Siri Imefichuka! Yesu Kristo sio Nabii Isa

Siri Imefichuka! Yesu Kristo sio Nabii Isa

Status
Not open for further replies.

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Kuna watu wanafundisha kwamba jina jingine la Yesu ni Nabii Isa. Ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Yesu Kristo na Nabii Isa.

Yesu Kristo ana sifa kuu zifuatazo:

Ni Mwana wa Mungu na pia ni Mungu.
Katika Mt 16:15-17 – Yesu alimwuliza Petro, "Nanyi mwanisema mimi kuwa ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai." Yesu alimpongeza kwa kuujua ukweli huo, akamwambia kuwa amefunuliwa na Baba wa mbinguni.

Asiyeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu hana uzima
Yohana 3:36
"Amwaminiye Mwana anao uzima wa milele; asiye mwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia."

1 Yohana 2:23
"Kila amkanaye Mwana, hana Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia."

Yesu alisulibiwa, alikufa msalabani na kufufuka siku ya tatu ili sisi tupate wokovu.
Ili mtu apate wokovu ni lazima akiri kama ilivyoandikwa katika
Warumi 10:9
"Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka."

Yesu Kristo ni Alfa na Omega; ni wa milele.
Katika Ufunuo 22:13 – Yesu anasema, "Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho." Hakuna nabii yeyote anayeweza kusema maneno hayo.

Yesu Kristo ana mamlaka ya kusamehe dhambi
Katika Marko 2:5-7 – Yesu alimwambia mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako." Mafarisayo walishangaa, wakisema, "Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?"

Katika Ufunuo 19:16 – Yesu anaitwa Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, hadhi ambayo manabii wa kawaida hawakuwa nayo.

Wanaosema kwamba Yesu ni Nabii Isa, waulize: je, wanakubaliana na sifa hizo za Yesu? Watakujibu kwamba Nabii Isa sio Mwana wa Mungu...

Kwahiyo kama wewe ni Mkristo unayeongozwa na Maandiko ya Biblia, usimwite Yesu kwa jina la Isa, kwa sababu majina hayo mawili hayana maana sawa.

Nimekufunulia siri hiyo, usidanganyike tena!
 
Kuna watu wanafundisha kwamba jina jingine la Yesu ni Nabii Isa. Ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Yesu Kristo na Nabii Isa.

Yesu Kristo ana sifa kuu zifuatazo:

Ni Mwana wa Mungu na pia ni Mungu.
Katika Mt 16:15-17 – Yesu alimwuliza Petro, "Nanyi mwanisema mimi kuwa ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai." Yesu alimpongeza kwa kuujua ukweli huo, akamwambia kuwa amefunuliwa na Baba wa mbinguni.

Asiyeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu hana uzima
Yohana 3:36
"Amwaminiye Mwana anao uzima wa milele; asiye mwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia."

1 Yohana 2:23
"Kila amkanaye Mwana, hana Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia."

Yesu alisulibiwa, alikufa msalabani na kufufuka siku ya tatu ili sisi tupate wokovu.
Ili mtu apate wokovu ni lazima akiri kama ilivyoandikwa katika
Warumi 10:9
"Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka."

Yesu Kristo ni Alfa na Omega; ni wa milele.
Katika Ufunuo 22:13 – Yesu anasema, "Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho." Hakuna nabii yeyote anayeweza kusema maneno hayo.

Yesu Kristo ana mamlaka ya kusamehe dhambi
Katika Marko 2:5-7 – Yesu alimwambia mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako." Mafarisayo walishangaa, wakisema, "Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?"

Katika Ufunuo 19:16 – Yesu anaitwa Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, hadhi ambayo manabii wa kawaida hawakuwa nayo.

Wanaosema kwamba Yesu ni Nabii Isa, waulize: je, wanakubaliana na sifa hizo za Yesu? Watakujibu kwamba Nabii Isa sio Mwana wa Mungu...

Kwahiyo kama wewe ni Mkristo unayeongozwa na Maandiko ya Biblia, usimwite Yesu kwa jina la Isa, kwa sababu majina hayo mawili hayana maana sawa.

Nimekufunulia siri hiyo, usidanganyike tena!
Unajua kwa kituruki Yesu anaitwaje?
 
Kuna watu wanafundisha kwamba jina jingine la Yesu ni Nabii Isa. Ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya Yesu Kristo na Nabii Isa.

Kwahiyo kama wewe ni Mkristo unayeongozwa na Maandiko ya Biblia, usimwite Yesu kwa jina la Isa, kwa sababu majina hayo mawili hayana maana sawa.
Yaani ndio leo unajua hili? Sie hawa jamaa tulikuwa tunawasanifu tu, tunawaacha vipofu waongozwe na vipofu wenzao siku nyingi! Mungu mmoja atatoaje majina tofauti kwa ajili ya mtu mmoja kwa waumini tofauti?
 
Siku zote huwa nauliza kama Yesu sio Isa kwamba wana sifa tofauti sasa mbona malaika waliyoasi tunaambiwa ndio majini hali ya kuwa wana sifa tofauti?
 
Kwani wewe sio wa milele,kwamba ukifa hutafufuka na kuishi milele kama alivofufuka yesu kwa mujibu wa maandiko?
 
Wewe Setfree na Marelia 2 ni virusi hatari sana aisee. Mmekuja kwa kasi sana.

Mods haya mambo mnachekea ila trust me ipo siku mtashindwa kuya control ndani ya JF na nje ya JF!

Ondoeni virusi hivi kungikali bado hakujaharibika sana. Ni ushauri tu
 
Yaani ndio leo unajua hili? Sie hawa jamaa tulikuwa tunawasanifu tu, tunawaacha vipofu waongozwe na vipofu wenzao siku nyingi! Mungu mmoja atatoaje majina tofauti kwa ajili ya mtu mmoja kwa waumini tofauti?
Najua hilo siku nyingi, Synthesizer ila leo nimesukumwa na upendo wa Mungu kuwajulisha ukweli hao wanaoamini kwamba Yesu ni Nabii Isa.

By the way, mbona kauli yako[tulikuwa tunawasanifu tu, tunawaacha vipofu waongozwe na vipofu wenzao] inapingana na signature yako?(Usimpuuze mjinga, muelimishe)

Nafikiri kauli yako umeinukuu katika Mathayo 15:14. Hapo Yesu alikuwa anamaanisha kwamba Mafarisayo waliokataa ukweli wa Mungu waachwe waendelee katika upofu wao wa kiroho, kwa sababu walishikilia mapokeo yao badala ya Neno la Mungu.

Hii haimaanishi kuwa Wakristo wasiwajali watu wanaopotea, bali inamaanisha kwamba kama mtu anapinga ukweli kwa ukaidi, basi usiendelee kubishana naye (Tito 3:10).
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom