Slaa: Kikwete akipuuza nchi haitatawalika

Mimi nafikiri ni kipindi cha Dr Slaa kujipanga tena kwa ajili ya 2015. Na kuacha kabisa kuchochea wanachama na wapenzi wa chama chake kufanya hujma kwa serikali iliyopo madarakani kwa ajili ya manufaa ya nchi yenu na wananchi wake.

Hakika uchochezi sio mzuri kwa mustakabali wa nchi yenu. Hakika amani ya nchi enu inategemea busara zenu viongozi kwa wanachama wenu.

Fuata za maalim Seif kwa Znz na waZnz.

Kawachochea lin na wapi? ugumu wa maisha ndo unasababisha yote haya Dr. hata hahusiki? cku zote mwenye shibe hamjui mwenye njaa, so km tumbo limejaa kaa kimya mkuu, cjui km kwasasa upo Tanzania ndo ujionee hali ilvyo, wagonjwa wanakufa mahospitalini km kuku Dr. Slaa anahusikaje? crap
 
Ni hali ngumu tu ya utashi wa utatuzi wa mambo yanayolikabili taifa na kuangalia vipao mbele vya taifa.
 
Cha msingi tuendelee kuwakataa viongozi hawa na serikali yao na chama chao,na tujitokeze waziwazi kukataa kila tunapoona wanakiuka haki za binadamu hasa wanapozidi kuendeleza mauaji ya wananchi,na siku hizi mauaji ya raia ni jambo la kawaida sana kufanywa na polisisiemu na serikali yake na wala hakuna anayehoji wala kuchukua hatua ndani ya serikali na wala CCM magamba hawajawahi kukemea mauaji na uonevu wote unaofanywa na serikali ya CCM-magamba
 
Tanzania ni nyepesi sana na wananchi wake tupo tupo tu ndiyo mana ccm inafanya lolote wawezalo wakijua na kuamin kuwa hatuna lolote la kuwafanya.
 
Siwapendi ccm kutoka moyon. Makamanda mje moro huku watu wamelala usingizi wa pono wanahitaji kuelimishwa.
 
Mapinduzi ya Libya yalianzishwa na mpigania haki aliyekuwa akitetea haki za ndugu wa wale waliouwawa kwenye maandamano ya waislam, yale ya kupinga ile katuni ya udhalilishaji wa mtume wao.

Serikali ni kweli kuwa lazima iwe makini.

Gaddafi alidhani west wangemsapoti kwasababu wale walikuwa ni mujahedeen, na yeye alisema walikuwa alkaeda, hakusikilizwa licha ya kwamba kuna ukweli kwenye madai yake.

Cha msingi hapa ni haki ya raia, unauwa raia wenye kuandamana?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mapinduzi ya Libya yalianzishwa na mpigania haki aliyekuwa akitetea haki za ndugu wa wale waliouwawa kwenye maandamano ya waislam, yale ya kupinga ile katuni ya udhalilishaji wa mtume wao.

Serikali ni kweli kuwa lazima iwe makini.

Gaddafi alidhani west wangemsapoti kwasababu wale walikuwa ni mujahedeen, na yeye alisema walikuwa alkaeda, hakusikilizwa licha ya kwamba kuna ukweli kwenye madai yake.

Cha msingi hapa ni haki ya raia, unauwa raia wenye kuandamana?
Si kuandamana tu walikuwa wanadai serikali yao iwalinde badala yake wakatandikwa risasi.
 
Mapinduzi ya Libya yalianzishwa na mpigania haki aliyekuwa akitetea haki za ndugu wa wale waliouwawa kwenye maandamano ya waislam, yale ya kupinga ile katuni ya udhalilishaji wa mtume wao.

Serikali ni kweli kuwa lazima iwe makini.

Gaddafi alidhani west wangemsapoti kwasababu wale walikuwa ni mujahedeen, na yeye alisema walikuwa alkaeda, hakusikilizwa licha ya kwamba kuna ukweli kwenye madai yake.

Cha msingi hapa ni haki ya raia, unauwa raia wenye kuandamana?

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba kiongozi wa nchi ambaye anatakiwa kuhakikisha usalama wa Watanzania hatatia neno kufuatia kuuawa kinyama kwa Watanzania hawa. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi~AMEN
 
Ee Mwenyezi Mungu ilinde nchi yetu Tanzania inaangamia kwa kukosa kiongozi bora!!
 
Kinachosikitisha zaidi ni kwamba kiongozi wa nchi ambaye anatakiwa kuhakikisha usalama wa Watanzania hatatia neno kufuatia kuuawa kinyama kwa Watanzania hawa. Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi~AMEN
Hivi hata Waziri wa mambo ya ndani naye hajatoa kauli au ndio wanasubiri tume?
 
Historia inatakiwa itufundishe lakini mmm! wengi wetu ni viziwi. Hebu tujikumbushe kidogo tarehe 25 December, 1989 wananchi wa Romania walipomchoka aliyekuwa Kiongozi wao Nikolai Ceusesku pamoja na mkewe Elena.



Iko siku!

 
Last edited by a moderator:
Historia inatakiwa itufundishe lakini mmm! wengi wetu ni viziwi. Hebu tujikumbushe kidogo tarehe 25 December, 1989 wananchi wa Romania walipomchoka aliyekuwa Kiongozi wao Nikolai Ceusesku pamoja na mkewe Elena.



Iko siku!


Nakumbuk alikuwa tu ametoka ziarani nchini Tanzania. Nakumbuka kumpungia mkono pale msimbazi roundabout. Mkuu watu wake walikuwa wamezichoka siasa za kikomunist na walichochewa na kuanguka kwa USSR; sijui kama ina uhusiano na huu uzi.
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuk alikuwa tu ametoka ziarani nchini Tanzania. Nakumbuka kumpungia mkono pale msimbazi roundabout. Mkuu watu wake walikuwa wamezichoka siasa za kikomunist na walichochewa na kuanguka kwa USSR; sijui kama ina uhusiano na huu uzi.
Hapana Mkuu, Soviet union ilianguka miaka miwili baada ya mapinduzi ya Romania. Somo nililotaka kulitoa ni kuwa ilifika wakati ambapo hata jeshi lake alilolitumia kukandamiza watu wake waliweka silaha chini na kusalimu amri kwa Umma. Huko ndiko tunakoelekea kwa hivi sasa - hata mbwa iko siku anaweza kumgeuka bwanake na kumng'ata!
 
Dk. Slaa akizungumza kwa uchungu alisema mauaji ya Songea yalitokana na uzembe wa hali ya juu wa viongozi wa serikali na vyombo vya dola ngazi ya wilaya na Mkoa wa Ruvuma.

"Napenda kutoa kauli juu ya mauaji dhidi ya raia yaliyofanywa na Jeshi la Polisi huko Songea. Kwa taarifa nilizonazo, mauaji yale yametokea kwa sababu ya uzembe wa hali ya juu na ufinyu tu wa akili ya viongozi, akiwamo mkuu wa Mkoa na polisi wale. Hivi unawaambiaje raia wenye uchungu na vifo vya wananchi wenzao, waliojikusanya na kuamua kuandamana kudai haki, eti wachague kiongozi wa kuonana na mkuu wa mkoa," alisema.

Aliitaka serikali kuunda tume huru ya kuchunguza mauaji hayo ya Songea na kudai kuwa hakuna uhalali wowote wa viongozi wa serikali wa mkoa ambao ni watuhumiwa wa mauaji hayo kuunda chombo cha kuchunguza.

"Tunawapongeza wananchi na hasa vijana wa Songea kwa kuandamana kudai haki. Tunataka ufanyike uchunguzi huru juu ya mauaji hayo, yatakayoihusisha mahakama (Korona) na mkuu wa mkoa na polisi hawana uhalali wa kuunda tume za kuchunguza kwani wao pia ni watuhumiwa katika tukio hilo," alisema.

Katibu mkuu huyo wa CHADEMA alilaani tukio la juzi usiku, ambapo polisi katika mji wa Tunduma wanadaiwa kushusha bendera za chama hicho katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

Alisema kitendo hicho ni uchokozi tosha kwa CHADEMA na kimelenga kuleta fujo nyingine zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani.

"Niliwasiliana na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, pia mkuu wa mkoa, niliwaambia mimi sipendi kugombana nao kwa masuala ya hovyo kama hayo, tupo kwa mujibu wa sheria, bendera zetu zinatokana na kodi za Watanzania, wakasema eti zingine ziko sokoni, nikawauliza za CCM huwa zinawekwa wapi?

"Watu hawana maji, hawana zahanati, elimu inashuka, mkuu wa wilaya hajawahi kuamuka usiku, lakini kwenye kushusha bendera za CHADEMA wanaamka usiku wa manane," alisema.


DR. SLAA ni zaidi ya Rais kwa kazi azitendazo. I'm very impressed with his bolded quotes.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom