Spika Sitta Kung'olewa?

hizi habari zisizokuwa na jina la chanzo chake inakuwa tabu kuzitathmini kwa undani....au ni habari tu za tetesi ambazo zipo unfounded

Hapa jamvini sio CNN, wala Fox News Channel.

Uvumi, ukweli, uzushi, uongo, tetesi, udaku yote cha mbele!

Hivyo ndivyo wanavyosema ukiuliza vyanzo.
 
AAAAAAAHhhhhhhhhhhhh jamani eeeh mimi nachanganyikiwa kabisa au nipo ndotoni nini??? wee Shy umepewa mgao wako na sasa unawawatetea mafisadi?? Hayaa huenda nami nikipewa nitakuwa upande wao!!!! Eeeh Mafisadi nawaombea kwa mungu muweze kunikumbuka nami nipate huo mgao maana tangu mlipoanza kuzichota hali imekuwa mbaya sana mkinipa mgao nitaendelea kuwaombea kwa mola muweze kuendelea kuumbuana na wadanganyika kuzinduka usingizini
 
Ni kama kulanyama ya mtu ukianza kuilautakula tu hata mtoto wako, SS alishiriki kuvuruga matokeo fulani ya mtu wangu wa karibu miezi michache iliyopita, hata jua halijazama mara risiti feki, mara nini sijui ! na urambo twa msubiri , SS ana unyama wa hali ya juu mnaodhani ni mtetezi wa wanyonge mmeliwa! au mnataka mfatilie na kujua jinsi gani yeye mama walivyojikatia eneo la heka kibao nje ya Dar kwa maandalizi ya chuo kikuu binafsi yeye na mkewe wakati jimboni kwake kuko taabani, laiti watanzania wangemjua SS kwa undani hata hayo anayoendelea kuyafanya nadhani ni exdentally thats not SS i know!
 
mnataka mfatilie na kujua jinsi gani yeye mama walivyojikatia eneo la heka kibao nje ya Dar kwa maandalizi ya chuo kikuu binafsi yeye na mkewe !

Mkuu si inaruhusiwa DAR kununua mashamba? Si ametumia hela zake? Mimi hapa sioni kama kuna jambo kubwa.
 
2009-08-03 09:09:00​

PM speaks out on Sitta security plea
14153.jpg

'Following Honorable Sitta's appeal in Parliament, i think there is a need for the matter to be discussed in depth and an appropriate decision made' says Prime Minister Mizengo Pinda.​

Premier says it's too early to state whether the Government would immediately bolster security for the Speaker following his appeal in Parliament last week

By Mkinga Mkinga

The Government will treat National Assembly Speaker Samuel Sitta's appeal for more security with the urgency it deserves, according to Prime Minister Mizengo Pinda.

Speaking exclusively to The Citizen at the weekend, Mr Pinda said the issue was sensitive and had to be handled with "great care".

"I need to get more details about Honourable Sitta's request so that we can be in a position to determine if bolstering security around him is the right solution," he said.

Mr Sitta stunned MPs last week when he said in Parliament that his life was in danger, and asked the Government to step up security for him and his office.

Mr Pinda said he was not aware that Mr Sitta's life was in danger before the Speaker made his passionate plea in the House.

"Following Honourable Sitta's appeal in Parliament, I think there is a need for the matter to be discussed in depth and an appropriate decision made."

Mr Pinda added that Parliament had its politics and, as the head of government business in the House, he had to carefully weigh all such requests.

He said, therefore, that it was too early to state whether the Government would immediately bolster security for the Speaker.

"It's the Government's responsibility to provide the Speaker with security, but we first have to establish exactly what is happening before making a decision."

In a surprise announcement in Parliament in Dodoma last Thursday, Mr Sitta turned to Mr Pinda, who was in the debating chamber, and pleaded with him to ensure that he is accorded better security for himself and his office.

Mr Sitta's appeal was apparently prompted by a mounting wave of accusations against him. Reports being circulated on the Internet, and which have been picked up by some newspapers, make serious allegations against the Speaker. His accusers allege that he has misappropriated public funds and plots to cover up his tracks.

"At this rate, Mr Prime Minister, my life could be in danger. I feel that this is perhaps the time to bolster my security, as the current arrangement is inadequate," the Speaker said after the questions and answers session.

Currently, Mr Sitta is entitled to only one official bodyguard when he is out of parliament grounds. Within the National Assembly, two intelligence officers give him all-round protection.

But he does not have a chase car or outrider motorcycle security service, except when there is a national event at Parliament. Mr Pinda, who sits a few steps away in the front-row seats reserved for Cabinet ministers, listened attentively as the Speaker made his plea amid applause from the MPs.

This is not the first time the issue of the Speaker's security has come up in the House. Legislators, including CCM's outspoken Same MP, Mrs Anne Kilango-Malecela, have expressed concern at the "scant protection and respect" accorded to the holder of that key office.

The Prime Minister is the Leader of Government Business in the august House, and at least for now, it falls directly under his office, hence the growing clamour to give the institution more autonomy.

On Thursday, Mr Sitta appeared upset about reports in a section of the media that implicated him in an alleged conspiracy to reportedly destroy parliamentary documents to conceal supposed incriminating evidence of embezzlement of funds by his office.

He said: "These newspapers have alleged that I am plotting with other people to torch the offices here in Parliament to destroy accounting records! If I had wanted to do that, who in the National Assembly would have denied me access to any file anytime?"

He said the reports as the machinations of "my enemies out to tarnish my image and political reputation". He stopped short off calling the alleged conspirators mafisadi, a term usually associated in public with the corrupt.

Mr Sitta said: "All these reports you are hearing now are from my enemies who have chosen four newspapers to play their dirty political games.:"

He added: "They have been monitoring me, they are even looking at me even at this moment.:" The group, he went on, had concocted false claims against him, which were then posted on the Internet, from where the newspapers picked them up and reported them "as they are gospel truth."

It is at this juncture that he turned to Mr Pinda and said: "Honourable Prime Minister, I plead for more security as this war is now getting bigger. My security is not enough."
He said the group "was growing bolder and now appears to be doing things at will and without any fear".

Asked to identity his perceived enemies, Mr Sitta told The Citizen at parliament grounds that there were people fighting him politically, but whom he did not wish to name.

"Their aim is to tarnish my name in the belief they will cripple me politically. I am ready to fight them and equally play the political card," Mr Sitta, who has in the past declared that he is being fought for his steadfast war against corruption, said.

In Parliament, the Speaker revealed that the same people had invaded his Urambo East constituency "where they are dishing out money, motorcycles and other goodies to woo voters in a plot to unseat me in the coming General Election."

However, he declared that he would defeat them "hands down in the Urambo duel and, if God wishes, I will still be the Speaker after the elections".
It was not the first time that Mr Sitta had spoken about his personal safety and that of his immediate family members.

In the wake of a similar move in March this year, Mr Sitta pleaded with his enemies to leave his family out of political intrigue.
 
samwelsitta1.jpg

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Samuel Sitta, serikali imeahidi kumwongezea ulinzi.

Sadick Mtulya na Nora Damian
Mwananchi


SERIKALI imesema itamlinda Spika wa Bunge, Samuel Sitta kwa hali yoyote ile; ili kutekeleza ombi lake la kuongezewa ulinzi akihofia maisha yake kutokana na kuandamwa na wabaya wake kisiasa.

Wiki iliyopita Sitta alimwomba Waziri Mkuu aongezewe ulinzi kutokana na hila anazofanyiwa na maadui zake kisiasa ambao alisema wamefikia hatua ya kutumia vyombo vya habari kumchafua ikiwemo madai kwamba, anataka kuchoma nyaraka muhimu za Bunge.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani jana, baada ya kupokea msaada wa magari sita aina Landcruiser Hardtop, pikipiki 10 na simu za upepo (rediocall) 50, kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR); Masha alisema viongozi wanaotakiwa kulindwa na serikali wanafahamika na kwamba Spika Sitta ni mmojawapo.

“Pamoja na yote, Serikali imekwishajiandaa vya kutosha kuhusu usalama wa viongozi wa kitaifa na litamlinda Spika kwa hali yoyote ile; ila kwa sasa tupo tunafuatilia kiini cha Spika Sitta kuomba aongezewe ulinzi,” alisema Masha na kuongeza.

“Pamoja na Spika Sitta kuwa na ulinzi mzuri pia kwa sasa tupo katika mchakato kuona kama kuna haja ya kumwongezea ulinzi kuliko huo alio nao sasa.”

Hata hivyo, serikali imemtaka Spika kuwasilisha vielelezo na mbinu anazohisi zinaweza kutumiwa na maadui wake wa kisiasa kumwangamiza.

Mwishoni mwa wiki, Msemaji Mkuu wa Polisi ACP, Abdallah Mssika alisema mazingira ya kiusalama ya Spika yamekwisha hakikishwa, lakini hawezi kuweka hadharani aina ya ulinzi waliomwekea kwa sababu za kiusalama.

“Ni kawaida kwa viongozi wa kitaifa kupewa ulinzi, aina ya ‘VIP Protection’ huu upo katika muundo wa wazi na siri..., lakini siwezi kukuambia ni ulinzi upi upo kwa Spika Sitta, kwa sababu za kiusalama,” alifafanua Mssika.

ACP Mssika alisema kutokana na mfumo wa nchi, ipo taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya ulinzi na hadi sasa mazingira ya kiusalama yanakwenda vizuri.

“Ulinzi upo madhubuti wakati wote na si kwa Spika Sitta pekee, bali kwa viongozi wote wa kitaifa wa nchi hii,” aliongeza Mssika.

Mssika alisema vyombo vyote vya kiusalama vimejiimarisha na hali ya ulinzi ipo madhubuti wakati wote.

Spika Sitta aliomba ulinzi huo alipokuwa akizungumzia tuhuma dhidi yake, zilizoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari (sio Mwananchi) kuwa, anafanya njama kuchoma moto nyaraka za Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Spika anadaiwa kula njama ili kuchoma ofisi ya mhasibu wa Bunge ili kuharibu nyaraka muhimu zinazomhusisha na ubaridhifu wa fedha za Bunge.

Lakini, Spika Sitta alijibu tuhuma hizo bungeni akisema zina mkono wa wabaya wake, wenye lengo la kumchafua katika utendaji wake.

Mara kwa mara Spika Sitta amekuwa akidai kwamba, anaandamwa na mafisadi ambao wanataka aache kufichua maovu yao.

Spika amekuwa akitoa malalamiko ya kutishiwa maisha na watu ambao wanasadikiwa ni mafisadi, wanaopinga namna anavyoendesha Bunge kwa kuwabana wasipumue.

Hatua hiyo imekuwa ikimfanya pia kuandamwa hadi jimboni kwake Urambo Mashariki, ambako kumekuwa na harakati za kumng'oa mwakani.

Hata hivyo, mwenyewe ameapa kutorudi nyuma, bali atazidi kuwabana mafisadi kwani wamekuwa wakirudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Spika pia ameapa kwamba, mwakani kama atakuwa hai ataweza kurejea katika nafasi yake ya ubunge na kiti hicho cha uspika.

Tangu mkutano wa 10 wa Bunge ambao uliibua tuhuma za Richmond, Bunge limekuwa na mpasuko mkubwa ambao unatokana na kambi mbili zikiwemo zile za wabunge wapambanaji wa ufisadi ambayo iko nyuma ya spika na ile inayotetea watuhumiwa.

Miongoni mwa wabunge ambao wako kambi kuu ya vita ya ufisadi chini ya Spika ni pamoja na Anne Kilango Malecela, Lukasi Selelii, Christopher Ole Sendeka, Dk Harrison Mwakyembe, Fred Mpendazoe, Hurbert Mtangi ambao pia wamelalamika kufanyiwa hujuma.
 
Kweli anahitaji ulinzi kwa sababu wanamsakama/tunamsakama...Kisiasa?

He added: "They have been monitoring me, they are even looking at me even at this moment.:" The group, he went on, had concocted false claims against him, which were then posted on the Internet, from where the newspapers picked them up and reported them "as they are gospel truth."
Yaani hili group la JF?

Halafu waandishi wanaenda kuongeza chumvi na kudai tunataka kummaliza!

Anahitaji ulinzi wa mtandao, cybersecurity, and that is it!

Sidhani kama kuna mtu anataka kumdhuru kimwili(maoni yangu)
 
Sidhani kama kweli Mheshimiwa Sitta anahitaji ulinzi wa ziada maana madai anayotoa hayana uthibitisho. Ingekuwaje kama Mheshimiwa Pinda naye angetumia vigezo vya "speed na standard"? Si angetakiwa kuthibitisha kauli vinginevyo kufuta! Yoyote yale sijaona jipya la ziada ambalo Mheshimiwa Sitta amefanya zaidi ya kutekeleza majukumu yake ya kawaida! Ongezeko la ulinzi ni inaambatana na ongezeko la gharama pia, hii inaongeza mzigo kwa wananchi na walipa kodi kwa ujumla. Huu ni ubadhirifu tu na inachangia kuongezeka kwa matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali.
 
Date::8/4/2009Waziri Masha atoa ahadi ya kutoa ulinzi zaidi kwa Spika SittaSpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Samuel Sitta, serikali imeahidi kumwongezea ulinzi................

It is reasonable to endorse security to this claimant meanwhile investigating the authenticity of the information. Then, upon approval or the opposite, the security agents can decide anyhow.

However, my problem is the promptness of the government on this fellow’s request.
Why have they failed to provide similar protection to fellow Albinos?

But Again is the Speaker exposed to all rights of making allegations without providing any proof!

Yabidi tuwe macho yaonekana Bunge sasa linapata immunity ambayo ni excessive, kiasi kwamba mbunge hahitaji kutoa ushahidi wowote anapomtuhumu mtu au chombo kilicho nje ya Bunge. Ila wao kwa wao eti tunasikia “ Mwongozo wa Spika!”
 
Na Romana Mallya

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Laurence Masha amesema suala la Spika wa Bunge, Samuel Sitta, la kuomba kuongezewa ulinzi bado wanalifanyia kazi.

Masha alisema jana kuwa, kwa sasa wanachokifanya ni kujua sababu za Sitta kuomba ulinzi na kama zitaonekana zina uzito wa kuongezewa ulinzi watafanya hivyo.

Alisema kwa kawaida viongozi wote hupewa ulinzi na kwamba hakuna hata siku moja viongozi hao walishaachwa kulindwa.

Alisema ikiwa Sitta aliomba ulinzi wa ziada, wao hawana pingamizi lakini lazima wapate maelezo ya kutosha kutoka kwake na wayafanyie kazi ili kujua kama kuna sababu za kupatiwa ulinzi huo.

Sitta alitoa ombi hilo bungeni Alhamis wiki iliyopita kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Alisema kuwa ulinzi alio nao haumtoshi kutokana na kuadamwa na wabaya wake kwa njia mbalimbali, zikiwemo za kumchafua kupitia katika mitandao.

Aidha, Jumapili ya wiki hii, Sitta akizungumza na Nipashe alisema kuwa, alitakiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma na Usalama wa Taifa wa mkoa huo kupelekea maelezo hayo.


Chanzo: NIPASHE
 
Kama ulinzi keshapewa na CCM na Serikali yake. Kwa sasa anachohitaji ni ulinzi wa kumlinda kutumia hela za Wananchi bila ya matatizo. Masha usiwazuge wananchi kwamba mnafanyia kazi hilo suala. Nyinyi kama Wizara ya mambo ya ndani mlitakiwa muwakamate watu kama hawa; na siyo kuwalinda.
 
Kama ulinzi keshapewa na CCM na Serikali yake. Kwa sasa anachohitaji ni ulinzi wa kumlinda kutumia hela za Wananchi bila ya matatizo. Masha usiwazuge wananchi kwamba mnafanyia kazi hilo suala. Nyinyi kama Wizara ya mambo ya ndani mlitakiwa muwakamate watu kama hawa; na siyo kuwalinda.

Wana ubavu wa kumkamata mtu hawa na wote wamewekwa mifukoni mwa mafisadi? Wanajibaraguza baraguza tu kutaka kuudanganya umma wa Watanzania kwamba "they are are doing something" lakini ukweli ni kwamba ni usanii wa hali ya juu ndiyo unaendelea wa serikali hii kuonyesha jinsi kazi ilivyowashinda.
 
Kama ulinzi keshapewa na CCM na Serikali yake. Kwa sasa anachohitaji ni ulinzi wa kumlinda kutumia hela za Wananchi bila ya matatizo. Masha usiwazuge wananchi kwamba mnafanyia kazi hilo suala. Nyinyi kama Wizara ya mambo ya ndani mlitakiwa muwakamate watu kama hawa; na siyo kuwalinda.

Hii ni moja katika sera ya CCM kuiba na kulindana, Chukulia wewe M-Tz umekwenda Somalia na umedhuliwa na msomali ukaenda kushtaki, siku ya mahakamani ukamuona ulimshtaki ni Msomali na wakili wake na wako ni wasomali na la mwisho Jaji ni Msomali, sasa we Braza kutoka Bongo una lako hapo?
Hii ndio sera ya kwetu Bongo. Wanalindana hawa. Wataiba au watachota watakula mpaka vijukuu vyao as long as CCM is on power nobody can touch them. Imagine Mr.JK alivyoingia kwa kasi na kutoa ahadi kadha wa kadha, nini amefanya? Nothing, watu watumbua kama kawaida, maisha yanazidi kua magumu. Ukiangalia Rasli mali yetu na maisha tunayoishi, YANASIKITISHA. Na mpaka hii leo kuna watu wanakwambia hakuna au haoni chama mbadala kwa CCM kinachoweza kuleta maendeleo Tz. Mbona wenzetu wamejaribu kukipa chance chama kingine ku-rule na wakafanikiwa? Hapa ndio ninaposema kama Democracy can not be aplied in Africa over night, people need to understand what they believe in. Still kuna watu wanaona kubadili chama ni kama kubadili Dini. That's wrong man. Let's wake up
 
huyo bwana Sitta nadhani ni mnafiki, swali la kujiuliza ni kuwa kama yeye Sitta anajua ana maadui na wanajulikna kwa nini asipeleke hiyo list kwa huyo Maasha ili kusudi washughulikiwe, na huyo Masha inaonekana ni kibuyu kwelikweli, wakati Bwana Mengi aliposemwa anaandamwa na waziri Kijana Masha alikuja juu na kumwambia Mengi amtaje kwa muda wa siku saba, sasa iweje kwa Bwana Sitta iwe swala lake linashughulikiwa?
 
huyo bwana Sitta nadhani ni mnafiki, swali la kujiuliza ni kuwa kama yeye Sitta anajua ana maadui na wanajulikna kwa nini asipeleke hiyo list kwa huyo Maasha ili kusudi washughulikiwe, na huyo Masha inaonekana ni kibuyu kwelikweli, wakati Bwana Mengi aliposemwa anaandamwa na waziri Kijana Masha alikuja juu na kumwambia Mengi amtaje kwa muda wa siku saba, sasa iweje kwa Bwana Sitta iwe swala lake linashughulikiwa?

Mmh kesi ya Nyani apelekewe Tumbili......tumbili lazima atanywea tu kwa sababu ya ubabe wa nyani.
 
Sitta usijali Mungu atakulinda kama alivyomlinda Mwakyembe,ushujaa wako utaliokoa Taifa hili msiwape punzi mafisadi.
 
Sitta usijali Mungu atakulinda kama alivyomlinda Mwakyembe,ushujaa wako utaliokoa Taifa hili msiwape punzi mafisadi.

Tumaini la sisi kondoo liko mikononi mwa mbweha hivyo Mungu amlinde mbweha atuokoe sisi kondoo tutoke kwenye makucha ya fisi - la, haulaaa !!
 
Hapa mafisadi wanapambana wenyewe kwa wenyewe.Pengine yanayosemwa ni kweli, lakini ukisoma utaona article ni one sided na si ajabu muandishi analipwa na Sitta.

Hapo nyuma katika mchango wangu kuhusu Sitta niliwahi kuandika kuwa huyu bwana ni hatari sana kwani ni ndumila kuwili; yeye mara zote ni POPO akitaka kuridhisha pande zote!! I have no doubt in my mind kuwa Sitta hizo tuhuma zinazomkabili ni za kweli kwani hajaonesha kwa ushahidi uliokamilika kuwa ni uongo! Nyumba anazohusishwa nazo zipo na wanawake zake sio siri wapo na magari ya bunge wanayoyatumia yapo; jambo la kushangaza ni kwanini hachukuliwi hatua za kukiuka maadili ya kazi? Asilindwe kwa kivuli cha kupambana na ufisadi kumbe yeye mwenyewe ni fisadi!
 
  • Genge lajipanga kutumia NEC
    [*]Kikwete kuwekwa njia panda

Na Saed Kubenea


MwanaHALISI



NJAMA za kumwangamiza kisiasa Spika Samwel Sitta zimegundulika kabla waandaaji wake kuzifikisha kwenye vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zinasema maandalizi hayo yamejengwa kwenye misingi miwili ambayo inadhaniwa ingevuta wajumbe wengi wa vikao vya Kamati Kuu (CC) na Hamashauri Kuu ya Taifa (NEC) vinavyoanza Jumamosi ijayo mjini Dodoma.

Msingi wa kwanza umejengwa kwenye madai kuwa Sitta, kwa kutumia nafasi yake, amekuwa akiruhusu baadhi ya wabunge wenye hoja kali kuituhumu serikali na kwa hiyo kuidhalilisha.

Msingi wa pili ni kwamba, Sitta ameendeleza ukaidi dhidi ya taarifa ya serikali kuhusu kashfa ya Richmond iliyomg'oa Edward Lowassa kwenye nafasi ya waziri mkuu.
Kwa madai hayo mawili, inajengwa hoja kwamba Sitta haheshimu CCM na serikali yake na kwa hiyo "anadharau mamlaka."

Lakini Spika Sitta akiongea kwa simu kutoka Kampala, nchini Uganda, alisema hana taarifa juu ya kuwapo kwa suala hilo, na kwamba anachofanya hivi sasa ni kusimamia sera za CCM na kuendesha bunge bila upendeleo.

"Mimi sina taarifa na kitu hiki, lakini hata kama kipo hakiwezi kunizuia kutimiza wajibu wangu. Wananchi na baadhi ya viongozi duniani watambua kazi ninayofanya," alisema.

Alisema, "Mimi natekeleza misingi ya Baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ya kusimamia haki na usawa katika jamii. Katika hili, hakuna wa kunizuia."
Katika mkutano wa bunge uliomalizika mwanzoni mwa mwezi huu, baadhi ya wabunge walitoa kauli kali za kubana watendaji wa serikali, hasa mawaziri, kufikia hatua ya wengine kumwomba spika awakemee.

Hata hivyo, hata baada ya baadhi ya wabunge kusema mawaziri walaaniwe, spika alijibu hoja kwa kusema hana uwezo wa kuzuia kauli na hasira za wabunge.
Vikao vya juu vya chama vitakuwa na mikutano yake ya kawaida kuanza Agosti 15 hadi 18 mwaka huu. Vitatanguliwa na kikao cha Kamati ya Maadili kilichopangwa kufanyika siku mbili kabla.

Spika Sitta ndiye aliunda Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa kufua umeme wa dharura kati ya TANESCO na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) ya Marekani. Kamati iliongozwa na mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Mapendekezo ya Kamati ndiyo yalizaa maazimio 23 ya Bunge ambayo yalikabidhiwa kwa Waziri Mkuu ili serikali iweze kuyatekeleza.
Kabla ya kumalizika kwa kikao cha bunge kilichopita, serikali iliwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa baadhi ya maazimio. Wabunge walipinga taarifa hiyo na kusababisha serikali kuiondoa bila mjadala.

Taarifa zinasema baadhi ya wajumbe wa CC na NEC wanaopanga kumbamiza Sitta wanakutana na kutumia mtandao mpana wa mawasiliano ya simu za mkononi ili kujenga msimamo wa pamoja ambao ungeibukia kwenye vikao.

Hata hivyo, gazeti hili lina orodha ya wanaodaiwa kuwa wajumbe kweye "kamati ya siri" dhidi ya Sitta ingawa hakuna taarifa zozote juu ya walipokutana, lini na nani hasa anaongoza kundi hilo ndani ya vikao vya juuu vya chama chao.

Kauli za "Sitta hafai" zilisikika zaidi kwenye mkutano wa bunge uliomalizika mwezi huu. Baadhi ya wabunge walisema Sitta anasaliti wenzake aliokuwa nao kwenye mtandao huku wengine wakisema anaangamiza chama.
Joto la tuhuma dhidi ya Sitta liliongezeka pale aliposema bungeni kuwa anaiomba serikali imwongezee ulinzi kwa kuwa wale wanaotuhumiwa ufisadi wamejipanga kumdhuru.
Pale shutuma za chinichini zilipoongezeka, Sitta akaibuka hadharani na kusema bungeni kuwa hawezi kukubali watu waibe halafu bunge linyamaze. Akaongeza, "Wanataka bunge hili liwe bunge poa."

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba alipoulizwa kama ni kweli kuwa ofisi yake imeandaa taarifa za siri juu ya Sitta, alisema, "Sijui."
"Hii ni ofisi kubwa, haiwezi kufanya vitu vya kijinga namna hiyo. Nyie acheni kutafuta vitu vya kuokoteza," alisema kwa sauti ya juu kama anayekemea.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita ambaye gazeti lilidhani angeweza kujua kinachoendelea, aliiambia MwanaHALISI, hakuweza kupatikana "vizuri" kujibu maswali juu ya hoja hii.
Katika kelele na kushindwa kusikilizana vizuri, Guninita alisema yuko safarini kwenda Dodoma (kwa gari) na kwamba angepata mahali pazuri akaegesha gari, "ningekupigia." Hakupatikana tena.
Jumapili iliyopita, gazeti la Mwananchi lilimnukuu Makongoro Mahanga, mmoja wa wajumbe wa NEC wenye ushawishi mkubwa katika chama hicho, akitoa wito wa kudhibitiwa kwa makada wenzake wanaodai kupambana na ufisadi nchini.

Mahanga ambaye ni naibu waziri katika serikali ya Kikwete, ni miongoni mwa wabunge wasiotamka waziwazi lawama au shutuma dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi.
Mbunge huyo wa Ukonga, Dar es Salaam anadai kama wanaotuhumu wenzao ufisadi hawatadhibitiwa, "CCM itapoteza viti vingi katika uchaguzi ujao."
Kauli ya chama hicho kupoteza wabunge wengi katika uchaguzi mwakani ilitolewa mara ya kwanza wiki iliyopita na John Malecela na mke wake Anne Kilango.

Malecele ambaye amekuwa makamu wa rais, waziri mkuu na makamu mwenyekiti wa CCM taifa, ni miongoni mwa viongozi wanaoheshimika katika chama chake na nguzo muhimu katika kuandaa mikakati ya ushindi wakati wa uchaguzi.

"Sikiliza bwana mdogo, Sitta anawasemea wananchi wa ngazi ya chini na kati. Anguko la Sitta litawapa nguvu mafisadi. Lakini kumfukuza au hata kumdhalilisha kutaleta mitafaruku ndani ya chama," ameeleza mmoja wa wajumbe wa NEC anayemsifia Sitta kwa kile anachoita "kazi yake nzuri."
Katika hili, alisema hata Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete hawezi kuunga mkono mgawanyiko hivi sasa.

"Machoni mwa wananchi wengi Sitta anaonekana kupiga vita ufisadi. Na hili peke yake limemjengea heshima ya CCM na serikali yake. Lakini ni kweli kwamba kuna watu ambao wameathirika na msimamo wake, hivyo wanaweza kutaka kumwondoa," alisema waziri mmoja bila kutaka kutajwa jina.
Taarifa za kiusalama zimethibitishia gazeti hili kuwapo kwa mpango huo, na kwamba wahusika watatumia vikao vya CCM kuufanikisha.

Malalamiko dhidi ya Sitta yaliwahi kusikika katika moja ya vikao vya Kamati Kuu mwaka huu. Aliyepeleka malalamiko hayo alikuwa Haji Omari Kheri, mwakilishi wa Tumbatu na Katibu wa wajumbe wa CCM katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Mwenyekiti, Rais Kikwete aliepusha mjadala kuhusu suala hilo kwa kusema panahitajika siku nzima kujadili masuala hayo ya bunge.
 
Last edited:
hawa wajumbe wa NEC watakivuruga chama kama watakuwa na maamuzi kama hayo kwa maslahi ya watu wachache, kwa mtazamo wangu SITTA kwa sasa ni mhimili mkubwa/muhimu sana kwa CCM na serikali yake
 
Back
Top Bottom