Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
Wengi watashangazwa na huu uzi.
Nimekuwa nakosoa tena kwa lugha kali utendaji wa hovyo usiozingatia uhalisia hususani kuanzia awamu hii ya sita.
Tembea uone.
Nilifanikiwa kutembelea soko la Machinga pale mji mkuu Dodoma, nilijihakikishia kuwa plan na ukamilishwaji wa mradi wa soko hilo la Machinga umefanikiwa kwa kiasi kukubwa.
Sijajua kwa undani soko hilo likikamilika linapaswa liweje lakini kwa kila Mtanzania na mgeni anayetembelea atakubaliana nami kuwa soko hilo linaweza kuwa la kisasa kwa afrika mashariki na kati.
Nimekuta wamachinga wamepangwa vizuri, alama za wapi utakuta aija ya bidhaa unazotafuta zinaonekana kwa uwazi. Zimeandikwa kwa lugha yetu tukuka ya kiswahili ambapo ni uamuzi wa dhahabu. Usafi wa soko na hata huduma mbalimbali muhimu kwa machinga na wanunuzi zipo. Nimekuta lipo eneo limetengwa ndani ya soko la wamama kunyonyeshea, kuna ATM, store, vyoo vizuri. Maeneo ya baba na mama lishe yametengwa vizuri hata sehemu za nyama choma nje ya soko zinashawishi kwani meza za wateja ni za marble ambazo zinadumu kuliko mabati na mbao.
Kelele ndani ya soko zimedhibitiwa ambapo wenye vipaza sauti hawaruhusiwi kufungulia sauti kubwa.
Kuhusu usafiri, soko limejengwa pembezoni mwa barabara kuu huku kukiwa na kituo kikubwa cha daladala kuelekea maeneo mengi ya jiji la dodoma. Kimsingi serikali imewatendea haki wamachinga kwani imeamua kuwaweka mahala sahihi ambapo haimlazimishi mteja kwenda umbali mrefu kutafuta petty goods. Nilimuuliza mmachinga mmoja wanalipa kiasi gani kwa siku akasema wanalipa Tshs 1,000 na akaenda mbali zaidi kuwa anaiona ni fair kwa sababu soko halikauki wateja pia alilinganisha na eneo lake la biashara pale Kariakoo aliloamuq kuachana nalo kwa sababu hata hrla wlizokuwa wanatoa kwa jiji hazikuzuia harassments za mgambo na kukithiri kwa uchafu.
Tofauti na majiji mengine kama Dar, wamachinga wanaondolewa maeneo potential kwao na kutupwa nje pembezoni mwa mji ambapo hata miundombinu kama vyoo, umeme , usafiri vinakuwa ni taabu.
Kwa mfano pale Kariakoo wangechukua mfumo wa soko la Machinga Dodoma hakika wangeweza kukidhi takwa la serikali kuwakusanya machinga na hata wakachangia pato la jiji kwa tozo watakazolipa. Serikali inaweza kuongea na NHC wakapanua eneo lile kulifanya liwe efficiency kwa biashara.
Pale Mbagala Zakhiem kuna utopolo umejengwa ambapo wamachinga hawatakuwa na nafasi zaidi ya wafanyabishara wenye msuli wa fedha.
Kwenye hili soko la Machinga Dodoma, tuungane kumpongeza Mama Samia kwa sababu amefanikiwa kuwapatia machinga sehemu stahiki kwa shughuli zao. Pia kama ikipendeza masoko kama haya yajengwe kwenye majiji hapa nchini na kuangalia pale Mbezi Mwisho kujenga soko la Machinga la kisasa ili kuongeza wigo wa nchi jirani kuja kununua bidhaa kama wanavyofanya Kariakoo na Mbagala.
Muwe na weekend njema
CC: Pascal Mayalla ChoiceVariable bubex_jr johnthebaptist emback Ne91cM Mzee Mwanakijiji Dr. Mariposa Dr Matola PhD FaizaFoxy Mohamed Said
Nimekuwa nakosoa tena kwa lugha kali utendaji wa hovyo usiozingatia uhalisia hususani kuanzia awamu hii ya sita.
Tembea uone.
Nilifanikiwa kutembelea soko la Machinga pale mji mkuu Dodoma, nilijihakikishia kuwa plan na ukamilishwaji wa mradi wa soko hilo la Machinga umefanikiwa kwa kiasi kukubwa.
Sijajua kwa undani soko hilo likikamilika linapaswa liweje lakini kwa kila Mtanzania na mgeni anayetembelea atakubaliana nami kuwa soko hilo linaweza kuwa la kisasa kwa afrika mashariki na kati.
Nimekuta wamachinga wamepangwa vizuri, alama za wapi utakuta aija ya bidhaa unazotafuta zinaonekana kwa uwazi. Zimeandikwa kwa lugha yetu tukuka ya kiswahili ambapo ni uamuzi wa dhahabu. Usafi wa soko na hata huduma mbalimbali muhimu kwa machinga na wanunuzi zipo. Nimekuta lipo eneo limetengwa ndani ya soko la wamama kunyonyeshea, kuna ATM, store, vyoo vizuri. Maeneo ya baba na mama lishe yametengwa vizuri hata sehemu za nyama choma nje ya soko zinashawishi kwani meza za wateja ni za marble ambazo zinadumu kuliko mabati na mbao.
Kelele ndani ya soko zimedhibitiwa ambapo wenye vipaza sauti hawaruhusiwi kufungulia sauti kubwa.
Kuhusu usafiri, soko limejengwa pembezoni mwa barabara kuu huku kukiwa na kituo kikubwa cha daladala kuelekea maeneo mengi ya jiji la dodoma. Kimsingi serikali imewatendea haki wamachinga kwani imeamua kuwaweka mahala sahihi ambapo haimlazimishi mteja kwenda umbali mrefu kutafuta petty goods. Nilimuuliza mmachinga mmoja wanalipa kiasi gani kwa siku akasema wanalipa Tshs 1,000 na akaenda mbali zaidi kuwa anaiona ni fair kwa sababu soko halikauki wateja pia alilinganisha na eneo lake la biashara pale Kariakoo aliloamuq kuachana nalo kwa sababu hata hrla wlizokuwa wanatoa kwa jiji hazikuzuia harassments za mgambo na kukithiri kwa uchafu.
Tofauti na majiji mengine kama Dar, wamachinga wanaondolewa maeneo potential kwao na kutupwa nje pembezoni mwa mji ambapo hata miundombinu kama vyoo, umeme , usafiri vinakuwa ni taabu.
Kwa mfano pale Kariakoo wangechukua mfumo wa soko la Machinga Dodoma hakika wangeweza kukidhi takwa la serikali kuwakusanya machinga na hata wakachangia pato la jiji kwa tozo watakazolipa. Serikali inaweza kuongea na NHC wakapanua eneo lile kulifanya liwe efficiency kwa biashara.
Pale Mbagala Zakhiem kuna utopolo umejengwa ambapo wamachinga hawatakuwa na nafasi zaidi ya wafanyabishara wenye msuli wa fedha.
Kwenye hili soko la Machinga Dodoma, tuungane kumpongeza Mama Samia kwa sababu amefanikiwa kuwapatia machinga sehemu stahiki kwa shughuli zao. Pia kama ikipendeza masoko kama haya yajengwe kwenye majiji hapa nchini na kuangalia pale Mbezi Mwisho kujenga soko la Machinga la kisasa ili kuongeza wigo wa nchi jirani kuja kununua bidhaa kama wanavyofanya Kariakoo na Mbagala.
Muwe na weekend njema
CC: Pascal Mayalla ChoiceVariable bubex_jr johnthebaptist emback Ne91cM Mzee Mwanakijiji Dr. Mariposa Dr Matola PhD FaizaFoxy Mohamed Said