Sishauri mtu kusoma PhD OUT

Sishauri mtu kusoma PhD OUT

Mkuu sijui unafeli wapi? Unasoma PhD na unalalamika upo serious kweli? Unafikiri supervisor wanakula email?
Tengeneza na weka mazingira supervisor wako akutambue na siku moja moja akupigie simu akijidai amekosea au anataka kukusalimia tu!
Nimewahi kuambiwa na mtu mmoja kwamba, " ni rahisi sana kubadili pesa kuwa elimu ila sio elimu kuwa pesa"
 
Kwa yule Supervisor mambo ya rupia hapendi. Anaonekana Hana njaa kabisa. Halafu mkali Sana haingiliki.
Huko ni ku invest kwenye short term life

Wengine huko wanasoma nj secret service wanatumwa ku evaluate yupi awe promoted hata nje ya chuo kikuu

Wengine waweza toa rushwa sio kuwa takukuru watamdaka lakini atarudisha report kwa waliomtuma kuwa yule mla rushwa mkubwa ila ni mwalimu mzuri mwacheni astaafu kwa kuandika chaki ubaoni

Kumbe hata hiyo Masters au Phd waweza hata kuwa nazo au wanaandaliwa kusoma nje ya nje hapo walikuwa hata hawahitaji ila wanasoma hasa walikuja tu kufanya evaluation ya hai ma supervisor kama wafaa higher posts hata nje ya mfumo wa chuo wapo sababu mfumo wa kupanda vyeo vyuo vikuu uko skewed kama pyramid unavyopanda juu kunakuwa kuwa ku finyu hivyo kupanua wigo wengine wanatakiwa wapate teuzi au nje ya vyuo

Ila kama mla rushwa hapana
 
Msimamizi (supervisor) anapokuwa anasimamia mwanafunzi wa postgraduate ana majukumu muhimu sana katika kuhakikisha mwanafunzi anafanikiwa katika utafiti wake na kuhitimu kwa wakati.
yafuatayo ni majukumu
1. Kutoa Mwongozo wa Utafiti – Kumsaidia mwanafunzi kuchagua mada inayofaa, kuboresha maswali ya utafiti, na kuelekeza mbinu sahihi za utafiti.

2. Kusimamia Maendeleo – Kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi kupitia mikutano ya mara kwa mara na kutoa mrejesho wa kujenga.


3. Kuhakikisha Ubora wa Kazi – Kuhakikisha kuwa utafiti unakidhi viwango vya kitaaluma na kitaaluma, ikiwemo tafiti za awali na mbinu za uchambuzi wa data.


4. Kumsaidia Katika Uandishi wa Tasinifu (Thesis/Dissertation) – Kutoa mwongozo katika uandishi wa sura mbalimbali za tasinifu na kusahihisha makosa kabla ya kuwasilisha.


5. Kutoa Ushauri wa Kitaaluma – Kumwelekeza mwanafunzi kuhusu fursa za utafiti, machapisho ya kisayansi, na mitandao ya kitaaluma.


6. Kusaidia Katika Maandalizi ya Viva Voce – Kumpa mwongozo kuhusu jinsi ya kujibu maswali ya mtihani wa mdomo (defense) na kusimamia maandalizi yake.


7. Kuhimiza Nidhamu na Ufanisi – Kuhamasisha mwanafunzi kufuata ratiba ya kazi, kudhibiti muda, na kukamilisha utafiti kwa wakati.


8. Kuwa Kiungo na Chuo au Taasisi – Kuwasiliana na idara ya chuo kuhusu masuala ya kitaaluma, taratibu za chuo, na fursa za ufadhili au usaidizi mwingine.


9. Kumjengea Uwezo wa Kujitegemea – Kumfundisha mwanafunzi kuwa mtafiti huru, kufanya maamuzi ya kitaaluma, na kujenga msingi wa taaluma yake ya baadaye.

NOTE:Hapa hakuna sehemu yoyote inayoelekeza kuwa mwanafunzi atoe rushwa

hebu tuone wajibu wa supervisor akitumiwa kazi ya research proposal
Msimamizi (supervisor) wa mwanafunzi wa PhD anapopokea kazi ya dissertation (tasnifu), ana wajibu wa kuhakikisha kuwa kazi hiyo inakidhi viwango vya kitaaluma na kitaaluma kabla ya kuwasilishwa rasmi. Wajibu wake ni pamoja na:

1. Kusoma na Kutoa Maoni ya Kina
• Kupitia kila sura kwa umakini ili kuhakikisha mtiririko mzuri wa mawazo na hoja.
• Kutoa mrejesho kuhusu nguvu na udhaifu wa kila sehemu ya tasnifu.

2. Kuhakikisha Ubora wa Utafiti
• Thibitisha kuwa utafiti unafuata misingi sahihi ya kitaaluma.
• Hakikisha kuwa maswali ya utafiti yamejibiwa kwa kina na kwa ushahidi wa kutosha.

3. Kusahihisha Makosa ya Kiufundi
• Kurekebisha makosa ya sarufi, uandishi wa kitaaluma, na upangaji wa sentensi.
• Kuhakikisha matumizi sahihi ya rejea na mtindo wa kunukuu (e.g., APA level one au saba ,MLA, Harvard).

4. Kutoa Mwongozo wa Kuboresha Mbinu za Utafiti
• Kushauri kuhusu uthibitisho wa data, tafsiri ya matokeo, na uchambuzi wa kina.
• Kuelekeza marekebisho katika sehemu ya mbinu (methodology) ikiwa kuna mapungufu.

5. Kuhakikisha Muundo wa Tasnifu Unafuatwa
• Kudhibitisha kuwa tasnifu imepangwa kulingana na mwongozo wa chuo.
• Kuangalia iwapo kuna utangulizi sahihi, sura za msingi, hitimisho, na mapendekezo.

6. Kuandaa Mwanafunzi kwa Viva Voce
na kumpa tarehe maalumu kuwa siku fulani utatakiwa kufanya vivavoce kwa kubandika matangazo kwenye mbao za chuo pamoja na kwenye websites kama mwanafunzi fulani atafanya viva voce hivyo umma unaalikwa
hii inafanywa na SAUT main campus na UDSM kwa ubora wa hali ya juu kabisa
• Kumpa mwongozo wa jinsi ya kutetea tasnifu yake mbele ya kamati ya mitihani.
• Kumuandaa kwa maswali yanayoweza kuulizwa na jinsi ya kuyajibu kwa weledi.

7. Kufanikisha Kuwasilishwa kwa Tasnifu
• Kuridhika kuwa kazi iko tayari na inaweza kuwasilishwa kwa ajili ya tathmini rasmi.
• Kusaini fomu za idhini na kuwasilisha kazi kwenye idara husika.
8.kujibu maulizo,kutoa ushauri pamoja kama una tatizo usaidiwe
kama haya supervisor hafanyi basi sio supervisor tena kama management haifatilii basi ni tatizo kubwa na linashusha ubora wa chuo
 
Katika makosa niliyofanya katika maisha ni kujiunga na masomo ya PhD pale Open University of Tanzania. Ningelijua ningeeda UDSM. Kwa matatizo ninayopitia sishauri mtu akasome PhD pale OUT.

Chamgamoto nilizopitia ni kama ifuatavyo:

1. Supervisor kutojibu email zangu au hata sms kwa zaidi ya mwaka mmoja.

2. Supervisor kukaa kimya bila kupitia proposal kwa zaidi ya mwaka mzima na Wala hajali. Unamtumia kazi zaidi ya mara kumi ila hajibu na yupo kimya kana kwamba hakujui.

3. Process ya kubadilisha supervisor ni ngumu Sana, unaweza kukaa mwaka mzima unahangaika tu. Nilijaza fomu ya kubadilisha supervisor wakaa kimya, nilipowakomalia wakanipa fomu nyingine, stori ikaishia hapo.

4. Yule mdada au secretary wa ofisi ya post graduate research wa OUT ana dharau Sana. Ukimpigia simu hapokei na hata akipokea akajua ni wewe ana kata simu yako. Yule dada ni shida Sana.

5. Kwa sisi tulioko mikoani ni shida kusoma PhD OUT. Hawajali kabisa. Na ukisema usafiri kwenda huko Dar utazungushwa mpaka uchoke. Nimeenda Dar kituoni kwao pale Biafra ni shida tu hakuna la maana la kunisaidia.

Kutokana na OUT kunisumbua kwa muda wa miaka mitatu huku ada yangu wamekula ila kunisaidia kwao wanaona mzigo au usumbufu kwakweli ni Bora niache kusoma hiyo PhD nifanye mambo mengine. Ila wamenipotezea muda, hiyo miaka mitatu imeenda Bure. Yani miaka mitatu unahangaika na proposal haijawahi kusahishwa hata kusomwa tu na supervisor. Ukienda ofisini kwao Biafra unaambiwa supervisor wako hayupo amesafiri.

7. Kwa kweli OUT mnakatisha tamaa, mtu anakuwa kama hasomi PhD. Kama uwezo wa kusimamia tafiti za wanafunzi wa PhD hapo si mnamwambia mwanafunzi atafute chuo kingine kuliko kupoteza muda wa mtu.
Halafu wanapenda rushwa sana. Ukiwapa chochote kitu supervisor anasoma chap. Yaani ni balaa. Mimi nilitaka kusoma PhD OUT nikashtika baada ya kuona jamaa yangu anvyosumbuliwa.
 
Kuna lecturer wangu mmoja alisema Namnukuu "mimi nilipata kwa tabu sana hii phd yangu alafu wewe ndo uje upate course work kirahisi"
Nakwambia robo tatu ya darasa tulikunja "C" lile somo 🙌
😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom