Siungi mkono hotuba ya Rais Kikwete, SA

Siungi mkono hotuba ya Rais Kikwete, SA

Nikiwa kama mtanzania mwenye mtazamo tofauti, nimejaribu kusikiliza hotuba nyingi mpaka sasa naona ya Kikwete imejaa sana ubinafsi na dhihaka wengi wanasifu na kuutambua mchango wa Madiba lakini yeye ameonesha kuwa Madiba si lolote si chochote na asingeyafanya hayo bila Tanzania.

Historia haijirudii na ukweli ubaki kuwa ukweli kuwa tumeshiriki vyema bt yeye katumia chance hiyo kama kujihalalishia masifasifa.

Kama mlikuwa makini, vicheko vya watu havikuwa vya kuvutiwa kwa hotuba bali ni utoto na ulimbukeni wake aliyokuwa anatoa. Just imagine Madiba kusahau viatu na yeye kumpelekea, INAHUSU!!

Kikubwa ameonge mambo sahihi lakini si mahala pake.

Mwenye akili timamu ataona kuwa kuna madhala makubwa juu ya speech hii

Ametudhalilisha sana

Amekudhalilisha umejidhalilisha?
 
Mandela alifungwa miaka 27. Nyerere hakukaa selo hata mwezi.
Mandela hakutaifisha mali ya mtu alipotoka jela wala hakuleta azimio la Arusha wala azimio la Cape Town.
Mandela alisamehe wote waliomtenda na hakulipiza kama Kambarage alivyofanya. Kambarage alimfunga Kassanga Tumbo, Chief Fundikira, Chief Lugwishwa, na akamkimbiza Oscar Kambona nk
Mandela alitaka uhuru kwa watu wote bila kubagua mtu. Kambarage aliwafanyizia wote waliokuwa na mawazo tofauti. (Kambona, Mtei, Mapalala etc).
Mandela alikuwa anashaurika na anaambilika. Kambarage alikuwa hashauriki wala haambiliki.
Mandela hakutaka kuwatesa watu na siasa uchwara za ujamaa na kujitegemea. Kambarage alituletea balaa kiuchumi. Hata Colgate ama soda ilikuwa ni luxury item kwa watanzania!!
Mandela hakuwalazimisha watu kuhama kwenye makazi yao. Kambarage aliwalazimisha watu kuhama bila ridhaa yao.
Mandela hakuwa mnafiki. Kambarage alisababisha vita ili amrudishe swahiba wake Milton Obote madarakani.
Mandela alikuwa rafiki kwa wote na hata wale waliompinga. Kambarage aliwachukia waliokuwa maadui zake i.e.chief Fundikira, Kambona, Mtei, Kassanga Tumbo.
Mandela hakutaka vita bali amani. Kambarage alijiingiza kwenye vita na kuwaita majirani zake nduli. (Idd Amin/Biafra/Banda)
Mandela alitawala kipindi kimoja. Kambarage alikaa miaka 30 madarakani.
Mandela alijali free enterprise economy. Kambarage alitaka African socialism ambayo haikutekelezeka hadi leo.
Mandela alijali vyama vingi na wapinzani. Kambarage aliogopa na hakutaka multipartism wala kusikia wapinzani hadi alipotoka.
Mandela aliwapenda viongozi wote barani Africa. Kambarage alikuwa na siasa za makundi na majungu na hakuheshimu sovereignity ya nchi nyingine (alitaka kumrudisha Obote wakati alikuwa sio raisi wa Uganda, alimsupport Ojukwu na Biafra).
Mandela alipenda ku-reason na watu hata opponents wake. Kambarage aliwatisha opponents wake.
Mandela hakutishika wala kuwaogopa machifu wa makabila mengine. Kambarage aliogopa na kuwapiga marufuku machifu wa makabila mengine nlakini akamwacha chifu wa kabila lake tu (Chief Wanzagi).
Mandela haku-take sides. Nyerere alikumbatia Warsaw pact during the cold war.
Mandela alitaka uhuru wa kisiasa na kiuchumi. Nyerere alipinga uhuru wa kisiasa wala kiuchumi na kutusababishia majanga e.g. bidhaa ziliadimika kiasi cha kwamba hata kumiliki mafuta ya Kimbo au TV ilikuwa ni kuhujumu uchumi.

c/o SHERRIF

hii nayo ni nini?
 
Rais Kikwete alialikwa kutoa hotuba hii katika mazishi ya Mzee Mandela kwa niaba ya the former Front Line States [FLS] zilizo ongoza mapambano ya kukomboa nchi za kusini mwa Afrika kuanzia Mozambique miaka ya 1960s. The FLS zilikuwa ziki-ongozwa na Mwalimu Nyerere mpaka mwaka 1985 alipostaafu na uenyekiti ukaenda kwa Kaunda wa Zambia mpaka 1991 aliposhindwa kwenye kura ya Urais wa Zambia na Chiluba. Rais Mugabe wa Zimbabwe ali take over mpaka 1994 when South Africa ilipopata uhuru na kazi ya FLS ikawa imemalizika. FLS ilibadilishwa na kuwa the Security Organ ya SADC.

Viongozi wote was Kusini mwa Afrika wanamtambua Julius Nyerere kuwa ndiye aliyekuwa chief strategist wa vita vya ukombozi wa nchi zao kuanzia Mozambique iliyopata uhuru 1975; Angola 1975 and Zimbabwe 1980. Baada ya Zimbabwe makaburu walikuwa mbogo na kuzi-sabotage nchi za FLS wakiwatumia kina Savimbi & UNITA in Angola and Renamo in Mozambique.

Hii ilifanya vita vya ukombozi wa Namibia na Afrika ya Kusini kuwa ngumu. Hata hivyo Makaburu walipata pigo kubwa sana katika the battle of Cuito Canavale huko Angola mwaka 1987/88 wakati vikosi vyao vya askari zaidi ya 30000 [elfu thelathini] vilipopigwa vibaya sana na combination ya vikosi vya Angola; SWAPO na ANC wakisaidiwa na askari wa ki Cuba na Ugermani ya Mashariki. Vikosi vya SWAPO na ANC vilikuwa trained Mgagao, Tanzania na inasemekana pia kuwa vilikuwa vikipata technical support ya JWTZ. Inasemekana brigedi mbili au tatu za makaburu ziliteketezwa kabisa hapo Cuito Canavalle na ndipo hapo makaburu wakasalimu amri na wakaanza kukubali kutoa Uhuru kwa Namibia ambayo ilifanyika mwaka 1991.

Kushindwa kwa Makaburu katika vita vya Cuito Canavalle vilisababisha kuanguka kwa serikali ya P. W. Botha huko South Africa na badala yake akaingia de Klerk ambaye ndiye aliye mwachilia kutoka Gerezani Nelson Mandela mwaka 1991. Kutoka hapo historia ya South Africa ikabadilika na wakapata uhuru/serikali ya demokrasia mwaka 1994 chini ya Mzee Mandela.

Katika hotuba yake ya leo Kikwete did an excellent job in explaining the role of Nyerere and Tanzania in the liberation of Southern Africa. Watu wengi huko Southern Africa na hata wengine hapa Tanzania hawajui hii role ya Nyerere and Tanzania vizuri. This was therefore a God given opportunity for Tanzania through Rais Kikwete to inform the World of this contribution. Indeed Mzee Kaunda alipoitwa naye kuzungumza alimtaja Mwalimu Nyerere several times pamoja na Mama Maria Nyerere na kumshukuru Kikwete kwa hotuba yake.

Utaona pia baada ya hotuba yake ya leo Rais Banda wa Malawi kama Mwenyekiti wa SADC - the master of ceremony ali comment kuwa hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Malawi kujisafisha kwa Wa South Africans maana nchi yao ilijulikana kama kikaragosi and kibaraka mkuu was Makaburu hata mpaka mwaka 1994 wakati Rais Kibaraka Hastings Banda alipo-ondolewa madarakani - indeed umati katika Mazishi yale ulicheka kwa dharau.

In short Rais Kikwete did an EXCELLENT JOB TODAY IN TELLING THE SOUTH AFRICANS AND THE WORLD of THE ROLE OF JULIUS NYERERE AND TANZANIA IN THE LIBERATION OF THE SOUTHERN AFRICA STATES. THIS WAS A GOLDEN OPPORTUNITY AND ONLY A NAIVE PERSON WOULD NOT HAVE TAKEN IT UP. LET US GIVE DUE CREDIT TO OUR PRESIDENT WHEN HE REPRESENTS THE COUNTRY WELL. THERE WERE NO OTHER PRESIDENTS/external leaders FROM AFRICA or elsewhere who were ALLOWED TO SPEAK AT THIS FUNERAL CEREMONY TODAY OTHER THAN THE CHAIRPERSON OF AFRICAN UNION - PM of Ethiopia and the SADC Chair President Banda of Malawi and of course President Zuma himself. So Let us give our President the due credit he deserves.


Safi sn Mkuu!
Watu hawaelewi kazi kubwa ya taifa letu iliyofanya ktk kufanikisha uhuru Wa Africa!

Na nimeshangaa sn kuona baadhi ya watu kumsifu J Banda na wakati wanasahau ktk harakati za ukombozi Wa Africa Malawi chini ya Dr K Banda walikua vibara Wa makaburu na Mara nyingi walikua wanatuletea vurugu Kule mpakani Songea na pia tulikua na wakimbizi Wa kimalawi ambao walikimbia utawala Wa K Banda Kule Kigwa Tabora na Wote wamerudi kwao!

Tz imefanya Kz kubwa sn kukomboa nchi za kusini mwa Africa
 
Hotuba ile murua kabisa, lazima kubainisha mchango wetu kwenye vita vya ukombozi afrika. Zipo nchi na viongozi jirani zetu wanajinadi hata kwa uongo na ukizubaa wanakukandia hata sifa yako wanakupora.
 
mh siku hiz kikwete ana ni suprise na speeches nzuri ..ile ya bungeni kuhusu EAC , ya kwenye sherehe za uhuru wa kenya na hii hapa..safi sana ka improve kwelikweli
 
Namkubali sana jk!!so we sema ugalegale lkn jk ni jembe mara trilion....

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hotuba ile murua kabisa, lazima kubainisha mchango wetu kwenye vita vya ukombozi afrika. Zipo nchi na viongozi jirani zetu wanajinadi hata kwa uongo na ukizubaa wanakukandia hata sifa yako wanakupora.

:amen:
 
Yani humu kuna mijitu kazi yao ni kupinga tu kila kitu hata kama ni kizuri,cjui wamekula kiapo cha upinzani?
 
Sasa kama hauungi mkon speech ya JK si ungekaa kimya tu mkuu wangu...Ama na wewe unataka kuonekana umeanzisha thread?

Wewe kweli ni mtamu....

Kwanini akae kimya? Lengo moja wapo la kuwa na JF ni kupata uwanja wa kutoa mawazo na hisia zetu. Kutoa mawazo mbadala. Kukosoa. Kuunga mkono na mambo mengi tu.
 
Kwa kutojua tu kiswahili, nakutilia mashaka.

ume-skip hoja,hatujadili lugha hapa mdau,,,,hoja ya robert ni umaskin wetu na harakat za ukomboz,,,,,,
pia pitien ripot mpya ya WB JUU YA HALI YA UMASKIN TZ,,,,,,
 
Sio vbaya kukosoa penye kasoro zilizo thibitika ila ni ustaarabu na maarifa ya kiwango cha juu unapoweza kuweka hadharani vitu ambavyo vlitakiwa kuwemo kwenye hötuba ya JK ambavyo yumkini mleta mada anadhani vingeleta ukamilifu wa hotuba anayo hisi ilikuwa na mapungufu.
 
Nikiwa kama mtanzania mwenye mtazamo tofauti, nimejaribu kusikiliza hotuba nyingi mpaka sasa naona ya Kikwete imejaa sana ubinafsi na dhihaka wengi wanasifu na kuutambua mchango wa Madiba lakini yeye ameonesha kuwa Madiba si lolote si chochote na asingeyafanya hayo bila Tanzania.

Historia haijirudii na ukweli ubaki kuwa ukweli kuwa tumeshiriki vyema bt yeye katumia chance hiyo kama kujihalalishia masifasifa.

Kama mlikuwa makini, vicheko vya watu havikuwa vya kuvutiwa kwa hotuba bali ni utoto na ulimbukeni wake aliyokuwa anatoa. Just imagine Madiba kusahau viatu na yeye kumpelekea, INAHUSU!!

Kikubwa ameonge mambo sahihi lakini si mahala pake.

Mwenye akili timamu ataona kuwa kuna madhala makubwa juu ya speech hii

Ametudhalilisha sana

hakuna aliyedhalilishwa pale,labda Jay Z(ZUMA) aliyekua akizomewa muda wote,kwenye hotuba yake mlitaka azungumzie nn?amezungumza yale yanayohusu madiba ya nchi yetu,na nimemsifu kwa kuwajulisha vijana mambo ya nchi yenu msiyoyajua.
 
Nilichopenda kuongeza hapa karibu wale Wote waliokua kwenye system ya kuikomboa SA walikua mazimbwi Morogoro na pia ata baadhi walioko sasaivi kwenye system SA walikua hapa Morogoro!

Ni MAZIMBU sio MAZIMBWI mkuu!!
 
Back
Top Bottom