Huihui2
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 5,277
- 8,004
Hata mimi nina threads kadhaa za kuuponda mkataba wa DP World na Tanzania kutokana na vipengere visivyo na manufaa kwa nchi yetu. Kimsingi kila mwananchi kwa sasa amekuwa bingwa wa mikataba na uwekezaji kutokana na maamuzi ya Rais Samia kufungua uhuru wa maoni ambao ulidhibitiwa na mtangulizi wake.
Aidha watu wanaongea kwa vile teknolojia ya mawasiliano imepanuka sana ukilinganisha na miaka ambayo akina Mkapa au Kikwette walipokuwa wanafanya maamuzi mbalimbali.
Maamuzi ya Rais Samia pamoja na mapungufu yake ni maamuzi ya kawaida tu kwa Marais waliopita au kwa Marais wengine wa Afrika. Ila yeye ameshambuliwa left, right, front and back kutokana na wakati, vilevile na haiba yake kama Rais Mwanamke, Muislamu na Mzanzibari.
Bado kwa mtazamo wangu huyu ndiye Rais aliyeituliza nchi iliiyokuwa imekumbwa na sintofahamu za kibabe na kidikteta zilizofanywa na mtangulizi wake. Nitampa kura yangu kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kuwa yeye ndiye mwenye uwezo kuliko Watanzania wengine wenye visasi, jazba na taharuki.
Aidha watu wanaongea kwa vile teknolojia ya mawasiliano imepanuka sana ukilinganisha na miaka ambayo akina Mkapa au Kikwette walipokuwa wanafanya maamuzi mbalimbali.
Maamuzi ya Rais Samia pamoja na mapungufu yake ni maamuzi ya kawaida tu kwa Marais waliopita au kwa Marais wengine wa Afrika. Ila yeye ameshambuliwa left, right, front and back kutokana na wakati, vilevile na haiba yake kama Rais Mwanamke, Muislamu na Mzanzibari.
Bado kwa mtazamo wangu huyu ndiye Rais aliyeituliza nchi iliiyokuwa imekumbwa na sintofahamu za kibabe na kidikteta zilizofanywa na mtangulizi wake. Nitampa kura yangu kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa kuwa yeye ndiye mwenye uwezo kuliko Watanzania wengine wenye visasi, jazba na taharuki.