Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,320
- 24,191
- Thread starter
- #101
Sawa mkuu ungweza kuelezea kwa picha kuliko hiyo ya Daily News ingependeza kidogo.Poleni sana kwa speculations zenu!
Kwa taarifa yako kuanzia stesheni (mwanzo wa mradi) hadi Ilala (umbali wa km 2.5) treni inapita juu (via duct). Kwenye umbali huo (2.5km) tayari nguzo zote zimeshajengwa na kukamilika. Juu ya hizo nguzo zinalazwa beams ambazo hupachikwa (zaidi ya 70% ya beams zote kwenye eneo hilo zimeshawekwa). Beam hizo zinatengenezwa ndani ya kambi ya Ilala (Njoo ndani ya kambi ya Ilala uone kama beams hazitengenezwi). Katika eneo hilo almost kazi ya zege imebaki kidogo sana ndiyo maana huoni magari ya zege yakikimbizana.
Kuhusu magari ya kifusi inabidi nicheke kwanza😁😁😁!! Kifusi kinatumika kwenye ujenzi wa tuta (embankment), sasa kifusi cha nini katika eneo hilo wakati treni inapita juu? Acha ukilaza.
Hata hivyo maeneo ya mbele kama Vingunguti, Banana, nk. ambapo treni inapita chini hivyo tuta (embankment) kujengwa, ujenzi wa tuta haufanyiki wakati wa mvua. Kusisitiza ujenzi wa tuta wakati mvua inanyesha ni kudhihirisha tena kwamba wewe ni KILAZA MKUBWA wa mambo ya uhandisi ujenzi.
Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe! Halafu watu wenye nongwa kama nyie ndio mtakao kuwa wa kwanza kwa kiherehere kupanda treni reli itakapokamilika.