Sijui alikuwa anafikiria nini.Kuna uhuru wa maoni Kenya. Msanii akichora katuni isiyomfurahisha Sitta sio kosa la serikali ya Kenya. Ni lini hawa wazee watakomaa kimawazo?
Sita aache kuyumbisha mambo wakenya wako sahihi maana bunge chini ya uongozi wa Makinda ni zaidi ya hiyo katuni,Sita anasemaje juu ya Serukamba kumtukana mbunge mwenzake"---- you" na spika hakumwadhibu, hivyo hiyo katuni inasema ukweli
Sitta ang'aka, aionya Kenya
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mshariki, Samuel Sitta, ameionya Kenya kutokana na mipango yake ya siri ya kuichafua Tanzania. Sitta alisema mipango hiyo ya Kenya imedhihiri baada ya gazeti la Sunday Nation kuchora katuni ambayo ililifananisha Bunge la Tanzania na klabu ya pombe