dalalitz
JF-Expert Member
- Sep 6, 2013
- 3,332
- 1,862
Kwa wengine hii ingekuwa furaha, shangwe, nderemo na vifijo.
Kwa mama huyu wa KiNaigeria yeye anaona 'mapichapicha' tu.
.
Huku akibubujikwa na machozi mithili ya mtu aliefikwa na msiba na akihanikiza na kushinikiza Polisi wahusike kuchunguza imekuwaje mwanae ambae ndio kwanza kamaliza masomo ya Sekondari,
Leo hii eti mtoto anatimba nyumbani huku akiendesha Gari mpya bora ingekuwa ya kuazima,
dogo anajimwayamwaya huku akidai kuwa hiyo ni Mali yake yeye na ambayo ameinunua kwa Pesa zake mwenyewe. Gari husika si si Gari tu bora Gari, unaambiwa ni Ni MERCEDES BENZ.
Dingi yeye nae amestaajabu na kukosa cha kuongea.
Niitieni Polisi jamani,
Hapana hapana hapana haiwezekani"
Anaongea kwa hisia za kumaanishaanachokisema na huku akigaragara.
Kumbuka sio Sinema hii.
Unadhani mama yupo sahihi?
Kwa mama huyu wa KiNaigeria yeye anaona 'mapichapicha' tu.
.
Huku akibubujikwa na machozi mithili ya mtu aliefikwa na msiba na akihanikiza na kushinikiza Polisi wahusike kuchunguza imekuwaje mwanae ambae ndio kwanza kamaliza masomo ya Sekondari,
Leo hii eti mtoto anatimba nyumbani huku akiendesha Gari mpya bora ingekuwa ya kuazima,
dogo anajimwayamwaya huku akidai kuwa hiyo ni Mali yake yeye na ambayo ameinunua kwa Pesa zake mwenyewe. Gari husika si si Gari tu bora Gari, unaambiwa ni Ni MERCEDES BENZ.
Dingi yeye nae amestaajabu na kukosa cha kuongea.
Niitieni Polisi jamani,
Hapana hapana hapana haiwezekani"
Anaongea kwa hisia za kumaanishaanachokisema na huku akigaragara.
Kumbuka sio Sinema hii.
Unadhani mama yupo sahihi?