NANDERA
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 2,023
- 2,492
Hii issue ilitakiwa kumalizwa kifamilia zaidi, sijui flora kapatwa na nini, haijalishi ni kweli Emma amebaka but hakupaswa kumfanyia hivi mumewe, sijui anajenga mazingira gani Kati baba na mtoto wao Eliza, so sad kwakweli
em nielewesheni jamani labda umbea wa mujini ulinipita. Kwani flora ndo alienda kumshtaki mumewe kuwa kabaka? Kesi ua ubakaji si jamhuri vs mbakaji? hata kama binti hakubakwa kwa maana ya kuingiliwa kinguvu, kisheria si binadamu under 18 hana consent kwa sababu ni mtoto? Na tunavyosema hizi kesi za ubakaji kwenye familia zisiwe exposed, hivi tunajua ni watoto wangapi wananajisiwa na baba zao na mama zao wanaugulia maumivu kutokana na mitazamo kama hii ya kwenu? hapo sijaongelea idadi ya mahausgel na mashemeji wanaotumiwa na waume zetu bila hiyari yao au kwa hiyari lakini kutokana na hofu. Kama ningetaka flora amsapoti mumewe basi ni kwa kumpelekea chakula mahabusu na kuhudhuria kwenye kesi na kutoa msaada utakaohitajika wakati wa kesi na si kuzuia kesi isifunguliwe. Huyo flora nae ni binadamu. Aliyebaka ni mumewe, aliyebakwa ni mdogo wake. Mi naona ni vizuri akaendelea kukaa kwenye fensi tu. Sidhani kama anafurahia kinachoendelea kama wengi tunavyoonyesha humu. Wala tusitake kumbebesha mzigo wa lawama kuwa kuondoka kwake ndani ndo kulimfanya mumewe azini na mdogo wake. Kila mtu mwenye akili timamu ana uwezo wa kuutiisha mwili wake. kwa hiyo kama mbasha kabaka ni kwa tamaa zake. Kama hakubaka basi ni kipindi chake cha kupitia mapito hayo, na inshallah atapita salama.