Spika Sitta Kung'olewa?

Spika Sitta Kung'olewa?

Kumbe ubabe wa 6 unawakera wote wapinzani na wapingwaji? Juzi juzi hapa alimnyanyasa sana bwana Mapesa pale mjengoni, na watu walisikitika sana, especially wale wa upinzani. Sasa kama hata sisiem wanamuita mbabe, basi jamaa atajikuta yuko peke yake !!
 
Kumbe ubabe wa 6 unawakera wote wapinzani na wapingwaji? Juzi juzi hapa alimnyanyasa sana bwana Mapesa pale mjengoni, na watu walisikitika sana, especially wale wa upinzani. Sasa kama hata sisiem wanamuita mbabe, basi jamaa atajikuta yuko peke yake !!
mimi namuona anafanya kazi yake vizuri, unajua siku hizi ukifanya kazi kwa uadilifu wewe ndio unakuwa mbaya...
 
Heshima Mkuu,
Jamaa wako very serious maana kuna waraka unaosambazwa mtandaoni ukidaiwa kuwa watoka kwa wafanyakazi wa ofisi za bunge ukiwa na tuhuma kibao dhidi ya spika 6, wanadai anataka kuipiga moto ofisi ya uhasibu ili kupoteza ushaidi wa matumizi mabaya pesa ya walipa kodi.

tusubiri tuone.
 
Mafisadi washika hatamu CCM

Monday, 17 August 2009 16:43
*Aundiwa fitna za kung'olewa

Na John Danieli, Dodoma

Majira


HALI ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imezidi kuwa tata, baada ya kundi linalodaiwa kuwa na mlengo wa 'kubeba' mafisadi, kutaka Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta awajibishwe kwa madai ya kukisumbua chama hicho kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya wazembe serikalini.

Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama hicho (NEC) kinachoendelea hapa, Mjini Dodoma, zilieleza kwamba mara baada ya kuanza jana majira ya saa 12 jioni wajumbe waliopangwa walisimama mmoja mmoja na kueleza kwamba bila CCM kumwondoa kiongozi huyo wa Bunge, mambo ya kisiasa hususani hatima ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao itakuwa mashakani.

Hivyo dawa pekee ni kumwondoa katika nafasi yake ya uspika na kumfukuza uanachama wa CCM hoja ambayo hata hivyo ilipingwa vikali na kundi la wajumbe linalopinga ufisadi, huku wakitaka kabla ya kiongozi huyo kuchukuliwa hatua, watuhumiwa wote wa ufisadi wakamatwe na wafukuzwe uanachama wa CCM kwanza.

"Hawa watu walijipanga wiki mbili zilizopita kabla ya NEC, walifanya vikao vyao, wakatenga mabilioni ya pesa........ (anamtaja mmoja wa wajumbe wa NEC, jina tunalihifadhi kwa sasa), akatumwa kwenda Zanzibar akagawa pesa kwa baadhi ya wajumbe wa NEC kutoka Zanzibar, sasa wamekuja kwenye kikao na ajenda moja tu, nayo ni kutaka kumg'oa Spika Sitta," kilisema chanzo chetu ndani ya NEC na kuongeza.

"Baada ya hapo watawashughulikia wafuasi wake wote wanaopinga ufisadi, lakini tunajua tatizo ni nini, tunatambua uongozi wa huyu spika Sitta umewabana na kuwakosesha amani, lakini tunasubiri uamuzi wa kikao, na mwenyekiti, lakini wakishindwa kuwadhibiti mafisadi hawa tumekwisha," kilisema chanzo hicho.

Habari zaidi zilieleza kwamba kundi hilo linaloaminika kudhaminiwa na watuhumiwa ufisadi ndani ya CCM, linaongozwa na mmoja wa Manaibu Waziri, Mwenyekiti wa CCM Mkoa na Katibu wake pamoja na wajumbe kadhaa kutoka Kanda ya Ziwa pamoja na Zanzibar.

Kutokana na ajenda hiyo kuzua mjadala mkali, jana siku nzima wajumbe wa NEC walishinda wakijadili ajenda moja tu ya hali ya kisiasa nchini huku mafisadi wakionekana kuzidi kujiimarisha zaidi ndani ya CCM

Baada ya mashambulizi kuongezeka zaidi kwa siku nzima dhidi ya Spika Sitta na wafuasi wake wanaopinga ufisadi, ilielezwa kuwa juhudi za baadhi ya wajumbe wanaofurahishwa na kasi ya Spika Sitta zilionekana kutokuzaa matunda hadi jana jioni kutokana na kundi hilo la mafisadi kuonesha dalili toka awali kutaka kuteka kikao cha NEC, kwa hoja zao ambazo kwa nje zilionekana kutaka kudai maslahi ya CCM, lakini kwa ndani zinaonekana kuipeleka CCM kaburini kama ilivyofanyika kwa Chama cha KANU nchini Kenya.

Ilielezwa kuwa licha ya Spika Sitta, kutakiwa kung'olewa kwenye wadhifa wake, pia Spika wa Baraza la Wawakilishi, Bw. Pandu Kificho, naye hakuweza kuepuka dhahama hiyo, baada ya wajumbe kadhaa kutaka naye awajibishwe kwa kung'olewa kwenye wadhifa wake kutokana na Baraza lake kutuhumiwa kumtukana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali kwa ujumla pamoja na Bunge la Muungano.

"HIvyo ndivyo hali ilivyokuwa ndani ya NEC, hata sisi hatukutegemea. Wajumbe walimtaka Kificho naye ang'olewe kwa kuwa Baraza lilimtukana Waziri Mkuu, Serikali ya Jamhuri ya Muungano na hata Bunge. Kama hali itaendelea hivi, ni wazi kwamba CCM inachungulia ilipo KANU kwa sasa, lakini yote hayo bado ni mchango wa wajumbe, tusubiri mamuzi ya kikao leo usiku (jana)," kilisema chanzo chetu ndani ya NEC.

Ilielezwa kwamba chanzo cha Spika Sitta kutaka kutolewa inatokana na itikadi yake kutokuyumba katika masuala mazito yanayohusu ufisadi kama vile Richmond, TRL, TICTS,na kukataliwa kwa mswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali.

Hali hiyo imeelezwa kufanya baadhi ya mawaziri kumchukia kwa kuwa kasi yake inawapa wakati mgumu bungeni. Jumla ya mawaziri 7, wametajwa kuwa wanahusika na kuungana na kundi la mafisadi kutaka kiongozi huyo ang'olewe.

"Bunge chini ya Spika Sitta linajadili maslahi ya watanzania wanaokadiriwa kuwa milioni 40 kwa sasa, anayezungumza kuwa Sitta anawasaliti CCM anajali maslahi ya kundi lake, watoto wake, marafiki zake na ndugu zake. Tunaelkea kufikia ndoto ya Mwalimu Nyerere, kuwa CCM ikiyumba nchi itayumba. NI wazi sasa ufisadsi unayumbisha CCM, kama hatutawang'oa nchi itayumba," alisema mmoja wa wajumbe wa NEC bila kufafanua.

Hadi tunakwenda mitamboni, kikao cha NEC kilikuwa bado kinaendelea japo wajumbe kadhaa walionesha kutoridhika na mwenendo wa kikao hicho.
 
Hawa mafisadi wanatapatapa. Wala kwa sasa hawana uwezo wa kumfanya chochote spika wetu . Tukiite kiama chao ,wasitake kumchanganya JK . walizokula zinatosha , sasa wakae pembeni . Kingunge anajitahidi kuwatetea sana lakini mwisho wa siku itakula kwao.

TO SUFFER IS NOT TO DIE BUT YOU TAKE IT EASY TIME WILL TELL...............................
 
mimi namuona anafanya kazi yake vizuri, unajua siku hizi ukifanya kazi kwa uadilifu wewe ndio unakuwa mbaya...

Niliona mijadala takribani yote ya Bunge. Bwana spika anaonekana kwa kawaida kazi anaijua na muda mrefu anajitahidi kuifanya kama inavyotakiwa.

Kama kawaida ukifanya hivyo inakuwa taaabu kwa Serikali maana Mawaziri wanashindwa kuonyesha wajibu wao maana walizoea kunyenyekewa na kuonekana wako juu ya wabunge wengine. Hujibu wanavyotaka.

Lakini kuna wakati Spika nilimuona akikumbuka CCM inachokitaka na anapokuwa anarudi kwenye mstari huo wa chama tawala, anajikuta akiwa caesar wa Bunge. Akina Cheyo wanaambiwa "sit down!"

Inabidi aamue. Atimize wajibu wake kama spika, au awe spika anayelinda matakwa ya CCM hata kama ni uozo.
 
Hata kama hana uadilifu,alifanikisha vita ya kuwaibua walioshiriki kuingiza richmond kinyemela.Pia msimamo wake bungeni kwa siku za hivi karibuni unasaidia katika mapambano yetu dhidi ya ufisadi na hicho ndicho kinachoikera CCM.

Hata kama hamumpendi SITTA basi yapendeni hata mazuri yake tu.
 
Hawa mafisadi wanatapatapa. Wala kwa sasa hawana uwezo wa kumfanya chochote spika wetu . Tukiite kiama chao ,wasitake kumchanganya JK . walizokula zinatosha , sasa wakae pembeni . Kingunge anajitahidi kuwatetea sana lakini mwisho wa siku itakula kwao.

TO SUFFER IS NOT TO DIE BUT YOU TAKE IT EASY TIME WILL TELL...............................


Jeremiah unataka kusema katika hao mafisadi Kikwete hayumo?
 
Kind of news that excites Tanzanian for years now!
 
Ndungu wana jf,

mwenye data atupe full report ya mchezo ulivyochezwa ndani ya cc na nec.


Mp
 
Dah mafisadiso wanakazi kweli kweli kinacho niuma mimi yanakubalika sana kwa wananchi sijui yanatumia uchawi?

Hawa jamaa hawana lolote; uchawi wao ni pesa wanazowahonga hawa jamaa wa CCm wenye njaa.Hawa jamaa wa CCM kwavile ni vilaza hawajui kuwa hizo pesa wanazohongwa ni zao hawa jamaa wamewaibia kwa kutumia RICHMOND na KAGODA!!
 
Kitu kizuri ni kuwa wameamua kuachana na taratibu walizoziweka...naam, wanaandaa ugumu wa kutekeleza ilani yao bila kujua. Maana baadae itakuwa ni nani anamujua nani ili mambo yaende. Ndivyo walivyozoea
 
siita.jpg


(Picha) Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta

*Shilingi milioni 50 zilimwagwa kummaliza
*Mrithi wake aliandaliwa kabla ya kikao
*Kikwete adaiwa kuweka mtego kubaini ukweli


SIKU mbili baada ya mkakati wa kumng'oa Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta, kukwama ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), siri nzito zimeendelea kubainika.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Kikao NEC kilichomalizika Jumatatu iliyopita zilidai kwamba zaidi ya sh. milioni 50 zilitumika kugawa kwa baadhi ya wajumbe kuhakisha kwamba wanasimama kidete kuhakikisha wanamng'oa Bw. Sitta na kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete aliwatega ili ajiridhishe na tuhuma hizo.

“Unajua ni wazi kwamba hawa jamaa walitumia zaidi ya sh. milioni 50 kuwagawia baadhi ya wajumbe waliowaandaa ili wahakikishe wanaibua hoja dhidi ya Sitta kwenye kiti chake, lakini bahati nzuri Mwenyekiti alidokezwa na huenda hata vielelezo kadhaa alipewa,”kilidai chanzo chetu ndani ya NEC

Ilielezwa kwamba kama mpango wa kumng'oa Bw. Sitta ungefanikiwa zingefanyika kampeni za papo kwa papo kumpata mtu wa kumrithi ambapo mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini alikwishaandaliwa kugombea na kuchukua nafasi hiyo kwa gharama yoyote ile.

“Tayari timu ya kampeni ilikwishaandaliwa kutembea nchi nzima kwa wabunge ili aliyeandaliwa apate Uspika na kazi yake ya kwanza ilikuwa ni kutangaza kwamba tuhuma zote zinazotikisa Serikali ndani ya Bunge zitajadiliwa upya au kufungwa kwa kuwa zimeleta mgawanyiko, huo ndio ungekuwa mwisho wa CCM kuongoza nchi,”kilisema chanzo chetu bila kutoa ufafanuzi wa kina wa kauli hiyo.

Habari zaidi kutoka kwa watu walio karibu na Rais Kikwete zilidai kwamba Kiongozi huyo wa CCM alipata taarifa zote za maandalizi ya genge hilo la kifisaidi na kwamba katika kikao chao kilichofanyika mjini hapa ndicho kilichoandaa hoja ya kumng'oa Bw. Sitta na kwamba baada ya kupata taarifa hizo, aliwatega kwa kuwaacha wafanye kila wanachotaka kwanza ili awabaini na kujiridhisha na ushahidi aliopewa.

Ilielezwa kwamba katika siku ya kwanza ambapo baadhi ya Wajumbe walifika mbali kwa kutoa lugha zinazoweza kutafsiriwa kuwa ni matusi kwa Bw. Sitta ndani ya NEC, siku ya pili Rais Kikwete aliwaacha wajumbe hao kujieleza kwa kina wakidhani wanatumia uhuru wao kama wajumbe kumbe alikuwa amewatega ajiridhishe na yale aliyopewa na vyombo husika vinavyofuatilia nyendo za mafisadi.

“Unajua hata hawa jamaa hawamtambui vizuri Kikwete (Rais), wanadhani ukimya wake hawaujui, jamaa anawatega tena safari hii amewapatia kweli kweli, anajua fika mipango yao yote lakini kama tunavyomjua ni mtu asiyekurupuka katika maamuzi na anafanya kwa upole, alipojiridhisha dakika za mwisho alimaliza mzizi wa fitna kwa kuunda Kamati ya kurejesha umoja na kumaliza mgongano ndani ya chama,”kilisema chanzo chetu na kuongeza;

“Ni wazi kwamba CCM sasa inataka kwenda kinyume na matakwa ya Watanzania, lakini bahati nzuri Mwenyekiti ni mwerevu sana, amekiokoa chama kufuata mkumbo wa KANU, lakini kama asipokuwa makini zaidi wanaweza kumweka pabaya mwakani, hawa wana mbinu nyingi na kila siku wanakuja na jipya.”

Habari zaidi zilieleza kwamba Kamati hiyo inayojumuisha Rais mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Bw. Pius Msekwa na Spika mstaafu wa Bunge la Afrika Mashariki Bw. Abdulrahman Kinana imepewa jukumu la kukutana na wabunge wote wa CCM na kuzungumza nao kwa undani na kuhakikisha vikao vya wabunge wa chama hicho vinafanyika vizuri na kuweka msimamo mpya wa jinsi ya kumaliza mambo mzito yenye maslahi kwa chama kupitia vikao hivyo kabla ya Bunge.

Kwa kumjibu wa taratibu za Bunge ni wazi kwamba Kamati hiyo ambayo ina watu wenye sifa za ushawishi itakutana na wabunge katika Kikao cha 17 cha Bunge Oktoba mwaka huu mjini hapa.

Majira lilipomtafuta Bw. Sitta ili kujua msimamo wake kuhusu uendeshaji Bunge kwa kasi na viwango kutokana na mashambuzi yaliyoelekezwa kwake kwenye NEC hakupatikana mara moja.

Hata hivyo habari za uhakika kutoka kwa watu waliokaribu na kundi linalopinga ufisadi zilisema hivi sasa wabunge hao wanaendelea na mikakati mizito ya kuendeleza vita hivyo kwa mbinu za kisasa.

Taarifa hizo zilidai kwamba huenda Bw. Sitta akaongeza kasi na viwango zaidi vya kusimamia Bunge na kuwabana zaidi mafisadi pamoja na mawaziri wazembe jambo ambalo litaibua hasira za kundi hilo kwa kiongozi huyo wa Bunge.


Source: Gazeti la majira.

Hii kitu sio kampeni jamani,embu fikirieni vizuri...!
 
UFISADI AT ITS BEST!
Kwa wale ambao hawaielewielewi vizuri hii dhana ya ufisadi, sasa wajionee jinsi ulivyo na nguvu! Watu utawaona wamevaa tai vizuuri, kumbe mbele ya ufisadi wanafyata mkia!
Kwanini Sitta na wenzake wasijiunge na chama Pinzani next year tumunge vidole, na sisiemu wabaki midomo wazi?
 
UFISADI AT ITS BEST!
Kwa wale ambao hawaielewielewi vizuri hii dhana ya ufisadi, sasa wajionee jinsi ulivyo na nguvu! Watu utawaona wamevaa tai vizuuri, kumbe mbele ya ufisadi wanafyata mkia!
Kwanini Sitta na wenzake wasijiunge na chama Pinzani next year tumunge vidole, na sisiemu wabaki midomo wazi?

Sitta akisema ajiunge na chama kingine ndio basi tena sidhani kama atakikalia kile kiti tena!
Na yeye mwenyewe sidhani kama ataweza kuhama kwa sababu alikiomba chama cha mapinduzi radhi kwa yale aliyosema kwamba kina mafisadi...So sitta kuachia ngazi kwenye CCM ni vigumu!
 
Mi namkakati wa kweli, afanye kuwahadaa kidogo, then next year bunge la mwisho yeye na wenzake wajiunge na upinzani. Ila cha kufanya saizi aongeze kasi ya bunge na viwango vyake. mbona mi nampa mia kwa mia. naimani watz tumeona utendaji wake vizuri, msimamo wake ni wa manufaa kwetu sote. Kwa nini basi Sitta asisome alama za nyakati akatuongoza mwakani au mwaka 2015? Mi naimani na Sitta wewe Je?
 
Waandishi Makanjanja, Wamechukua Uchambuzi wa Mkandara na dataz za FMES hata aknowledgement?
 
🙂Safari ya kutenga mijusi kwenye msafara wa kenge naona ndio imeshaanza!! Nadhani katika historia ya uchaguzi wa Tanzania, 2010 unaweza kuwa mwaka wa kukumbukwa!!
 
Back
Top Bottom