Siungi mkono Rais kutukanwa!

Siungi mkono Rais kutukanwa!

Kwa hiyo unataka kujilinganisha na Rais wa nchi?

Gharama za kukutunza unataka kuzilinganisha na gharama za kumtunza Rais?

kwa hiyo sheria za nchi kuna watu zinawaruhusu kutukana kwa sababu ya nyadhifa zao?. Malofa Wa Lumumba mna matatizo kweli
 
Ok so ukiona mwana wa jiran anatukana mama yake na wewe utaenda kumtukana wako??

Inawezekana mwenzako ni utamaduni wao na wewe je?????

ila kiongozi akitukana ni sawa, unakumbuka tusi la malofa? unajua kiwango cha matusi yanayoporomoshwa kwa viongozi wa upinzani? mi hatua gani zimewahi kuchukuliwa? mbona mnapenda kutukuzwa? kama ni matusi yachukuliwe hatua kwa wote.
 
Ni wazi kwa post hii ya Lema hajapendezwa na kile kitendo tena kuchanga hadharani ndio kumeonesha kejeli zaidi na kuyaunga mkono matusi dhidi ya Rais...!

Hakika Lema kanitoa machozi kwa uzalendo alio onesha!

Lema amepingana nao wazi wazi wala hajajificha!

Machozi yako wapi?
 
Ni Kweli, Lakini Busara Ya Kumkanya Na Kumsaidia Ni Bora Zaidi Kuliko Kumwacha Akaozee Jela Wakati Inawezekana Kumrekebisha Mtaani.
Je, Huyo Hakuwa Mmoja Kati Ya Vijana Walioitwa Wapumbavu Kisa Wanataka Mabadiliko?

Hii NJI ni hatare mnoo DUH!! asee challiangu mbona yule poyoyo aliekuja jangwani huku kabugia virroba afu akatutapikia eti sisi ni MALOFA aseee!!! WAPUMBAVU!!! mbona hili poyoyo halijakamatwa mpaka leo lipo kitaa tu linapiga virrroba kwenda mbeleASEE!!
 
Ukiona manyoya ujue kaliwa. Upinzani umekamatwa pabaya. Tatizo mnachezea akili kubwa mno. Wananchi wengi wanafahamu nia njema ya Mhe. Rais kupitia mambo makuu anayoyafanya. Sina haja ya kuwakumbusha maana yako wazi. Naona kila hoja inazimwa. It is open that you cannot win him please join the movement. Naona ujuha mwingi mara kuziba midomo, mara nguo nyeusi kama mmefiwa, mara kidole cha kati, mara lugha za vijiweni. Nawashauri mjifunze kwa wapigania haki mfano Mandela na Martin king kama kweli mnaamini kwamba kuna uminywaji wa demokrasia nchini. Ukisoma vitabu vyao utaona hakuna hata sehemu waliwahi kutumia lugha isiyo na staha. Jibaba zima linakuwa kama toto dogo. Zero kabisa.
 
Ukiona manyoya ujue kaliwa. Upinzani umekamatwa pabaya. Tatizo mnachezea akili kubwa mno. Wananchi wengi wanafahamu nia njema ya Mhe. Rais kupitia mambo makuu anayoyafanya. Sina haja ya kuwakumbusha maana yako wazi. Naona kila hoja inazimwa. It is open that you cannot win him please join the movement. Naona ujuha mwingi mara kuziba midomo, mara nguo nyeusi kama mmefiwa, mara kidole cha kati, mara lugha za vijiweni. Nawashauri mjifunze kwa wapigania haki mfano Mandela na Martin king kama kweli mnaamini kwamba kuna uminywaji wa demokrasia nchini. Ukisoma vitabu vyao utaona hakuna hata sehemu waliwahi kutumia lugha isiyo na staha. Jibaba zima linakuwa kama toto dogo. Zero kabisa.
 
"Ninafikiri ni vyema na muhimu tukaendelea kukosoana kwa njia mbali mbali, lakini kwa hakika kabisa siungi mkono rais kutukanwa kwa kejeli ambazo zina sura ya mizaha na sio mabadiliko, Rais kuitwa BWEGE ni kosa na utovu wa nidhamu.

Kosa hili halipaswi kutiwa moyo wala kuungwa mkono, lakini kumwambia Kijana huyu kuwa alikosea ni jambo muhimu zaidi na la busara"

Godbless Lema (Mp)
Great thinking Godbless
 
Mkuu Godbless J Lema Mbona wewe ulimuita waziri Mkuu Pinda MWONGO kama SHETANI? Bwege na shetani lipi kubwa?

Hata mimi siungi mkono, ila adhabu aliyopewa huyu kijana ni kubwa kuliko! Hatukuwa na namna zaidi ya kumuwezesha ili amalizane na tatizo hilo.

Hata hivyo hii sheria ya mtandao ni kandamizi mno halafu inakata upande mmoja.
Sasa nikikuita wewe bwege unaonaje? Halafu ndio mtu kwa chuki tu anamuita rais wa jamhuri bwege. Yaani Watanzania wengi waliyomchagua na wao ni mabwege. Kumchangia huyo kijana ni sawa na kuunga mkono alichokifanya.
 
"Ninafikiri ni vyema na muhimu tukaendelea kukosoana kwa njia mbali mbali, lakini kwa hakika kabisa siungi mkono rais kutukanwa kwa kejeli ambazo zina sura ya mizaha na sio mabadiliko, Rais kuitwa BWEGE ni kosa na utovu wa nidhamu.

Kosa hili halipaswi kutiwa moyo wala kuungwa mkono, lakini kumwambia Kijana huyu kuwa alikosea ni jambo muhimu zaidi na la busara"

Godbless Lema (Mp)

Hongera Mh Lema kuliona na kulikemea hili.
 
Sawa, lakini hata mimi sidhani kabisa kama hilo kosa linaendana na adhabu aliyopewa huyo kijana.

Angeniita mimi 'bwege' unadhani hata angekamatwa?

Au hata ningeenda kumfungulia mashitaka unadhani angepewa hiyo adhabu aliyopewa?
Haiyumkini utadai nawe uongozwe na ving'ora kama ilivyo kwa rais. Tuifunze kuheshimu mamlaka hata kama waliokabidhiwa hatuwapendi.

Hivi kwa mfano kumuita Kingwendu kichaa na kumuita mh. rais kichaa, ipi ni habari ya magazeti ya udaku na ipi itaingia main stream?
 
Haiyumkini utadai nawe uongozwe na ving'ora kama ilivyo kwa rais. Tuifunze kuheshimu mamlaka hata kama waliokabidhiwa hatuwapendi.

Hivi kwa mfano kumuita Kingwendu kichaa na kumuita mh. rais kichaa, ipi ni habari ya magazeti ya udaku na ipi itaingia main stream?

Hoja yako ni nini sasa hapo?
 
Back
Top Bottom