Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Duh! miaka minne anausoma mchezo! domo zege au kibisa? fanya mautundu yako ya kike utuokolee mwanaume mwenzetu inawezekana kwa jinsi anavyokuona ulivyo umbika akikutamkia unaweza kumtosa so kama nawe umemridhia basi anzisha move uone reaction yake.
 
Habari za kutwa waungwana,

Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa.

Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.

Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.

Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
Mkuu nawe emevutiwa kama jimbo lipo wazi tia nia
 
Huyo muulize ashawahi kuwa na Mke au mchumba hapo ndo mtaanzia story we mwambie tuuu akuowe
 
Inawezekana, lakini anaiomba tutoke kwa chakula kwenye hoteli nzuri, sasa kama sina mvuto mbona haoni haya kwenda na mimi in public places, pia tunakwenda wote kanisani J2.
Umepata mume..jitahidi.mutoke.toke.umuelewe naye akuelewe
 
Unaweza ukute anakujali tu kama rafiki, hii kitu ishawahi kunitokea nami nilihisi tofauti kumbe walaaaa! So kuwa huru.
Ila ni kama umeshajenga hisia kwake so unatamani afunguke!!
 
Unaweza ukute anakujali tu kama rafiki, hii kitu ishawahi kunitokea nami nilihisi tofauti kumbe walaaaa! So kuwa huru.
Ila ni kama umeshajenga hisia kwake so unatamani afunguke!!
Exactly, yani haya mambo bana hata hayaeleweki. Kuna wanawake pia mnaweza mkawa marafiki mno, akakujali mno hadi nafsi ikagusika. Siku mkaka akiamua kufunguka ndo na urafiki unafwariki. Utasikia zile "nilimuheshimu kama kaka yangu ila kanitongoza", so kanivunjia heshima teh. Moyo wa mtu kichaka
 
Exactly, yani haya mambo bana hata hayaeleweki. Kuna wanawake pia mnaweza mkawa marafiki mno, akakujali mno hadi nafsi ikagusika. Siku mkaka akiamua kufunguka ndo na urafiki unafwariki. Utasikia zile "nilimuheshimu kama kaka yangu ila kanitongoza", so kanivunjia heshima teh. Moyo wa mtu kichaka
Ni kweli doughter, haya mambo hata hayaelewekagi.
 
He hee umeanza uchokonozi sasa. Ebu mwambie Sky niko tayari kujitolea kumrahisishia hii kazi akiniunganisha na jamaa
Aaah we noma, mifupa ilosinda fisi wewe nawesa yote.
 
Back
Top Bottom