Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 286
CHADEMA sasa ni zaidi ya chama kikuu cha upinzani nchini. Bungeni ikiwa na Wabunge 48 ambao ni sawa na asilimia 13.445 ya Wabunge wote 357,inafanya mambo makubwa. Inabuni,inahoji,inajenga hoja na kuomba miongozo ya Spika mambo yanapokwenda mrama. Nje ya Bunge ndio usiseme. Mikutano ya kueleza ukweli na ya kujadili mstakabali wa taifa inafanyika kwa ubunifu,ufanisi na mafanikio makubwa. Sasa imejijengea heshima na uaminifu mkubwa kwa wananchi. Inasubiriwa kutwaa dola. Siri ya mambo haya ni tatu. Kwanza,imesimama yenyewe. Inapambana na yeyote anayeweza kupambana nayo kisiasa. Haiogopi. Pili,inatumia kila nafasi ijitokezayo ipasavyo. Si nje wala ndani ya Bunge. Pia,ina uongozi bora uliojaa ubunifu,busara na uwezo.Natamani na kutumai kujiunga nayo nikijiunga siasani...
Mkuu unazungumzia chadema ipi? Maana sifa ulizozitoa ni kinyume na mwenendo wa chama husika.
Hao viongozi wenye ubunifu, busara na uwezo unaowazungumzia ndio hawa kina Mbowe, Dr. Slaa, Lema, Mch. Msigwa, Marando, Mbilinyi, Lissu etc?
Pole kijana, ingawa bado naamini una nafasi ya kujifunza zaidi haya mambo kama ukiwa tayari.
Katika viongozi ninaowajua ndani ya chadema, ni Mh. Mnyika mwenye sifa ulizotaja hapo juu so far...kidogo na comrade Zitto ingawa naye ana udhaifu wake wa kupenda utukufu binafsi.
Seriously speaking, Mnyika is so far a good leader ila yuko kwenye chama ambacho si sahihi (kwa mwenendo wa sasa wa chama chake). Huwezi compare Mnyika na kina Mbowe au Lema, Mnyika is more composed and looks far better matured.