Slaa awalipua Rostam, Riziwan

Slaa awalipua Rostam, Riziwan

siezi bishana nawe bana umeongea point.ndo maana siwamini wanasiasa.alikuepo obama akajidai mtu wa wanyonge kumbe mnafiki mkubwa.anapokea amri kutoka kwa mabanker,oil companies kama agip,chevron,military industries complex wanaenedesha vita ili silaha ziuzwe na makampuni ya mafuta yapate contracter,huku makampuni ya kina dick chen ,HALIBUTON yakipata tenda za kusupply jeshini kuanzia magari,chakula hadi uniform,itakua hapa.we need evidence

Du kweli bwana kumbe hata akina Lowassa,RA,Chenge watakuwa wameonewa tu, na hakuna wizi ndani ya CCM! Kumekucha kweli ila tutafika tu
 
mijitu mingine bwana HOVYO,hivi hadi leo bado kuna watu hawajaamini kuwa mabadiliko yote haya yakiwemo kujivua gamba ni harakati za Dr Slaa tangu akiwa bungeni hadi sasa ,,kama TAKUKURU ni wasikivu wafwatilie watupe ukweli, DR KISHASEMA
 
Huyo dogo ametumia mgongo wa baba yake kufisadi taifa! Kwani pale IMMA mshahara wake ulikuwa wakawaida tu na alishatimuliwa, sasa hebu tujiulize dunia kote hakuna kijana aliyezaliwa ktk familia masikini halafu ndani ya miaka miwili tangu amalize masomo akawa bilionea! Hapa kuna kitu!

Hata kama mshahara wake ukitajwa still bado kuna haja ya kujiuliza within a short period of time? And esp During the election time alikuwa ndio mkuu wa fungu la baba yeye na mdogo wake kwani mwakumbuka dhahili campeni za mwaka jana za ubunge na urais zijawa na tatizo la Familiarize sasa hao vijana kwanini wapikwapue pesa hiyo kutembea mikoa yote na kuwaweka makada wa CCM si mchezo na sio wote kawamaliza lazima change ilibaki.

Kwa kawaida tuuu taya Ridhwani shemeji yangu ajitoe tu kwenye UVCCM kimaadili ukisha kumbwa na kashifa kama hiyo period ur dead in politics sasa nae mwisho wake ndio huo , Mwingine ni Mtoto wa EL huko Arusha kwa jina linalo anzia na E nayeye je mwisha chunguza pesa zake je ni mali ya kurithi au ni mali ya baba?

Wajua huwa najiuliza hawa vijana wadogo ndani ya UVCCM wanakuwa na kiburi sana na jeuri na pesa wamezitoa wapi ni vijna wa juzi tuu hapa vyuo wamemaliza hajazidi 3yrs jamani khaaa na ndio maana UVCCM inayumba sana na inamatatizo makubwa hata kuliko ya UWT,CCM

 
Slaa ni kiongozi ambaye tunamhitaji sana.. Ana uchungu na nchi sio wale wavua magamba wanao tuhadaa kwa kuvua magamba lakini sumu bado ni ileile.
 
Mdau ungetupa walau kwa ufupi huo 'utajiri mkubwa' unaanzia wapi hadi wapi. Hizi statement za jumla jumla zina kama harufu ya majungu hivi! Yaani tuambie kwa mfano, Mzee wa Kijiji ana nyumba sabini, magari ya kifahari 20, viatu jozi mia, nk. Anayesoma anajua kweli huu ni utajiri mkubwa. Lakini kusema tu dogo Ridhwani ni tajiri mkubwa haina tofauti na wale vijana wa kijiweni waliomzushia Nyerenere kuwa ana viwanda vya meli Sweden!
Usijifanye juha eti hujui maana ya tajiri.
 
Huyu majuzi tu alikuwa hana kitu kabisa alipokuwa anamaliza shule yake,sasa ni fisadi kijana.Abanwe.
 
Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

Alisema mapato ya Rostam kwa mwaka yanafikia sh bilioni 280, hivyo TAKUKURU haina budi kumkamata na kumchunguza kwani aliwahi kutangaza kuwa hana shida ya kuwa kiongozi au kung’ang’ania madaraka yoyote, kwani pesa alizonazo zinamtosha.
source: Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam



Alipotakiwa kueleza iwapo yeye ni mmoja wa watu wanaotarajia kufaidika na malipo ya shilingi bilioni 185 ambazo TANESCO inatakiwa kuilipa fidia Dowans, mfanyabiashara huyo alikana kuimiliki kampuni hiyo.


Mbali ya kukanusha hilo, Rostam aliyabeza madai ya baadhi ya wanasiasa wanaohusisha fedha hizo na yeye akisema katika mkusanyiko wa biashara zake anazofanya ndani na nje ya nchi kiasi hicho cha fedha wanazotarajiwa kulipwa Dowans ni sawa na mapato yake ya miezi minne tu.

source: Rostam Aziz aikana Richmond

Sasa KIPYA KIPI alichofichua huyo mzinifu? Mwenyewe ameshapata kusema kuwa billioni 185 ni kipato chake cha miezi minne, i.e. kipato chake cha mwaka ni billioni 185 x 3 = billioni 555.

Halafu hayo madai ya neno UFISADI kalianzisha yeye ndiyo kichekesho cha mwaka!!!!! Kwiiiiiiiii kwi kwi!!!!!!

Hivi kelele na maandamano ya katiba mpya, hali ngumu ya maisha, noti mpya yameishia wapi? Yaani yote hayo sasa yamewekwa pembeni na sasa ni kuwa wao ndiyo walioanzisha neno fisadi?
 
Watu mnakazania eti aende mahakamani,mahakama zipi hizo mnazoziongelea hizi hizi zinazopendelea watawala na wawekezaji mchana kweupe?! Kama tunadhani ni 'haki' kwa mtoto wa Rais ambaye hatujui biashara anazofanya hapa duniani kuwa bilionea halafu asiulizwe basi demokrasia tuyaipigia kelele tunayo basi haipo kabisa..

Sidhani kama ni 'husda' kuwahoji watu wanaokula na kuvaa kwa kodi zetu kisa ni watoto wa Rais ni wajibu wao na wetu kuhakikisha kodi zetu hazibadhirifiwi kwa namna yoyote ile na wakibainiki wataanikwa mpaka hatua za uwazi na sahihi zichukuliwe juu ya wote wanaohusika..
 
mijitu mingine bwana HOVYO,hivi hadi leo bado kuna watu hawajaamini kuwa mabadiliko yote haya yakiwemo kujivua gamba ni harakati za Dr Slaa tangu akiwa bungeni hadi sasa ,,kama TAKUKURU ni wasikivu wafwatilie watupe ukweli, DR KISHASEMA
unajua hata mie naishangaa mijitu ya humu au labda kila siku inakuja migeni swala la rizwani lilishajadiliwa sana humu ndani kwamba anamiliki maghorofa morogoro ss lipi jipya alilosema dr unajua kuna watu wanataka watufanye watz tuamini tunastahili kuwa maskini hivi tulivyo na wengine wawe matajiri na kifupi yoyete anaetetea ufisadi huu ni wale wala makombo
 
Kosa liko wapi Ridhwan kuwa tajiri ? wacheni husda.(Naye pia anastahili kumiliki kama wanavyomiliki wengine mali roho mbaya haijengi sio kila anaepata kaiba) Juhadharini na dhana kwani hakika ya dhana ni kusema uongo.

Pepombili,

Hivi majuzi CCM kimewataka mafisadi waachie ngazi ama sivyo kinawamwaga. Chiligati anasema hawana haja ya ushahidi, public opinion inatosha, yeyote anayetajwa tajwa kwenye kashfa kadhaa apime na aachie ngazi.
Kwenye chama mlisema hakuna mafisadi ghafla mmewataja kwa majina

Sasa hii ya kutaka Dr Slaa alete ushahidi ambao nyie wenyewe hamhitaji inatoka wapi.....Jipangeni upya maana badala ya kuwatetea watu wenu ndio mnazidi kuharibu.
 
Pepombili,

Jamvi hili si maahali pa kutoa ushahidi. Kuna mahali pa kutolea ushahidi. Kauli zangu zimetolewa kwenye hotuba ya kuwaelimsha Watanzania, tena in this case wa Jimbo la Igunga Jimbo la Rostam Aziz. Kazi yangu kama Katibu Mkuu katika mikutano ya hasdhara si kutoa ushahidi bali kueleza na kuonyesha uozo ndani ya CCM na Serikali yake ili Watanzania waweze kufunguka macho. Mwenye kuona kaonewa ana mahali pa kutaka "redress" kama anafikiri nilichosema siyo kweli.

Nilikwisha kueleza kuwa "mahakamakubwa kuliko zote kwa mwanasiasa ni 'wananchi' (Ibara ya 8 ya Katiba). Tuliowataja leo wako mahakamani, Fedha za EPA mlizobishia angalau JK aliutangaza Bungeni kuwa zimerudishwa sehemu (Japo CAG katika Taarifa yake ya Hesabu za Serikali Kuu anasema fedha hizo hadi Machi 2011 hajaona zimeingizwa akaunti gani japo zilihamishiwa TIB June, 20, 2010 (Jambo linalozua utata mpya kabisa katika historia ya ufisadi ikizangatiwa kuwa 2010 ilikuwa mwaka wa Uchaguzi-au zilirudishwa zikaenda tena kwenye uchaguzi kuisaidia CCM au hazikurudishwa kabisa na inakuwa usanii tu).

Kama Rizwani anaona ameonewa aende yeye mahakamani mimi nimemaliza kesi kwenye mahakama ya wananchi, lakini nadhani ni vema ungelinukuu vizuri "conclusion yangu badala ya kuchakachua statement yangu".

Dr let me join hands with you in a very different way; kwamba as from today I command the greater light to smite these fisadis in the day time and the lesser light in the night. Let west and the east whirl wind come against them and let the water they drink and food they eat turn into the blood (innocent blood which was shed by all the victims of their evil fellowships) which to you is the cause of sanctification because of what you chosen to do and to them the source of condemnation. Let them by this cause never rest in day or night times until they are destroyed by their own doings. If at all they can live without being serviced by the sun which is the source of all energy in living and non living and if they would live in the planet which is not serviced by the moon that causes the tides to rise and fall and the weather to change according to its movement they can defeat you, otherwise let them count their days! You are under safe hands just do whats right and nothing shall by any means hurt you; I decree and declare in the most high and powerfull name of Jesus Christ my Lord ans saviour and under the diktat of the mighty power of hollyghost. If you believe say Amen and to all people who are in this good fight let you all say Amen.
 
wasukuma wakimkana kwamba sio msukuma ndipo nitaelewa lakini km sivyo` basi ni haki yake kula nchi kwani katiba ya ccm iko wazi kuwa mwenye uwezo wa kula nyama nyingi ni yule mwenye kisu kikali.................mwacheni rostamu wetu sisi ccm ametusaidia sana bila yeye kikwete asingeingia madarakani 2005 na km mnavyojua kikwete ametufanyia mengi sana...............mnafikiri tungeweza kupata rais km yeye hapa tz?......kwa hiyo rostamu kasaidia sana nchi hii ni haki yake naye kufaidi matunda ya jasho lake na pesa alizowekeza ccm na serikalini
 
Hivi kama ana ushahidi si awapeleke mahakamani jamani, kwa niaba ya wananchi. Achukue hatua zaidi ya kutaja tu.

Mahakama gani unaongelea dadangu?
Mahakama ambayo jaji mkuu ni mteuliwa wa rais kisha wenda kumshtaki mtoto wa rais tuache.
Mahakama ipi katika nchi ambako DPP mteuliwa wa mtukufu rais ana mamlaka ya nani ashitakiwe na nani asishtakiwe.

Tuache masihala
 
unaongea pumba tu kwani kipato cha mtu ni mshahara peke yake wacha uzembe wewe tunataka ushahidi wenu hapo sio husda mlizo nazo roho mbaya ndio zinawasumbua na zitawauma sana aliepata kapata tu
Ni afadhali umejipambanua kwa kusema "kwa uelewa wangu". Unaonyesha unauelewa mdogo saaana.

Naomba nikusaidie kidogo kutoa ujinga wako:
Kikwete kawa waziri kwa miaka 15 na Uraisi kwa miaka 6.
Tufanye baba yake alipata mshahara wa 2,000,000/= kwa mwezi (mshahara ambao haukuwepo, na hapo hajatumia hata shilingi wala kukatwa kodi) zidisha mara 12 mara miaka 15. Kisha jumlisha mshahara wa uraisi wa miaka 5 na miezi 4. Utupe jibu ni kiasi gani. Amekusanya.

Jipambanue vizuri. Ridhiwan mtoto wa tajiri? Huyo tajiri baba yake utajiri wake ulianza lini?
 
endelea kudai katiba mpya
Mahakama gani unaongelea dadangu?
Mahakama ambayo jaji mkuu ni mteuliwa wa rais kisha wenda kumshtaki mtoto wa rais tuache.
Mahakama ipi katika nchi ambako DPP mteuliwa wa mtukufu rais ana mamlaka ya nani ashitakiwe na nani asishtakiwe.

Tuache masihala
 
Back
Top Bottom