Stand zote wapewe Tanroads au Bus Terminals Authority (BUTA)

Tabutupu

JF-Expert Member
Nov 26, 2010
13,111
18,327
Serikali imewekeza fedha nyingi sana kutoa huduma bora kwa wananchi hasa kwenye secta ya usafiri..

Ila Halmashauri ambazo zimepewa jukumu la kuzisimamia stand za mabasi zimekua zikichukua fedha na kuziacha stand zikiwa chafu hadi zinahatarisha maisha ya wananchi.

Madharani stand ya Dodoma ambayo ni moja ya stand za gharama kubwa Africa, ukipita sasa viti vimevunjika, vyoo vichafu, maeneo ya nje ya ya hovyo, restaurant zote zimevungwa, kimekua kijiwe cha wahuni tuu..

Stand ya Magufuli Mbezi Luis ni hivyo hivyo, wakati ilitakiwa hizi stand ziwe ni maeneo mazuri hata watu kwenda kutembea..

Kwanini Airports hata zile ambazo zinaingiza fedha chache kiliko hizi stand zipo well maintained, zina garden safi, vyoo safi, miti ya vivuli , walking ways safi etc..

Cha pili kwanini stand hizi zina toza fedha abiria wanao safiri wakati airports hazitozi?

Kwani wasiregemee tuu wanao toa huduma?

Tunahitaji serikali iliangalie swala hili maana stand ya bil 55 kuwa kijiwe cha wahuni ni.bora wangejenga hospitali.

Mapendekezo

1. Stand zote zisimamiwe na chambo kimoja.. na fedha zinazopatikana zigawanywe kuhudumia stand na halmashauri husika ..

2. Serikali iunde chombo cha kusimamia stand hizi kama ilivyo kwenye usafiri wa anga. Let say chombo hicho kiitwe BUS TERMIANLS AUTHORITY (BUTA). chombo hiki kitakua na jukumu la kuhakikisha stand zinakua ni sehemu nzuri na salama kwa raia kupata huduma pamoja na kuendeleza na kujenga stand za mabasi nchi nzima.

Kinacho tokea kwenye stand ndicho kinatokea kwenye hospitali zote zinazo simamiwa na halmashauri.. sio kwamba hawana pesa ila pesa zote zinaishia kulipana posho.

Ikiwezekana hospitali zote sisimamiwe na wizara husika pamoja na shule zote zisimamiwe na wizara ya elimu.

Kuna matatizo mengi sana kuachia halmashauri majukumu makubwa.

Mungu ibariki Tanzania na naamini siku moja usafiri wa ardhini utapata msimamizi wa stand za mabasi (BUTA)
Screenshot_20230412-175108_Google.jpg
 
Serikali imewekeza fedha nyingi sana kutoa huduma bora kwa wananchi hasa kwenye secta ya usafiri..

Ila Halmashauri ambazo zimepewa jukumu la kuzisimamia stand za mabasi zimekua zikichukua fedha na kuziacha stand zikiwa chafu hadi zinahatarisha maisha ya wananchi.
Mawazo mazuri sana hapo kwenye shule sisi wadau tunajua kinachoendelea huko mashuleni.. ni upopoma tu.
 
Watanzania tuko na shida Sana kuendeleza kitu cha umma kikawa na mwonekano ule ule na ufanisi changamoto kubwa Sana tazama stand watu wanakusanya tu pesa ila hawakumbuki kufanya marekebisho panapotakiwa, usafi, kuboresha huduma mbalimbali licha ya gharama kubwa zilizotumika kuzijenga hii nayo mpka wawekezaji waje kutufundisha au kuwekeza?​
 
Watanzania tuko na shida Sana kuendeleza kitu cha umma kikawa na mwonekano ule ule na ufanisi changamoto kubwa Sana tazama stand watu wanakusanya tu pesa ila hawakumbuki kufanya marekebisho panapotakiwa, usafi, kuboresha huduma mbalimbali licha ya gharama kubwa zilizotumika kuzijenga hii nayo mpka wawekezaji waje kutufundisha au kuwekeza?​
Cha ajabu kuna waziri anaitwa Waziri wa TAMISEMI
 
Nilipita stendi kuu ya ma-bus katika mkoa wa katavi (Mizengo Pinda) hakika niliyo yaona ndani ya vyoo ni mambo ya aibu na fedhea kubwa sana suala la personal hygiene and good manner hakika sisi waafrika hatuna ustaarabu huo na hii ndio hali ya bus terminals nchi nzima

Nalo hii tutasema mabeberu yanatuhujumu vifaa vya usafi
 
Cha ajabu kuna waziri anaitwa Waziri wa TAMISEMI
Sijui kama niko sahihi kwa maoni yangu hii wizara Jafo aliimudu Sana kipindi kile Kairuki naona kama imekuwa nzito Sana kwake ukizingatia ilivyo kubwa na mambo mengi inahitaji mtu kweli asiyechoka anayekimbia huku na kule kuhakikisha mambo yanaenda
 
Nilipita stendi kuu ya ma-bus katika mkoa wa katavi (Mizengo Pinda) hakika niliyo yaona ndani ya vyoo ni mambo ya aibu na fedhea kubwa sana suala la personal hygiene and good manner hakika sisi waafrika hatuna ustaarabu huo na hii ndio hali ya bus terminals nchi nzima

Nalo hii tutasema mabeberu yanatuhujumu vifaa vya usafi
Masuala ya usafi Afrika tuko na shida kubwa kuliko abiria anajisaidia hata kuacha sehemu safi kama alivyoikuta hajali bora kamaliza haja zake anakimbia ustaarabu tatizo
 
Nilipita stendi kuu ya ma-bus katika mkoa wa katavi (Mizengo Pinda) hakika niliyo yaona ndani ya vyoo ni mambo ya aibu na fedhea kubwa sana suala la personal hygiene and good manner hakika sisi waafrika hatuna ustaarabu huo na hii ndio hali ya bus terminals nchi nzima

Nalo hii tutasema mabeberu yanatuhujumu vifaa vya usafi
Ile stand bora wangejenga hospitali, tuendelee kuchimba dawa kwenye vichaka
 
Yaani wamewekewa vitu vizuri tena viwango wao na ustaarabu wao wanaenda kuharibu, kuchafua, kuiba tuna safari ndefu Sana
Mkurugenzi anakusanya mapato lakini harudishi kutoa huduma kwa wanao lipa
 
Sijui kama niko sahihi kwa maoni yangu hii wizara Jafo aliimudu Sana kipindi kile Kairuki naona kama imekuwa nzito Sana kwake ukizingatia ilivyo kubwa na mambo mengi inahitaji mtu kweli asiyechoka anayekimbia huku na kule kuhakikisha mambo yanaenda
Huyu mama naona analemewa ila pia shule na hospitali ziobdolewe TAMISEMI.. TAMISEMI ibakie na vyoo vya stand na masoko
 
Serikali imewekeza fedha nyingi sana kutoa huduma bora kwa wananchi hasa kwenye secta ya usafiri..

Ila Halmashauri ambazo zimepewa jukumu la kuzisimamia stand za mabasi zimekua zikichukua fedha na kuziacha stand zikiwa chafu hadi zinahatarisha maisha ya wananchi.

Madharani stand ya Dodoma ambayo ni moja ya stand za gharama kubwa Africa, ukipita sasa viti vimevunjika, vyoo vichafu, maeneo ya nje ya ya hovyo, restaurant zote zimevungwa, kimekua kijiwe cha wahuni tuu..

Stand ya Magufuli Mbezi Luis ni hivyo hivyo, wakati ilitakiwa hizi stand ziwe ni maeneo mazuri hata watu kwenda kutembea..

Kwanini Airports hata zile ambazo zinaingiza fedha chache kiliko hizi stand zipo well maintained, zina garden safi, vyoo safi, miti ya vivuli , walking ways safi etc..

Cha pili kwanini stand hizi zina toza fedha abiria wanao safiri wakati airports hazitozi?

Kwani wasiregemee tuu wanao toa huduma?

Tunahitaji serikali iliangalie swala hili maana stand ya bil 55 kuwa kijiwe cha wahuni ni.bora wangejenga hospitali.

Mapendekezo

1. Stand zote zisimamiwe na chambo kimoja.. na fedha zinazopatikana zigawanywe kuhudumia stand na halmashauri husika ..

2. Serikali iunde chombo cha kusimamia stand hizi kama ilivyo kwenye usafiri wa anga. Let say chombo hicho kiitwe BUS TERMIANLS AUTHORITY (BUTA). chombo hiki kitakua na jukumu la kuhakikisha stand zinakua ni sehemu nzuri na salama kwa raia kupata huduma pamoja na kuendeleza na kujenga stand za mabasi nchi nzima.

Kinacho tokea kwenye stand ndicho kinatokea kwenye hospitali zote zinazo simamiwa na halmashauri.. sio kwamba hawana pesa ila pesa zote zinaishia kulipana posho.

Ikiwezekana hospitali zote sisimamiwe na wizara husika pamoja na shule zote zisimamiwe na wizara ya elimu.

Kuna matatizo mengi sana kuachia halmashauri majukumu makubwa.

Mungu ibariki Tanzania na naamini siku moja usafiri wa ardhini utapata msimamizi wa stand za mabasi (BUTA)
View attachment 2600039
Kwanza nakushangaa sana kusema stand ni chanzo cha fedha.

Stand za bus (bus terminals) hazipaswi kutoza fedha kwa wasafiri hata kidogo maana ule ni uwekezaji wa umma. Ni pesa za umma kama kujenga barabara, shule etc. Wanaopaswa kulipia ni wapangaji kwa maana wanaofanya biashara kwenye eneo la stand na bus operators.

Kumtoza msafiri gharama za kuingia au kutoka stand ni unyonyaji kwa wananchi. Na ni Tanzania pekee.

Swali: kwa nini airport ambapo gharama za ujenzi ni kubwa kuliko stand wasafiri au wasindikizaji hawatozwi kingilio?
 
Back
Top Bottom