Ingawa sasa CCM ndiyo habari ya mjini, Dr. Wilbrod Peter Slaa asisahaulike. Ingawa mchakato wa kutangaza nia ndani ya CCM umeteka kilamedia hapa nchini, Dr. Slaa ni mwiba mkali kwa CCM yetu kama akiridhiwa na UKAWA kupeperusha bendera yao hapo Oktoba.
Kwa mwitikio anaoupata kwenye mikutano ya UKAWA huko apitapo na ninayoyaona humu nitembeapo,Dr. Slaa ni silaha tegemezi ya UKAWA.
CCM iwe pamoja au iwe vipandevipande baada ya mchakato wa ndani wa kumpata mgombea wetu, Dr. Slaa hatatetereka wala kuimarika.Atabaki kama alivyo: imara as ever. Iko wazi kuwa Dr. Slaa ana mtaji kuanzia safari yake ya Oktoba endapo UKAWA wakimpitisha.
Anaweza kubezwa na kukejeliwa lakini yeye ni mwanasiasa wa kufanyiwa maandalizi ya kutosha. Mgombea yeyote wa CCM na wengineo angetamani kikombe cha Dr. Slaa kimuepuke.
Yupo kwenye kumbukumbu ya watanzania kama mwanasiasa aliyethubutu kupambana na mafisadi,kwa vitendo, kwakuanika a List of Shame pale Mwembeyanga-Temeke, orodha ya mafisadi inayojidhihirisha kila kukicha.
Niseme tu, Dr. Slaa is one of the most complete politicians from the opposition. He is, normally, slow but sure! Hata asipokuwa mgombea wa UKAWA, atakuwa kiungo muhimu kwenye timu ya UKAWA.
Nitasema ukweli daima, fitina kwangu ni mwiko!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kwenda Tabora)