Siungi mkono hotuba ya Rais Kikwete, SA

Nikiwa kama mtanzania niishie SA nakubaliana na speech ya JK
Ujue wasouth wengi walikua hawajui mchango wa TZ kwao.
Nikiwa kama Mtanzania mzelendo nimefurahishwa sana na JK kwa kumtaja baba wa taifa NYERERE
Mzee kifimbo alikua mchango mkubwa sana kwa MANDELA
Dunia ijue hvyo
 
Nadhani hilo tu ndo ulilolielewa....tatizo wakati JK anaongea ulikuwa anaangaika na kamusi....!acha chuki,mbona yameongelewa mengi yenye kufurahisha watu tofauti pale?tena nadhani Nyerere angekuwepo pale watu wangetambaa kwa vicheko.
 
Kuna watu mnakera sana, Baba yako hawezi hata kutoa speech kwenye ngazi ya familia akaeleweka halafu unamponda Young Man from Tanzania?
 
Mandela alifungwa miaka 27. Nyerere hakukaa selo hata mwezi.
Mandela hakutaifisha mali ya mtu alipotoka jela wala hakuleta azimio la Arusha wala azimio la Cape Town.
Mandela alisamehe wote waliomtenda na hakulipiza kama Kambarage alivyofanya. Kambarage alimfunga Kassanga Tumbo, Chief Fundikira, Chief Lugwishwa, na akamkimbiza Oscar Kambona nk
Mandela alitaka uhuru kwa watu wote bila kubagua mtu. Kambarage aliwafanyizia wote waliokuwa na mawazo tofauti. (Kambona, Mtei, Mapalala etc).
Mandela alikuwa anashaurika na anaambilika. Kambarage alikuwa hashauriki wala haambiliki.
Mandela hakutaka kuwatesa watu na siasa uchwara za ujamaa na kujitegemea. Kambarage alituletea balaa kiuchumi. Hata Colgate ama soda ilikuwa ni luxury item kwa watanzania!!
Mandela hakuwalazimisha watu kuhama kwenye makazi yao. Kambarage aliwalazimisha watu kuhama bila ridhaa yao.
Duuh! u're suffering from dwarfism of thinkings!
apo ndo nmekupata vzur ndo mana ukaleta mada iyo! amakweli!!
 
Nikiwa kama mtanzania mwenye mtazamo tofauti, nimejaribu kusikiliza hotuba nyingi mpaka sasa naona ya Kikwete imejaa sana ubinafsi na dhihaka wengi wanasifu na kuutambua mchango wa Madiba lakini yeye ameonesha kuwa Madiba si lolote si chochote na asingeyafanya hayo bila Tanzania.

Historia haijirudii na ukweli ubaki kuwa ukweli kuwa tumeshiriki vyema bt yeye katumia chance hiyo kama kujihalalishia masifasifa.

Kama mlikuwa makini, vicheko vya watu havikuwa vya kuvutiwa kwa hotuba bali ni utoto na ulimbukeni wake aliyokuwa anatoa. Just imagine Madiba kusahau viatu na yeye kumpelekea, INAHUSU!!

Kikubwa ameonge mambo sahihi lakini si mahala pake.

Mwenye akili timamu ataona kuwa kuna madhala makubwa juu ya speech hii

Ametudhalilisha sana

Ama kweli Watanzania wenzangu exposure nikitu kizuri sana.
Kama hukuona Kikwete kazungumza la msingi nadhani wewe ni kati ya wale waandishi wa habari ambao wamekuwa wakiibeza nchi yetu.
Naomba nikuulize toka Mandela amefariki hivi kuna media yeyote ambayo imeigusia Tanzania, Baba yetu Nyerere au hata kuulizia ni kwa jinsi gani tumeshiriki katika UKOMBOZI WA MWAFRIKA HUKU KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA.
Umemsikiliza Ramaphosa MC alivyosifu juhudi za nchi yetu au ulikuwa unaangalia TV ZA KUNASA NA MANATI? Umemsikia Kaunda alivomalizia, jamani sasa nimeamini kuwa kweli ELIMU YETU INAFAA KUANGALIA UPYA NA HATA UKWELI NDANI MIOYO YETU PIA.
Nimetoka kuangalia BBC hakuna hata neno toka Tanzania iki maanisha kuwa wameumbuka na elimu ya ujuzi wa historia. THE WORLD HATE TANZANIA NA WEWE UNASUPPORT Samahani ingawa umesema ni mawazo yako lakini think BROAD. Juzi MADIBA CHANNEL sijui kama uliona hakuna historia hata kidogo juu ya Tanzania ilivyojitolea.
Hivi Nyerere angekataa kuwapa fadhila ingekuwaje?
Rais wangu mpendwa kwa hapo kafanya kweli kuelezea UMUHIMU WA TANZANIA KATIKA STRUGGLE FOR FREEDOM IN AFRICA NA HASA JINSI ALICHOKIFANYA AFRIKA KUSINI na nampa HEKO kwa kuenda na MAMA NYERERE ili waandishi uchwara waumbuke na wote ambao hawelewi kama wewe ufunguke!
Ebu rudi tena kama unaweza kuapata jinsi Kaunda alivyomalizia..... pole sana
Nadhani hii itakufungua angalau usome INTERNATIONAL NEWS NA UWEZE KUANGALIA UPUUZI UNAOANDIKWA KUHUSU NCHI ZENYE MSIMAMO BAADALA YA KUSOMA MAGAZETI YA UDAKU TU NDUGU YANGU
Je ulibahatika kuhudhuria mkutano wa AFRICAN AMERICAN uliofanyika Arusha miaka ya nyuma, kuna mwandishi wa CNN aliulizwa kwa nini hawandiki ukweli kuhusu Afrika? ALISHINDWA KUJIBU LAKINI UKWELI NI KWAMBA WANAOGOPA UKWELI!
Sasa nani amfunge PAKA KENGELE KAMA SIO SISI WENYEWE ? Leo Kikwete kaonyesha mfano it was all about REALITY and not FAME..!PERIOD
 
Sasa kama hauungi mkon
speech ya JK si ungekaa kimya tu mkuu wangu...Ama na wewe unataka
kuonekana umeanzisha thread?

Wewe kweli ni mtamu....

Angekaa kimya ungejua je haungi mkono? ama wewe unadhani kuanzisha uzi ndo issue?
 
Ndo maana slaa akiukwaa uraisi watu kama hawa atawa favour kwa kuruhusu viroba na Gongo
 
KUNA MTU KANITUMIA HII, ISOMENI

Tukiwa tunaendelea kuangalia funeral rites za Nelson Mandela, mliosikiliza hotuba ya JK ni kwamba kaeleza umati kwamba Mandela alifika Tanganyika kwa mara ya kwanza January 1962. Kwamba safari hiyo alikuja kisiri akipitia Mbeya na kuingia Tanganyika. Kisha akapewa passport ya Tanzania kusafiria.

Hapa ndipo tunaposema viongoziwetu hawapekui vitabu au documents au hata kukumbuka tu. Ukweli ni kwamba histroia haisemi hivyo. Historia inasema kwamba January 1962 ulikuwa ni mweiz mmoja tu tangu Tangayika ijitawale ikiwa na Prime Minister Nyerere. Tukio kuu la kihistoria ni kwamba Huo mwezi karibi wiki mbili zilitawaliwa na NEC ya TANU ambayo ilipomalizika Nyerere akajiuzulu u-Prime Minister na akamuachia Rashid Kawawa.

Gavana-General Richard Turnbull asingeweza kutoa passport Nelson Mandela kirahisi.

Ukweli kuhusu ujio wa Mandela ni kwamba alikuja hapa December 1962, yaani mwaka huohuo, na akawepo kushuhudia Tanganyika ikipata status ya Republic. Hapo ndipo angeweza kupata passport ya Tanganyika na ndicho kilichotokea.

Sikuweza kuamini JK alipokuwa anasoma zile tarehe mbele ya dunia nzima, kwa sababu mtu aliyechimubka historia ya Mandela kokote ilikoandikwa anajua wazi kwamba Mandela alikuja hapa December 1962.

Na hata Mandela kwenye kitabu chake alichoandika kiitwacho A LONG WALK TO FREEDOM, ISBN: 9780349106533, pg. 345: {..we arrived in Dar Es Salaam the next day and I met Julius Nyerere, the newly independent country's firss President..}

Hivyo, wakati ule asingemkuta Nyerere akiwa President, na wakati pekee alipokuwa President ni kuanzia December 09, 1962.

Tuwe tunasoma kabla ya kwenda public.

----------------------------
 
Mandela alifungwa miaka 27. Nyerere hakukaa selo hata mwezi.
Mandela hakutaifisha mali ya mtu alipotoka jela wala hakuleta azimio la Arusha wala azimio la Cape Town.
Mandela alisamehe wote waliomtenda na hakulipiza kama Kambarage alivyofanya. Kambarage alimfunga Kassanga Tumbo, Chief Fundikira, Chief Lugwishwa, na akamkimbiza Oscar Kambona nk
Mandela alitaka uhuru kwa watu wote bila kubagua mtu. Kambarage aliwafanyizia wote waliokuwa na mawazo tofauti. (Kambona, Mtei, Mapalala etc).
Mandela alikuwa anashaurika na anaambilika. Kambarage alikuwa hashauriki wala haambiliki.
Mandela hakutaka kuwatesa watu na siasa uchwara za ujamaa na kujitegemea. Kambarage alituletea balaa kiuchumi. Hata Colgate ama soda ilikuwa ni luxury item kwa watanzania!!
Mandela hakuwalazimisha watu kuhama kwenye makazi yao. Kambarage aliwalazimisha watu kuhama bila ridhaa yao.
Mandela hakuwa mnafiki. Kambarage alisababisha vita ili amrudishe swahiba wake Milton Obote madarakani.
Mandela alikuwa rafiki kwa wote na hata wale waliompinga. Kambarage aliwachukia waliokuwa maadui zake i.e.chief Fundikira, Kambona, Mtei, Kassanga Tumbo.
Mandela hakutaka vita bali amani. Kambarage alijiingiza kwenye vita na kuwaita majirani zake nduli. (Idd Amin/Biafra/Banda)
Mandela alitawala kipindi kimoja. Kambarage alikaa miaka 30 madarakani.
Mandela alijali free enterprise economy. Kambarage alitaka African socialism ambayo haikutekelezeka hadi leo.
Mandela alijali vyama vingi na wapinzani. Kambarage aliogopa na hakutaka multipartism wala kusikia wapinzani hadi alipotoka.
Mandela aliwapenda viongozi wote barani Africa. Kambarage alikuwa na siasa za makundi na majungu na hakuheshimu sovereignity ya nchi nyingine (alitaka kumrudisha Obote wakati alikuwa sio raisi wa Uganda, alimsupport Ojukwu na Biafra).
Mandela alipenda ku-reason na watu hata opponents wake. Kambarage aliwatisha opponents wake.
Mandela hakutishika wala kuwaogopa machifu wa makabila mengine. Kambarage aliogopa na kuwapiga marufuku machifu wa makabila mengine nlakini akamwacha chifu wa kabila lake tu (Chief Wanzagi).
Mandela haku-take sides. Nyerere alikumbatia Warsaw pact during the cold war.
Mandela alitaka uhuru wa kisiasa na kiuchumi. Nyerere alipinga uhuru wa kisiasa wala kiuchumi na kutusababishia majanga e.g. bidhaa ziliadimika kiasi cha kwamba hata kumiliki mafuta ya Kimbo au TV ilikuwa ni kuhujumu uchumi.

c/o SHERRIF

Kilaza mwingine at work
 
Ukiacha kuchapia kiingereza hapa na pale(mwandishi wake inabidi awe makini), hotuba ilikuwa nzuri na inayofaa kwa muktadha husika. Ametufungua macho hata kwa masuala ambayo pengine yalikuwa ni siri sana kwa wakati huo!
 
Hotuba ilikuwa nzuri na yakawaida, ameitendea haki mamlaka ya rais,

Tatizo lipo kwa kizazi hiki cha nyoka, watu hawapendi kusoma wala kujifunza, mambo yote aliyoyaongea jk yapo katika maandiko mengi sana, ninashangazwa sana kuona baadhi ya watu wanamuona jk kama mvumbuzi wao wa histori iliyofichwa,

Huu sio uungwana kabisa ndugu zangu, hebu tujipe muda wa kusoma machapisho na maandiko ya kila aina, tutayaona makuu na ya ajabu kuliko hii
 
Nikiwa kama mtanzania mwenye mtazamo tofauti, nimejaribu kusikiliza hotuba nyingi mpaka sasa naona ya Kikwete imejaa sana ubinafsi na dhihaka wengi wanasifu na kuutambua mchango wa Madiba lakini yeye ameonesha kuwa Madiba si lolote si chochote na asingeyafanya hayo bila Tanzania.

Historia haijirudii na ukweli ubaki kuwa ukweli kuwa tumeshiriki vyema bt yeye katumia chance hiyo kama kujihalalishia masifasifa.

Kama mlikuwa makini, vicheko vya watu havikuwa vya kuvutiwa kwa hotuba bali ni utoto na ulimbukeni wake aliyokuwa anatoa. Just imagine Madiba kusahau viatu na yeye kumpelekea, INAHUSU!!

Kikubwa ameonge mambo sahihi lakini si mahala pake.

Mwenye akili timamu ataona kuwa kuna madhala makubwa juu ya speech hii

Ametudhalilisha sana








Hii hapa hotuba yake tuambie katudhalilisha sehemu gani?
 
Last edited by a moderator:
KUNA MTU KANITUMIA HII, ISOMENI

Tukiwa tunaendelea kuangalia funeral rites za Nelson Mandela, mliosikiliza hotuba ya JK ni kwamba kaeleza umati kwamba Mandela alifika Tanganyika kwa mara ya kwanza January 1962. Kwamba safari hiyo alikuja kisiri akipitia Mbeya na kuingia Tanganyika. Kisha akapewa passport ya Tanzania kusafiria.

Hapa ndipo tunaposema viongoziwetu hawapekui vitabu au documents au hata kukumbuka tu. Ukweli ni kwamba histroia haisemi hivyo. Historia inasema kwamba January 1962 ulikuwa ni mweiz mmoja tu tangu Tangayika ijitawale ikiwa na Prime Minister Nyerere. Tukio kuu la kihistoria ni kwamba Huo mwezi karibi wiki mbili zilitawaliwa na NEC ya TANU ambayo ilipomalizika Nyerere akajiuzulu u-Prime Minister na akamuachia Rashid Kawawa.

Gavana-General Richard Turnbull asingeweza kutoa passport Nelson Mandela kirahisi.

Ukweli kuhusu ujio wa Mandela ni kwamba alikuja hapa December 1962, yaani mwaka huohuo, na akawepo kushuhudia Tanganyika ikipata status ya Republic. Hapo ndipo angeweza kupata passport ya Tanganyika na ndicho kilichotokea.

Sikuweza kuamini JK alipokuwa anasoma zile tarehe mbele ya dunia nzima, kwa sababu mtu aliyechimubka historia ya Mandela kokote ilikoandikwa anajua wazi kwamba Mandela alikuja hapa December 1962.

Na hata Mandela kwenye kitabu chake alichoandika kiitwacho A LONG WALK TO FREEDOM, ISBN: 9780349106533, pg. 345: {..we arrived in Dar Es Salaam the next day and I met Julius Nyerere, the newly independent country's firss President..}

Hivyo, wakati ule asingemkuta Nyerere akiwa President, na wakati pekee alipokuwa President ni kuanzia December 09, 1962.

Tuwe tunasoma kabla ya kwenda public.

----------------------------

Pimbi wewe umetumiwa na nani wakati hii ni copy & paste kutoka humu humu JF.
 
kwa mila na desturi za kiafrika. utani kwenye msiba ni jambo la kawaida sana, japo aliyoongea jk, yote ni ukweli mtupu na wala hakukosea kuyasema yale yote. watu kufurahi kwenye msiba ni njia mojawapo ya kuwafariji wafia.
 
Back
Top Bottom