Jamani,
Hivi FISADI ni nani? Mnaowaita Mafisadi mna ushaidi nao wa kimahakama, au ni kwa sababu tu mfanyabiashara mmoja mashuhuri aliyejawa na chuki na anayependa umaarufu, anadai hivyo? Hivi fisadi ni yule ambaye baadhi ya Wabunge waliokosa nafasi katika vyombo vya dola, waliojaa gele na chuki, wanaona hivyo? Nani mwenye ushahidi, unaofaa mahakamani? Hata hao ambao wamefikishwa Mahakamani kwa hizo tuhuma za ufisadi bado hata hawajahukumiwa lakini baadhi ya watu wazuri na waadilifu wanahukumiwa na watu katika magazeti na kwenye blogu! Wewe mbona ukiitwa fisadi unaruka, je mbona mnawataja baadhi ya viongozi kuwa ni mafisadi kwa uashahidi usio na uhakika kama wa Kamati Teule ya Bunge, ambayo sasa inabainika, kila kukicha, kuwa ilitoa mapendekezo kwa chuki na fitina za kisiasa badala ya uhalisia wa mambo?
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu, FISADI ni:-mbaya, mtongozaji, mharibifu, mpotevu, muasherati, k.v. guberi; GUBERI naye ni:- malaya. mfanya visa kiayari, mjanja; AYARI naye ni:-mtu mdanganyifu, mwongo, laghai, mzushi!
Sasa nani fisadi, kwa tafsiri huiyo sanifu? Ni Lowassa? Lowassa kweli anaweza kuitwa fisadi? Je, mfanyabiashara fulani mashuhuri ambaye aliachana na mke wake, aliachana na mke mdogo na sasa ana binti mwingine (Kanisa lake linajua, siyo uzushi) anayemzidi umri kwa miaka 50 hivi, anayewadanganya na kuwazuga wafanyakazi wake(wengine wamemkimbia!), anaghilibu watu (mara anaisaidia Chadema, mara ni mwana-CCM safi!), anayetumia vyombo vyake kuwaandama watu asiowapenda au wanaomzidi kete kibiashara, anayewadanganya mabalozi wa nje na anayeona fahari kufanya hivyo, utamuitaje? Tuseme ukweli jamani, tuache porojo na fitina za kisiasa! Tutakuwa hatufiki kokote, kinchi na tutakuwa wanafiki wakubwa!
Bwassa