Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Ningeelewa kama ingekuwa company tu, sasa na mambo ya kuniwekea pesa kwenye bahasha nayo ni company?

Kuna wanaume husema kwa vitendo kwa sababu vinywa vyao havikujaliwa kufunuka sawasawa.Mungu anatuumba hivyo.Ni juu yako kutafisiri hayo matendo yake na uchukue hatua.Nina imani kwa sababu ni rafiki yako wa Karibu kwa miaka minne sasa ukikaa naye na kumuuliza juu ya destination ya urafiki wenu ataweza kusema.Aibu haichagui jinsia wala umri na hata rangi.
 
Inawezekana, lakini anaiomba tutoke kwa chakula kwenye hoteli nzuri, sasa kama sina mvuto mbona haoni haya kwenda na mimi in public places, pia tunakwenda wote kanisani J2.
Mvuto wa kutoka Dinner unao lakn wa mambo ye2 ndio upo kdogo
 
Inawezekana, lakini anaiomba tutoke kwa chakula kwenye hoteli nzuri, sasa kama sina mvuto mbona haoni haya kwenda na mimi in public places, pia tunakwenda wote kanisani J2.
Kanisa gani hilo mnaloenda pamoja?
 
ipo hv, yawezekana anakupenda bt anashndwa kukuambia.. au anaenjoy tu uwe rafik yake bt kwa akili ndogo tu ni kwamb mshkaji anakupenda bt hana uzoefu na swala zima la mapenzi,
ushauri] kama na wew unajihc kama unampenda bs just show that you love him.
 
Ningeelewa kama ingekuwa company tu, sasa na mambo ya kuniwekea pesa kwenye bahasha nayo ni company?
Sasa si anakusaidia kama rafiki yako? Urafiki si ni kusaidiana pia?

Hivi ninyi wanawake huwa mnataka nini? Mara nyingine mtu akifanya hivyo then akakutongoza mnasema ooh.. kwani hatuwezi tu kuwa marafiki bila ngono?

Wanawake huwa hamueleweki na hamna msimamo.
 
Sasa si anakusaidia kama rafiki yako? Urafiki si ni kusaidiana pia?

Hivi ninyi wanawake huwa mnataka nini? Mara nyingine mtu akifanya hivyo then akakutongoza mnasema ooh.. kwani hatuwezi tu kuwa marafiki bila ngono?

Wanawake huwa hamueleweki na hamna msimamo.
Well, kusema ukweli hata lile kanisa nililipenda kwajili yake, lakini sioni maendeleo.
 
Siku 1 mwambie umekuja kwa ajili ya kulala kwake uone response yake
 
Naomba nikuhakikishie kuwa huyo anakupenda na anaogopa kukuambia..hivyo ndivyo wanavyokuwa watu wenye vinywa vizito..
 
Naomba nikuhakikishie kuwa huyo anakupenda na anaogopa kukuambia..hivyo ndivyo wanavyokuwa watu wenye vinywa vizito..
Na mimi ninaogopa kumuudhi, niko mwangalifu sana nikiongea nae.
 
Rafiki yangu mkubwa sana wa kike aligeuka ghafla na kuwa adui yangu.Yani akaanza kunichukia kwa namna ambayo si ya kawaida.

Siku zikaenda akaolewa na sasa ana watoto wawili ndo kaweza kunambia kwanin aliamua kunuchukia that much.

Anadai nlikua namdhalilisha na sikuwa nathamini hisia zake akidai kuwa alinipa ishara nyingi akaona sina dalili.

At the same time,binafsi nlikua namuelewa lakin nlikua nahofia uwezekano wa kuharibu urafiki wetu kama hatokubaliana na swala la mapenzi so nikawa nakaa tu kimya.

Maelezo yako yanaonesha wazi unampenda huyo jamaa, kabla siku hazijaganda mwambie jamaa ukweli hata kwa kumpa vifungu vya biblia vya kutongozea,zawad kama card na vitu romantic ambavyo ujumbe utafika direct.Ukiona bado hakupi green light basi mwambie kweli unampenda.Jikaze tu umwambie.
Note: Kwa kila utachofanya,usihusishe ngono atakudharau.
 
Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.

Sijaelewa hata hivyo maana ya ulokole wa kutupa.Je ni kuhudhuria kanisani mara kwa mara?Je Ulokole ni Kumcha Mungu au nini hasa? Je unafikiria Ulokole inaweza kuwa qualification mojawapo ya wewe kuwa mchumba wake iwapo atajiweka wazi mbele yako siku moja?Wewe kama binadamu una udhaifu na hivi mwanaume anayekufaa ni yule atakayekuwa na sifa kinyume na udhaifu wako ili kuleta ukamilifu(mkamilishano).Nje ya ukweli huo na msingi wa maumbile yetu kama binadamu huo ulokole utageuka kuwa " siki" badala ya maji utakapokuwa umebeba " msalaba ndoa"
 
vipi wewe una mchumba/mpenzi? je kwa macho ya juu juu unamuona huyo kaka anaweza kua mchumba/mme anaefaa kwako?

je unamuomba Mungu akupe mchumba/ mme?

mwisho kabisa UNAMPENDA HUYO Kaka MLOKOLE?
 
Back
Top Bottom