Slaa awalipua Rostam, Riziwan

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
Dk. Slaa afichua mabilioni ya Rostam

Asema anapokea bil. 280/- kwa mwaka, ataka akamatwe

Na Joseph Senga

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza mapato ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), kwa kile alichodai yana uhusiano mkubwa na ufisadi.

Dk. Slaa aliyasema hayo juzi jioni katika mkutano wake mjini Igunga, mkoani Tabora katika mwendelezo wa ziara zake.

Alisema mapato ya Rostam kwa mwaka yanafikia sh bilioni 280, hivyo TAKUKURU haina budi kumkamata na kumchunguza kwani aliwahi kutangaza kuwa hana shida ya kuwa kiongozi au kung'ang'ania madaraka yoyote, kwani pesa alizonazo zinamtosha.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa TAKUKURU haitamchukulia hatua Rostam, atawashawishi wananchi kutotoa ushirikiano wowote kwa taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwazomea maofisa wake kila wanapowaona.

Akifafanua tuhuma hizo za ufisadi, alisema kuwa kati ya makampuni 17 yanayosemekana kuwa ni ya Rostam hakuna jina lake hata moja.

Alisema kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa na nia ya kweli angemshirikisha kuwakamata mafisadi badala ya kuwapa siku 90 kuondoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa Kikwete amewapa mafisadi hao siku hizo kuondoka ndani ya chama pamoja na kuachia ubunge, naye hana budi kujipa siku hizo, kwani naye ni fisadi.

Alisema kujitokeza kwa mmiliki wa Dowans Brigedia Jenerali (mstaafu), Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, ulikuwa ni usanii wa picha ya Rostam kwani baadaye ndiye atakayelipwa fedha hizo za Dowans.

Alisema CHADEMA haitakubali fedha hizo zilipwe na kwamba itaitisha maandamano nchi nzima kupinga.

Dk. Slaa alisema ufisadi mwingine wa serikali katika sakata hilo la Dowans ni serikali kuweka mawakili watatu kinyemela na kupanga kuwalipa sh bilioni tano.

"Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema ;nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli," alisema Dk. Slaa.

Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema moto uliowashwa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) umeifanya serikali ya CCM akiwamo Rais Jakaya Kikwete kushindwa kulala.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikungi katika Jimbo la Singida Mashariki jana aliposimama kuwasalimia wakati akitokea Singida kuelekea Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema Lissu ni mbunge jasiri katika Bunge ambaye amediriki kumnyooshea kidole hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema.

Katika hotuba yake hiyo alisema wananchi hawana imani tena na serikali ya Jakaya Kikwete na kama atafanya mchezo hataweza kurudisha imani hiyo wala kumaliza kipindi chake cha utawala.

Alisema mambo mengi yamejitokeza ambayo yamesababisha wananchi kukosa imani naye, yakiwamo ya ufisadi unaofanywa na yeye mwenyewe pamoja na watu walio karibu naye.

"Wananchi wanaona yanayofanyika, mtoto wa rais, Ridhiwani Kikwete, amemaliza shule hivi karibuni lakini leo ni bilionea. Haya yote hayawezi kuvumilika hata kidogo."

Akiwashukuru wananchi wa kijiji hicho, Dk. Slaa alisema si tu kwamba wamemchagua mbunge wa Jimbo la Singida, bali ni mbunge wa nchi nzima na kwamba ni nyundo itakayotumika kuwaponda CCM.

Akizungumzia suala la CCM kujivua gamba, alisema neno fisadi alilianzisha yeye na chama chake na kwamba anayepaswa kujivua gamba hilo ni Kikwete halafu awavue wengine.

source: Free Media
 
280 bilion kwa kweli hapa ndipo umuhimu wa kuwa na kiongozi kama Dr Slaa huyo RIZWANI kama ni bilioni hiyo n hela ya baba yake anamshikia tu kwa muda,
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza mapato ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), kwa kile alichodai yana uhusiano mkubwa na ufisadi.

Dk. Slaa aliyasema hayo juzi jioni katika mkutano wake mjini Igunga, mkoani Tabora katika mwendelezo wa ziara zake. Alisema mapato ya Rostam kwa mwaka yanafikia sh bilioni 280, hivyo TAKUKURU haina budi kumkamata na kumchunguza kwani aliwahi kutangaza kuwa hana shida ya kuwa kiongozi au kung'ang'ania madaraka yoyote, kwani pesa alizonazo zinamtosha.

Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa TAKUKURU haitamchukulia hatua Rostam, atawashawishi wananchi kutotoa ushirikiano wowote kwa taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwazomea maofisa wake kila wanapowaona. Akifafanua tuhuma hizo za ufisadi, alisema kuwa kati ya makampuni 17 yanayosemekana kuwa ni ya Rostam hakuna jina lake hata moja.

Alisema kama Rais Jakaya Kikwete angekuwa na nia ya kweli angemshirikisha kuwakamata mafisadi badala ya kuwapa siku 90 kuondoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa mujibu wa Dk. Slaa, ikiwa Kikwete amewapa mafisadi hao siku hizo kuondoka ndani ya chama pamoja na kuachia ubunge, naye hana budi kujipa siku hizo, kwani naye ni fisadi.

Alisema kujitokeza kwa mmiliki wa Dowans Brigedia Jenerali (mstaafu), Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi, ulikuwa ni usanii wa picha ya Rostam kwani baadaye ndiye atakayelipwa fedha hizo za Dowans. Alisema CHADEMA haitakubali fedha hizo zilipwe na kwamba itaitisha maandamano nchi nzima kupinga.

Dk. Slaa alisema ufisadi mwingine wa serikali katika sakata hilo la Dowans ni serikali kuweka mawakili watatu kinyemela na kupanga kuwalipa sh bilioni tano. "Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema …nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli," alisema Dk. Slaa.

Katika hatua nyingine, Dk. Slaa alisema moto uliowashwa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) umeifanya serikali ya CCM akiwamo Rais Jakaya Kikwete kushindwa kulala. Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikungi katika Jimbo la Singida Mashariki jana aliposimama kuwasalimia wakati akitokea Singida kuelekea Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema Lissu ni mbunge jasiri katika Bunge ambaye amediriki kumnyooshea kidole hata Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema. Katika hotuba yake hiyo alisema wananchi hawana imani tena na serikali ya Jakaya Kikwete na kama atafanya mchezo hataweza kurudisha imani hiyo wala kumaliza kipindi chake cha utawala.

Alisema mambo mengi yamejitokeza ambayo yamesababisha wananchi kukosa imani naye, yakiwamo ya ufisadi unaofanywa na yeye mwenyewe pamoja na watu walio karibu naye. "Wananchi wanaona yanayofanyika, mtoto wa rais, Ridhiwani Kikwete, amemaliza shule hivi karibuni lakini leo ni bilionea. Haya yote hayawezi kuvumilika hata kidogo."

Akiwashukuru wananchi wa kijiji hicho, Dk. Slaa alisema si tu kwamba wamemchagua mbunge wa Jimbo la Singida, bali ni mbunge wa nchi nzima na kwamba ni nyundo itakayotumika kuwaponda CCM. Akizungumzia suala la CCM kujivua gamba, alisema neno fisadi alilianzisha yeye na chama chake na kwamba anayepaswa kujivua gamba hilo ni Kikwete halafu awavue wengine.

Chanzo: Tanzania Daima
 
don't blame the messenger, blame jk who decided to sit on his hands and let his crooks friends destroying the country.
 
dah! Kweli noma,wanataka nini zaidi ya hiyo mihela? Jamani tudanganyeni kwa kutujengea nchi yetu.na kuyawezesha maisha bora kwa kila Mtz
 
Kumbe Dr Slaa ndio Mwalimu wa Kuzomea! Hopeless!

Senior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png



Join Date : 16th February 2011

Hivi Kwenye Hiyo habari yenye zaidi ya paragraph 6 hilo la kuzomea tu ndo umeliona
ama kweli umetumwa kuja kuwakilisha chama cha Magamba!!!

Lakini sikushangai ni umejiunga siku mbili kabla ya Valentine day kwa hiyo mawazo yako yatakuwa ya Ki-valentine valentine.
 
Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao.

Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari? Naelewa kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa waziri katika wizara nyingi sana hapa Tanzania kabla ya kuwa Rais; ninavoelewa mimi Rizwan kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu, eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hiyo ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa.

Kama mna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi?) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujue ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi.
 
Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao.

Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari? Naelewa kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa waziri katika wizara nyingi sana hapa Tanzania kabla ya kuwa Rais; ninavoelewa mimi Rizwan kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu, eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hiyo ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa.

Kama mna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi?) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujue ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi
Ni sahihi mawazo yako, kama ni kweli tumekwisha
 
["Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema …nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli," alisema Dk. Slaa.

Hapa Dr.Slaa anatupiga fix , Rostam Aziz hawezi kuwa mjinga hivyo!!
 
"Nilimtaja Rostam kuwa ni mmoja wa mafisadi kule Mwembeyanga, naye alinitumia vitisho kwa ujumbe mfupi kuwa nina sekunde chache za kuishi hivyo nipige magoti, nisali. Nilimjibu na nasema …nilizaliwa siku moja na nitakufa siku moja, sitaogopa kusema ukweli," alisema Dk. Slaa.
Duh hii kali
 
Mke wa Mbowe alivyotishiwa kufa alikwenda polisi kushtaki na sasa kesi ipo mahakamani kama kweli Dr Slaa na wewe umetishwa kama utauwawa sasa peleka hizo taarifa polisi sio kuwashtakia wananchi suala lako la kuuliwa.

RA ni Mtanzania na ana haki ya kumiliki hizo pesa, Dr Slaa naamini wewe ni Dr wa ukweli hasa nilipoangalia kwenye youtube ulipokuwa unamuelezea yule mama kuhusu mtoto wake mlemavu nilifurahi sana juu ya upeo wako wa elimu ya Afya ulionayo lakini je mbona kwenye suala hili la sasa la Riz na RA kutaka kukuuwa mbona huweki vidhibitisho? Tutakuamini vipi?
 
Pepombili,

Jamvi hili si maahali pa kutoa ushahidi. Kuna mahali pa kutolea ushahidi. Kauli zangu zimetolewa kwenye hotuba ya kuwaelimsha Watanzania, tena in this case wa Jimbo la Igunga Jimbo la Rostam Aziz. Kazi yangu kama Katibu Mkuu katika mikutano ya hasdhara si kutoa ushahidi bali kueleza na kuonyesha uozo ndani ya CCM na Serikali yake ili Watanzania waweze kufunguka macho. Mwenye kuona kaonewa ana mahali pa kutaka "redress" kama anafikiri nilichosema siyo kweli.

Nilikwisha kueleza kuwa "mahakamakubwa kuliko zote kwa mwanasiasa ni 'wananchi' (Ibara ya 8 ya Katiba). Tuliowataja leo wako mahakamani, Fedha za EPA mlizobishia angalau JK aliutangaza Bungeni kuwa zimerudishwa sehemu (Japo CAG katika Taarifa yake ya Hesabu za Serikali Kuu anasema fedha hizo hadi Machi 2011 hajaona zimeingizwa akaunti gani japo zilihamishiwa TIB June, 20, 2010 (Jambo linalozua utata mpya kabisa katika historia ya ufisadi ikizangatiwa kuwa 2010 ilikuwa mwaka wa Uchaguzi-au zilirudishwa zikaenda tena kwenye uchaguzi kuisaidia CCM au hazikurudishwa kabisa na inakuwa usanii tu).

Kama Rizwani anaona ameonewa aende yeye mahakamani mimi nimemaliza kesi kwenye mahakama ya wananchi, lakini nadhani ni vema ungelinukuu vizuri "conclusion yangu badala ya kuchakachua statement yangu".

Dr Slaa siwezi kupinga unachokiongea maana wewe ni miongoni mwa viongozi wa kisiasa hapa Tanzania, je? vipi wananchi tunaweza kuthibitisha kauli zako unazosema tunaomba utuletee na ushahidi na sio maneno maana tunawaelewa wana siasa mulivyo na maneno mengi vinywani mwenu, kama unazo hizo documents za ushahidi wa mapato ya Muheshimiwa RA na RIZ kwa nini musiwatumie wanasheria wenu wa CHADEMA kuwapeleka mahakamani kama muna wasiwasi na source za mapato yao.

Mengi unayoyaongea ni kwa ajili ya maslahi ya nchi lakini je Rizwan Kumiliki mabilioni ni kitu cha hatari? Naelewa kwa ufahamu wangu Rizwan ni mtoto wa RAIS na baba yake alikuwa waziri katika wizara nyingi sana hapa Tanzania kabla ya kuwa Rais; ninavoelewa mimi Rizwan kumiliki Bilioni moja si kitu cha ajabu, eti kamaliza shule juzi ndio asiweze kumiliki hiyo ela haiingii akilini hata kidogo kwa mtoto wa kimasikini sawa ila Riz sio mtoto wa kimasikini akashindwa kujiingiza kwenye masuala ya kutafuta pesa.

Kama mna ushahidi wa wizi wa fedha muende mahakamani au kama ni siasa tu basi endeleeni (sikupingi Dr Slaa huwa napenda ila ushahidi wako uko wapi?) tuwekee ushahidi ila tunapomwita mtu fisadi kama Riz kweli tujue ili tusipate dhambi kumjadili mtu bila ya ushahidi.
 
Ahsante mheshimiwa DR Slaa kwa ufafanuzi wako mzuri.

Naamini kwamba mnao wanasheria wengi kwenye chama chenu kweli umeshtaki kwa wananchi hilo sio baya je nini mpango wenu juu ya kupeleka ushahidi wenu mahakamani na sisi wananchi ili tuweze kufuatilia na kama ukweli ukithibitisha basi tukuunge mkono Mheshimiwa DR
Pepombili,

Jamvi hili si maahali pa kutoa ushahidi. Kuna mahali pa kutolea ushahidi. Kauli zangu zimetolewa kwenye hotuba ya kuwaelimsha Watanzania, tena in this case wa Jimbo la Igunga Jimbo la Rostam Aziz. Kazi yangu kama Katibu Mkuu katika mikutano ya hasdhara si kutoa ushahidi bali kueleza na kuonyesha uozo ndani ya CCM na Serikali yake ili Watanzania waweze kufunguka macho. Mwenye kuona kaonewa ana mahali pa kutaka "redress" kama anafikiri nilichosema siyo kweli.

Nilikwisha kueleza kuwa "mahakamakubwa kuliko zote kwa mwanasiasa ni 'wananchi' (Ibara ya 8 ya Katiba). Tuliowataja leo wako mahakamani, Fedha za EPA mlizobishia angalau JK aliutangaza Bungeni kuwa zimerudishwa sehemu (Japo CAG katika Taarifa yake ya Hesabu za Serikali Kuu anasema fedha hizo hadi Machi 2011 hajaona zimeingizwa akaunti gani japo zilihamishiwa TIB June, 20, 2010 (Jambo linalozua utata mpya kabisa katika historia ya ufisadi ikizangatiwa kuwa 2010 ilikuwa mwaka wa Uchaguzi-au zilirudishwa zikaenda tena kwenye uchaguzi kuisaidia CCM au hazikurudishwa kabisa na inakuwa usanii tu).

Kama Rizwani anaona ameonewa aende yeye mahakamani mimi nimemaliza kesi kwenye mahakama ya wananchi, lakini nadhani ni vema ungelinukuu vizuri "conclusion yangu badala ya kuchakachua statement yangu".
 
Mkuu, Dr wa ukweli kaisha kwambia kapeleka kwa mahakama kubwa ambayo ni wananchi sasa unataka apeleke kwenye mahakama za CCM ambazo wanachakachua haki kila siku? Kesi ya Mtikila kuhusu mgombea binafsi hukona jinsi mahakama zinavyokologana, halafu wakilipeleka mahakamani mahakama zitapiga marufuku kuzungumzia ufisadi kwa kisingizio kuna kesi mahakamani au wakatoa sababu kama kwenye kesi ya Mengi, na sisi wananchi tutakosa haki ya kujua nini mafisadi wanafanya maana kesi inaweza kuchukua hata miaka kumi.

Hongera sana mh Dr Slaa tuko pamoja
Ahsante mheshimiwa DR Slaa kwa ufafanuzi wako mzuri.

Naamini kwamba mnao wanasheria wengi kwenye chama chenu kweli umeshtaki kwa wananchi hilo sio baya je nini mpango wenu juu ya kupeleka ushahidi wenu mahakamani na sisi wananchi ili tuweze kufuatilia na kama ukweli ukithibitisha basi tukuunge mkono Mheshimiwa DR
 
Back
Top Bottom