Slaa awalipua Rostam, Riziwan

Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao.

Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari? Naelewa kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa waziri katika wizara nyingi sana hapa Tanzania kabla ya kuwa Rais; ninavoelewa mimi Rizwan kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu, eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hiyo ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa.

Kama mna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi?) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujue ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi.

Huyo Slaa, hebu mwambieni aende unyantuzu (Bariad) akawaone vijana wadogo under 25 wakimiliki mali za mabilioni, hawajaenda hata zaidi ya std seven. Sio watoto wa katibu tarafa wala rais.

Ajue kuwa ukiwa na mtaji ku-make ni suala la mwaka. Aende Kahama aone vijana wa kinyantuzu wanavyoporomosha maghorofa, hawakusoma wamefanya biashara ya maduka, mifugo leo wana pesa.

Aache kulalama afanye kazi
 
Mi nadhani kuna haja ya maraisi kutaja mali zao before hawajaingia ikulu na baada ya kumaliza pamoja na familia zao tena in public hii itaondoa yote haya. Ila being honest tutaishia kuongea na kuumumuia roho haki ni ngumu sana kupatikana hasa kwa mataifa ya afr ika
 
huyo silah,hebu mwambieni aende unyantuzu(bariad)akawaone vijana wadogo under25 wakimiliki mali za mabilion ,hawajaenda hata zaidi ya std seven.
Sio watoto wa katibu tarafa wala rais.
Ajue kua ukiwa na mtaji kumake ni suala la mwaka.aende kahama aone vijana wa kinyantuz wanavyoporomoa maghorofa,haakusoma wamefanya biashara maduka,mifugo leo wanapesa.
Ache kulalama afanye kazi


Ndugu wewe huelewi kinachoendelea huko usukumani waulize wanaotoka huko watakupa uhalali wa utajiri wa hao vijana. Kwa taarifa yako mali ile si ya hao unaowaona wewe wwale ni washika pembe tu wenyewe ni walewale unaowajua. Fatilia vizuri huwezi kuamini mtu anapata utajiri wa kumiliki maroli na viwanda ndani ya mwaka au miwili na huku alikuwa anafanya biashara ya kondoo na hata hawakuwahi kufika kumi miaka michache iliyopita. Nakumbuka mtu huyu hajui hata kusoma wala kuandika.

Mafisadi huwatumia hawa mbumbu kuficha utajiri wao maana hawajui chochote hawataweza kuwadhulumu maana hawana hata elimu ya mikataba ya biashara.

Karagabaho endelea kuamini kuwa kutajirika ni rahisi kiasi hicho! Bila kuwa mwizi hakuna utajiri wa mwaka mmoja a miwili it take you time and proper management to get you up there!

Kama utajiri ungekuwa rahisi hivyo hakuna ambaye angebaki masikini wa kutupwa ilihali kumbe hata ukiwa na mtaji wa elufu hamsini unaweza kuboresha maisha. pia kila mtu angeachana na kazi zingine akafanya biashara.

Unaowaona wana kwea juu ni wizi wa mali ya umma kwa kufanya madili na serikali. hakuna biashara inayolipa zaidi ya tenda hewa za serikali kama tulivyoona mikataba ya umeme na madini


Hivi kwako utajiri wa namna hii ni halali kwako au ni ufisadi tu.

Tulishuhudia biashara za mabasi ya scandinavia, wakubwa walipochomoa hisa zao leo hii wakowapi?

Fikiri mara mbili kama na wewe sio mshika pembe wa kwa mafisadi ndo maana unatetea hoja kama hii bila kujali maumivu wanayofanyiwa watz na hizi biashara hewa za wizi wa jasho la walalahoi.
 
Kama alivyosema Dr, ushahidi huwa hautolewi kwenye mikutano ya hadhara. Ushahidi wa mambo nyeti kama hayo hutolewa mahakamani pindi yule aliyetuhumiwa au kuhusishwa na kashfa ile atakapoenda kusema nimedhalilishwa.

Sasa kwenye hili anayetakiwa kushtaki ni Riz, na Dr ataitwa kuthibitisha, na hapo ndipo atatakiwa kutoa vielelezo.
 
wakuu...

mimi si mwanasiasa per say lakini hili la ridhiwani LIMENISTUA

mnaojua tunaomba mtuorodheshee mali za huyu dogo

CHADEMA: Tutahoji utajiri wa Ridhiwan
Thursday, 21 April 2011 08:17 0diggsdigg

Geofrey Nyang'oro, Singida
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Willbroad Slaa amesema chama chake kinajipanga kuhoji kile alichodai utajiri mkubwa wa ghafla wa Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji na pia Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Dk Slaa alisema hayo jana katika Kijiji cha Ikungi, mkoani Singida alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

Alisema anajua kuwa mjumbe huyo (jina tunalihifadhi kwa kuwa jitihada za kumpata kujibu tuhuma hizo hazikufanikiwa), licha ya umri wake mdogo hivi sasa ana fedha nyingi.

Katika mkutano huo Dk Slaa alimtuhumu kuwa na utajiri uliopindukia ambao alisema haulingani na umri wake.

Dk Slaa alisema chama chake kina shaka na wingi wa fedha alizonazo kijana huyo na kwamba atahakikisha kwamba kigogo huyo anaiambia Chadema na Watanzania alipozipata.

Alisema kijana huyo alimaliza masomo yake muda mfupi uliopita, lakini tayari amekuwa bilionea akisisitiza kuwa chama chake kitahoji alipopata mabilioni hayo.

"Ninajua kwamba ana fedha nyingi, lakini huyu alikuwa mtoto wa shule juzi tu. Leo amekuwa bilionea! Atatuambia amepata wapi hizo fedha, Chadema tutahoji ni wapi amezipata," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa pia alizungumzia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kelele za wapinzani hazimnyimi usingizi na kusema watahakikisha halali.

Mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana alitoa kauli hiyo alipozungumzia ushindi wa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akisema umeimarisha ngome ya upinzani bungeni.

"Rais Kikwete alisema kelele za upinzani hazimnyimi usingizi, lakini kwa kumchagua Lissu mmeongeza nguvu ya upinzani na sasa hatalala," alisema na kuongeza:

“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba sasa mmemchagua mbunge jasiri anayeweza kumwambia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mbele ya Waziri Mkuu kuwa amekuwa mvivu kusoma.”

Alisema kutokana na ujasiri huo wa Lissu sasa miswada mibovu haitapelekwa bungeni.

Awali, akizungumza katika mkutano huo, Lissu alisema Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo akisema kuwa ni mara ya kwanza fedha hizo kutengwa huku akijigamba kwamba ni kutokana na wapinzani kubana mianya ya wizi.
 
Ndugu wewe huelewi kinachoendelea huko usukumani waulize wanaotoka huko watakupa uhalali wa utajiri wa hao vijana. Kwa taarifa yako mali ile si ya hao unaowaona wewe wwale ni washika pembe tu wenyewe ni walewale unaowajua. Fatilia vizuri huwezi kuamini mtu anapata utajiri wa kumiliki maroli na viwanda ndani ya mwaka au miwili na huku alikuwa anafanya biashara ya kondoo na hata hawakuwahi kufika kumi miaka michache iliyopita. Nakumbuka mtu huyu hajui hata kusoma wala kuandika.

Mafisadi huwatumia hawa mbumbu kuficha utajiri wao maana hawajui chochote hawataweza kuwadhulumu maana hawana hata elimu ya mikataba ya biashara.

Karagabaho endelea kuamini kuwa kutajirika ni rahisi kiasi hicho! Bila kuwa mwizi hakuna utajiri wa mwaka mmoja a miwili it take you time and proper management to get you up there!

Kama utajiri ungekuwa rahisi hivyo hakuna ambaye angebaki masikini wa kutupwa ilihali kumbe hata ukiwa na mtaji wa elufu hamsini unaweza kuboresha maisha. pia kila mtu angeachana na kazi zingine akafanya biashara.

Unaowaona wana kwea juu ni wizi wa mali ya umma kwa kufanya madili na serikali. hakuna biashara inayolipa zaidi ya tenda hewa za serikali kama tulivyoona mikataba ya umeme na madini


Hivi kwako utajiri wa namna hii ni halali kwako au ni ufisadi tu.

Tulishuhudia biashara za mabasi ya scandinavia, wakubwa walipochomoa hisa zao leo hii wakowapi?

Fikiri mara mbili kama na wewe sio mshika pembe wa kwa mafisadi ndo maana unatetea hoja kama hii bila kujali maumivu wanayofanyiwa watz na hizi biashara hewa za wizi wa jasho la walalahoi.

siezi bishana nawe bana umeongea point.ndo maana siwamini wanasiasa.alikuepo obama akajidai mtu wa wanyonge kumbe mnafiki mkubwa.anapokea amri kutoka kwa mabanker,oil companies kama agip,chevron,military industries complex wanaenedesha vita ili silaha ziuzwe na makampuni ya mafuta yapate contracter,huku makampuni ya kina dick chen ,HALIBUTON yakipata tenda za kusupply jeshini kuanzia magari,chakula hadi uniform,itakua hapa.we need evidence
 
don't blame the messenger, blame jk who decided to sit on his hands and let his crooks friends destroying the country.

Brilliant, hawana makosa hao bali mkulu ndie mwenye kuwajibika kwa yote yatokeayo.
 
Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je ? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao. Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari, naelewa Kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa wazizri katika wizara nyingi sana hapa tanzania kabla ya kuwa Rais ninavoelewa mimi Rizwan Kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hio ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa ( kama muna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujuwe ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi.

Ni afadhali umejipambanua kwa kusema "kwa uelewa wangu". Unaonyesha unauelewa mdogo saaana.

Naomba nikusaidie kidogo kutoa ujinga wako:
Kikwete kawa waziri kwa miaka 15 na Uraisi kwa miaka 6.
Tufanye baba yake alipata mshahara wa 2,000,000/= kwa mwezi (mshahara ambao haukuwepo, na hapo hajatumia hata shilingi wala kukatwa kodi) zidisha mara 12 mara miaka 15. Kisha jumlisha mshahara wa uraisi wa miaka 5 na miezi 4. Utupe jibu ni kiasi gani. Amekusanya.

Jipambanue vizuri. Ridhiwan mtoto wa tajiri? Huyo tajiri baba yake utajiri wake ulianza lini?
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Willbroad Slaa amesema chama chake kinajipanga kuhoji kile alichodai utajiri mkubwa wa ghafla wa Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji na pia Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Dk Slaa alisema hayo jana katika Kijiji cha Ikungi, mkoani Singida alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

Alisema anajua kuwa mjumbe huyo (jina tunalihifadhi kwa kuwa jitihada za kumpata kujibu tuhuma hizo hazikufanikiwa), licha ya umri wake mdogo hivi sasa ana fedha nyingi.

Katika mkutano huo Dk Slaa alimtuhumu kuwa na utajiri uliopindukia ambao alisema haulingani na umri wake.

Dk Slaa alisema chama chake kina shaka na wingi wa fedha alizonazo kijana huyo na kwamba atahakikisha kwamba kigogo huyo anaiambia Chadema na Watanzania alipozipata.

Alisema kijana huyo alimaliza masomo yake muda mfupi uliopita, lakini tayari amekuwa bilionea akisisitiza kuwa chama chake kitahoji alipopata mabilioni hayo.

"Ninajua kwamba ana fedha nyingi, lakini huyu alikuwa mtoto wa shule juzi tu. Leo amekuwa bilionea! Atatuambia amepata wapi hizo fedha, Chadema tutahoji ni wapi amezipata," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa pia alizungumzia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kelele za wapinzani hazimnyimi usingizi na kusema watahakikisha halali.

Mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana alitoa kauli hiyo alipozungumzia ushindi wa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akisema umeimarisha ngome ya upinzani bungeni.

"Rais Kikwete alisema kelele za upinzani hazimnyimi usingizi, lakini kwa kumchagua Lissu mmeongeza nguvu ya upinzani na sasa hatalala," alisema na kuongeza:

“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba sasa mmemchagua mbunge jasiri anayeweza kumwambia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mbele ya Waziri Mkuu kuwa amekuwa mvivu kusoma.”

Alisema kutokana na ujasiri huo wa Lissu sasa miswada mibovu haitapelekwa bungeni.

Awali, akizungumza katika mkutano huo, Lissu alisema Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo akisema kuwa ni mara ya kwanza fedha hizo kutengwa huku akijigamba kwamba ni kutokana na wapinzani kubana mianya ya wizi

Source;Mwananchi newspaper
 
Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

• Asema anapokea bil. 280/- kwa mwaka, ataka akamatwe

na Joseph Senga

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza mapato ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), kwa kile alichodai yana uhusiano mkubwa na ufisadi.

Dk. Slaa aliyasema hayo juzi jioni katika mkutano wake mjini Igunga, mkoani Tabora katika mwendelezo wa ziara zake.

Alisema mapato ya Rostam kwa mwaka yanafikia sh bilioni 280, hivyo TAKUKURU haina budi kumkamata na kumchunguza kwani aliwahi kutangaza kuwa hana shida ya kuwa kiongozi au kung’ang’ania madaraka yoyote, kwani pesa alizonazo zinamtosha.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa TAKUKURU haitamchukulia hatua Rostam, atawashawishi wananchi kutotoa ushirikiano wowote kwa taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwazomea maofisa wake kila wanapowaona.

Akifafanua tuhuma hizo za ufisadi, alisema kuwa kati ya makampuni 17 yanayosemekana kuwa ni ya Rostam hakuna jina lake hata moja.

Alisema kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa na nia ya kweli angemshirikisha kuwakamata mafisadi badala ya kuwapa siku 90 kuondoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa Kikwete amewapa mafisadi hao siku hizo kuondoka ndani ya chama pamoja na kuachia ubunge, naye hana budi kujipa siku hizo, kwani naye ni fisadi.

Alisema kujitokeza kwa mmiliki wa Dowans Brigedia Jenerali (mstaafu), Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, ulikuwa ni usanii wa picha ya Rostam kwani baadaye ndiye atakayelipwa fedha hizo za Dowans.

Alisema CHADEMA haitakubali fedha hizo zilipwe na kwamba itaitisha maandamano nchi nzima kupinga.

Dk. Slaa alisema ufisadi mwingine wa serikali katika sakata hilo la Dowans ni serikali kuweka mawakili watatu kinyemela na kupanga kuwalipa sh bilioni tano.

“Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema …nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli,” alisema Dk. Slaa.

Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema moto uliowashwa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) umeifanya serikali ya CCM akiwamo Rais Jakaya Kikwete kushindwa kulala.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikungi katika Jimbo la Singida Mashariki jana aliposimama kuwasalimia wakati akitokea Singida kuelekea Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema Lissu ni mbunge jasiri katika Bunge ambaye amediriki kumnyooshea kidole hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema.

Katika hotuba yake hiyo alisema wananchi hawana imani tena na serikali ya Jakaya Kikwete na kama atafanya mchezo hataweza kurudisha imani hiyo wala kumaliza kipindi chake cha utawala.

Alisema mambo mengi yamejitokeza ambayo yamesababisha wananchi kukosa imani naye, yakiwamo ya ufisadi unaofanywa na yeye mwenyewe pamoja na watu walio karibu naye.

“Wananchi wanaona yanayofanyika, mtoto wa rais, Ridhiwani Kikwete, amemaliza shule hivi karibuni lakini leo ni bilionea. Haya yote hayawezi kuvumilika hata kidogo.”

Akiwashukuru wananchi wa kijiji hicho, Dk. Slaa alisema si tu kwamba wamemchagua mbunge wa Jimbo la Singida, bali ni mbunge wa nchi nzima na kwamba ni nyundo itakayotumika kuwaponda CCM.

Akizungumzia suala la CCM kujivua gamba, alisema neno fisadi alilianzisha yeye na chama chake na kwamba anayepaswa kujivua gamba hilo ni Kikwete halafu awavue wengine.


source: Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

hapo kwenye red nina mashaka kidogo, kama ni kweli kwanini Dr. Slaa hakumfungulia mashtaka huyo Fisadi R.A kwa kumtishia maisha?? tena kwa kumtumia ujumbe mfupi, ushahidi tosha kabisa.
 
Kama alivyosema Dr, ushahidi huwa hautolewi kwenye mikutano ya hadhara. Ushahidi wa mambo nyeti kama hayo hutolewa mahakamani pindi yule aliyetuhumiwa au kuhusishwa na kashfa ile atakapoenda kusema nimedhalilishwa.

Sasa kwenye hili anayetakiwa kushtaki ni Riz, na Dr ataitwa kuthibitisha, na hapo ndipo atatakiwa kutoa vielelezo.

Sheria za wapi hizo? Hivi ikitokea hao watuhumiwa wakakaa kimya na huyo Slaa akiwa na ushahidi akaendelea kukaa nao kuna chochote cha maana kitaendelea? Je tutakuwa tumetatua tatizo la ufisadi?
Chadema ina timu ya wanasheria wazuri Lissu akiwemo kama anavyomsifia, kama wana nia njema na Tz na wala sio maslahi yao kisiasa kwa nini wasiwashitaki na ushahidi wanao badala yake kuendelea "kuwalipua" na pesa zikiendelea kuibwa?
A big excuse huwa ni legal system iko corupt, hawaiamini kwa sababu inalinda mafisadi! If thats the case kumbe mbona hao watuhumita huchukuliwa kuwa wamethibitisha ufisadi wao kwa kutowashitaki Chadema? Kwa nini wasiwafungulie mashitaka ikiwa wana uhakika na ushindi mahakamani?
Kwa nini basi Slaa asitoe ushahidi huo kwa umma wa watanzania ikiwa anaamini kuwa hiyo ndiyo mahakama ya haki? Pengine anapenda sana kuwatumia kwa sababu ana hakika hatoulizwa ushahidi na bado akaendelea kuaminika!!
As to my point of view that is a problem, sir...
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk Willbroad Slaa amesema chama chake kinajipanga kuhoji kile alichodai utajiri mkubwa wa ghafla wa Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji na pia Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Dk Slaa alisema hayo jana katika Kijiji cha Ikungi, mkoani Singida alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

Alisema anajua kuwa mjumbe huyo (jina tunalihifadhi kwa kuwa jitihada za kumpata kujibu tuhuma hizo hazikufanikiwa), licha ya umri wake mdogo hivi sasa ana fedha nyingi.

Katika mkutano huo Dk Slaa alimtuhumu kuwa na utajiri uliopindukia ambao alisema haulingani na umri wake.

Dk Slaa alisema chama chake kina shaka na wingi wa fedha alizonazo kijana huyo na kwamba atahakikisha kwamba kigogo huyo anaiambia Chadema na Watanzania alipozipata.

Alisema kijana huyo alimaliza masomo yake muda mfupi uliopita, lakini tayari amekuwa bilionea akisisitiza kuwa chama chake kitahoji alipopata mabilioni hayo.

"Ninajua kwamba ana fedha nyingi, lakini huyu alikuwa mtoto wa shule juzi tu. Leo amekuwa bilionea! Atatuambia amepata wapi hizo fedha, Chadema tutahoji ni wapi amezipata," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa pia alizungumzia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kelele za wapinzani hazimnyimi usingizi na kusema watahakikisha halali.

Mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana alitoa kauli hiyo alipozungumzia ushindi wa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akisema umeimarisha ngome ya upinzani bungeni.

"Rais Kikwete alisema kelele za upinzani hazimnyimi usingizi, lakini kwa kumchagua Lissu mmeongeza nguvu ya upinzani na sasa hatalala," alisema na kuongeza:

“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba sasa mmemchagua mbunge jasiri anayeweza kumwambia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mbele ya Waziri Mkuu kuwa amekuwa mvivu kusoma.”

Alisema kutokana na ujasiri huo wa Lissu sasa miswada mibovu haitapelekwa bungeni.

Awali, akizungumza katika mkutano huo, Lissu alisema Halmashauri ya Wilaya ya Singida imetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo akisema kuwa ni mara ya kwanza fedha hizo kutengwa huku akijigamba kwamba ni kutokana na wapinzani kubana mianya ya wizi.
 
namshukuru sana Dk Slaa kutoa ufafanuzi kwa mwana-JF mwenzetu kuhusu kauli yake, na kwa wale tuliokuwepo mwaka 2007 mwembe yanga hatakuwa na cha kubisha juu ya tuhuma mbalimbali zinazotolewa kwa kuwa ushahidi unasomwa na watu wanaelewa. Kimsingi ukufuatilia namna wanavyotajwa (mafisadi) na ukisoma magazeti yanavyoripoti unaweza ukapotoshwa.
 
matajiri wangapi vijana wamemaliza chuo juzi mbona hamuwafatilii ? Husda ndio zinawasumbua

Toa mfano wa hao matajiri vijana waliomaliza shule juzi ili na wenyewe wachunguzwe. Hoja hapa ni Amepataje utajiri huo, kama kihalali bila uhusianao na rushwa au ufisadi basi ruksa hata kuingiza bil 500 kwa mwaka, hakuna atakaye kufuatilia
 
Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao.

Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari? Naelewa kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa waziri katika wizara nyingi sana hapa Tanzania kabla ya kuwa Rais; ninavoelewa mimi Rizwan kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu, eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hiyo ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa.

Kama mna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi?) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujue ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi.
Stop speaking nonsense here! wewe ni nani uanyewasemea hao mafisadi waache wao waombe ushahidi yeye anao ndiyo maana kasema
 
Mmh haya makubwa tena. Basi tunasubiri kujua mengi.

Kwani naamini wazi kuwa Kijana ni mwanasheria na anajua fika sheria za nchi hivyo kama ataona au kuhisi kuwa amedhalilishwa basi atafikisha suala hili mahakamani ili zilijulikane mbivu na mbichi.

Thanks for the info Dr
 
Huyo dogo ametumia mgongo wa baba yake kufisadi taifa! Kwani pale IMMA mshahara wake ulikuwa wakawaida tu na alishatimuliwa, sasa hebu tujiulize dunia kote hakuna kijana aliyezaliwa ktk familia masikini halafu ndani ya miaka miwili tangu amalize masomo akawa bilionea! Hapa kuna kitu!
 
Back
Top Bottom