Sio siri watumishi wameshuka moyo

Sio siri watumishi wameshuka moyo

Kwanini nilimpa kura yangu Bwana nywele nyeupe?...Ni kwasababu nilijua pamoja na wizi wake uliokubuhu lakini anajua kuzungusha pesa.Hii ni kama biashara lazima uzungushe pesa izaliane,Jk aliiba sana lakini alizungusha pesa sanaa ndio sababu watu walikula bata...kila siku kuongea na wazungu kujua dunia ikoje na kujifunza pia.

Sasa huyu ndugu yenu kamtaji hako hako anakafungia ndani ,ela itazaa vipi...kabakia kusema anabana matumizi huku mtaji ukiisha taratibu.

Uongozi ni kipaji sio lazima kila MTU awe kiongozi


Pambana na hali yako cc2025
 
Humu ndani watu mnajidai tu ili huo uzi unawagusa sana tu,...unless kama sio mtumishi wa serikali.....acheni unafiki

Sent using Jamii Forums mobile app

Na kweli lakini acha tujipe moyo maana hata ukipovuka haisaidii umeshaambiwa kabisa hutaki kazi acha ,enzi za JK tulikuwa tunabembelezwa kwasasa ,wahitimu kibao mtaani wanatafuta ajira tena wengine wana masters na wapo tayari kwa mshahara wa hata 400,000 kwa mwezi
 
Acha KAZI ili mkuu utapata kazi NZURI ZAIDI yenye MASLAHI MAKUBWA Zaidi
 
Kwa watumishi wa serikali waliowengi hawana morale na tija ya kufanya kazi.Serikali ingekua na uwezo wa kuchunguza mioyo ya watu hao hakika wangestaajabu.Wengi wanahudhuria na kuwepo ila spirit hakuna.Huko kwenu hali ikoje.Binafsi ile kauli ya ukitaka acha kazi kama mishahara mdogo haiwezi kunifanya nife moyo au kuacha kazi.Siasa haziwezi athiri maisha ya wengi kwa ukatili.
Hata ukisema uache kaz hali ya mtaani unaielewa vzur lkn .....hali n tete kila kona ,na kama mtumishi unasound noise iv VP wenzangu na mm#makapuku#maisha ndo haya haya pambana na hali yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2019, 2020 Inshaallah,,,, sijui ndo inavyoandika mshahara na posho kwa watumishi wa uuma vitakuwa bwerereeeeeee
 
Binafs nshakata tamaa..nnachohitaj kwa sasa n kufungua shule..nursery,tuition centers, computer courses...na kilimo kwa wingi..lazima tutaheshimiana tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau japo nimeandika Uzi huu ila ninapofanyia kazi na marafiki wote wanalalamika wametelekezwa mama wa kipare

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa Mzalendo zaidi. Fanyia kazi taifa lako kwa faida ya vizazi vijavyo. Kama unaona maslahi hayakutoshi fungua hata genge ufanye biashara maisha yatasonga tu.

Kuliko kufanya kazi kwa shingo upande ma manung'uniko chungu nzima bora uache kazi ukashike jembe, unatuharibia nchi yetu inayohitaji watu wafanye kazi kwa moyo mmoja.

Kwa watu wenye moyo kama wa mleta mada hata akilipa milioni 10 atataka aongezewe. Nia yao ni kuitafuna tu nchi kuliko kuitumikia na kuijenga kiuchumi.
Kuwa mzalendo zaidi ndo kukoje, mmeambiwa several times gharama za maisha ziko juu, mshahara uko pale pale. Mnaendelea kuwaambia watumishi wawe wazalendo, nyie watu iko siku vinywa vyenu vinavyotoa kauli zilizojaa kila aina ya kiburi na dharau vitalighalimu Taifa.
 
Mtaongezewa 2019 ili mpige kura ya ndio kwa Magufuli na CCM.Subiri tu
Mkuu haitobadilisha kitu, na kwa akili zao watafanya kila aina ya wema ili wakubalike na hawatoungwa mkono.
 
Kuwa Mzalendo zaidi. Fanyia kazi taifa lako kwa faida ya vizazi vijavyo. Kama unaona maslahi hayakutoshi fungua hata genge ufanye biashara maisha yatasonga tu.

Kuliko kufanya kazi kwa shingo upande ma manung'uniko chungu nzima bora uache kazi ukashike jembe, unatuharibia nchi yetu inayohitaji watu wafanye kazi kwa moyo mmoja.

Kwa watu wenye moyo kama wa mleta mada hata akilipa milioni 10 atataka aongezewe. Nia yao ni kuitafuna tu nchi kuliko kuitumikia na kuijenga kiuchumi.
Wakati huohuo wako wanaoibomoa kwa ari na moyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom