Inaendelea
2.Kukosekana kwa wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali kama vile Maprofesa(Professors), Madaktari(Doctors), Wakufunzi waandamizi(senior lecturers) kwenye vitivo vya UALIMU,CSE,EEE,CIVIL,ECE,MECHANICAL kulingana na sheria za vyuo vikuu, mapungufu haya yanapelekea kukiukwa kwa sheria za nchi na kupelekea kukosekana kwa ubora wa elimu inayotolewa katika chuo hiki na kutokidhi mahitaji ya kitaifa na kimataifa, wanafunzi wanasikitishwa na mwenendo wa chombo chenye dhamana ya kusimamia Elimu ya juu katika nchi yetu kwa kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa kipindi kirefu jambo lililopelekea wanafunzi kukosa imani na serikali yao na kukatishwa tamaa ya kuendelea na masomo katika chuo hiki.
3. Uwepo wa wakufunzi wasiokuwa na sifa stahiki na uzoefu katika kufundisha masomo ya Elimu ya juu.Wakufunzi wasiokuwa na sifa stahiki huletwa kwa wingi kutokea nchini India, na wengine huajiriwa kwa sababu ya kuwa na undugu/familia na baadhi ya viongozi wajuu wa chuo hiki. Jambo hili ni kinyume na sheria za ajira Tanzania kwa uongozi kushindwa kutoa fursa sawa za ajira kwa wazawa na wageni pia kwa kuajiri zaidi ya asilimia 80 ya watumishi wa chuo hiki ni wageni na sio wazawa jambo ambalo ni kinyume na sheria na taratibu za ajira kwasababu ajira zinazofanywa na wageni zinaweza kufanywa na wazawa, ushahidi wa kutokidhi sifa za ukufunzi upo kwa baadhi ya wakufunzi kukosa sifa za kitaaluma ambazo wanapaswa kuwa nazo ili kutimiza majukumu katika ngazi mbali mbali za vitivo mfano mkuu wa idara ya shahada ya Uhandisi wa Umeme akiwa na sifa ya mkufunzi msaidizi (assistant lecturer).
4. Kuwa na maabara zenye vifaa duni (chakavu), zisizokidhi ubora na mahitaji ya fani mbali mbali zifundishwazo chuoni, kwa mfano kozi ya uhandisi wa mekanika kukosa maabara muhimu katika masomo yao na kozi nyingine za ualimu na uhandisi kuwa na maabara zisizo na vifaa, wataalam na zisizokidhi ubora wa kitaifa na kimataifa.Upungufu huu unapelekea taifa kuzalisha wataalamu na walimu wasio na ujuzi wa kutosha katika fani husika jambo ambalo ni hatari kwa ajira zao na ustawi mzima wa taifa.
5. Maktaba isiyokidhi viwango vya ubora wa kutoa huduma kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu. Hili linatokana na kukosekana kwa vitabu muhimu na vya kutosha na kukosekana kwa miundombinu rafiki kulingana na idadi ya wanafunzi wa fani zote, hili linadhoofisha ufanisi wa shughuli za kitaaluma kwani masomo ya Elimu ya juu yanamuhitaji mwanafunzi kujisomea na kufanya tafiti mbalimbali katika fani husika na hivyo kuwafanya