuwahi Jasmine.

Baada ya kumaliza kuoga Yusuf aliingia ndani na kuzikuta nguo zake zikiwa tayari zimenyooshwa vizuri na kuwekwa sehemu maalumu tayari kwa kuvaliwa. Alijiandaa na kuvaa huku moyoni akiwa amefurahi sana, hasa baada ya kuonekana kuwa mkewe alikuwa amemsamehe kabisa.

Yusuf alipomaliza zoezi lile la kujiandaa alimuaga mkewe kwa kumbusu kwenye paji la uso, kisha akambusu mwanawe Jasmine na kutoka, akaelekea kituo cha daladala cha Bungoni huku akipiga mluzi wa ushindi.

* * * * *

Saa ya ukutani sebuleni nyumbani kwa Carlos na Jacky ilisomeka kuwa saa sita na robo mchana. Katika ile sebuleni kulikuwa na wanaume wanne waliokuwa wameketi wakijadiliana hili na lile huku maongezoi yao yakisindikizwa na pombe kali.

Juu ya meza kulionekana chupa kadhaa kubwa pombe aina ya whisky, Grant na mvinyo mwekundu wa Kifaransa wa Navette de Marseille na bilauri ndefu nne.

Kwenye kochi dogo la sofa Carlos alikuwa ameketi akizungumza na vijana wawili waliokuwa wameketi kwenye kochi kubwa lililokuwa mkabala na lile aliloketi.

Vijana hao ni Kabwe, ambacho kilikuwa kifupi cha majina ya Kassim Bwenzi. Huyu alikuwa na kimo cha wastani na mweusi kama Mjaluo akiwa na misuli imara ya mikononi iliyotuna kikamilifu kwa namna kuonesha kuwa alikuwa na kawaida ya kufanya mazoezi ya nguvu yasiyokuwa na kikomo.

Kabwe alikuwa amevaa fulana nyeupe iliyombana na kulionesha vyema umbo lake lililojengeka kwa misuli na alivaa suruali ya jeans ya rangi ya bluu na buti ngumu aina ya ‘safari boot’ za rangi ya hudhurungi.

Kichwani alivaa kofia aina ya kapelo ya rangi nyekundu iliyokuwa imetuama vizuri kwenye upara wake uliokuwa unawaka na usiokuwa na unywele hata mmoja.

Japokuwa alikuwa mzungumzaji mzuri na mwenye kujua mambo mengi lakini Kabwe hakupata nafasi ya kupata elimu bora kutokana na hali ya ufukara uliopindukia wa famili yake, alilelewa na mama pekee na alikuwa na ndugu zake wengine watano, huku baba yao akiwatelekeza na kwenda kusikojulikana wakati Kabwe akiwa na miaka saba tu.

Kuanzia hapo walijikuta wakiishi maisha ya ufukara uliopindukia, na hata hayo madarasa manne ya shule ya msingi ambayo Kabwe alisoma aliyapata kwa taabu sana.

Wakati akisoma ilimlazimu Kabwe na ndugu zake kwenda shuleni wakiwa na njaa, wakashinda huko na njaa na waliporudi nyumbani walilazimika kumsaidia mama yao aliyekuwa mlemavu kutafuta chakula kwa kufanya kazi za vibarua, ndipo Kabwe akajionea upuuzi kuendelea na shule. Akaachana na shule, akawa anarandaranda mitaani na watoto wengine wa mtaani.

Hapo ndipo alipoanza kujifunza uporaji madukani na mitaani ili kujipatia riziki, na ndipo pia alipoanza kujenga mzuka wa kujisikia kuua. Alianza polepole kwa kunyonga shingo za kuku na kuwatazama wakipaparika kwa maumivu makali hadi kufa. Kisha akahamia kwenye kuvizia paka akijifanya Manyaunyau, aliwakamata na kuwatenganisha miili yao na vichwa. Ukatili huu uliuburudisha sana moyo wa Kabwe.

Alipofikisha umri wa miaka ishirini Kabwe alikwisha toa roho tatu za watu waliokuwa wameingia katika anga zake.

Kijana mwingine aliyekaa pamoja na Kabwe aliitwa Liston George, huyu alikuwa mrefu na mweupe kiasi, mwenye umbo kakamavu kama wachezaji wa mpira wa kikapu wa Marekani. Alikuwa amevalia shati jeupe la mistari ya rangi ya bluu la mikono mirefu, suruali ya jeans ya rangi nyeusi na raba nyeusi.

Macho yake yalikuwa makubwa na mekundu yenye uchovu lakini yaliyokuwa na kila dalili ya kuonya na muda wote alikuwa akimtazama Carlos huku tabasamu jepesi likijitokeza taratibu usoni mwake.

Itaendelea...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
 
Kizungumkuti! - 35

Na Bishop Hiluka

Kijana mwingine aliyekaa pamoja na Kabwe aliitwa Liston George, huyu alikuwa mrefu na mweupe kiasi, mwenye umbo kakamavu kama wachezaji wa mpira wa kikapu wa Marekani. Alikuwa amevalia shati jeupe la mistari ya rangi ya bluu la mikono mirefu, suruali ya jeans ya rangi nyeusi na raba nyeusi.

Macho yake yalikuwa makubwa na mekundu yenye uchovu lakini yaliyokuwa na kila dalili ya kuonya na muda wote alikuwa akimtazama Carlos huku tabasamu jepesi likijitokeza taratibu usoni mwake.

Endelea...

Liston alikuwa mkimya sana, asiyependa kuongea lakini alikuwa mwingi wa vitendo. Na kama mtu angemuona asingeweza kudhani kuwa amekwisha fanya matukio makubwa sana katika nchi mbalimbali pasipo kushtukiwa.

Liston alikuwa msomi wa shahada ya kwanza aliyoipata kutoka katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alisomea Uhandisi wa umeme. Akiwa chuoni alitumia mwanya huo kujiunga na programu maalumu iliyokuwa imeanzishwa na Jeshi la Wananchi kwa ajili ya kuchukua vijana wasomi na walioko vyuoni.

Baada ya kumaliza chuo Liston alikwenda kulitumikia Jeshi kwa muda mfupi na kituo chake cha kazi kikiwa Kambi ya Mzinga na akiwa huko alipata mafunzo maalumu ya kijeshi, huo ulikuwa mpango maalumu wa kuandaliwa kama Jeshi la Akiba. Liston pia alipata mafunzo ya kujihami ya karate and judo na kufanikiwa kupata mkanda mweusi.

Baada ya kupata mafunzo ya kijeshi Liston alijaribu kurudi tena chuoni kusoma shahada ya pili lakini alilazimika kukatisha masomo kutokana na matatizo makubwa yaliyoikumba familia yake.

Hakuna aliyejua ni kipi hasa kilichomsukuma kuingia kwenye uhalifu, japo alikuwa msomi mwenye taaluma ya uhandisi na hakupenda kabisa kuongea mambo yaliyohusu maisha au familia yake, nadhani ndiyo sababu ya kupenda kuwa mkimya muda wote.

Katika kochi jingine aliketi Kisu akiwa mtulivu sana huku akiendelea kugida pombe kali taratibu. Wote watatu walikuwa wakimsikiliza Carlos aliyekuwa akitoa maelekezo ya namna ambavyo kazi ingefanyika, aliwaeleza ugumu wa kazi husika uliowakabili mbele yao na jinsi ambavyo kila mmoja wao angeweza kufaidika kwa kupata mgao wake kutokana na kazi ile.

Lakini kabla hajaeendelea zaidi Jacky aliingia pale sebuleni kutokea jikoni akiwa mwenye furaha sana, mkononi alikuwa ameshika simu yake na alikuwa akimtazama Carlos kwa tabasamu. Jacky alikuwa amevaa fulana nyepesi nyeusi iliyoyaficha vyema matiti yake imara na juu yake alikuwa amevaa aproni, vazi maalumu lililotumika alipokuwa katika shughuli za mapishi.

Chini alivaa suruali yake ya rangi nyeusi ya jeans iliyolichora vyema umbo lake matata na miguuni alikuwa amevaa sandals nyepesi za kufunga na kamba.

Darling, things have gone well,” (Mpenzi, mambo yameiva) Jacky alipaza sauti yake kumwambia Carlos na kuwafanya watu wote wageuke kumtazama kwa shauku kubwa ya kutaka kusikia kile alichokuwa anataka kuwaambia.

Yusuf called me right now, says he has got a copy of their signed check, so I will meet him later in the evening,” (Yusuf kanipigia simu sasa hivi, anasema amepata kopi ya hundi yao yenye saini, hivyo nitakutana naye baadaye jioni) Jacky alisema huku akisimama jirani na kochi alilokuwa ameketi Carlos.

Habari ile ilikuwa njema zaidi kwa watu wote waliokuwepo pale sebuleni, walitazamana na kutabasamu huku wakibetua vichwa kuonesha kuwa tayari walishapiga hatua kubwa kuelekea kwenye ushindi.

That's good news, I'll make sure we don't lose this opportunity,” (Hiyo ni habari njema kabisa, nitahakikisha hatuipotezi nafasi hii) Carlos alisema huku akinyanyua mkono wake na kuupitisha nyuma ya Jacky na kumpapasa mgongoni huku akiendelea kutabasamu.

Jacky alimtazama Carlos kwa utulivu, hata hivyo uso wake haukuwa na tashwishwi yoyote. Aliwatupia jicho la wizi Kabwe na Liston kisha alianza kupiga hatua zake kwa madaha kuelekea jikoni.

Kisu, Kabwe na Liston walimsindikiza Jacky kwa macho huku wakionesha kuwakwa na tamaa, hata hivyo hakuna aliyethubutu kusema chochote kumhusu Jacky kwa kuwa walimhofia sana Carlos. Hivyo, kitambo kifupi cha ukimya kikafuatia mle ndani huku kila mmoja akiwaza lake.

Okay, nadhani kila kitu kipo kwenye mstari, sasa inakuwaje kuhusu malipo yetu?” hatimaye Kabwe alivunja ukimya huku akimkazia macho Carlos.

“Mnataka mlipwe leo leo kabla hata ya kufanya kazi?” Carlos alimuuliza Kabwe kwa mshangao huku akimkazia macho.

“Unajua nini, lazima niseme ukweli… umetutia hamasa kubwa sana kwa huu mjengo kama ikulu na asset mbalimbali unazomiliki, hata sisi tunahitaji kuishi maisha kama haya… kwa hiyo tunataka kujua tutalipwaje baada ya kazi, namaanisha malipo yetu ni shilingi ngapi?” Kabwe alisema huku akigeuza shingo yake kuwatazama Liston ambaye muda mwingi alikuwa kimya na Kisu.

Liston alibetua kichwa chake kuonesha kukubaliana na kauli ya Kabwe kisha akanyanyua bilauri yake na kugida pombe yote iliyokuwemo huku akisisimkwa mwili na kuikita ile bilauri juu ya meza.

“Ooh, nikadhani labda mnataka mlipwe kabisa pesa zenu hata kabla ya kazi haijafanyika!” Carlos alisema na kuongeza, “Kuhusu Kisu nimeshaongea naye kivyake, ila ninyi mtapata shilingi milioni hamsini, ishirini na tano kwa kila mmoja,” Carlos alisema kwa sauti tulivu huku akiwatazama kwa makini.

Kabwe na Liston walitazamana, kisha kitambo kifupi cha ukimya kikafuatia tena mle ndani, walionekana kuongea kwa ishara na kuonesha kuafikiana.

“Basi hakuna noma, kamanda, wacha sisi tusepe tukawahi mishemishe zingine, nakuaminia na ninaamini tutafanya kazi nzuri kwani Liston amenihakikishia kuwa hunaga longolongo kabisa,” Kabwe alisema huku akibetua kichwa chake kuonesha msisitizo. Aliinuka na kumpa ishara Liston waondoke.

“Ukishaweka mambo yote sawa mjulishe tu braza Kisu, yeye anajua pa kutupata, sisi tupo kamiligado,” Kabwe aliongezea huku akibeba chupa moja kubwa ya whisky, ambayo ilikuwa haijatumika ikiwa juu ya meza. Liston naye aliinuka, wakaagana na Carlos wakipeana mikono kisha Kabwe na Liston waliondoka wakiwaacha Carlos na Kisu bado wanatafakari huku wakiendelea kunywa pombe taratibu.

* * * * *

Zilikuwa zimesalia dakika chache kabla ya kutimia saa moja kamili usiku, giza tayari lilikuwa limeanza kutanda. Hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam ilikuwa ya baridi kidogo na manyunyu ya mvua yalikuwa yameanza kuanguka kutoka angani.

Pamoja na mvua ile lakini haikuzuia pilika pilika za watu zilizokuwa zimeshamiri katikati ya jiji hilo na hivyo kulifanya liendelee kuchangamka sana kama ilivyokuwa kawaida yake.

Wakati huo Jacky akiwa ndani ya chumba kikubwa chenye hadhi cha hoteli moja iliyokuwa katika ghorofa ya kwanza ya jengo la NSSF katika makutano ya barabara za mitaa ya Samora na Nnamdi Azikiwe, katikati ya jiji la Dar es Salaam. Ndani ya chumba kile kulikuwa na hewa safi iliyokuwa ikisambazwa taratibu na kiyoyozi kikubwa.

Alikuwa amefika pale na kulipia chumba kwa siku moja akijiandikisha kwa jina la Diana Mulenga kutoka Zambia na kwamba alikuwa jijini Dar es Salaam kuja kumtembelea rafiki yake wa kiume ambaye ni Mtanzania.

Itaendelea...
 
Wakuu, nawashukuru sana wote mlioguswa, kuniombea au kunitakia heri nipone haraka, sijaweza kuzisoma posti zenu zilizomo humu (nadhani nitazisoma taratibu nikipata muda), ila naamini wengi wenu mmeguswa. Bado sijaanza kwenda kazini lakini siwezi kuendelea kukaa nje ya jukwaa hili, acha tuendelee mdogo mdogo na simulizi yetu ya Kizungumkuti, kwani hata tatizo lililonipata (naamini kabisa) limekuwa kizungumkuti kama ilivyo stori hii...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole sana Bishop tunazidi kukuombea urudi kwenye hali yako
 
Kizungumkuti! - 36

Na Bishop Hiluka

Wakati huo Jacky akiwa ndani ya chumba kikubwa chenye hadhi cha hoteli moja iliyokuwa katika ghorofa ya kwanza ya jengo la NSSF katika makutano ya barabara za mitaa ya Samora na Nnamdi Azikiwe, katikati ya jiji la Dar es Salaam. Ndani ya chumba kile kulikuwa na hewa safi iliyokuwa ikisambazwa taratibu na kiyoyozi kikubwa.

Alikuwa amefika pale na kulipia chumba kwa siku moja akijiandikisha kwa jina la Diana Mulenga kutoka Zambia na kwamba alikuwa jijini Dar es Salaam kuja kumtembelea rafiki yake wa kiume ambaye ni Mtanzania.

Endelea...

Wakati anaingia katika ile hoteli, Jacky alikuwa katika muonekano tofauti kabisa, kwa yeyote aliyemfahamu kama angemuona pale ingemchukua muda mrefu kubaini kuwa aliyekuwa akimtazama alikuwa ndiye Jacky.

Alikuwa amevaa wigi la nywele ndefu zilizolalia mgongoni na kumfanya afanane na machotara wa Kizungu huku sura yake yenye mvuto wa asilimia mia moja ikipendezeshwa zaidi kwa kope ndefu za bandia zilizong’arishwa na kuyafanya macho yake yawe wazi nusu, na mikononi alikuwa na kucha ndefu za bandia.

Alivaa miwani ya kijasusi ambayo kwa macho ya kawaida ilionekana kama ya mtu mwenye matatizo ya uoni, ilikuwa na lenzi maalumu iliyokuwa na kamera ya kurekodi matukio mbalimbali aliyoyataka. Jioni ile alikuwa amevaa gauni refu la kitenge cha wax lililodariziwa vizuri na kichwani alivaa kilemba kikubwa. Alionekana ni mwanamke mwenye uwezo mkubwa kifedha, na pengine mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio.

Now I’m ready… let me wait for Yusuf to accomplish my mission,” (Sasa niko tayari… ngoja nimsubiri Yusuf ili kukamilisha misheni yangu) Jacky aliwaza mara tu baada ya kutoka bafuni na kujibwaga kitandani kumsubiri Yusuf, kwani walikuwa wamekubaliana kukutana katika hoteli ile jioni ili akabidhiwe nakala kivuli ya hundi iliyokuwa na saini.

When I finish this project, I’ll go back to a normal life like other married women…” (Nitakapomaliza kazi hii, nitarudi katika maisha ya kawaida kama wanawake wengine walioolewa…) Jacky alishtuliwa na sauti ya mtu aliyegonga mlangoni taratibu.

Aliinuka na kufungua mlango kidogo ilia pate upenyo wa kumuona aliyekuwa nje, na hapo akakutana na sura ya Yusuf aliyekuwa amesimama akiwa na tashwishwi. Jacky akaufungua mlango kumkabili Yusuf, lakini Yusuf alipomuona Jacky, ambaye yeye alimfahamu kwa jina la Belinda, akashtuka.

Yusuf alishikwa na bumbuwazi akidhani labda alikuwa amekosea namba ya chumba, kwani alikuwa akimuona msichana mwingine kabisa ambaye hakumtarajia. Aliinua macho yake kusoma namba kwenye kibao kilichokuwa juu ya mlango wa kile chumba.

Akiwa bado ameshikwa na bumbuwazi na kabla hajajua afanye nini akashtukia amevutwa na kuingizwa ndani ya kile chumba huku mlango ukifungwa haraka, na kilichofuata baada ya ahapo Jacky alimkumbatia na kumwagia mabusu mfululizo huku akijitambulisha kwake kuwa yeye ni yule yule Belinda aliyemfahamu.

“Nilikuwa na wasiwasi kuwa pengine usingeweza kuja baada ya kunieleza kuwa kulitokea mabadiliko ya ratiba zako baada ya kutembelewa ghafla nyumbani ya wakwe zako,” Jacky alisema huku akiupokea mkoba mdogo mweusi aliokuja nao Yusuf na kuuweka kando ya kitanda, kisha akamshika mkono akimuongoza kuketi juu ya kitanda.

“Unajua siwezi kupuuza miadi hii ya muhimu kwetu sote, hasa nikikumbuka namna ulivyonikimbiza mchakamchaka siku ile na vilio vyako vya mahaba ambavyo hadi leo bado havijanitoka akilini mwangu. Kwa ahadi hii hata kama baba yangu mzazi angefariki leo nisingeshindwa kuja kwako,” Yusuf alisema huku akizidi kumtazama Jacky kwa makini.

Hmm! Stop joking, I know you’re not serious!” (Hmm! Acha utani, najuaa haumaanishi hivyo!) Jacky alisema kwa utani huku akirembua macho yake kwa lengo ya kuzidi kuivuruga akili ya Yusuf.

It’s true, you are very gorgeous, more than beautiful. Your prettiness I do not know what to compare with. Every time I see you it’s like I have seen an angel pulled from above,” (Ni kweli, wewe ni mrembo sana, zaidi ya mzuri. Uzuri wako sijui niufananishe na nini. Kila ninapokuona ni kama nimeona malaika uliyeshushwa toka juu) Yusuf alisema na kumfanyia Jacky atoe tabasamu bashasha huku akimkumbatia Yusuf na kumpiga mabusu mfululizo.

Belinda, you are a very exceptional woman I have ever met…” (Belinda, wewe ni mwanamke wa kipekee kabisa kuwahi kukutana naye…) Yusuf alimwambia Jacky huku akimkumbatia kwa nguvu.

And since we met that day it’ll not pass even a second without thinking about you. Within a short period of time you have entered into my veins and I am wondering if there is anything you have put in my body in this way,” (Na tangu tulipokutana siku ile haipiti hata sekunde moja bila kukuwaza. Ndani ya kipindi kifupi tu umeniingia katika kila mshipa wa mwili wangu hadi najiuliza kama kuna kitu umeniwekea kiasi cha kunichanganya namna hii!” maneno mfululizo yalizidi kumtoka Yusuf.

Yusuf, we still have a lot of time to talk about all these things but now there is only one thing we have to do,” (Yusuf, bado tuna muda mwingi tutaongea mambo hayo yote lakini kwa sasa kuna jambo moja tu ambalo tunatakiwa kulifanya) Jacky alimwambia Yusuf na kumvutia kifuani kwake kisha akapeleka mkono wake ikulu na kuanza kutomasa malighafi zake kwa ufundi wa hali ya juu, mara zikafura kwa hasira.

Jacky alitumia utundu wa hali ya juu kumfanya Yusuf aongee lugha aliyoitaka kwani Waswahili wanasema kuwa ‘kichwa cha chini kikisimama cha juu huwa hakifanyi kazi sawasawa’.

“Belinda, umeichanganya akili yangu kiasi kwamba najihisi kuwa nataka kuwa mwendawazimu kwa ajili yako…” Yusuf alisema huku akihema kwa nguvu na muda mfupi uliofuata Jacky na Yusuf walikuwa juu ya kitanda kikubwa wakiwa wamemezwa na ulimwengu mwingine kabisa, wa sinema ya mapenzi na mahaba mazito yenye kila aina ya kionjo cha kumtoa nyoka pangoni.

Kwa wakati ule hawakukumbuka kingine chochote isipokuwa kuivunja amri ya sita, huku mapenzi yakionekana kunoga kwa namna yake na miguno ya mahaba ikahanikiza kila mahali mle ndani.

Katika purukshani zile mito ya kujiegemeza pale kitandani iliangukia sakafuni, mmoja huku na mwingine kule lakini hakuna aliyejishughulisha kuiokota. Shuka lilikuwa limevurugwa ovyo wakati wazinzi wale walipokuwa wakivingirishana kwa sarakasi za aina yake pale kitandani.

Takribani muda wa saa moja ulipoyeyuka wote wawili walikuwa hoi huku kila mmoja akionekana kutosheka na mwenzake. Jacky alikuwa wa kwanza kuamka na kuketi kwenye ukingo wa kile kitanda huku akiwa mtupu kama alivyozaliwa.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom