Spika Ndugai: Wabunge 19 waliofukuzwa CHADEMA wapo kwenye mikono salama

Haya yote atayalipia tu huyu andunje, ni suala la muda tu. Wewe mtu mmoja mpumbavu Hauwezi ukalitia taifa aibu kubwa kiasi hiki. Haiwezekani.

Mwenzie alijifanya kichwa maji hivi hivi.
 
Nape zamu hii lazima avuliwe uanachama wa ccm, apoteze na hako kaubunge kake, akaungane na wenzake chadema. He is too much. Zamu ile aliomba samahani na akasamehewa (kwa mazungumuzo yake kwenye simu yaliyodukuliwa, wakimsema vibaya aliyekuwa rais wa JMT wakipanga mipango mibaya dhidi ya serikali).

Avuliwe uanachama wake wa ccm na tuone kama atang'ang'ania huo ubunge.
Juzi tulimwona akiwa na akina Lissu kwenye zoom wakiisema vibaya serikali ya awamu ya 6 chini ya mama yetu SSH!
Umepanic
 
Ili kuwapokea Bungeni wabunge 19 wa Chadema kama wabunge wa kuteuliwa, Spika alibidika kuhakikisha kwamba hao kina mama wameteuliwa kweli na Chadema. Anasema sasa “kipeperushi” tu hakitoshi, ni lazima apewe pia minutes za mkutano uliofanya uamuzi na katiba. Alipewa hivyo vitu kabla ya kuwapokea? Spika ni shurti awe consistent.

Vile vile Spika anasema ni lazima kuwatendea akina mama kwa upole na sio kuwatendea kama unavyotendea wanaume. Ni kweli Spika anafanya hivyo? Mbona kuna wakati aliamuru Halima Mdee akamatwe, afungwe pingu na kuletwa Bungeni? Soma hii thread:


Na aliamuru Mdee afungwe pingu kwa “kosa” la kumwita mheshimiwa mmoja MPUMBAVU. Na aliyeitwa mpumbavu ni kweli alionyesha upumbavu. The Speaker must be consistent. Kipindi hicho, Mbunge Serukamba alitoa tusi la nguoni Bungeni na Spika hakuamuru afungwe pingu.

Hivi Spika Ndugai anafahamu kwamba anatakiwa asionyeshe upendeleo kwa chama chochote Bungeni? Mbona anacheka “Kindugai” sana anapozungumzia anaowaita “wale wa upande mwingine”?
 
Huu Ujanjaujanja Wa CCM una Mwisho Ipo Siku Inakuja
Unajidanganya, hakuna mwisho wa ccm ndani ya Tanzania, jua lirapatwa na supernova ila ccm wataendelea kuwepo labda wachoke wao tu.
Tz ni walking deads land..
Waliopo ccm wanalijua ilo ndo maana wanaweza fanya chochote kile bila KUJALI ikiwa anavunja sheria ama lah.
 
Nape zamu hii lazima avuliwe uanachama wa ccm, apoteze na hako kaubunge kake, akaungane na wenzake chadema. He is too much. Zamu ile aliomba samahani na akasamehewa (kwa mazungumuzo yake kwenye simu yaliyodukuliwa, wakimsema vibaya aliyekuwa rais wa JMT wakipanga mipango mibaya dhidi ya serikali).

Avuliwe uanachama wake wa ccm na tuone kama atang'ang'ania huo ubunge.
Juzi tulimwona akiwa na akina Lissu kwenye zoom wakiisema vibaya serikali ya awamu ya 6 chini ya mama yetu SSH!
Unaongea as if ccm ni Mari ya Familia yenu.
Bogus kabisa
 
Ikiwezekana kila NDUGAI atakapoonekana hadharani azomewe kwa aibu anayoiletea Taifa.
Chadema ni wasanii sana
Badala ya kuandika vibarua kila siku,itisheni Baraza kuu ambalo ndio hao wabunge wamekata rufaa
Mnaelewa kabisa kwamba hamkufuata taratibu za kuwatimua,mnasumbua wafuasi wenu
 
Chadema ni wasanii sana
Badala ya kuandika vibarua kila siku,itisheni Baraza kuu ambalo ndio hao wabunge wamekata rufaa
Mnaelewa kabisa kwamba hamkufuata taratibu za kuwatimua,mnasumbua wafuasi wenu
Ndugai mwongo
 
Ona sasa wana chadema walioko huku Jf wanavyomtetea Nape. Hii inadhihirisha Nape ni mwenzao. Ni kati ya watu wanaompelekea taarifa Tundu Lissu huko Ubeligiji ili aendelee kuichafua nchi yetu.
Ndugu,
Ukijiharishia hadharani umejichafua mwenyewe, kamwe usiwasingizie wanaokusema na kukucheka
 
Kwa alichokifanya na anachoendelea kufanya Tundu Lissu hakupaswa tu kufukuzwa ubunge bali pia uraia wa Tanzania. Kenya walishamfukuza uraia wa Kenya Bw. Miguna Miguna aliyeikimbilia kuishi nchini Canada.
Hilo jina lako haliendani kabisa na hoja butu unazotoa. Kwani Jiwe aliendanazo kabisa za vichwani mwenu. Tutaongeza maombi kuwakomboa ili muwe na mchango katika maendeleo ya taifa letu.
 
Leo Bungeni baada ya kipindi cha maswali na majibu, Spika wa Bunge Job Ndugai amesimama na kumkemea Nape Nauye, Mbunge wa Mtama ambaye hivi karibuni alitoa maoni yake binafsi kuwa wale wabunge 19 waliotimuliwa na CHADEMA sio wabunge halali..
Daah kama NCHI tuna safar ndefu mnoo!
 
Nape Nnauye ni mwanasiasa makini na anajua siasa kuliko Ndugai.

Nape amekuwa kwenye sekretarieti ya chama lakini Job ameishia kwenye ujumbe wa kamati kuu tu sawa na akina Bulembo au yule dada albino ambaye ni mwanamuziki.

Katika hili la covid 19 Nape yuko sahihi!
Word
 
atarudi kama cargo (mzigo)...na itabidi iandaliwe kampuni ya clearing ya ku import na ku-clear mzigo pale cargo airport
 
Back
Top Bottom