Sizonje usichanganyikiwe, Mambo bado!!

Sizonje usichanganyikiwe, Mambo bado!!

Mpendwa Sizonje habari za siku.... natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti...

Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi... kocha mzembe na anafuga uvundo....

Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!!

Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo!! Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!!

Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha!!

Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe!!

Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora!!

Sizonje usichanganyikiwe... mambo bado ndio kwanza safari inaanza!! Ishike ngao na kigao kuyahimili majira!!!

Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.
Uzi uko pale pale hakuna cha matangazo ya NSSF au NIHF wala nini sasa macho kodo..kilichopo ngoja tujaribu kumnanga..hivi kweli na uwezo wote ule Kitaifa Nchi nzima walijua kuwa jamaa anajiweza na kipimo ni jinsi aliyoweza kusimamia mazoezi pale kocha alipo mkabidhi idala ya uwanja na miundo mbinu kuhakikisha mashabiki na wachezaji wanapata kila kinachostahiki kama running truck za uwanja na ambullance zikivuka madaraja na kufika kwenye kiwanja bila shida...na hata mashabiki wanasafiri kwa mabasi nchi nzima kwa sababu kocha alimwamini msaidizi kuwa anaweza..na kweli aliweza kujenga miundo mbinu ya viwanja.

Sasa hili la mnangaji eti Sizonje akuweza toka awali, kwanini mnangaji nae alijua Szonje hawezi akaenda kuvaa vibwebwe mbele ya hadhara na matambala mwili mzima na kushabikia Kocha ampe ukocha Sizonje wakati yeye binafsi alijua kuwa kocha kasema alimbeba Sizonje yeye pia anashiriki vipi usichokiamini.

Na kweli mlikutana na Sizonje wakati kocha anampitisha na uongozi wa timu kwa mashabiki ...wewe ulijua Sizonje akija atakufaidisha kama Kocha mstaafu ulivyomfanyia akaamua kukuzawadia fursa. Sasa fursa ya cheki toka kweye mifuko ya vyanzo vya Team Kocha kasema hapana viende kuboroshea Timu ili Wachezaji na Wanachama na Wapenzi wa Timu wapate matokeo sahihi na si kuwa kichwaa cha mwendawazimu kila mmoja anajifunzia kunyolea kama alivyosema Mzee Mwinyi.

Ili la kusema alikua anakwambia inakuwaje Mazungumzo binafsi mlioyayafanya na kocha wa zamani na huyu kocha wa sasa ukadiriki kuyaweka hadharani kwanini hukuyaweka hadharani kipindi hicho..na si baada ya matarajio uliyoyatarajia MNANGAJI kushindwa sasa ukaamua kumnanga huku ukitumia fursa hiyo kujifurahisha kwa kukosa weredi wa kuhalalisha malalamiko yako.

Sizonje ana maalifa na anajua anachofanya na hata ilipomlazimu kocha kumkabidhi timu Sizonje utendaji wa Szionje ndio ulikuwa turufu namba moja...kwani pamoja na kuwa kocha mstaafu aliwahi kumpereka jikoni akawandaliwe na kupima chakula cha wachezaji na wapenzi wa timu wanaofika kula kwenye club bado Sizonje alionyesha umahiri kiasi kuwa wachezaji waliweza kujua vitu mbalimbali vilivyoko jikoni kiasi ikawapa hamasa kuanza kufuatilia ni aina gani ya chakula kinafika kwenye jiko lao na kuandaliwa kwa ajili yao ..ili wajue ni aina gani ya vyakula walivyo navyo na vina thamani gani kwa afya yao na maendeleo ya Team yao. Ni Sizonje aliyekua mstari wa mbele kusimama na kusema kile alichokiamii kwenye vikao vya clabu toka enzi hizo za kocha Mkubwa Mstaafu kabla ya alieondoka kumpisha Sizonje.

Muache Sizonje apige kazi ushapata mtaji fanya FURSA nyingine ...ikibidi hata Mataifa ya Nje waweza tembea nao kwenye fursa milango itafunguka ...lakini hii kulazimisha milango ya Club..itumike ovyo kutunisha mifuko ya wachache nooooo Mnangaji tafuta jingine la kumnanga Sizonje ...ametutoa kimaso maso sie wengine wenye mapenzi ya kuona keki ya TEAM YA TAIFa inaliwa na wengi na si viongozi wachache wa Klub
 
Ni wapuuzi sana hawa, hii nchi imejaa wanafiki sana, angalia majina ya kinafiki anayopewa raisi, nyie ndio mtasababisha hii forum ifungiwe, endeleeni kumchafua chafua, mwenzenu kafungwa kisa ameota, kufungiwa hii ni issue ndogo sana
Dawa inafanya kazi. Sizonje kang'ang'ania posho za watu na pia anawapunguzia watu mishahara ili waishi km mashetani.
Acha wamseme sbb sihataki kushauriwa. Hakuna uzi mtamu JF km huu
 
Japo umetumia mafumbo Lakini meseji yako mbovu
Mara tulipokuwa tunashabikia mpira Mara wachezaji wenzio wanakujua hujui tuelewe lipi sasa....!!
 
Sinzonje nguvu sio mtaji ,mtaji wa kweli ni akili pole sana sizonje nchi haiendeshwi kwa hisia kali za hasira na uchungu wa mama aliyekua labor
 
Sizo***** kubali kucheza mechi za kirafiki ili kuijengea uwezo timu yako....ni kweli mashabiki hawakufundishi sheria za mchezo lakini kelele zao huongeza chachu na hamasa uwanjani. Takwimu za mhazini wa timu zinaonesha kuwa "gate collection" inazidi kupungua siku hadi siku na hata sponsors wa timu nao wanasuasua kutekeleza ahadi zao kwa hiyo sintoshangaa sana ukisema kuwa umekosa nauli ya kusafirisha wawakilishi wa timu yako kwenda kushiriki mechi za ughaibuni......kama ikikupendeza wewe kama kocha waruhusu basi hata wacheze ligi za mchangani hapahapa nyumbani......Yakikufika shingoni, usione aibu kurudisha mpira kwa benchi la ufundi ili usukwe upya ....... waswahili walisema, Kukubali kushindwa ni uungwana pia... BADO TUNAKUOMBEA SIZONJE
 
Uzi uko pale pale hakuna cha matangazo ya NSSF au NIHF wala nini sasa macho kodo..kilichopo ngoja tujaribu kumnanga..hivi kweli na uwezo wote ule Kitaifa Nchi nzima walijua kuwa jamaa anajiweza na kipimo ni jinsi aliyoweza kusimamia mazoezi pale kocha alipo mkabidhi idala ya uwanja na miundo mbinu kuhakikisha mashabiki na wachezaji wanapata kila kinachostahiki kama running truck za uwanja na ambullance zikivuka madaraja na kufika kwenye kiwanja bila shida...na hata mashabiki wanasafiri kwa mabasi nchi nzima kwa sababu kocha alimwamini msaidizi kuwa anaweza..na kweli aliweza kujenga miundo mbinu ya viwanja.

Sasa hili la mnangaji eti Sizonje akuweza toka awali, kwanini mnangaji nae alijua Szonje hawezi akaenda kuvaa vibwebwe mbele ya hadhara na matambala mwili mzima na kushabikia Kocha ampe ukocha Sizonje wakati yeye binafsi alijua kuwa kocha kasema alimbeba Sizonje yeye pia anashiriki vipi usichokiamini.

Na kweli mlikutana na Sizonje wakati kocha anampitisha na uongozi wa timu kwa mashabiki ...wewe ulijua Sizonje akija atakufaidisha kama Kocha mstaafu ulivyomfanyia akaamua kukuzawadia fursa. Sasa fursa ya cheki toka kweye mifuko ya vyanzo vya Team Kocha kasema hapana viende kuboroshea Timu ili Wachezaji na Wanachama na Wapenzi wa Timu wapate matokeo sahihi na si kuwa kichwaa cha mwendawazimu kila mmoja anajifunzia kunyolea kama alivyosema Mzee Mwinyi.

Ili la kusema alikua anakwambia inakuwaje Mazungumzo binafsi mlioyayafanya na kocha wa zamani na huyu kocha wa sasa ukadiriki kuyaweka hadharani kwanini hukuyaweka hadharani kipindi hicho..na si baada ya matarajio uliyoyatarajia MNANGAJI kushindwa sasa ukaamua kumnanga huku ukitumia fursa hiyo kujifurahisha kwa kukosa weredi wa kuhalalisha malalamiko yako.

Sizonje ana maalifa na anajua anachofanya na hata ilipomlazimu kocha kumkabidhi timu Sizonje utendaji wa Szionje ndio ulikuwa turufu namba moja...kwani pamoja na kuwa kocha mstaafu aliwahi kumpereka jikoni akawandaliwe na kupima chakula cha wachezaji na wapenzi wa timu wanaofika kula kwenye club bado Sizonje alionyesha umahiri kiasi kuwa wachezaji waliweza kujua vitu mbalimbali vilivyoko jikoni kiasi ikawapa hamasa kuanza kufuatilia ni aina gani ya chakula kinafika kwenye jiko lao na kuandaliwa kwa ajili yao ..ili wajue ni aina gani ya vyakula walivyo navyo na vina thamani gani kwa afya yao na maendeleo ya Team yao. Ni Sizonje aliyekua mstari wa mbele kusimama na kusema kile alichokiamii kwenye vikao vya clabu toka enzi hizo za kocha Mkubwa Mstaafu kabla ya alieondoka kumpisha Sizonje.

Muache Sizonje apige kazi ushapata mtaji fanya FURSA nyingine ...ikibidi hata Mataifa ya Nje waweza tembea nao kwenye fursa milango itafunguka ...lakini hii kulazimisha milango ya Club..itumike ovyo kutunisha mifuko ya wachache nooooo Mnangaji tafuta jingine la kumnanga Sizonje ...ametutoa kimaso maso sie wengine wenye mapenzi ya kuona keki ya TEAM YA TAIFa inaliwa na wengi na si viongozi wachache wa Klub
Mkuu umemaliza.... shukrani sana.
 
Dawa inafanya kazi. Sizonje kang'ang'ania posho za watu na pia anawapunguzia watu mishahara ili waishi km mashetani.
Acha wamseme sbb sihataki kushauriwa. Hakuna uzi mtamu JF km huu
Hahahaha Sizonje anatisha!! Ameanza nunua mashabiki toka timu pinzani ili kumpamba!!!
 
Sinzonje nguvu sio mtaji ,mtaji wa kweli ni akili pole sana sizonje nchi haiendeshwi kwa hisia kali za hasira na uchungu wa mama aliyekua labor
Hahahahaha sikutegemea hata nyie mashabiki wa Sizonje mtasema haya sikumoja doh kweli Sizonje kachokwa!!
 
Sizo***** kubali kucheza mechi za kirafiki ili kuijengea uwezo timu yako....ni kweli mashabiki hawakufundishi sheria za mchezo lakini kelele zao huongeza chachu na hamasa uwanjani. Takwimu za mhazini wa timu zinaonesha kuwa "gate collection" inazidi kupungua siku hadi siku na hata sponsors wa timu nao wanasuasua kutekeleza ahadi zao kwa hiyo sintoshangaa sana ukisema kuwa umekosa nauli ya kusafirisha wawakilishi wa timu yako kwenda kushiriki mechi za ughaibuni......kama ikikupendeza wewe kama kocha waruhusu basi hata wacheze ligi za mchangani hapahapa nyumbani......Yakikufika shingoni, usione aibu kurudisha mpira kwa benchi la ufundi ili usukwe upya ....... waswahili walisema, Kukubali kushindwa ni uungwana pia... BADO TUNAKUOMBEA SIZONJE
Kocha wetu hashauriki na hafundishiki!! Timu inashuka daraja kila uchao!!
 
Mkui weka kumbukumbu sawa sikumpigia kura sizonje
Kwa habari ya kura sijui coz ni siri ya mtu ila wewe ni miongoni mwa mashabiki mlolpigia chapuo Sizonje awe kocha!!
 
hiyo jana tu kabadilisha full beki wote, sizonje kaa mbali naye ana moto wa kasi kama chesea
 
Tusiposhuka daraja na kocha huyu, hatutakaa tushuke tenaaa. Twende Kazi Sizonje, kaba mwenyewe, shambulia mwenyewe, fanya sub mwenyewe, sajili mwenyewe, timua mwenyewe, mapato ya ticket kusanya kwa mbinu unazozijua ww, yani maliza kila kitu, ikiwezeka ata filimbi ya mwamuzi chukua uchezeshe mwenyewe maana hakuna linalokushinda chini ya jua
 
Mpendwa Sizonje habari za siku.... natumaini u buheri wa afya kibaiolojia japokuwa kiroho u tofauti...

Rafiki yangu Sizonje nakumbuka enzi zile tukijadili mpira ulivyokua hodari kumlaumu kocha!! Kwamba kocha wa timu yetu hawezi... kocha mzembe na anafuga uvundo....

Kadiri tulipokutana kila baada ya sentensi tatu lazima umseme kocha kila siku ikawa hamkani si shwari!!

Sizonje utakumbuka kocha alikuvumilia sana japokuwa ulikua huwezi!! Mdomo na maneno mengi yalikubeba kwa mashabiki lakini wachezaji wenzio walikujua!! Ulikua bingwa wa kukariri tarakimu za mchezo bila ujuzi na weledi wa mchezo!! Hata kocha alipoonywa sana juu ya kiwango chako kibovu bado alikubeba ingawa ulimsogoa!!

Hayawi hayawi yakawa Sizonje!! Kauli zako zikalipa!! Kocha akastaafu na ukocha ukapewa wewe!! Kila mtu ndani ya timu akiduwaa mashabiki waliolewa kauli zako tamu ziso kifani walikubeba hatimaye ukawa kocha!!

Awali ulionesha uwezo wa kukonga mashabiki kwa sifa na vitimbi kemkem!! Siku zikasonga mashabiki wakaona timu inarejea nyuma kuliko ilikokuwa kwa kocha mzembe!!

Nakujua Sizonje!! Hupendi kukosolewa na wala hupendi kimya cha sifa!! Vigelegele vya mashabiki na vifijo vimekoma!! Mbinu zote za michezo ulizotumia zimebuma!! Timu inarudi nyuma kwa kasi na wachezaji wameshapoteza mori!! Kila ugusapo sasa hapagusiki!! Wachezaji wanaonesha ari machoni pako tu lakini uwanjani wamedorora!!

Sizonje usichanganyikiwe... mambo bado ndio kwanza safari inaanza!! Ishike ngao na kigao kuyahimili majira!!!

Kwa leo naishia hapa Sizonje nikija mjini ntakutembelea tule maboga ya enzi zetu.
Cha ajabu sasa kocha Sizonje hapendi mechi za ugenini ameng'ang'ana na game za ndani...
 
Back
Top Bottom