Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Shunie, my Jacky na wengineo, kwanza naomba samahani sana maana mmenivumilia tangu Jumatano nilipoingia humu mara ya mwisho, sijaweza tena kuingia kwa kuwa nilivamiwa na nimeumizwa vibaya, siku zote hizi nilikuwa hospitali ila hivi sasa nimetafuta kila njia niweze kuwajulisha lakini bado sipo vizuri. Nawashukuru kwa kunivumilia, endeleeni hivyo hivyo natumaini baada ya siku mbili au tatu tutakuwa pamoja katika kizungumkuti...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole Sana baba Jacky
 
Shunie, my Jacky na wengineo, kwanza naomba samahani sana maana mmenivumilia tangu Jumatano nilipoingia humu mara ya mwisho, sijaweza tena kuingia kwa kuwa nilivamiwa na nimeumizwa vibaya, siku zote hizi nilikuwa hospitali ila hivi sasa nimetafuta kila njia niweze kuwajulisha lakini bado sipo vizuri. Nawashukuru kwa kunivumilia, endeleeni hivyo hivyo natumaini baada ya siku mbili au tatu tutakuwa pamoja katika kizungumkuti...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole sana Bishop Mungu akuponye na kukutia nguvu jamani tutavumilia mpaka uwe sawa tu wala usijali ilikuwaje ulikua njiani usiku au
 
Shunie, my Jacky na wengineo, kwanza naomba samahani sana maana mmenivumilia tangu Jumatano nilipoingia humu mara ya mwisho, sijaweza tena kuingia kwa kuwa nilivamiwa na nimeumizwa vibaya, siku zote hizi nilikuwa hospitali ila hivi sasa nimetafuta kila njia niweze kuwajulisha lakini bado sipo vizuri. Nawashukuru kwa kunivumilia, endeleeni hivyo hivyo natumaini baada ya siku mbili au tatu tutakuwa pamoja katika kizungumkuti...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole Sana mkuu. Ndio dunia hii....
KIZUNGUMKUTI.

Mola akupe afya njema.
 
Shunie, my Jacky na wengineo, kwanza naomba samahani sana maana mmenivumilia tangu Jumatano nilipoingia humu mara ya mwisho, sijaweza tena kuingia kwa kuwa nilivamiwa na nimeumizwa vibaya, siku zote hizi nilikuwa hospitali ila hivi sasa nimetafuta kila njia niweze kuwajulisha lakini bado sipo vizuri. Nawashukuru kwa kunivumilia, endeleeni hivyo hivyo natumaini baada ya siku mbili au tatu tutakuwa pamoja katika kizungumkuti...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Pole mkuu Mungu akufanyie wepesi
 
Wakuu, nawashukuru sana wote mlioguswa, kuniombea au kunitakia heri nipone haraka, sijaweza kuzisoma posti zenu zilizomo humu (nadhani nitazisoma taratibu nikipata muda), ila naamini wengi wenu mmeguswa. Bado sijaanza kwenda kazini lakini siwezi kuendelea kukaa nje ya jukwaa hili, acha tuendelee mdogo mdogo na simulizi yetu ya Kizungumkuti, kwani hata tatizo lililonipata (naamini kabisa) limekuwa kizungumkuti kama ilivyo stori hii...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
 
Kizungumkuti! - 30

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

Yusuf akashtuka na kufumbua macho yake, macho yake yakaanza kutambaa katika mwili wa mkewe, yakianza na mapaja yaliyonona kuelekea juu kisha yakakutana na nyonga zilizofinyangwa barabara.

Macho yake yakatuwama kwa muda katikati ya mapaja ya mkewe, kisha yakafunga safari kuelekea kiunoni yakakutana na kiuno kilichobonyea na kuacha fursa ya nyonga kuchanua zilivyotaka. Kiuno kilirembwa na tumbo dogo ambalo lilikana kuwa wakati fulani lilishabeba kiumbe kwa muda wa miezi tisa.

Hamu haikuishia hapo, macho yalielekea kwenye kifua kilichobeba matiti madogo yaliyokuwa yamesimama kana kwamba hakuwahi kunyonyesha hapo kabla. Hamu ya mapenzi ikamjaa juu ya mkewe.

Macho yake hayakuishia hapo bali yalipanda hadi kwenye uso wa mkewe, akauona uso wa mkewe ukiwa mkavu usio na tashwishwi yoyote. Yusuf akatweta na hamu ya mapenzi ikamuisha mara moja.

Endelea...

Akiwa bado anatafakari jinsi ya kuanzisha maongezi na mkewe mara akamuona mkewe akiondoka haraka na baada ya muda akarudi akiwa amebeba jagi lililokuwa na maji ya kunawa na beseni dogo la kunawia, akaviweka pale mezani na kuondoka tena na baada ya muda akarudi akiwa amebea sahani ya chakula na kukitenga pale mezani bila hata kusema kitu, kisha akaelekea chumbani na kufunga mlango.

Yusuf alimtazama kwa kila hatua aliyopita bila kusema neno kisha akakaa pale kwa kitambo kirefu akikiangalia kile chakula, muda wote hakuwa akihisi njaa. Japo kile chakula kilikuwa kimepikwa vizuri sana lakini hakuweza kula. Alibaki kukikodolea macho akiutazama wali uliokolea nazi, samaki wa maji baridi, mboga za majani na maharage.

Baada ya kitambo kirefu cha ukimya huku akikitazama kile chakula hatimaye aliamua kula japo matonge kadhaa ili isionekane kuwa alikuwa amesusa chakula, kisha alikifunika na kuinuka akaingia chumbani kumfuata mkewe. Alipoingia chumbani alimkuta mkewe ameketi kwenye pembe ya kitanda akiwa kajiinamia anawaza na mara alipomuona mumewe alimtazama kwa jicho kali sana.

“Mama Jasmine, hivi ni mambo gani haya yasiyoisha? Nimeshakuomba samahani zaidi ya mara tatu lakini naona mwenzangu bado una kinyongo…” Yusuf aliongea kwa sauti ya chini na ya kusihi.

“Hayawezi kuisha kirahisi kama unavyodhani!” Mama Jasmine alisema kwa sauti tulivu lakini yenye hasira.

“Kwa hiyo tutaishi maisha haya hadi lini?” Yusuf aliuliza tena huku akimwangalia mkewe kwa huzuni.

“Niache bwana, nahitaji kupumzika. We nenda kwa huyo huyo malaya wako,” Mama Jasmine alijibu kwa hasira na kujilaza kitandani.

“Dah, natamani hii siku ifutike kabisa akilini mwangu. Hata kama ikibaki niione kama ndoto tu. Nahisi kama vile unanichukia sana,” Yusuf alimweleza mkewe bila kumtazama wala kusubiri jibu, akatoka zake kimya kimya.

Alifungua mlango wa chumbani akapita sebuleni na kuelekea nje hadi barazani. Muda ule alikuwa bado hajavua saa yake ya mkononi. Hivyo aliitazama na kugundua kuwa ilishatimu saa tatu na ushee.

Alisimama pale nje akainua macho yake kutazama angani. Anga lilikuwa wazi na la rangi ya samawati liking’arishwa kwa wingi wa nyota na mwezi mkubwa uliokuwa umevaa rangi nyekundu aliouona vizuri kutokea pale alipokuwa amesimama.

“Mwezi mwandamo huanza mchanga, pole pole hukua na kuwa mpevu na huweza kuonekana kwa wote hata wale waonao ukungu mbele ya macho yao, na baadaye huwa mwekundu na huogopesha manyani porini,” Yusuf aliwaza akiyakumbuka maneno ya mwanazuoni mmoja aliyemsoma kitabuni wakati akiwa sekondari.

Aliendelea kuutazama ule mwezi mwekundu, akaanza kutafakari kuhusu masimulizi aliyowahi kuyasikia kuwa ukifikia hatua hiyo huogopesha manyani porini.

Muda huo upepo wa usiku uliipuliza ngozi yake na kumfanya ajisikie vizuri na hapo ndipo alipogundua kuwa ngozi yake ilinata kutokana na jasho. Alitamani kuingia ndani akachukue maji na kuelekea bafuni kuoga, hata hivyo, hakuwa na hamu ya kurudi ndani.

Donge la fadhaa lilimkaba kooni hasa alipohisi kuwa huenda mkewe aliamua kumchukia na wala hakutaka kumsamehe. Akawaza nini cha kufanya ili kuurudisha upendo katika familia yake. Mara akakumbuka msemo kuwa “hakuna mkate mgumu mbele ya chai” hii ilimaanisha kwa Yusuf kuwa njia pekee ilikuwa ni kupata fedha nyingi ambazo zingeweza kurudisha heshima na furaha ndani ya nyumba.

Alipowaza suala la pesa mara akamkumbuka Jacky ambaye yeye alimtambua kwa jina la Belinda. Alijilaumu kwa kuiacha simu yake ndani angempigia ili ingalau asikie sauti yake ya kubembeleza, huenda ingempunguzia stress. Alitamani kuingia ndani akachukue simu yake lakini alisita.

“Dah, Belinda ameyateka mawazo yangu na akili yangu yote inamuwazia yeye tu. Katika mazingira kama haya nahitaji kuwa naye tu karibu nimkumbatie mikononi mwangu, nikimbembeleza kama mtoto mdogo huku nikiisikia miguno yake na sauti yake nyororo anapolalama kwa raha…” Yusuf aliwaza na kushusha pumzi.

“Ki ukweli Belinda yuko tofauti sana na wanawake wengine wote na ana mvuto wa ajabu mno, pia amebarikiwa vitu vya kipekee ambavyo ni vigumu hata kuvielezea…” Yusuf alizidi kusumbuliwa na mawazo juu ya Jacky, kwa muda mrefu alimuwazia Jacky tu. Mara akachoka kusimama na kuamua kukaa kwenye ngazi za baraza.

Alipoitazama tena saa yake akashtuka kuona kuwa ilikuwa imeshatimia saa sita na dakika kumi na tano usiku! Ilikuwa imeshaingia siku nyingine akiwa anapigwa na ubaridi pale nje. Aliamua kukiegemeza kichwa chake kwenye nguzo ya ukuta na kufumba macho kwani uchovu ulimuelemea sana, na mbu nao hawakumwacha salama.

Mama Jasmine akiwa chumbani amelala kitandani alishtuka na kuangaza macho yake huku na kule, Yusuf hakuwepo ndani. Akapuuzia na kufumba tena macho yake kulala, hata hivyo, alijikuta akianza kupatwa na wasiwasi.

“Mke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe, lakini mwenye busara huijenga na kuiboresha nyumba yake,” Mama Jasmine alijikuta akiyakumbuka maneno hayo kutoka ndani ya Biblia ambayo aliwahi kuyasikia kutoka kwa mchungaji mmoja wa kanisa lililokuwa jirani na nyumba waliyokuwa wakiishi.

Japo hakuwa Mkristo lakini maneno yale yalikuwa yamemuingia na aliyakariri japo hakujua yalipatikana wapi ndani ya hiyo Biblia. Mara akajikuta akiinuka kutoka pale kitandani na kutoka, akamwangalia mumewe pale sebuleni hakumuona, akafungua mlango na kumwangalia kule uani, hayupo!

Sasa akaingiwa na hasira akidhani kuwa labda aliondoka kwenda kulala kwa kimada wake waliyekesha wote kabla hajarudi nyumbani asubuhi, akipanga kumkomoa.

Akatoka nje na kumkuta Yusuf akiwa amejikunyata pale kibarazani kwenye ngazi akiwa chakula cha mbu, alijikuta akiingiwa na huruma, alisimama akimtazama kwa huruma na kuamua kumwamsha kwa kumpiga piga taratibu mgongoni huku akimwita. Yusuf alishtuka na kuamka, mkewe akamuinua na kumuongoza ndani.

Yusuf alipoingia chumbani alivua fulana yake na kujitupa kitandani, wala hakuwa tena na wazo la kuoga. Dakika mbili baadaye alikuwa anakoroma.

Mama Jasmine alisimama pale akimtazama mumewe kwa makini kisha akarudishia chandarua vizuri na kuzima taa halafu akapanda kitandani na kulala pembeni ya mumewe.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 31

Na Bishop Hiluka

Akatoka nje na kumkuta Yusuf akiwa amejikunyata pale kibarazani kwenye ngazi akiwa chakula cha mbu, alijikuta akiingiwa na huruma, alisimama akimtazama kwa huruma na kuamua kumwamsha kwa kumpiga piga taratibu mgongoni huku akimwita. Yusuf alishtuka na kuamka, mkewe akamuinua na kumuongoza ndani.

Yusuf alipoingia chumbani alivua fulana yake na kujitupa kitandani, wala hakuwa tena na wazo la kuoga. Dakika mbili baadaye alikuwa anakoroma.

Mama Jasmine alisimama pale akimtazama mumewe kwa makini kisha akarudishia chandarua vizuri na kuzima taa halafu akapanda kitandani na kulala pembeni ya mumewe.

Endelea...

* * * * *

Sauti ya kengele ya getini iliyokuwa ikilia kwa fujo kuashiria kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa getini iliwashtua Carlos na Jacky kutoka katika usingizi mzito uliokuwa umewachukua kwa muda mrefu.

Siku ya Jumanne ilikuwa imepita ikaipisha Jumatano, muda huo ilikuwa ni saa tatu za asubuhi wakati Carlos na Jacky wakiwa bado wamelala kitandani huku zile taa mbili za rangi nyekundu zilizokuwa juu ya droo mbili kila upande wa kile kitanda zikiwa zinatoa mwanga hafifu wenye mg’ao na kufanya nusu ya chumba kuwa kizani.

Carlos alipoitupia jicho saa yake ya mkononi aligundua kuwa walikuwa wamelala kwa muda mrefu kufuatia uchovu wa siku iliyotangulia. Muda ule miale ya jua la saa tatu asubuhi ilikuwa inapenya dirishani na kutuama pale kitandani walipokuwa wamelala.

Haraka Carlos alilitupa shuka pembeni na kutega masikio yake vizuri kusikiliza na kugundua kuwa alikuwa sahihi kwani aliweza kusikia vizuri sauti ya mwanamume akiita kule nje getini. Bahati mbaya nyumba ile haikuwa na mlinzi na wala hakupenda kuajiri mlinzi.

Ile nyumba ilikuwa imewekwa mitambo maalumu ya ulinzi, lakini pia alitaka kuwa huru zaidi akiwa yeye na Jacky tu ili wafanye mambo yao bila bughudha na hakupenda kabisa watu wasiohusika wajue nyendo zao. Ndiyo maana hata ndugu aliwapeleka kwenda kuishi kwenye nyumba zake zingine zilizokuwa Mbezi Beach na Sinza.

Alishuka haraka kutoka pale kitandani na kutoka haraka akimwacha Jacky anamtazama kwa mshangao, akaelekea kwenye ngazi ambazo alizishuka haraka na kukatiza katikati ya sebule na kuuendea mlango wa barazani. Aliufungua na kutoka kisha akakatiza katikati ya ile fensi hadi kwenye geti kubwa.

Alisimama pale akachungulia nje kupitia upenyo mdogo uliokuwepo kwenye geti dogo akiwa makini kumtazama mtu aliyekuwa akibonyeza ile kengele. Alilamba midomo yake kuilainisha huku akikunja sura yake na kutengeneza matuta madogo usoni.

Kupitia ule upenyo mdogo uliokuwepo kwenye geti dogo, aliweza kumuona mwanamume mmoja mrefu aliyekuwa amepanda hewani kisawasawa na mwenye mwili ulioshiba, alikuwa mweupe kama mzungu, akiwa na umri wa miaka takriban hamsini na misuli imara ya mikononi iliyotuna kikamilifu vilimfanya aonekane kama bondia mkongwe.

Alikuwa na upara mpana uliokuwa unawaka na uso wake ulikuwa mpana na ulitulia kama maji ya mtungini, huku miwani yake mikubwa myeusi ikiwa imeyahifadhi macho yake makubwa.

Yule mwanamume alikuwa amevaa suruali nyeusi ya jeans na juu alivaa fulana mchinjo nyekundu iliyokibana vyema kifua chake kiasi kwamba ungeweza kudhani ile fulana ingetatuka muda wowote. Miguuni alikuwa amevaa buti ngumu nyeusi za ngozi imara ya mamba.

Jina lake halisi aliitwa Joram Mbezi ila alijulikana kwa jina la Kisu kutokana na ufundi wake wa kutumia kisu katika mapigano. Pia kabla hajamuua mtu kwa kisu alipenda kumuuliza, “Jina langu nani?” na kilichofuata baada ya lile swali ilikuwa ni kukizamisha kisu sehemu ambapo angeweza kuutoa uhai wa mtu huyo.

Kisu alikuwa amepata mafunzo juu ya matumizi ya silaha ndogo ndogo, na alijifunza mambo mengine mengi, alipokuwa nchini Kenya ambako aliishi na msichana mmoja wa Kikikuyu aliyeitwa Njeli, Kisu alitambulishwa kwa vijana hatari wa kazi alioshirikiana nao katika matukio mbalimbali ya ujambazi.

Kati yao, kijana mmoja aliyejiita Spoiler, ndiye aliyempa mafunzo halisi juu ya matumizi ya kisu cha kurusha, na ikafikia hatua Kisu akawa fundi kuliko hata mwalimu wake, kwani alikuwa na uwezo wa kulenga mboni ya jicho, hata la kuku, na kisu kikatua pale pale. Na hapo ndipo jina la Kisu lilipoanza kutumika rasmi huku likilifunika jina halisi la Joram.

Carlos alipotazama vizuri alimuona mwanamume yule akiwa amesimama akiliangalia lile geti kwa makini na kando yake ilikuwepo pikipiki aina ya Boxer. Mara moja Carlos akamtambua yule mwanamume, na bila kusita akakitekenya kitasa cha lile geti kwa funguo kuifyatua kabari yake kisha taratibu akalifungua lile geti huku sura yake ikipambwa na tabasamu.

Ooh, Kisu, the devil himself!” (Ooh Kisu, shetani mwenyewe!) Carlos alisema kwa furaha huku akiachia tabasamu la makaribisho.

Oh, Carlos, long time no see!” (Oh Carlos, siku nyingi hatujaonana!) yule mwanamume aliitikia huku akimkumbatia Carlos kwa furaha. Wakatazamana, bila shaka wakikumbuka yaliyopita.

“Umepungua kidogo, Kisu,” Carlos alisema huku akimtazama Kisu kwa makini, mkono wake wa kushoto ukiwa juu ya bega la kulia la Kisu. Kisu alimtazama kwa chini kidogo kutokana na kuwa alikuwa mrefu zaidi ya Carlos.

“Ni maisha tu ndugu yangu. Si unajua tangu janga lile kule Arusha mambo hayakukaa sawa tena hadi leo, nimekuwa mtu wa kubangaiza? Kwa kweli mkasa ule haukuniacha salama kabisa, najaribu kujisahaulisha lakini bado mawazo yananijia tu. Ni jana mchana tu nilikuwa naukumbuka mkasa wote ule, nikakukumbuka na wewe, kumbe usiku unanipigia simu.”

“Ni kweli. Maisha, maisha, maisha…” Carlos alisema na kucheka kidogo huku akitazama pembeni. Aliweka mikono yake kiunoni na kuuma mdomo wa chini.

“Maisha ni kitu cha ajabu sana! Utakuta huyu anasumbuliwa na hili, na mwingine anasumbuliwa na lile, ndiyo dunia ilivyo…” Carlos alisema, kisha kama aliyekumbuka kitu, akamtazama Kisu kwa makini. “Okay ingiza usafiri wako yako ndani.”

Kisu akakokota pikipiki yake haraka haraka na kuiingiza ndani ya fensi ya lile jumba. Alipoiegesha vizuri ile pikipiki yake akajikuta akizidi kupata mshangao, alilitazama lile jumba huku akistaajabu ukubwa wake.

Wakati huo Kisu aliendelea kuliajabia lile jumba la kifahari la ghorofa mbili lililokuwa katika hali ya ukimya sana likiwa limezungukwa na ukuta mrefu uliofungwa mfumo maalumu wa umeme wa kuzuia wezi juu yake usiomwezesha mtu kuona ndani, na lilikuwa na sehemu za wazi zenye bustani nzuri ya maua na nyasi za kijani kibichi zilizokatwa vizuri.

Alizitazama zile gari za kifahari, BMW X6 xDrive 50i la rangi ya samawati, Range Rover Sport L494 la rangi nyeupe na Toyota Landcruiser GX V8 lililokuwa na rangi nyeusi zilizokuwa kwenye banda la wazi la kuegeshea magari.

Kisha akazungusha macho yake haraka kutazama vizuri sehemu ya mbele ya hiyo nyumba iliyokuwa imezungukwa na bustani nzuri ya maua ya kupendeza. Carlos alitabasamu na kumkaribisha ndani.

Kisha wakaanza kuzitupa hatua zao kuelekea ndani wakipita katikati ya bustani ambapo kulitengenezwa njia nzuri ya kutembea kwa miguu kwa matofali madogo madogo yaliyokuwa yanavutia, Kisu alitembea kikakamavu katika namna iliyofanya hatua zake zitetemeshe ardhi kila alipokanyaga ardhi kwa buti zake ngumu miguuni.

Carlos alitangulia kuingia ndani huku akimkaribisha Kisu ambaye alipoingia tu akamkuta Jacky akiwa amesimama kwenye mlango uliokuwa ukielekea kwenye jiko, akiwa bado amevaa nguo yake nyepesi ya pinki ya kulalia iliyolichora vizuri umbo lake na kuionesha nguo yake ya ndani.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 30

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

Yusuf akashtuka na kufumbua macho yake, macho yake yakaanza kutambaa katika mwili wa mkewe, yakianza na mapaja yaliyonona kuelekea juu kisha yakakutana na nyonga zilizofinyangwa barabara.

Macho yake yakatuwama kwa muda katikati ya mapaja ya mkewe, kisha yakafunga safari kuelekea kiunoni yakakutana na kiuno kilichobonyea na kuacha fursa ya nyonga kuchanua zilivyotaka. Kiuno kilirembwa na tumbo dogo ambalo lilikana kuwa wakati fulani lilishabeba kiumbe kwa muda wa miezi tisa.

Hamu haikuishia hapo, macho yalielekea kwenye kifua kilichobeba matiti madogo yaliyokuwa yamesimama kana kwamba hakuwahi kunyonyesha hapo kabla. Hamu ya mapenzi ikamjaa juu ya mkewe.

Macho yake hayakuishia hapo bali yalipanda hadi kwenye uso wa mkewe, akauona uso wa mkewe ukiwa mkavu usio na tashwishwi yoyote. Yusuf akatweta na hamu ya mapenzi ikamuisha mara moja.

Endelea...

Akiwa bado anatafakari jinsi ya kuanzisha maongezi na mkewe mara akamuona mkewe akiondoka haraka na baada ya muda akarudi akiwa amebeba jagi lililokuwa na maji ya kunawa na beseni dogo la kunawia, akaviweka pale mezani na kuondoka tena na baada ya muda akarudi akiwa amebea sahani ya chakula na kukitenga pale mezani bila hata kusema kitu, kisha akaelekea chumbani na kufunga mlango.

Yusuf alimtazama kwa kila hatua aliyopita bila kusema neno kisha akakaa pale kwa kitambo kirefu akikiangalia kile chakula, muda wote hakuwa akihisi njaa. Japo kile chakula kilikuwa kimepikwa vizuri sana lakini hakuweza kula. Alibaki kukikodolea macho akiutazama wali uliokolea nazi, samaki wa maji baridi, mboga za majani na maharage.

Baada ya kitambo kirefu cha ukimya huku akikitazama kile chakula hatimaye aliamua kula japo matonge kadhaa ili isionekane kuwa alikuwa amesusa chakula, kisha alikifunika na kuinuka akaingia chumbani kumfuata mkewe. Alipoingia chumbani alimkuta mkewe ameketi kwenye pembe ya kitanda akiwa kajiinamia anawaza na mara alipomuona mumewe alimtazama kwa jicho kali sana.

“Mama Jasmine, hivi ni mambo gani haya yasiyoisha? Nimeshakuomba samahani zaidi ya mara tatu lakini naona mwenzangu bado una kinyongo…” Yusuf aliongea kwa sauti ya chini na ya kusihi.

“Hayawezi kuisha kirahisi kama unavyodhani!” Mama Jasmine alisema kwa sauti tulivu lakini yenye hasira.

“Kwa hiyo tutaishi maisha haya hadi lini?” Yusuf aliuliza tena huku akimwangalia mkewe kwa huzuni.

“Niache bwana, nahitaji kupumzika. We nenda kwa huyo huyo malaya wako,” Mama Jasmine alijibu kwa hasira na kujilaza kitandani.

“Dah, natamani hii siku ifutike kabisa akilini mwangu. Hata kama ikibaki niione kama ndoto tu. Nahisi kama vile unanichukia sana,” Yusuf alimweleza mkewe bila kumtazama wala kusubiri jibu, akatoka zake kimya kimya.

Alifungua mlango wa chumbani akapita sebuleni na kuelekea nje hadi barazani. Muda ule alikuwa bado hajavua saa yake ya mkononi. Hivyo aliitazama na kugundua kuwa ilishatimu saa tatu na ushee.

Alisimama pale nje akainua macho yake kutazama angani. Anga lilikuwa wazi na la rangi ya samawati liking’arishwa kwa wingi wa nyota na mwezi mkubwa uliokuwa umevaa rangi nyekundu aliouona vizuri kutokea pale alipokuwa amesimama.

“Mwezi mwandamo huanza mchanga, pole pole hukua na kuwa mpevu na huweza kuonekana kwa wote hata wale waonao ukungu mbele ya macho yao, na baadaye huwa mwekundu na huogopesha manyani porini,” Yusuf aliwaza akiyakumbuka maneno ya mwanazuoni mmoja aliyemsoma kitabuni wakati akiwa sekondari.

Aliendelea kuutazama ule mwezi mwekundu, akaanza kutafakari kuhusu masimulizi aliyowahi kuyasikia kuwa ukifikia hatua hiyo huogopesha manyani porini.

Muda huo upepo wa usiku uliipuliza ngozi yake na kumfanya ajisikie vizuri na hapo ndipo alipogundua kuwa ngozi yake ilinata kutokana na jasho. Alitamani kuingia ndani akachukue maji na kuelekea bafuni kuoga, hata hivyo, hakuwa na hamu ya kurudi ndani.

Donge la fadhaa lilimkaba kooni hasa alipohisi kuwa huenda mkewe aliamua kumchukia na wala hakutaka kumsamehe. Akawaza nini cha kufanya ili kuurudisha upendo katika familia yake. Mara akakumbuka msemo kuwa “hakuna mkate mgumu mbele ya chai” hii ilimaanisha kwa Yusuf kuwa njia pekee ilikuwa ni kupata fedha nyingi ambazo zingeweza kurudisha heshima na furaha ndani ya nyumba.

Alipowaza suala la pesa mara akamkumbuka Jacky ambaye yeye alimtambua kwa jina la Belinda. Alijilaumu kwa kuiacha simu yake ndani angempigia ili ingalau asikie sauti yake ya kubembeleza, huenda ingempunguzia stress. Alitamani kuingia ndani akachukue simu yake lakini alisita.

“Dah, Belinda ameyateka mawazo yangu na akili yangu yote inamuwazia yeye tu. Katika mazingira kama haya nahitaji kuwa naye tu karibu nimkumbatie mikononi mwangu, nikimbembeleza kama mtoto mdogo huku nikiisikia miguno yake na sauti yake nyororo anapolalama kwa raha…” Yusuf aliwaza na kushusha pumzi.

“Ki ukweli Belinda yuko tofauti sana na wanawake wengine wote na ana mvuto wa ajabu mno, pia amebarikiwa vitu vya kipekee ambavyo ni vigumu hata kuvielezea…” Yusuf alizidi kusumbuliwa na mawazo juu ya Jacky, kwa muda mrefu alimuwazia Jacky tu. Mara akachoka kusimama na kuamua kukaa kwenye ngazi za baraza.

Alipoitazama tena saa yake akashtuka kuona kuwa ilikuwa imeshatimia saa sita na dakika kumi na tano usiku! Ilikuwa imeshaingia siku nyingine akiwa anapigwa na ubaridi pale nje. Aliamua kukiegemeza kichwa chake kwenye nguzo ya ukuta na kufumba macho kwani uchovu ulimuelemea sana, na mbu nao hawakumwacha salama.

Mama Jasmine akiwa chumbani amelala kitandani alishtuka na kuangaza macho yake huku na kule, Yusuf hakuwepo ndani. Akapuuzia na kufumba tena macho yake kulala, hata hivyo, alijikuta akianza kupatwa na wasiwasi.

“Mke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe, lakini mwenye busara huijenga na kuiboresha nyumba yake,” Mama Jasmine alijikuta akiyakumbuka maneno hayo kutoka ndani ya Biblia ambayo aliwahi kuyasikia kutoka kwa mchungaji mmoja wa kanisa lililokuwa jirani na nyumba waliyokuwa wakiishi.

Japo hakuwa Mkristo lakini maneno yale yalikuwa yamemuingia na aliyakariri japo hakujua yalipatikana wapi ndani ya hiyo Biblia. Mara akajikuta akiinuka kutoka pale kitandani na kutoka, akamwangalia mumewe pale sebuleni hakumuona, akafungua mlango na kumwangalia kule uani, hayupo!

Sasa akaingiwa na hasira akidhani kuwa labda aliondoka kwenda kulala kwa kimada wake waliyekesha wote kabla hajarudi nyumbani asubuhi, akipanga kumkomoa.

Akatoka nje na kumkuta Yusuf akiwa amejikunyata pale kibarazani kwenye ngazi akiwa chakula cha mbu, alijikuta akiingiwa na huruma, alisimama akimtazama kwa huruma na kuamua kumwamsha kwa kumpiga piga taratibu mgongoni huku akimwita. Yusuf alishtuka na kuamka, mkewe akamuinua na kumuongoza ndani.

Yusuf alipoingia chumbani alivua fulana yake na kujitupa kitandani, wala hakuwa tena na wazo la kuoga. Dakika mbili baadaye alikuwa anakoroma.

Mama Jasmine alisimama pale akimtazama mumewe kwa makini kisha akarudishia chandarua vizuri na kuzima taa halafu akapanda kitandani na kulala pembeni ya mumewe.

Itaendelea...
Mama Jasmeen nae
"Mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kizungumkuti! - 32

Na Bishop Hiluka

Kisha wakaanza kuzitupa hatua zao kuelekea ndani wakipita katikati ya bustani ambapo kulitengenezwa njia nzuri ya kutembea kwa miguu kwa matofali madogo madogo yaliyokuwa yanavutia, Kisu alitembea kikakamavu katika namna iliyofanya hatua zake zitetemeshe ardhi kila alipokanyaga ardhi kwa buti zake ngumu miguuni.

Carlos alitangulia kuingia ndani huku akimkaribisha Kisu ambaye alipoingia tu akamkuta Jacky akiwa amesimama kwenye mlango uliokuwa ukielekea kwenye jiko, akiwa bado amevaa nguo yake nyepesi ya pinki ya kulalia iliyolichora vizuri umbo lake na kuionesha nguo yake ya ndani.

Endelea...

Macho ya Kisu yalikuwa yakimtazama Jacky kiwiziwizi huku akizuga kuzungusha macho yake kustaajabia ukubwa wa ile sebule. Carlos aling’amua na kumtazama Jacky, akagundua kuwa kilichombabaisha Kisu ni lile vazi jepesi la Jacky lililokuwa likionesha umbo lake zuri.

Carlos akageuza shingo kumtazama Kisu kwa makini na mara akakiona kisu kikiwa ndani ya ala yake kilichotuna kiunoni kwake.

Carlos akajikuta akisisimkwa mwili wake huku damu ikianza kumchemka na kukimbia kwenye mishipa yake ya damu, hasa alipokumbuka ujuzi aliokuwa nao Kisu katika kutumia kisu kama silaha.

Akakumbuka siku moja alimshuhudia Kisu akionesha uwezo wake wa kutumia kisu pale alipochukua kisu na kukirusha kwenye picha yake ndogo ya ukubwa wa pasipoti aliyoibandika kwenye mlango wa pembeni wa kabati kwenye ghetto lake enzi hizo walipokutana jijini Nairobi.

“Naitoboa hiyo picha kichwani,” Kisu alisema kama utani bila kumtazama Carlos. Kufumba na kufumbua Carlos alisikia sauti ya kitu kikipenya ubaoni kwa kishindo. Alipoangalia kwa makini pale kwenye kabati akakiona kile kisu kikiwa kimezama katikati ya kifua juu ya ile picha ndogo ya pasipoti.

Carlos alitokwa na yowe dogo la mshangao. Hata hivyo, Kisu hakuonesha kufurahishwa, akasonya kwa hasira.

“Nini tena?” Carlos alimuuliza kwa mshangao.

“Nahitaji kufanya mazoezi,” nahitaji kufanya mazoezi.

“Mazoezi ya nini? Si umesema unailenga picha na kweli umefanikiwa?”

“Nilitaka kichwani, siyo kifuani. Nadhani nilichelewa kukiachia kisu mapema,” Kisu alisema huku akishusha pumzi.

“Lakini naamini hilo ni kosa dogo tu?”

“Kosa kubwa sana,” Kisu alisema na kwenda kukichomoa kile kisu, kisha alikichoma, akakirusha juu, akakidaka kwa mkono wa kushoto na kwa kasi ya umeme akakirusha tena akikipeperushia kabatini.

Carlos alichelewa nukta moja tu kugeuka na kukiona kilipokuwa kikizama katikati ya paji la uso wa ile picha. Carlos akapiga makofi huku akiachia mdomo wake wazi…

“Mbona mpo wima?” sauti ya Jacky ikamgutusha Carlos kutoka kwenye yale mawazo, akaachia tabasamu huku akimkazia macho Kisu.

“Kaa tafadhali,” Carlos alimwambia Kisu. Wote walikaa juu ya sofa maridhawa, Carlos akikaa sofa la pembeni na kushusha pumzi ndefu za kichovu huku akijiegemeza.

Macho ya Kisu yalianza kutalii tena mle ndani. Aliona kila kitu cha kifahari kilichotakiwa kuwepo ndani ya nyumba ya mtu mwenye fedha nyingi, kilikuwepo. Kuanzia samani nzuri hadi kumiliki demu mkali kama Jacky! Kisu alionekana kupatamani sana nyumbani kwa Carlos na kuisikitikia nafsi yake.

Alisikitika kwa kuwa kuna wakati alipata fedha nyingi mno kuliko alizokuwa nazo Carlos lakini akayachezea masiha, na sasa alikuwa anarudi tena kupewa kazi na Carlos ili apate fedha, jambo ambalo kama angekuwa makini na matumizi yake, pengine yeyé ndiye angemuajiri Carlos kumfanyia kazi zake.

Aliiangalia ile sebule kwa makini huku akivuta mizani ya kimawazo na kuiweka sebule yake upande mmoja na hiyo ya Carlos upande wa pili. Hapo ndipo alipoliona kwa dhahiri pengo kati ya aliyeamua kuwekeza kwenye mali na aliyewekeza kwenye starehe, kama yeye.

“Kwa nyumba hii na demu mkali kama huyo hata kama ni mgonjwa, akikaa hapa sebuleni ugonjwa ungeaga wenyewe,” Kisu aliwaza na kujikuta akiachia tabasamu.

Vitu vyote vilivyokuwemo pale sebuleni viliashiria kuleta ndani hewa mwanana yenye kutuliza hisia, huku muziki laini ukisikika kwa mbali. Muda wote wakati Kisu akistaajabia uzuri wa ile sebule Carlos na Jacky walikuwa kimya wakimtazama kwa makini.

“Shukrani kwa hao walioweza kuyageuza mawazo yao kuwa vitu halisi,” alijikuta akiwaza tena kisha akayahamisha macho yake na kumtazama Carlos.

“Carlos, mbona jumba kubwa sana namna hii, kwani humu ndani mnaishi watu wangapi?” swali la ghafla lilimtoka Kisu maana hakuweza kujizuia.

“Kwa nini? Tunaishi wawili tu, mimi na bibie hapo,” Carlos alijibu huku akigeuza shingo yake kumuonesha Kisu aliposimama Jacky.

“Wawili tu!” Kisu alionesha kushangaa huku akiendelea kupepesa macho mle ndani, sauti yake ilibeba mshangao.

“Kwani hujawahi kufika hapa?” Jacky akamuuliza Kisu huku akimtazama kwa makini.

“Ndiyo kwanza leo anafika, ila yupo makini sana, ni jana usiku ndiyo nimemuelekeza kwa simu na leo asubuhi kagonga getini,” Carlos akasema huku akimtazama Jacky kisha kama aliyekumbuka jambo akampiga ukope akimwonesha kwa ishara kwa Kisu.

By the way, huyu ni rafiki yangu wa kitambo sana tangu kipindi kile naanza biashara ya madini kule Mirerani, anaitwa Kisu, hapa katikati tulipoteana sana, jana usiku ndo nikakumbuka nikampigia simu aje kwa ajili ya ile ishu,” alisema Carlos.

“Ooh karibu sana, bwana Kisu,” Jacky alimkaribisha yule mwanamume huku akiachia tabasamu pana.

“Asante, lakini naona kama utambulisho wenyewe wa upande mmoja tu,” Kisu aliitikia huku akimtazama Jacky kwa macho ya matamanio.

“Huyu ni mke wangu, anaitwa Jacky, nilimuoa mwaka juzi jijini Arusha,” Carlos alisema.

“Okay, nashukuru kukufahamu shem,” Kisu alisema huku akijiweka vizuri pale kwenye sofa.

“Hata mimi nashukuru kukufahamu,” Jacky alisema huku akiachia tabasamu. Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya huku Kisu akiwa anatafakari.

“Sasa mkuu, nimeitika wito wako, nipe michongo,” hatimaye Kisu alivunja ule ukimya akimwambia Carlos kwa sauti nzito na tulivu huku akiendelea kumtupia jicho la wizi Jacky akionesha kumtamani. Alifanya vile akiwa hataki Carlos ashtukie, hivyo akayahamishia macho yake kwa Carlos. Muda ule ule Jacky aliondoka akaelekea jikoni huku akiwaacha wanamume wawili pale sebuleni.

“Sijui utakunywa nini, chai, kahawa, bia au…” aliuliza Carlos.

“Shusha mzinga wa whisky hapa twende sawa,” alijibu Kisu.

Carlos aliinuka na kwenda kwenye kaunta ndogo ya baa katika jengo lile kisha alifungua kabati kubwa la vioo la ukutani na kutoa chupa kubwa ya whisky na bilauri moja na kuviweka juu ya meza.

Kwa kitambo fulani kulizuka ukimya, Carlos alikuwa akimtazama Kisu kwa makini wakati akijimiminia pombe kwenye bilauri na kugida kwa pupa huku akisisimkwa mwili.

Aliendelea kunywa ile pombe kwa kitambo kirefu akiwa kimya hadi alipoanza kuchangamka zaidi, ndipo Carlos akaamua kuvunja ukimya.

“Sasa, ni kama nilivyokudokeza jana usiku, huenda wiki hii tutakuwa na kazi moja nzito…” Carlos alisema na kuongeza.

Itaendelea...
 
Wakuu, nawashukuru sana wote mlioguswa, kuniombea au kunitakia heri nipone haraka, sijaweza kuzisoma posti zenu zilizomo humu (nadhani nitazisoma taratibu nikipata muda), ila naamini wengi wenu mmeguswa. Bado sijaanza kwenda kazini lakini siwezi kuendelea kukaa nje ya jukwaa hili, acha tuendelee mdogo mdogo na simulizi yetu ya Kizungumkuti, kwani hata tatizo lililonipata (naamini kabisa) limekuwa kizungumkuti kama ilivyo stori hii...

Cc Shunie the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
Mungu ni mwema, inshallah akufanyie wepesi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom