Sizonje kasema waambieni wachezaji watakula pindi wakifanya mazoezi yakamridhisha na mechi wakashindaSizonje kubali wakwambie ukweli..!!!
Huku uwanjani wachezaji wanafanya mazoezi ya nguvu, ILA HAWAJALA!
Tia maji tia maji, huchelewi kuwakuta ni mizoga wanaliwa na ndege! NIKIJA DAR NTAKUNONG'ONEZA!!!
sizonje,naona wachezaji hawakabi wala kushambulia,mmoja yule kule kalala chali,mwingine yule kipa,hapigi mpira mbele,kakalia kupiga danadana tu,mwingine yule beki anaenda kubadili bukta,aliyonayo imechanika kwa nyuma,bora ulimwambia IGP asimamishe mpira kwanza,hawa ukawa wanashambulia sana,na nina hisi wana njumu za chuma,wachezaji wetu kila wakiwakaba wanaumia

umeandika vizuri sana...hongeraMpendwa Sizonje habari za siku.... natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti...
Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi... kocha mzembe na anafuga uvundo....
Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!!
Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo!! Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!!
Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha!!
Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe!!
Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora!!
Sizonje usichanganyikiwe... mambo bado ndio kwanza safari inaanza!! Ishike ngao na kigao kuyahimili majira!!!
Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.
SIZONJE sijui anapeleka wapi timu.....
Alafu mbona Sizonje amepewa majina mengi this time?.......
Mala Juma Ponda Mali ,Mala Nyampala,Tembo, Sasa nasikia anaitwa Trump ......
Kuna ukweli juu ya majina ya Shizonje?.......
Sema we mpigaji ndo huna hamu nae. Sisi huku ni mkombozi wetu wanyonge. 2020 lazima spate kula nyingi sana asilimia mia
Hajui pumba za mahindi ndio zina virutubisho vyote ndio maana siku hizi watu wanakula dona, sembe halina kituHahaahh Lakini Hizo Pumba Kuku Au Ng'ombe si Wanakula?
Mmesahau kuna mikataba ya miaka mia moja humu hembu tuwe na utu jama tumsaidie Rais kuendesha hili gurudumu la maendeleo tuache kulia lia Mungu hapendi namalizia kusema asiyefanya kazi na asile na mikono milegevu hujenga paa bovu
Sizonje kashachanganyikiwa,yeye ni kuteua kutengua.kila aliemzunguka hamuamini,anaona yy ni mtakatifu sanaa.Magufuli ana nia njema sana na chi hii na jitihada zake zinaonekana lakini tatizo alilonalo linalomrudisha nyuma ni kutotaka kusikiliza ushauri na kujifanya kuwa yeye ana majibu ya kila tatizo la nchi hii!! Mheshimiwa ni vyema ukasikiliza ushauri mzuri kutoka popote pale na ufanyie kazi; kazi uliyonayo ni ngumu na nzito lakini KUKUOMBEA TU hakutoshi sikiliza ushauri; A ONE MAN"S ARMY CAN NEVER WIN A WAR!!!