Slaa awalipua Rostam, Riziwan

Slaa awalipua Rostam, Riziwan

Nomba ieleweke kwamba; Moja ya kazi ya chama cha siasa cha upinzani kama CHADEMA ni kuitaka serikali iwajibike kwa wananchi wake. Ndio maana CHADEMA wamendelea kuitaka serikali kuchukua hatua kutokomeza ufisadi hapa nchini.
 
Mke wa Mbowe alivyotishiwa kufa alikwenda polisi kushtaki na sasa kesi ipo mahakamani kama kweli Dr Slaa na wewe umetishwa kama utauwawa sasa peleka hizo taarifa polisi sio kuwashtakia wananchi suala lako la kuuliwa.

RA ni Mtanzania na ana haki ya kumiliki hizo pesa, Dr Slaa naamini wewe ni Dr wa ukweli hasa nilipoangalia kwenye youtube ulipokuwa unamuelezea yule mama kuhusu mtoto wake mlemavu nilifurahi sana juu ya upeo wako wa elimu ya Afya ulionayo lakini je mbona kwenye suala hili la sasa la Riz na RA kutaka kukuuwa mbona huweki vidhibitisho? Tutakuamini vipi?
Watanzania ni watu wa ajabu sana, ndiyo binadamu pekee wanaoamini mambo ya kuambiwa bila ushahidi. Duniani kote wanasiasa wanapotoa tuhuma utoa na documents za ku-support tuhuma zao, lakini Tanzania ni tofauti kabisa tunaamini ya kuambiwa na mtu tu.

Poleni sisi wengine hatuamini wala kupinga kitu mpaka pawe na ushahidi unaoambatana na tuhuma hizo.
 
Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

• ASEMA ANAPOKEA BIL. 280/- KWA MWAKA, ATAKA AKAMATWE

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza mapato ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), kwa kile alichodai yana uhusiano mkubwa na ufisadi.

Dk. Slaa aliyasema hayo juzi jioni katika mkutano wake mjini Igunga, mkoani Tabora katika mwendelezo wa ziara zake.


Alisema mapato ya Rostam kwa mwaka yanafikia sh bilioni 280, hivyo TAKUKURU haina budi kumkamata na kumchunguza kwani aliwahi kutangaza kuwa hana shida ya kuwa kiongozi au kung'ang'ania madaraka yoyote, kwani pesa alizonazo zinamtosha.


Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa TAKUKURU haitamchukulia hatua Rostam, atawashawishi wananchi kutotoa ushirikiano wowote kwa taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwazomea maofisa wake kila wanapowaona.


Akifafanua tuhuma hizo za ufisadi, alisema kuwa kati ya makampuni 17 yanayosemekana kuwa ni ya Rostam hakuna jina lake hata moja.


Alisema kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa na nia ya kweli angemshirikisha kuwakamata mafisadi badala ya kuwapa siku 90 kuondoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa Kikwete amewapa mafisadi hao siku hizo kuondoka ndani ya chama pamoja na kuachia ubunge, naye hana budi kujipa siku hizo, kwani naye ni fisadi.


Alisema kujitokeza kwa mmiliki wa Dowans Brigedia Jenerali (mstaafu), Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, ulikuwa ni usanii wa picha ya Rostam kwani baadaye ndiye atakayelipwa fedha hizo za Dowans.


Alisema CHADEMA haitakubali fedha hizo zilipwe na kwamba itaitisha maandamano nchi nzima kupinga.


Dk. Slaa alisema ufisadi mwingine wa serikali katika sakata hilo la Dowans ni serikali kuweka mawakili watatu kinyemela na kupanga kuwalipa sh bilioni tano.


"Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema …nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli," alisema Dk. Slaa.


Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema moto uliowashwa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) umeifanya serikali ya CCM akiwamo Rais Jakaya Kikwete kushindwa kulala.


Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikungi katika Jimbo la Singida Mashariki jana aliposimama kuwasalimia wakati akitokea Singida kuelekea Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema Lissu ni mbunge jasiri katika Bunge ambaye amediriki kumnyooshea kidole hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema.


Katika hotuba yake hiyo alisema wananchi hawana imani tena na serikali ya Jakaya Kikwete na kama atafanya mchezo hataweza kurudisha imani hiyo wala kumaliza kipindi chake cha utawala.


Alisema mambo mengi yamejitokeza ambayo yamesababisha wananchi kukosa imani naye, yakiwamo ya ufisadi unaofanywa na yeye mwenyewe pamoja na watu walio karibu naye.


"Wananchi wanaona yanayofanyika, mtoto wa rais, Ridhiwani Kikwete, amemaliza shule hivi karibuni lakini leo ni bilionea. Haya yote hayawezi kuvumilika hata kidogo."

Akiwashukuru wananchi wa kijiji hicho, Dk. Slaa alisema si tu kwamba wamemchagua mbunge wa Jimbo la Singida, bali ni mbunge wa nchi nzima na kwamba ni nyundo itakayotumika kuwaponda CCM.

Akizungumzia suala la CCM kujivua gamba, alisema neno fisadi alilianzisha yeye na chama chake na kwamba anayepaswa kujivua gamba hilo ni Kikwete halafu awavue wengine.


Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam


Major Concerns for Tanzanians:
- Umaskini wa watanzania unatokana na kukubali kudanganywa na JK, Mkapa, Mwinyi. Leo wamewaleta Rostam, Ridhiwani, January, Nape kuwaibia watanzania sio kuwaongoza, hatafanikiwa!

- Watanzania tunakataliwa nafasi ya kujua uwezo wa kifedha za wasanii wa ccm na vyombo vya polisi vinahusika kuwalinda.

- Watanzania lazima tujue tunauwezo wa kuwaondoa na kuleta demokrasia ya ukweli. We need justice system to take place and start taking our country back
 
Tumepata tetesi ridwan kikwete ni tajiri wa kutisha,tunaombeni kama kuna mtu ana informatin atugee kiaina
 
Riz1 v/s Slaa W...

Ile Kampuni ya Mafuta nadhani Riz ameingia mkenge pale - he was so fast na nadhani wengi watamstukia!
 
Yes, ni bora kujua mali anazomiliki ili watanzania wajilirishe ikiwa yeye ni mtoto wa rais na jinsi alivyozipata
 
Kosa liko wapi Ridhwan kuwa tajiri ? wacheni husda.(Naye pia anastahili kumiliki kama wanavyomiliki wengine mali roho mbaya haijengi sio kila anaepata kaiba) Juhadharini na dhana kwani hakika ya dhana ni kusema uongo.
 
Kwani umefukuzwa? Andika kwa ufasaha halafu acha umbea!
Nafikiri ujumbe wa mtoa hoja upo very straightforward,unachofanya wewe ni kujenga mazingira ya kumtetea mtuhumiwa!Mkuu una kazi ngumu ya kumsafisha huyo Ridhiwani K!!!
 
Kosa liko wapi Ridhwan kuwa tajiri ? wacheni husda.(Naye pia anastahili kumiliki kama wanavyomiliki wengine mali roho mbaya haijengi sio kila anaepata kaiba) Juhadharini na dhana kwani hakika ya dhana ni kusema uongo.
swala si utajiri ameupateje?wakati amemaliza chuo juzi juzi tu!
 
Kama Rostam mapato yake bilioni 280 yeye DR Slaa inamuuma nini??

Kwani kuna limit ya kiasi cha pesa anazoweza kupokea mtu mmoja kwa mwaka kwenye Tanzania huru??
 
We are not here to be spoonfed lies or other crap like we are in kindergaten.someone should come with evidence.toa ushahdi hata humu watu waone ndo wahoji wamezipata vp
 
Kama Rostam mapato yake bilioni 280 yeye DR Slaa inamuuma nini??

Kwani kuna limit ya kiasi cha pesa anazoweza kupokea mtu mmoja kwa mwaka kwenye Tanzania huru??

Wewe Dr. Slaa anakuuma nini hadi kupost bila kufikiria? Umesoma na kuelewa kwa nini Dr Slaa ametaja hiyo bil 280? Kwani RA ndio bilionea pekee Tanzania? Soma tena hiyo article ujue kwa nini Dr.Slaa anataja hela za RA hata kama ni Sh 100, point yake ni HELA ZA WIZI, kawaibia wananchi, kama wewe, wazazi wako, ndugu zako, jirani zako na wengine wengi tu mmoja wapo ni Dr. Slaa ambaye kodi yake naye inaibiwa. Ana haki ya kuongea.
 
Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

• Asema anapokea bil. 280/- kwa mwaka, ataka akamatwe

Kwa hesabu za haraka ndani ya miaka minne RA anakusanya zaidi ya trillion 1.1 kwanini Forbes hawajamuweka kwenye list ya matajiri duniani? Kweli Tanzania ni shamba la Bibi.
 
Back
Top Bottom