Star TV na ITV kujitoa rasmi Startimes muda si mrefu!

Star TV na ITV kujitoa rasmi Startimes muda si mrefu!

kwa mazingira hayo wadanganyika itabidi wanunue vidubuasha vingine hii ni kuwaonea na wizi mtupu tume inabidi warejeshe fedha za wadanganyika kwa usumbufu inaowapa kwa kuanza kazi bila mipango ya maana na kuwaingiza gharama zisizo za msingi
mbaya sana
 
Hii ndo bongo bwana,kama kawa kila kitu kinafanywa kiolela tu.nashangaa sana wakubwa waliipigia debe sana hicho ki star times,kuna nini nyuma ya pazia?.
Nafikiri ikitoka star tv na ITV hicho king'amiz akina maana tena.so star times wajipange upya ua kama vp wasepe hapa bongo.
 
star tv wanajtoa kwa7bu ya kupromot king'amuz chao cha continental..
 
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!

Hii lugha ya walaj jaman mpka kwenye ving'amuzi si mngesema tu wateja? Nani anakula king'amuzi tz hii...!?????
 
Watanzania tumekuwa wapole sana, tunaendeshwa kama maroboti. Sijui kama watu wameumia kama nilivyoumia mimi. Ila ukweli ni kwamba Tanzania ni nchi ya ajabu sana, tukisema kuwa wanatukomoa watanzania kwa maslahi yao binafsi tutakuwa tumekosea? Tunahitaji mtu wa kututetea katika hili, wako wapi wamiliki wa vyombo vya habari? wako wapi wanaharakati wa haki za binadamu, wakati haki ya kupata habari inavunjwa? Kwanini tusidai haki hii kwa lazima mbele ya watawala?
 
. Sheria ya TCRA ndio inatakiwa ionekane ina nguvu hapa. Kila decoder itakayouzwa Tanzania inatakiwa lazima iwe inaonyesha local chanels zote bila malipo ya mwezi,na ndio ilikuwa ahadi yao wakati wanatulazimisha kuingia digital!. Sasa naona kama madudu yanaanza. Kila mwenye Tv station anaongea na wachina wanamtengenezea decoder yake anauza mitaani hata kama inarusha channel mbili tu. . Ina maana mtu atatakiwa kununua decoder zaidi ya kumi ili kuweza kuona local channel tu!. This is absurd! TCRA mkilala kwa hili mtakuwa hamuwatendei haki walaji/watazamaji na mtaleta confusion kubwa.
Maelezo yako nimeyakubali sana ,sina cha kuongezea
 
Nchi hii kila mtu anayo mamlaka ya kutunga sheria yake,kama sheria ya TCRA ilizitaja channel hizo zitakuwa free kwa vingamuzi vyote,iweje leo wanajitoa bila hata kusikia tamko la serikali?
 
Mambo ya ajabu sana.hili jambo walikurupuka sana.nimepata taarifa na ITV wanataka kujiondoa huko star times
 
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!
Mbona unasema stori za vijiweni wakati sisi tunaona tangazo (banner) likipita kwenye screen kuwa star times wanatuarifu startv imejitoa katika orodha za chaneli zao.
 
katika hal ya kawaida kinachoonekana hapa serikali imeshindwa kuingilia hili maana kila kituo cha tv sashv wana vingamuz vyao so atomatically lazima kila mmoja avutie kwake ili aweze pata wateja zaidi sas swali je kusipokuwa na mwingiliano na makubaliano ya tv tofauti si ndo pakuwa na vingamuz hadi vitano maana kama itv wakitoka star tv tayari,si ajabu hata tbc wakagoma kuingia kwenye vingamuz vya continental au hvyo vitakavyo kuja vya itv
 
mmmmh mbona kuna free chanel nyingi tu hazimo kwenye visumbuz hvyo,capital hawajaingia startime,ila eg zuku ndo kabis yaan kule kuna 10 na tbc tu wakati local zingine nying tu
 
Tunajua star tv wana ving'amuzi vyao! Lakini kwa nini waondoke statimes, na je mkataba walioingia kati ya startimes na serikali kuhakikisha tv 5 zinaonekana bure utakuwaje? Tv 5 ambazo zilipaswa kuonyeshwa bure hata kama mteja hajalipa ni hizi ITV, STAR TV,EATV,TBC1 NA CHANEL TENI, LAKINI TUNAONA SIKU HIZI CLOUDS TV NAYO IKO FREE KWA NINI STAR TV IONDOLEWE?

mambo mangapi yapo kwenye mikataba na bado hayatekelezwi?kwenye bajeti walikuwa wanabwabwaje local channels tano leo yako wapi?star haipo
 
Hao wanaojidai TCRA wapo wapi?????MAANA hata TBC1 haipatikani kwenye ungo kwa wiki ya nne sasa na hakuna king'amuzi kinachoshika..but me nipo wilaya ya rombo sijui huko mlipo wandugu kama tbc1 mnaipata kwa kutumia ungo
TCRA ni active member humu, nashangaa mpaka sahivi hawatoi majibu kuhusu hili jambo.
 
Last edited by a moderator:
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!

Za uongo haya isearch uangalie kama utaipata,maskini Tanzania yetu sijui itakuja kuwa na ving'amuzi vingapi.Naona nyumba yangu ntaweka ving'amuzi mpaka paa lidondoke mwaka huu
 
Mchakato ukikamilika watatualifu vizuri.
mchakato ukikamilika ata mwakan 2we 2nasubiri 2 sio.
hatuendi ivo kinachotakiwa ni tcra kusema kama kuna hitilafu za kiufundi au ni kwel kuna tv zitajitoa na sio 2subiiiiiiiiiri 2
 
Wapeni mda tu watarud hao! Wenyewe kama wanategemea DSTV kurusha matangazo yao imekula kwao.
Meneja masoko wao hajawashauri vizuri.
Na ITV hawawez kuwa wajinga kias hicho mana wanaakili nzur ya biashata na ndo mana wako juu ckuzote.
Wakawaulize clouds watawaelezea vizuri.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Naunga mkono asilimia mia moja coz hizo chanel ni free to air so once king'amuzi kikiisha vocha chanel zote zinakatika ina maana wao star times wanaangalia fedha zaidi kuliko makusudio ya chanel hizo,hii ni kwa watu wa mikoani sifahamu kwa dar ikoje
 
Back
Top Bottom