Hizi pilika pilika za uwingi wa Watu kutaka kujiandikisha katika Daftari la mpiga Kura kwa mtazamo wangu sio kwa ajiri ya kupiga Kura bali ni kutafuta Vitambulisho baada ya hapo hali itatulia kama hakuna kilichotokea, CCM ipo imefundishwa Mashuleni na Vyuoni kwa hiyo ipo Masikioni na Midomoni mwa Watu wengi kwa hiyo inafahamika na wengi UKAWA ni kitu kigeni miongoni mwa Watu vivyo hivyo Dr. Slaa, bado haijafanyika juhudi ya kutosha kumnadi na kuwaaminisha Watanzania kwamba anafaa kuliongoza Taifa hili.
Nasema hivi kwa sababu mbali ya Fitina za kisiasa walizonazo CCM sijaona Weledi hasa toka UKAWA juu ya kupambana na CCM, ninachokiona ni Misuguano ya chini chini katika yao juu ya Maslahi. Lakini pia Demokrasia ya namna ya kumpata Mgombea toka UKAWA haijawekwa wazi bado Watu wawili tu Lipumba na Slaa ndiyo wanatajwa kama vile hakuna watu wengine hili ni tatizo, wakati fulani Lissu aliwahi kuzungumza kwamba nae anautaka Urais inaelekea katishwa asiseme tena yupo kimya na hakuna mjadala kumuhusu tena.
Siasa ina mambo mengi kuna makundi ya wapiga Kura bado sijaona Jitihada za UKAWA za kufikia hayo makundi hata tukisema kwamba nchi yetu haina UDINI lakini DINI zipo na Makabila yapo Mikoa ipo na Kanda zipo, tumeona kilichotokea Mbeya wakati Mwandosya akitangaza NIA Vyama vyote vilimuunga mkono kwa hiyo Mchakato bado ni Mgumu ni suala la kusubiri lakini ukweli bado CCM wana nafasi kama watachanga vizuri karata zao