JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,462
Steve Nyerere anazungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Machi 22, 2022
“Nawashukuru wasanii wenzangu na Watanzania wote kwa mchakato ambao ulikuwa unaendelea na bado utaendelea.
“Muungano na ushirikiano wetu ndiyo utatutoa na kutufikisha mbali, kama tukishikamana tukatoa mioyo yetu chuki tutapiga hatua mbele…
"Mwaka 1992 wakati mwalimu Nyerere aliporuhusu upigwaji kura wa taifa kuingia kwenye vyama vingi au kubaki na mfumo mmoja, baada ya kura wale waliopiga kura asilimia 20 ndiyo waliopewa nafasi kwa kuwa aliona mbali.
"Sijawahi kwenda kuomba kazi Shirikisho, Bodi na uongozi na Rais ndiyo walikuwa wakinifuatilia na wao ndiyo walioniambia mimi, nikakataa kwa kuwa nimeishi maisha ya muziki na sinema ninajua.
"Walinifuata mara mbili nikakataa, ya tatu walimtumia rafiki yangu ambaye wanajua aniweza, ndipo nikakubali lakini mkumbuke sikuomba kazi.
"Kazi ya usemaji ni kutumwa siendi kuzungumza ya kwangu, kazi yangu ni kupewa na kuboresha kidogo kisha ndiyo nayazungumza, pia mkumbuke kazi hii haina mshahara.
"Shirikisho hili siyo jambo la kitoto, kuna matatizo mengi, mfano Muziki wa Dansi kuna matatizo mengi. Bongo Fleva ilipata bahati, Rais Kikwete aliwahi kusema anaupenda muziki huo, sasa hivi Taarab imepata bahati Rais Samia anapenda Taarabu, lakini Taarabu yenyewe iko wapi?
"Yaliyoongelewa jana ni maoni, maoni yanapokelewa. Nilimshangaa Mbunge yule, cha kwanza alichotakiwa ni kuwaunganisha watu siyo kuwagawa watu.
"Mbunge anazungumza kugawa watu 'Hatumtaki huyu, kama huyo wanamtaka Dansi wamchukue wao'. Huyo mbunge hatufai.
"Wabunge wa Darasa la Sba ndiyo wanaofanya vizuri kuliko wewe msomi, usisahau ulipotoka, mshindi wa sita ndiyo unakuja kuliongoza Jimbo, hatutaki ubunge wa vimemo, hii ni awamu ya sita.
"Binadamu akisahau unatakiwa kumkumbusha, yeye aliwahi kusema yeye ni 'Mtoto wa baba, mama hamjui'.
"Ukiangalia wale wote wanaonipinga mfano Nay wa Mitego ni Chadema, yule mwingine ni ACT, yule mwingine ni CUF unadhani watanikubali, sikutaka kuingiza uchama.
"Kikao kilichofanyika jana kimevunja katiba, Shirikisho wanachama wake ni vyama siyo watu wanamuziki binafsi, walivyokuwa wakiongea walikuwa wakijifurahisha tu.
"Sisi wengine ilikuwa ni kwa ajili ya kuhamasisha. Walitakiwa wapeleke malalamiko yao kwenye vyama vyao, na je ni wanachama? Siyo kwa kuwa ni mwanamuziki basi unakenua domo.
"Nikiwauliza hapa CEO wa Simba amecheza mpira? Waziri Ummy Mwalimu ni Dokta? Ritha Poulsen ni msanii?
"Mimi niliamini kikao kile kama kimeongozana na mtu ambaye ana nguvu, maana yeye ni Mbunge na katika Jimbo lake kuna wasanii wa Taarab, Dansi.
"Mimi siwezi kung'oka kwa saa 48, siwezi kung'oka kihunihuni. Masaa 48 ya nini?
"Tuna matatizo mengi, mfano bima za afya, studio, mirabaha... vitu kama hivyo ndivyo vya kukaa na kuzungumza.
"Nazungumza kama Msemaji wa Shirikisho Tanzania, hatoki mtu hapa, napongeza BASATA kwa kuandaa tuzo, tulitakiwa tukae tujiulize vitu kama tuzo tuwashirikishe Wazanzibar, siyo mambo kama yake, poor kabisa.
"Nilitegemea nguli kama wale waniite waniulize mipango yangu.
"Nitajiuzulu kama Mwenyekiti, Bodi na uongozi wataniita kama walivyonifuata na kuniambia kuhusu hilo. Jana nilipata misukosuko kutoka kwa watu wangu wa karibu kuhusu hili.
"Nimewaambia ndugu zangu kuwa SITOKI, tukianza kuulizana hapa nasi tutaanza kuuliza alishinda?
"Niwaombe radhi wanamuziki wa Dansi, jana walidhalilishwa sana, watu wanajiona wenyewe ndiyo wenyewe, wakati wengine mmewapokea nyinyi
"Wamekosa nidhamu ya kukaa chini na kuzungumza, wakati nyie mliwapokea na wengine wakiomba watumbuize jukwaani.
"Unamuita Katibu wako Rasta, huu ni ukosefu wa nidhamu.
"Nampa masaa 48 awaombe radhi Bongo Fleva, amuombe radhi kiongozi aliyemuita Zumaridi, amuombe radhi Steve Ake, Aombe radhi kwa Taarabu na aombe radhi kwa Shirikisho la Muziki. Nitashangaa uongozi wa Shirikisho kama hawatachukua hatua.
"Kama wangekuwa wanashiriki katika vikao, mimi nisingekuwa Msemaji, wao ndiyo wangekuwa wasemaji, lakini hawashiriki vikao.
"Ubunge una mwisho, muda wa vikaratasi 'namtaka huyo' umepita.
"Sijaanza kazi wanapuyanga, je nikianza kazi? Hata ofisi sijakabidhiwa na sijui iko wapi.
"Muda ukifika nitaondoka, nipo tayari kujiuzulu lakini siyo kwa kuondoka na watu, nataka niwaache wakiwa na umoja.
"Kama mwanashirikisho una hoja ya msingi nenda kwenye chama chako ukatoe maoni yatafanyiwa kazi. Namalizia kwa kusema nampa Mbunge saa 48 aombe radhi kwa kauli zake, NIMEMALIZA SIHITAJI MASWALI."
“Nawashukuru wasanii wenzangu na Watanzania wote kwa mchakato ambao ulikuwa unaendelea na bado utaendelea.
“Muungano na ushirikiano wetu ndiyo utatutoa na kutufikisha mbali, kama tukishikamana tukatoa mioyo yetu chuki tutapiga hatua mbele…
"Mwaka 1992 wakati mwalimu Nyerere aliporuhusu upigwaji kura wa taifa kuingia kwenye vyama vingi au kubaki na mfumo mmoja, baada ya kura wale waliopiga kura asilimia 20 ndiyo waliopewa nafasi kwa kuwa aliona mbali.
"Sijawahi kwenda kuomba kazi Shirikisho, Bodi na uongozi na Rais ndiyo walikuwa wakinifuatilia na wao ndiyo walioniambia mimi, nikakataa kwa kuwa nimeishi maisha ya muziki na sinema ninajua.
"Walinifuata mara mbili nikakataa, ya tatu walimtumia rafiki yangu ambaye wanajua aniweza, ndipo nikakubali lakini mkumbuke sikuomba kazi.
"Kazi ya usemaji ni kutumwa siendi kuzungumza ya kwangu, kazi yangu ni kupewa na kuboresha kidogo kisha ndiyo nayazungumza, pia mkumbuke kazi hii haina mshahara.
"Shirikisho hili siyo jambo la kitoto, kuna matatizo mengi, mfano Muziki wa Dansi kuna matatizo mengi. Bongo Fleva ilipata bahati, Rais Kikwete aliwahi kusema anaupenda muziki huo, sasa hivi Taarab imepata bahati Rais Samia anapenda Taarabu, lakini Taarabu yenyewe iko wapi?
"Yaliyoongelewa jana ni maoni, maoni yanapokelewa. Nilimshangaa Mbunge yule, cha kwanza alichotakiwa ni kuwaunganisha watu siyo kuwagawa watu.
"Mbunge anazungumza kugawa watu 'Hatumtaki huyu, kama huyo wanamtaka Dansi wamchukue wao'. Huyo mbunge hatufai.
"Wabunge wa Darasa la Sba ndiyo wanaofanya vizuri kuliko wewe msomi, usisahau ulipotoka, mshindi wa sita ndiyo unakuja kuliongoza Jimbo, hatutaki ubunge wa vimemo, hii ni awamu ya sita.
"Binadamu akisahau unatakiwa kumkumbusha, yeye aliwahi kusema yeye ni 'Mtoto wa baba, mama hamjui'.
"Ukiangalia wale wote wanaonipinga mfano Nay wa Mitego ni Chadema, yule mwingine ni ACT, yule mwingine ni CUF unadhani watanikubali, sikutaka kuingiza uchama.
"Kikao kilichofanyika jana kimevunja katiba, Shirikisho wanachama wake ni vyama siyo watu wanamuziki binafsi, walivyokuwa wakiongea walikuwa wakijifurahisha tu.
"Sisi wengine ilikuwa ni kwa ajili ya kuhamasisha. Walitakiwa wapeleke malalamiko yao kwenye vyama vyao, na je ni wanachama? Siyo kwa kuwa ni mwanamuziki basi unakenua domo.
"Nikiwauliza hapa CEO wa Simba amecheza mpira? Waziri Ummy Mwalimu ni Dokta? Ritha Poulsen ni msanii?
"Mimi niliamini kikao kile kama kimeongozana na mtu ambaye ana nguvu, maana yeye ni Mbunge na katika Jimbo lake kuna wasanii wa Taarab, Dansi.
"Mimi siwezi kung'oka kwa saa 48, siwezi kung'oka kihunihuni. Masaa 48 ya nini?
"Tuna matatizo mengi, mfano bima za afya, studio, mirabaha... vitu kama hivyo ndivyo vya kukaa na kuzungumza.
"Nazungumza kama Msemaji wa Shirikisho Tanzania, hatoki mtu hapa, napongeza BASATA kwa kuandaa tuzo, tulitakiwa tukae tujiulize vitu kama tuzo tuwashirikishe Wazanzibar, siyo mambo kama yake, poor kabisa.
"Nilitegemea nguli kama wale waniite waniulize mipango yangu.
"Nitajiuzulu kama Mwenyekiti, Bodi na uongozi wataniita kama walivyonifuata na kuniambia kuhusu hilo. Jana nilipata misukosuko kutoka kwa watu wangu wa karibu kuhusu hili.
"Nimewaambia ndugu zangu kuwa SITOKI, tukianza kuulizana hapa nasi tutaanza kuuliza alishinda?
"Niwaombe radhi wanamuziki wa Dansi, jana walidhalilishwa sana, watu wanajiona wenyewe ndiyo wenyewe, wakati wengine mmewapokea nyinyi
"Wamekosa nidhamu ya kukaa chini na kuzungumza, wakati nyie mliwapokea na wengine wakiomba watumbuize jukwaani.
"Unamuita Katibu wako Rasta, huu ni ukosefu wa nidhamu.
"Nampa masaa 48 awaombe radhi Bongo Fleva, amuombe radhi kiongozi aliyemuita Zumaridi, amuombe radhi Steve Ake, Aombe radhi kwa Taarabu na aombe radhi kwa Shirikisho la Muziki. Nitashangaa uongozi wa Shirikisho kama hawatachukua hatua.
"Kama wangekuwa wanashiriki katika vikao, mimi nisingekuwa Msemaji, wao ndiyo wangekuwa wasemaji, lakini hawashiriki vikao.
"Ubunge una mwisho, muda wa vikaratasi 'namtaka huyo' umepita.
"Sijaanza kazi wanapuyanga, je nikianza kazi? Hata ofisi sijakabidhiwa na sijui iko wapi.
"Muda ukifika nitaondoka, nipo tayari kujiuzulu lakini siyo kwa kuondoka na watu, nataka niwaache wakiwa na umoja.
"Kama mwanashirikisho una hoja ya msingi nenda kwenye chama chako ukatoe maoni yatafanyiwa kazi. Namalizia kwa kusema nampa Mbunge saa 48 aombe radhi kwa kauli zake, NIMEMALIZA SIHITAJI MASWALI."