Sina hamu ya kuendelea na mchakato wa ndoa tena

Za jioni wakuu,

Bila kupoteza muda kama kijana nilipata demu tukaenda sawa na process zote za ndoa ziko tayari bado mwezi mmoja tu ila cha ajabu kila nikimuona saa hivi naona hanivutii kabisa kila siku namtafutia sababu lakini anapangua maskini dada wa watu analia kila Siku sijui nimepatwa na nini wandugu sometimes sitamani hata kumuona ila hajanikosea kitu.

Naweza nisipende tu alivyo vaa nikachukia siku nzima. Akinisemesha najibu mbovu tu, kuna muda nahisi nimekosea kumchagua japo sioni udhaifu mkubwa wakutisha kwani nimehack sim yake sioni SMS mbovu wala maongezi mabaya ila ni hali tu imekuja ghafla tena mbaya zaidi baada ya kujitambulisha kwao.

NB mahusiano yana almost 2yrs

Ninachokiona either ulimtamani tu kwa muda, haukumpenda, umefahamiana nae kwa muda gani kabla ya kuingia kwenye process za ndoa? Next time kabla hujafanya maamuzi makubwa ya kujitambulisha kwa binti hakikisha moyo wako uneridhia kuwa na huyo binti katika hali zote
 
Jipeni mapumziko ya mda, kila mtu afanye yake.

Kwa mda mtakao pendelea.

Ukiona hata humkumbuki unapokuwa mbali naye....basi unaweza kusitisha zoezi zima la ndoa.

Yawezekana ni kipindi cha mapito....hutokea kwenye mahusiano (kukinai mwenza bila sababu)

Ushauri mujarab…ILA kwa maisha yetu SISI waswahili kuna neno KUJIPA MAPUMZIKO? put yourself in her shoes uambiwe tupumzike kidogo..si utakufa kwa kihoro tena home wanamjua!

Kama jamaa hamtaki aseme tu nilikosea naona sitawezana, black n white! Ngumu kumeza ila itaokoa muda wa binti wa watu, atalia yataisha .
 
Chukua Huu Ushauri Wangu Pia Ufanyie Kazi
Utakuja Kunishukuru Kwenye Thread Yako
Nenda Sehemu Hizi Haraka Sana
Sijui Upo Wapi Sasa Hivi Ila Anza Hapa
1 . Mirembe Hospital Dodoma
2 . Lutindi Mental Korogwe
 
Kwanza, hali hii hutokea na si kitu cha ajabu.

Tunapaswa kujua kuwa mtu ni roho iliyouvaa mwili. Lakini pia mtu anamoyo ambalo ndimo mawazo na hisia na maamuzi hufanyika. Roho zetu huwa kuna kipindi huona kitu na tunapatwa na mabadiliko fulani bila kujua yamekuja vipi, mfano mtu anasema nilichezwa na machale, si kweli kwamba ni machale ila ni namna ambazo roho zetu hupokea taarifa kutoka kwa Mungu wetu kwamba kuna jambo fulani halipo sawa sawa ama kuna shida mahali.

Ukiweza itambua njia na taarifa za rohoni husaidia sana maana hutokana na Manufacturer wetu (Mungu), kututaarifu juu ya mambo ya maisha yetu.

Jambo hili lililokutoea, limemtokea Kaka yangu mwaka 2002. Alikua ametoa mahari, na wameanza kuandaa harusi. Ila ilikuja ghafla tu, akamchukia Mchumba wake, na akasema hawezi kumuoa kwa jinsi alivyomchukia. Binti hakuwa na kasoro yoyote, hakufanya jambo lolote baya, na alikua mlokole huyo binti. Ikabidi Kaka aende kwa mchungaji wake na akamwambia hata mahari yangu sitaki kuichukua ila nakuomba uongee na binti mahusiano yaishe. Na kweli yote yalifanyika.

Mwaka 2003, akapata mke akaoa, hapakuwa na shida. Mpaka leo 2021 wako pamoja, katika mazungumzo yangu na yeye anasema changamoto alizopitia kwenye maisha tangu aoe, yule Mchumba wa kwanza asingeziweza, na njia anayopita ni njia ngumu sana na ananifundisha kuwa angekua na yule asingefika hapo alipo sasa

NB:
Yapo mengi kuhusu kesho yako ambayo huyajui ila Mungu tu, ukijua roho yako haitaki kuoa/kuolewa na fulani usilazimishe maana anaweza kuwa fit kwa muda huo ila hujui baada ya 20 years maisha yatakapo kupeleka, vipi mwenzako ataweza??

Pata muda wa kukaa na kusikiliza ndani yako (roho) kuliko hisia za moyo wako.

Jambo hili ni pana sana, siwezi andika kila kitu. Ukiona ushauri huu waweza kuwa njia na msaada kwako, basi njoo inbox.
 
Back
Top Bottom