Sina ujasiri wa kuacha kazi

Sina ujasiri wa kuacha kazi

Public

Hiki pia kinachangia, nilijaribu kumshirikisha mzazi wangu mmoja naacha kazi alifunga kuniombea sababu Taasisi ninayofanyia ni moja ya Taasisi ambayo inanibeba sn na inafanya mtu akijua upo sehemu hiyo unapata msaada kwa haraka, so kwetu wanaona kama nimechanganyikiwa.
Hilo ndo tatizo apo kwenye kukubebwa na hyo status.......ni sawa na wale ndugu zetu wa kwenye system ata awe na mapesa gani bado wanawaza uchaguzi ujao.

Kwasababu wanaamini wakiwa uko ni mwendo wa mbeleko tu na status kuwa mimi mtu mzito.....

Ushauri, kaa na mumeo chini muongee vzuri, mmeo ndo anamaamuzi ya mwisho,

Najua unaogopa ukiacha kazi afu biashara nayo ikaja kuyumba jamii itakuonaje.....!! Ila mmeo ndo final say
 
Siku moja nimeamka na wenge langu nikaenda moja kwa moja kwa MD nikamuambia kwa uwazi nataka nifanye mambo yangu, ila ikitokea mnahitaji msaada wangu nipo ( uzuri walikuja nitafuta badae walipitia heka heka ambazo zilikuwa kwenye eneo wa ujuzi wangu ).

Nakumbuka ilikuwa 2012 hapo baada ya hapo nikaanza mambo yangu maana na kazi yenyewe nilifanya mwaka mmoja tu kwa taabu. Na wewe ipo siku moja tu, utachukua uamuzi japo huwa sio rahisi kwenye hizi kazi kuna mazingira ukiyakumbuka kama yanakupumbaza kuacha kazi
 
Hilo ndo tatizo apo kwenye kukubebwa na hyo status.......ni sawa na wale ndugu zetu wa kwenye system ata awe na mapesa gani bado wanawaza uchaguzi ujao.

Kwasababu wanaamini wakiwa uko ni mwendo wa mbeleko tu na status kuwa mimi mtu mzito.....

Ushauri, kaa na mumeo chini muongee vzuri, mmeo ndo anamaamuzi ya mwisho,

Najua unaogopa ukiacha kazi afu biashara nayo ikaja kuyumba jamii itakuonaje.....!! Ila mmeo ndo final say
Ni kweli kabisa unachokiongea.

Asante kwa ushauri mzuri.
 
Biashara zako haziyumbi sabbu unalo pato la uhakika kila baada ya siku 30 ofisini .ukishategemea biashara pekee kama kila kitu chako ikiyumba kidgo huwezi kuiokoa , ofisn ukiwepo katika nyakati hizo waweze chukua mkopo wa sacoss ama salary loan.

Otherwise labda useme tu wewe ni maisha bora kitambo na vyote unavofanya si lazima uvifanye sababu maisha yako yataenda tu. / set new higher goals tumia hio taaluma hapo ofsn usiendee kuiweka nyumbani
 
Habari wana JF.

Mtanisamehe kama nitaandika bila mpangilio, wengine hatuna utaalamu sana wa Lugha.

Wale watu wa dhihaka na kuona mtu akileta mada humu mnaona anajisifia plz, naomba mkae pembeni.

Nilijiekea dhamira na malengo nikifikisha 40 yrs nitaacha kazi sababu malengo yangu yatakua yametimia, ila Mungu ni Mkuu nimetimiza malengo yangu mwaka jana December nikiwa na 38 yrs.

Ila naogopa sana kuacha kazi, nimejikuta sina ujasiri kabisa.

Kwanini naacha kazi??
1. Sina passion na kazi hata kidogo, sipendi kuajiriwa.

2. Mshahara ninaopata kazini, naupata kwenye biashara tena zaidi pia niliweka FDR ambako nako kunanipa hela nzuri tu kila baada ya miezi 3. Hivyo, hata nikiyumba kibiashara nina uhakika wa kupata hela nzuri tu. Pia nina vitega uchumi vingine nisingependa kuviweka wazi ila vipo vinajiendesha vyenyewe mimi ni kupita tu kuangalia mara chache.

3. Kulea watoto wangu kwa ukaribu zaidi roho inaniuma kwa week napata siku mbili za kukaa full na watoto wangu.

4. Mume wangu anasafiri sana, hivyo nakosa muda wa kukaa nae pia anakua ananihitaji nimsindikize kwenye safari zake nashindwa. Natamani nipate muda zaidi nimlee pia Mume wangu

pamoja na yote hayo najikuta nakosa ujasiri kabisa, mlioacha kazi mliwezaje? Mlipata changamoto gani? Mlijutia? naomba ushauri.

Nimeona heri niombe ushauri huku sehemu ambayo sifahamiki.
Kipato huleta majivuno
 
Nakosa namna ya kutoa neno la ushauri kwa sababu kwanza una mapendeleo yako, pili vipaombele vyako kwa hio ni ngumu kusimama kwenye hitimisho mojo.

Ushauri ukiwa wa kuacha kazi ama kundelea yote yote yana sababu za msingi sababu zenye hoja hivyo kwa sisi tulio nje ya wewe lazima tukose moja lenye nguvu.

Ila mimi binafsi natamani kukushauri usiache kazi, ingawa inasemekena ajira ni utumwa ila binafsi naamini kazi inalinda.

Hivyo vyote ulivyo navyo naamini kabisa msingi wake ni hio kazi, sasa kwa vile bado unasita kuacha , ama bado hautamani kuacha lakini unatamani pia kutimiza dhamiri yako uliojiweke hapo kabla ya kuacha kazi wakati fulani, nao wakati umefika ila moyo mwingine unakuambia usiache.

Ushauri wangu sikiliza moyo unaokuambia usiache.

Lakini pia pata ushauri wa mwenzi wako, anaweza kuliona kwa mapana zaidi.

Ilishindikana kabisa jaribu kuomba likiizo hata isio na malipo ya muda mrefu uone hali utakayo kuwa nayo kipindi haupo kazini.

Hongera kwa yote.
 
Public

Hiki pia kinachangia, nilijaribu kumshirikisha mzazi wangu mmoja naacha kazi alifunga kuniombea sababu Taasisi ninayofanyia ni moja ya Taasisi ambayo inanibeba sn na inafanya mtu akijua upo sehemu hiyo unapata msaada kwa haraka, so kwetu wanaona kama nimechanganyikiwa.
Msaada wa kuhamia tasisi yenu
 
Pole kwa changamoto na hongera kwa kutimiza malengo yako. Nikwambie tu maisha ni mafupi sana kukaa mahali ambapo hupafurahii hata kidogo ukizingatia una uwezo wa kuendesha maisha yako bila hiyo kazi, na hata kama ikitokea kipato kimeyumba hutalala njaa wewe na wanao kwa sababu mumeo yupo. Usijiumize sana kwaajili ya watu wengine, kama kuna watu wanapata msaada wa haraka kwa wewe kuwepo hapo nina imani umeshawasaidia wengi wanatosha maana ukweli ni kwamba huwezi kumsaidia kila mtu, kwa mara moja kuwa mbinafsi kidogo chagua furaha yako.
 
Hilo ndo tatizo apo kwenye kukubebwa na hyo status.......ni sawa na wale ndugu zetu wa kwenye system ata awe na mapesa gani bado wanawaza uchaguzi ujao.

Kwasababu wanaamini wakiwa uko ni mwendo wa mbeleko tu na status kuwa mimi mtu mzito.....

Ushauri, kaa na mumeo chini muongee vzuri, mmeo ndo anamaamuzi ya mwisho,

Najua unaogopa ukiacha kazi afu biashara nayo ikaja kuyumba jamii itakuonaje.....!! Ila mmeo ndo final say
Sio kwa ubaya ila unadhani amekuja kutuomba ushauri sisi ilhali hajaongea na mumewe kwa kina? Nionavyo mimi mumewe amemuachia hayo maamuzi mwenyewe afanye uamuzi wa mwisho. Apparently wapo wanaume wanaowatreat wake zao kama binadamu huru wenye uwezo wa kufanya maamuzi kuhusu mambo yao.
 
Biashara zako haziyumbi sabbu unalo pato la uhakika kila baada ya siku 30 ofisini .ukishategemea biashara pekee kama kila kitu chako ikiyumba kidgo huwezi kuiokoa , ofisn ukiwepo katika nyakati hizo waweze chukua mkopo wa sacoss ama salary loan.

Otherwise labda useme tu wewe ni maisha bora kitambo na vyote unavofanya si lazima uvifanye sababu maisha yako yataenda tu. / set new higher goals tumia hio taaluma hapo ofsn usiendee kuiweka nyumbani
Mkuu sijatoka maisha bora nimepambana sana kufika hapa!!

Sio kila aliefanikiwa kwao ni maisha bora.

Nilipambana kwa nguvu zangu bila msaada hata wa Mume.

Nilishaacha kutegemea mshahara muda tu, nishakataa safari za Ofisini nyingi tu nikisingizia mgonjwa, so nilishatoka huko kwa kutegemea mshahara.
 
Sio kwa ubaya ila unadhani amekuja kutuomba ushauri sisi ilhali hajaongea na mumewe kwa kina? Nionavyo mimi mumewe amemuachia hayo maamuzi mwenyewe afanye uamuzi wa mwisho. Apparently wapo wanaume wanaowatreat wake zao kama binadamu huru wenye uwezo wa kufanya maamuzi kuhusu mambo yao.
Ni kweli.

Alichoniambia fanya maamuzi yoyote nitakusupport, ukiacha kazi sawa ukiamua kuendelea sawa.
 
Habari wana JF.

Mtanisamehe kama nitaandika bila mpangilio, wengine hatuna utaalamu sana wa Lugha.

Wale watu wa dhihaka na kuona mtu akileta mada humu mnaona anajisifia plz, naomba mkae pembeni.

Nilijiekea dhamira na malengo nikifikisha 40 yrs nitaacha kazi sababu malengo yangu yatakua yametimia, ila Mungu ni Mkuu nimetimiza malengo yangu mwaka jana December nikiwa na 38 yrs.

Ila naogopa sana kuacha kazi, nimejikuta sina ujasiri kabisa.

Kwanini naacha kazi??
1. Sina passion na kazi hata kidogo, sipendi kuajiriwa.

2. Mshahara ninaopata kazini, naupata kwenye biashara tena zaidi pia niliweka FDR ambako nako kunanipa hela nzuri tu kila baada ya miezi 3. Hivyo, hata nikiyumba kibiashara nina uhakika wa kupata hela nzuri tu. Pia nina vitega uchumi vingine nisingependa kuviweka wazi ila vipo vinajiendesha vyenyewe mimi ni kupita tu kuangalia mara chache.

3. Kulea watoto wangu kwa ukaribu zaidi roho inaniuma kwa week napata siku mbili za kukaa full na watoto wangu.

4. Mume wangu anasafiri sana, hivyo nakosa muda wa kukaa nae pia anakua ananihitaji nimsindikize kwenye safari zake nashindwa. Natamani nipate muda zaidi nimlee pia Mume wangu

pamoja na yote hayo najikuta nakosa ujasiri kabisa, mlioacha kazi mliwezaje? Mlipata changamoto gani? Mlijutia? naomba ushauri.

Nimeona heri niombe ushauri huku sehemu ambayo sifahamiki.
Mbona kama unataka kututeka vijana hapo uliposema umefanikiwa kiuchumi na hapo uliposema mumeo anasafiri
 
Tusemu mshahara kwa mwez ni 5milioni kwa jinsi ulivosema unafanya kaz taasisi kubwa ya serikali

Haya hiyo biashara unayofanya inakuingizia mara 2 ya mshahara kwa mujibu wako

Kuna mleta mada kasema uwe na hisa 200m na utt 80m ili upate 22,000 faida per day, ukasema hii hela ni ndogo

Nikipiga mahesabu ya haraka haraka wewe utakua na utajir wa 500milion

Kwakawaida hizo ni pesa za watu wenye vitengo vizito uko serikalini

Mwisho nakupa hongera na kukupa cheo cha tajir la Jamii forum
 
Back
Top Bottom