Kibanga Ampiga Mkoloni
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 19,079
- 9,245
Yani tunawalipa posho kwa kodi zetu kujadili KATUNI ?
Kweli MACCM mufilisi kabisa!
Kweli MACCM mufilisi kabisa!
Ile katuni imechorwa na Mwampembwa mtu wa Mbeya lakini kikazi yupo based Kenya, kwahiyo ni katuni iliyochorwa na Mtanzania aliyechoshwa na Bunge hili hasa la ana makinda (Jina la Speaker wetu siku zote naliandika kwa herufi ndogo)
Tatizo linaanzia kwamba "Mkenya" ndiye kachora hivyo.Mchoraji ni MTANZANIA akiitwa GODFREY MWAMPEMBA na analindwa na katiba kufanya hivyo tatizo liko wapi?
![]()
Alikuwa hajapata jukwaa la kukamulia ujumbe huo. Je ujumbe una ukweli au la? Siyo kukanusha tu.Yaani jambo limetokea sijui miezi kadhaa ndio analaani leo?
He he he he, ama kweli hii ni kasi mpya
Maneno yakitafsiriwa kwenda kwenye pic/katuni..tunabaki uchi.!
asema jambo hilo si la kiuungwana wala si la kiurafiki na ujiran mwema.linaweza chochea mgogoro
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amelaani katuni ya kuwakashifu wabunge wa Bunge la Tanzania iliyochorwa kwenye gazeti la Sunday Nation la Kenya hivi karibuni na kusisitiza kuwa hatua hiyo haikubaliki.
Sitta alitoa msimamo huo jana mjini hapa wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/2014.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni gazeti la Sunday Nation la Kenya kupitia kwa mchora katuni wao, lilichapisha katuni ikionesha wabunge wa Bunge letu wakiwa kwenye ulevi huku wamevaa nguo fupi za hovyo.
Kitendo hicho ni kibaya, kisichoonesha ujirani mwema wala urafiki. Ni kitendo cha kihuni, kinachoweza kuchochea maelewano mabaya, alisema.
Waziri Sitta alisisitiza kuwa wanalaani kwa nguvu zote jitihada zozote zinazojaribu kulidhalilisha Bunge hilo tukufu.
Alifafanua kuwa ni kweli mara nyingine Bunge hilo linakuwa na mjadala mkali, lakini kuwalinganisha wabunge na ulevi na nguo nusu uchi hata kama metumika michoro kujaribu kukwepesha, hiyo haikubaliki hata kidogo.
................Raya pia aligusia uhuru wa habari kwa nchi wanachama huku akinukuu taarifa ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ya Mei 20 mwaka huu ambayo ilisema kuwa Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameamuru kufungiwa kwa gazeti la kila siku la nchi hiyo la The Daily Monitor, na gazeti lingine la Red Pepper.
Hatua hiyo ni kutokana na kuchapisha habari iliyofichua njama za Rais Museveni za kumuandaa mtoto wake, Muhoozi Kainerugaba ambaye ni brigedia wa jeshi kuwa rais wa nchi hiyo baada ya yeye kuondoka madarakani.
Hata hivyo, baada ya kuhitimisha hotuba yake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi aliomba mwongozo wa kiti akitaka wapinzani wakemewe kwa kukiuka kanuni na kutaja majina ya viongozi wakuu wa nchi kwa dhihaka.
Mimi sitaki kuzungumzia suala la Kinana maana hizo ni porojo wacha waendelee, lakini nazungumzia ukiukwaji wa makusudi wa kanuni na kumtaja Rais Museveni kwa mambo ambayo eti msemaji ameyasikia kwenye redio pamoja na lile la Kinana japo tumeishajibu, lakini wanaendelea kujifurahisha. Naomba ukemee jambo hili, alisema.
Source: Tanzania Daima
Ukisoma hiyo taarifa hapo juu unaweza kuona mkanganyiko wa mwazo ya Mawaziri hao 2 kutoka CCM. Sitta analaani Gazeti la Daily Nation la KENYA kwa kuchapisha KATUNI inayolidhalilisha Bunge la Tanzania kwa mchoro unaoonyesha Wabunge wa CCM wakiwa mamelewa na wengine wako nusu uchi.
Lukuvi yeye anaomba mwongozo wa Spika kukemea kauli ya msemaji wa KUB kuhusu Bajeti ya Afrika Mashariki kwa kuzungumzia kuhusu Uhuru wa vyombo vya Habari kwa kunukuu radio ya BBC kuhusu Serikali ya Uganda kuyafungia Magazeti ya Uganda, The Monitor na The Red Pepper kwa kuandika na kufichua siri za Museveni kuhusu mpango wa kumwachia Madaraka mwanae atakapostaafu!!!
Chama kimoja,serikali moja lakini mawazo tofauti. Aibu kwa ma-CCM!
[TD="bgcolor: #ffffff"][/TD]
Sitta: Hatutakubali Bunge lidhalilishwe
Edson Kamukara, Dodoma
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"][/TD]![]()
Mwaka jana sabasaba nilisoma gazeti moja hivi silikumbuki jina la Mwaka 1964, linasema kijana wa TANU anaeitwa Samweli Sitta ameende marekani alikoende kuiwakilisha nchi kwenye mambo muhimu huko....!!
Ajabu, Sitta toka mwaka 1964 ni kiongozi nchi...mfululizo...amaefanya nini cha maana kuikomboa nchi kutoka katika mikono ya mafiisadi wakiongozwa na watawala wenyewe?
Anetetea tu tumbo lake ....ili aendelee kula makuku ya ulaya aliyozoea kuyala toka akiwa na miaka 18 hadi sasa anakaribia 80!!