Kuelekea uchaguzi wa UWT: Bi Anne Kilango Malecela achafuliwa na wapinzani wake...

only83

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
5,343
2,525
....Katika kile kinachoonekana kama ni kuanza kwa mbio za uenyekiti wa UWT kati ya wagombea wakubwa wawili yaani Bi Anne Kilango na Bi Sophia Simba hali imeanza kuwa mbaya kwa Bi Anne Kilango. Taarifa zilizotoka leo zinadai kuwa Bi Anne Kilango amekusanya ameanza rafu kwa kukusanya pesa kiwango kikubwa kwa ajili ya kugawa takrima aka rushwa. Na fununu zinasema kuwa wanaume wengi wako nyuma yake kuliko hata wanawake na lengo ni kuhakikisha kuwa Bi Sophia Simba anang'olewa kwenye kiti kile.

....Itakumbukwa kuwa ugomvi na kusuguana kwa hawa wagombea wawili akujaanza leo wala jana, kumeanza tangu ambapo Bi Sophia Simba alipomtaja Bi Anne Kilango kama mchangiaji anayeropoka na anajifanya anatetea maslahi ya umma wakati harusi yake na Mzee Malecela ilichangiwa na mafisadi wakubwa. Hoja hii ilimfanya Mzee Malecela asimame na kuomba kuwa kuna wabunge wanapaswa wapelekwe mirembe akimlenge Bi Sophia Simba.

Source: Magazeti ya leo.

Habari zaidi:-

JUMATATU, AGOSTI 06, 2012 05:48 NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

WAKATI mbio za kuwania nafasi mbalimbali zikiendelea ndani ya Chama Cha Mapinduzi, hali ya mambo imeanza kubadilika. Kubadilika huko, kumeibuka ndani ya Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambapo mmoja wa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango baada ya kudaiwa kupewa kitita cha fedha na kampuni moja ya Kichina (jina tunalo).

Kampuni hiyo, ujenzi wa gati katika Bandari ya Dar es Salaam, inadaiwa kutoa kitita cha fedha, ili kuhakikisha Kilango, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge, anachaguliwa katika kwenye nafasi hiyo.

Kilango, ambaye hivi sasa amechukua fomu ya kuwania nafasi kwa ajili ya kugombea nafasi ya uenyekiti UWT), anatarajiwa kupambana na mwenyekiti wa sasa, Sophia Simba.

Kila mmoja wa wabunge ambao, wanasifika kwa kujipambanua kama wabunge wanapinga ufisadi ndani na nje ya Bunge.

Habari za kuamini zilizoifikia MTANZANIA, zinasema Kilango alianza kazi ya kuwafikia baadhi ya makatibu wa mikoa wa UWT na kuanza kuwashawi, ili wamchague katika nafasi ya Uenyekiti kwa ahadi ya kuondoa ukomo kwa wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM.

Chanzo hicho, kinasema baadhi ya makatibu wa mikoa ambao hakuwafikia alilazimika kuwapigia simu, ili wamuunge mkono, huku wale wote waliogoma kufanya hivyo, alitumia lugha kali.

Baadhi ya makatibu hao, waliiambia MTANZANIA na walikiri kupokea fedha kutoka kwa mbunge huyo, kama njia ya ushawishi katika harakati za kuwania nafasi hiyo.

Taarifa hizo, zinasema nguvu ya fedha ilianza kuonekana Machi 13-14 mkoani Dodoma, baada ya kuandaa semina kwa kukusanya wenyeviti wa wilaya na mikoa, waliokuwa wakihudhuria semina elekezi, kuelekea uchaguzi wa ndani na nafasi ya mwanamke katika kuwania uongozi.

Katika semina hiyo, inadaiwa mbunge huyo, alitumia nafasi hiyo hasa muda wa jioni kufanya ushawishi kwa viongozi wa mikoa na kuwataka kumchagua.

Viongozi hao, walisema wakati wa semina hiyo, Kilango alitumia nafasi hiyo na kueleza dhamira yake, huku akitoa vitisho hasa kwa watu wanaodaiwa kupewa Sh 30,000, kwa kila mmoja.

"Nguvu, aliyonayo mama Kilango, hivi sasa naye ni mmoja wa watu waliopata fedha kutoka kwa kampuni ya Kichina na baada ya kupata alianza kufanya ushawishi kwa wanawake wa UWT, hasa makatibu wa mikoa, lakini hivi sasa tutaona mwisho wake nini.

"Katika kikao cha Dodoma, nakumbuka tulikusanywa usiku na kupelekwa katika Hoteli ya Fity Six, iliyopo jirani na jengo la Bunge, na kuanza kutupatia kitu kidogo… baada ya hapo alituambia hela ya Mpare haiendi bure na kama ukiichukua na ukienda kinyume utakufa, tena akisema atatulisha yamini wote aliotupa fedha.

"Alisema Sophia Simba, hatakiwi na wabunge wanawake wa CCM, viongozi wa taifa na hata Rais nae hamtaki, hivyo achaguliwe yeye, kwani ana ushawishi ndani ya Kamati Kuu ya CCM (CC), na amekuwa akiungwa mkono na viongozi wote wa taifa," kilisema chanzo chetu.

MTANZANI ilipomtafuta Kilango, ili kupata ukweli juu ya tuhuma hizo, alimtaka mwandishi wa habari hizi kuandika chochote anachokijua dhidi yake.

Mahojiano kati ya MTANZANIA na mbunge Kilango, yalikuwa kama ifuatavyo;

MTANZANIA: Habari mama Kilango na pole na majukumu.

Kilango: asante na nani mwenzangu.

MTANZANI: ninaitwa …. kubwa nilitaka kufahamu ukweli juu ya tuhuma zinazokukabili kuhusu madai ya kupewa hongo na kampuni moja ya Kichina (jina tunalo), je suala hili lina ukweli wowote?

Kilango: kijana nasema hivi, andika habari zote kama ulivyosikia, ili Watanzania wajue uchafu wangu," alisema Kilango na kukata simu.


 
....Katika kile kinachoonekana kama ni kuanza kwa mbio za uenyekiti wa UWT kati ya wagombea wakubwa wawili yaani Bi Anne Kilango na Bi Sophia Simba hali imeanza kuwa mbaya kwa Bi Anne Kilango. Taarifa zilizotoka leo zinadai kuwa Bi Anne Kilango amekusanya ameanza rafu kwa kukusanya pesa kiwango kikubwa kwa ajili ya kugawa takrima aka rushwa. Na fununu zinasema kuwa wanaume wengi wako nyuma yake kuliko hata wanawake na lengo ni kuhakikisha kuwa Bi Sophia Simba anang'olewa kwenye kiti kile.

....Itakumbukwa kuwa ugomvi na kusuguana kwa hawa wagombea wawili akujaanza leo wala jana, kumeanza tangu ambapo Bi Sophia Simba alipomtaja Bi Anne Kilango kama mchangiaji anayeropoka na anajifanya anatetea maslahi ya umma wakati harusi yake na Mzee Malecela ilichangiwa na mafisadi wakubwa. Hoja hii ilimfanya Mzee Malecela asimame na kuomba kuwa kuna wabunge wanapaswa wapelekwe mirembe akimlenge Bi Sophia Simba.

Source: Magazeti ya leo.

kwani ni uongo? na sasa hivi anatuhumiwa na kuomba rushwa, Anna Kilango ni fisadi hana jipya anyway magamba mtajiju!
 
ww mtoa mada unaonekana kbs ni mpambe wa Sophia Simba na umetumwa hpa...........

wte ni magamba tu.............. simba + kilango = zero
 
Sophia Simba alitumia vibaya nafasi yake alipokuwa waziri anayehusika na mambo ya usalama.Alipitia mafaili na kapata nyepesi nyepesi za Malecela na kama kawaida ya wanawake wa Uswahilini alipoguswa kidogo akaropoka.
 
ndio siasa ilivyo, full kuchafuana mpaka mambo ya ndani.
 
Angel msofe niko pamoja na wewe pwagu na pwaguzi! Woote uozo mtupu, sera yao kubwa inajurikana ni rushwa kwenda mbele!
 
Wanajuana hawa wote mafisadi tu hakuna wa kumfunga paka kengele...wezi wakubwa.
 
Mmoja ni afadhali na mwingine ni potelea mbali. Watachagua wenyewe magamba yupi afadhali na yupi potelea mbali.
 
ww mtoa mada unaonekana kbs ni mpambe wa Sophia Simba na umetumwa hpa...........

wte ni magamba tu.............. simba + kilango = zero

Hata kama atakuwa mpambe au la, ukweli ndo huo.. Anne Kilango alikuwa anabwabwaja mwanzoni tukadhani mkombozi kumbe zilikuwa hasira za mumewe kukosa uteuzi wa ubunge nk.... alikuwa anapigania maslahi binafsi... sasa hivi ameshashtukiwa!!! hafai hana uzalendo wowote.. anapigania vya tumbo lake tu!!
 
Hata kama atakuwa mpambe au la, ukweli ndo huo.. Anne Kilango alikuwa anabwabwaja mwanzoni tukadhani mkombozi kumbe zilikuwa hasira za mumewe kukosa uteuzi wa ubunge nk.... alikuwa anapigania maslahi binafsi... sasa hivi ameshashtukiwa!!! hafai hana uzalendo wowote.. anapigania vya tumbo lake tu!!

si kilango tu,hata yule mzee wa RIPOT YA RICHMOND NA OLE S
 
Swali kwa wafurukutwa wa ccm, hivi huko uwt hakuna mwanamke mwingine mnayeweza kumpatia uenyekiti zaidi ya hawa waganga njaa??
au ndio aina ya wanawake mlionao ndani ya chama chenu, kwahiyo wote wanafanana tabia na mienendo yao?
 
kama Anne kilango na Sophia Simba tunaona hawatoshi kwa nini tusimjadili zaidi yule wa tatu nadhani anaitwa MaryRose aliletwa hapa na PASCO? ndio njia pekee ambayo itatusaidia kuwajua wagombea wote na kisha kuchagua iliye bora.

hakuna jambo baya kuelekea kwenye uchaguzi kama kutumia muda mwingi kujadili wagombea wasiotosha na kuwasahua wanaotosha.
 
[h=2][/h]JUMATATU, AGOSTI 06, 2012 05:48 NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

WAKATI mbio za kuwania nafasi mbalimbali zikiendelea ndani ya Chama Cha Mapinduzi, hali ya mambo imeanza kubadilika. Kubadilika huko, kumeibuka ndani ya Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ambapo mmoja wa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango baada ya kudaiwa kupewa kitita cha fedha na kampuni moja ya Kichina (jina tunalo).

Kampuni hiyo, ujenzi wa gati katika Bandari ya Dar es Salaam, inadaiwa kutoa kitita cha fedha, ili kuhakikisha Kilango, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu ya Bunge, anachaguliwa katika kwenye nafasi hiyo.

Kilango, ambaye hivi sasa amechukua fomu ya kuwania nafasi kwa ajili ya kugombea nafasi ya uenyekiti UWT), anatarajiwa kupambana na mwenyekiti wa sasa, Sophia Simba.

Kila mmoja wa wabunge ambao, wanasifika kwa kujipambanua kama wabunge wanapinga ufisadi ndani na nje ya Bunge.

Habari za kuamini zilizoifikia MTANZANIA, zinasema Kilango alianza kazi ya kuwafikia baadhi ya makatibu wa mikoa wa UWT na kuanza kuwashawi, ili wamchague katika nafasi ya Uenyekiti kwa ahadi ya kuondoa ukomo kwa wabunge wa Viti Maalum kupitia CCM.

Chanzo hicho, kinasema baadhi ya makatibu wa mikoa ambao hakuwafikia alilazimika kuwapigia simu, ili wamuunge mkono, huku wale wote waliogoma kufanya hivyo, alitumia lugha kali.

Baadhi ya makatibu hao, waliiambia MTANZANIA na walikiri kupokea fedha kutoka kwa mbunge huyo, kama njia ya ushawishi katika harakati za kuwania nafasi hiyo.

Taarifa hizo, zinasema nguvu ya fedha ilianza kuonekana Machi 13-14 mkoani Dodoma, baada ya kuandaa semina kwa kukusanya wenyeviti wa wilaya na mikoa, waliokuwa wakihudhuria semina elekezi, kuelekea uchaguzi wa ndani na nafasi ya mwanamke katika kuwania uongozi.

Katika semina hiyo, inadaiwa mbunge huyo, alitumia nafasi hiyo hasa muda wa jioni kufanya ushawishi kwa viongozi wa mikoa na kuwataka kumchagua.

Viongozi hao, walisema wakati wa semina hiyo, Kilango alitumia nafasi hiyo na kueleza dhamira yake, huku akitoa vitisho hasa kwa watu wanaodaiwa kupewa Sh 30,000, kwa kila mmoja.

“Nguvu, aliyonayo mama Kilango, hivi sasa naye ni mmoja wa watu waliopata fedha kutoka kwa kampuni ya Kichina na baada ya kupata alianza kufanya ushawishi kwa wanawake wa UWT, hasa makatibu wa mikoa, lakini hivi sasa tutaona mwisho wake nini.

“Katika kikao cha Dodoma, nakumbuka tulikusanywa usiku na kupelekwa katika Hoteli ya Fity Six, iliyopo jirani na jengo la Bunge, na kuanza kutupatia kitu kidogo… baada ya hapo alituambia hela ya Mpare haiendi bure na kama ukiichukua na ukienda kinyume utakufa, tena akisema atatulisha yamini wote aliotupa fedha.

“Alisema Sophia Simba, hatakiwi na wabunge wanawake wa CCM, viongozi wa taifa na hata Rais nae hamtaki, hivyo achaguliwe yeye, kwani ana ushawishi ndani ya Kamati Kuu ya CCM (CC), na amekuwa akiungwa mkono na viongozi wote wa taifa,” kilisema chanzo chetu.

MTANZANI ilipomtafuta Kilango, ili kupata ukweli juu ya tuhuma hizo, alimtaka mwandishi wa habari hizi kuandika chochote anachokijua dhidi yake.

Mahojiano kati ya MTANZANIA na mbunge Kilango, yalikuwa kama ifuatavyo;

MTANZANIA: Habari mama Kilango na pole na majukumu.

Kilango: asante na nani mwenzangu.

MTANZANI: ninaitwa …. kubwa nilitaka kufahamu ukweli juu ya tuhuma zinazokukabili kuhusu madai ya kupewa hongo na kampuni moja ya Kichina (jina tunalo), je suala hili lina ukweli wowote?

Kilango: kijana nasema hivi, andika habari zote kama ulivyosikia, ili Watanzania wajue uchafu wangu,” alisema Kilango na kukata simu.


 
Back
Top Bottom