Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,505
- 51,109
Ningeomba kumkumbusha Spika Ndugai kiapo alichokula, cha kuongoza bunge kwa kufuata kanuni na sheria za nchi.
Ningependa kumkumbusha Ndugai kuwa alikula kiapo hicho huku ameshika biblia na huku akilitaja jina la Mwenyezi Mungu.
Ningependa kumkumbusha Ndugai kuwa kila siku kabla ya bunge kuanza kuna sala ya kuliombea bunge huku Jina la Mungu likitajwa
Sasa kwa muktadha huo, Ndugu Spika ajitafakari, Je wakati anakula kiapo kizito namna ile huku analitaja jina la Mwenyezi Mungu haogopi?, Yaani ni mkavu kabisa na moyoni mwake ana amani kabisa kuwa alilofanya ni sawa?
Mzee Msekwa amesema kuwa uwepo wa akina Halima Mdee bungeni ni uvunjifu wa katiba ya nchi, Je Ndugai ameziba masikio kabisa na kushiriki uvunjifu mkubwa huu wa katiba bila wasiwasi wowote?
Nimkumbushe tu Ndugai, Jina la Mwenyezi Mungu huwa halichezewi, Hicho kiapo ulichokula kuwa utaheshimu sheria za nchi halafu ukazivunja makusudi huku Ukijua, basi jua Biblia uliyoikamata wakati unaapa na Mungu alishuhudia. Na imeandikwa katika maandiko USILITAJE BURE JINA LA MUNGU wako!
Ndugai, Waondoe hao wabunge 19 ambao unajua wazi wamo bungeni kinyume cha katiba, nje ya hapo kumbuka kiapo chako ulichoapa kwa kulitaja jina la Mungu.
Ndugu Ndugai, Mungu huwa hataniwi!
Ningependa kumkumbusha Ndugai kuwa alikula kiapo hicho huku ameshika biblia na huku akilitaja jina la Mwenyezi Mungu.
Ningependa kumkumbusha Ndugai kuwa kila siku kabla ya bunge kuanza kuna sala ya kuliombea bunge huku Jina la Mungu likitajwa
Sasa kwa muktadha huo, Ndugu Spika ajitafakari, Je wakati anakula kiapo kizito namna ile huku analitaja jina la Mwenyezi Mungu haogopi?, Yaani ni mkavu kabisa na moyoni mwake ana amani kabisa kuwa alilofanya ni sawa?
Mzee Msekwa amesema kuwa uwepo wa akina Halima Mdee bungeni ni uvunjifu wa katiba ya nchi, Je Ndugai ameziba masikio kabisa na kushiriki uvunjifu mkubwa huu wa katiba bila wasiwasi wowote?
Nimkumbushe tu Ndugai, Jina la Mwenyezi Mungu huwa halichezewi, Hicho kiapo ulichokula kuwa utaheshimu sheria za nchi halafu ukazivunja makusudi huku Ukijua, basi jua Biblia uliyoikamata wakati unaapa na Mungu alishuhudia. Na imeandikwa katika maandiko USILITAJE BURE JINA LA MUNGU wako!
Ndugai, Waondoe hao wabunge 19 ambao unajua wazi wamo bungeni kinyume cha katiba, nje ya hapo kumbuka kiapo chako ulichoapa kwa kulitaja jina la Mungu.
Ndugu Ndugai, Mungu huwa hataniwi!