Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

Simulizi ya kipelelezi: Idaiwe maiti yangu

STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA TATU
SONGA NAYO................

Zilipita dakika tano tangu tukio lile liweze kutokea ndipo Othman alikuwa anafika eneo la tukio akiwa kwenye mwendo wa kasi isivyokuwa kawaida. Alikuwa ana wasiwasi kubwa mno kwenye moyo wake kwani hakutamani jambo ambalo alikuwa analiwaza liweze kutokea. Alishuka kwenye gari ikiwa hata haijasimama vizuri huku akiwa anaita kwa sauti na kukimbia kwa sababu alikuwa anajua mahali ambapo walikuwepo lakini alikuwa amechelewa.
Aina ya mauaji ambayo aliyakuta lile eneo yalimsikitisha, alikagua kila gari hakuona mtu yeyote yule. Aliwagusa watu wale na kugundua kwamba miili yao ilikuwa ya moto bado kwa maana hiyo ni kwamba walikuwa wameuawa muda mchache tu uliokuwa umepita. Alikimbilia kila eneo la karibu na sehemu hiyo akiwa anaita kwa nguvu lakini hakuna kitu alifanikiwa kukipata. Alirudi kwenye eneo lile akaanza kuwakusanya wenzake ili awapakize kwenye gari na kwenda kuwazika kwa heshima, aliamini kwamba hawakustahili kufa vifo vya kikatili namna hiyo. Othman Chunga alipiga magoti kisha akapiga kelele kwa sauti kubwa sana kiasi kwamba kama kulikuwa na mtu wa karibu ndani ya lile eneo basi alimsikia vizuri kabisa bila tatizo.

*********
Usiku ulikuwa unazidi kuwa mzito, ilikuwa ni siku kwa ajili ya msiba wa mke wa raisi lakini mkuu wa majeshi alishiriki msiba huo kama vile alilazimishwa, hakuonekana kuwa mtu ambaye alikuwa anavutiwa nao sana jambo ambalo lilimshtua hata raisi mwenyewe, hakuwa akimwelewa vizuri mtu huyo, alihisi kulikuwa na jambo ambalo lilikuwa nyuma ya pazia na watu wengi hawakuwa wakilijua.
Alimpigia mtu huyo simu lakini simu yake ilikuwa inatumika, alichukizwa mno na jambo hilo, raisi mwenyewe hakuwa sawa kabisa tangu mchana wa siku hiyo aweze kumuona kiongozi wao hilo eneo, hakuona kama mambo yalikuwa sawa hivyo alihitaji kumdodosa mkuu wa majeshi ili kuona kama alikuwa na taarifa za kutosha aweze kumpatia kile ambacho kilikuwa kinaendelea. Alisonya na kumpotezea lakini wakati huo simu inaita mkuu wa majeshi alikuwa anaelekea nyumbani kwake, hakuwa kinyonge kiongozi huyo bali alikuwa akilindwa na makomando tisa kila anako tembea kwa sababu aliambiwa kwamba hakuwa salama.

Akiwa barabarani anatoka kwenye mizunguko yake alimpigia simu kijana wake kutaka kujua kama alikuwa wapi wakati huo na ndiyo wakati ambao raisi alikuwa anapiga simu hiyo hivyo ikamkutia akiwa anaendelea kuongea.
“Bashir uko wapi kwa sasa?”
“Nipo karibu na nyumbani kwako bosi, nimekuja kukusikiliza nafikiri ndani ya dakika kumi nitakuwa nimefika hapo”
“Safi, nina kazi ambayo nahitaji nikupatie mimi nafika ndani ya dakika kama ishiri zijazo kwahiyo unisubiri nje nafika mara moja”
“Sawa bosi”
Alimaliza kutoa maagizo kwa kijana wake mtiifu kisha akaikata simu hiyo na kuingia kuangalia simu zilizo ingia kipindi anaongea na simu hiyo. Alikutana na simu ya raisi, alisonya huku akiwa anaipiga. Mheshimiwa aliipokea huku akiwa na jazba kali, wote hao walijijua kwamba walikuwa ni vibaraka tu ni basi mmoja alikuwa na nafasi kubwa kumzidi mwenzake ila mwenye nafasi ndogo alitaka kuanza kujitengenezea ufalme wake bila mwenzake kujua wala kushtuka.
“Hello mheshimiwa” aliongea baada ya kupiga huku akiwa na sauti ambayo ilikuwa ya kujiamini kweli kweli.
“Naona siku hizi umekuwa na dharau kiasi kwamba unanisubirisha mimi kwenye simu?”
“Samahani kiongozi yalikuwa ni mambo yangu binafsi ila nadhani nimekupigia ili tuweze kuongea”
“Hivi unanionaje labda Medrick?”
“Sijakuelewa mheshimiwa”
“Namaanisha unanichukulia mimi kama nani kwako labda?”
“Wewe ni raisi wa taifa zima na ni bosi wangu pia kwahiyo nakuchukulia kwa uzito kama huo”
“Wote tunajua sio kweli, hakuna kitu unaheshimu kuhusu mimi”
“Hayo umesema wewe mheshimiwa”
“Whaaaaaat?”
“Unajua huwa unanidharau sana ila nimekuvumilia kipindi chote hiki hivyo kwa sasa sitakubali hizo dharau zako ziendelee kuwepo kwangu”
“Unajua unaongea na nani?”
“Naongea na Mr George, raisi wa Tanzania” raisi ni kama hakuwa anaamini kama alikuwa anaongea na mtu ambaye ni yeye aliyekuwa amemuweka kwenye hiyo nafasi”
“Kwahiyo umeamua kuionyesha rangi yako halisi kwangu sio?”
“Kama umesema hivyo ni sawa”
“Sitakusamehe katika hili Savato, nitakufanyia jambo baya ambalo hujawahi kufikiria kukutana nalo kwenye maisha yako yote”
“Una uhakika na jambo hilo George?” kwa mara ya kwanza bwana huyo alimuita raisi kwa jina lake bila kumpa hata ile heshima ya uheshimiwa, jambo hilo hata raisi mwenyewe lilimshtua kwa sababu mtu huyo alikuwa anaongea kwa dharau sana, haikuwa bure lazima kulikuwa na kitu kinampa hiyo jeuri.
“Kuna jambo ambalo unalijua na mimi silijui?”
“Sina uhakika, una ishu ya mhimu ya kuniambia George?”
“Ni kitu gani kinakupatia jeuri hiyo?”
“Hahahah hahaha kwamba unanitisha utanitoa kwenye hii nafasi? Huwezi kufanya hivyo bila kuwauliza wakubwa kwanza hivyo wewe mwenyewe ni kibaraka tu ambaye huwa unapenda kujificha kwenye mabawa ya hilo jumba jeupe ila huna lolote la maana ambalo unaweza kufanya kwa akili yako hivyo usije rudia kunitisha tena namna hiyo kwa sababu naweza nikafanya leo leo ukaondoka kwenye hiyo nafasi yako”

“Are you stupid?”
“Nisikilize George wewe ni miongoni mwa watu wapuuzi tu kuwahi kutokea hapa duniani, wewe ni mtu mjinga kwa sababu ulishindwa kujiongeza kabisa na kupiga hesabu zako vyema. Mimi nimekuelekeza alipo mlinzi wako na wewe umekurupuka kwenda kule bila kuumiza kichwa ukafanya ule ushenzi wako. Umefanya mwanamke amebakwa mbele ya mume wake kisha ukamuua mumewe tena ukitishia mpaka maisha ya watoto wake, unajua upuuzi wako uko wapi?
Kushindwa kujua kwamba lile eneo lilikuwa na kamera kila kona hivyo kila ulilo lifanya mle ndani mimi ninalo kwa video. Hivyo naweza kuamua kuisambaza video hiyo nina imani hautamaliza hata nusu saa hapo Ikulu kwa sababu hata mimi mwenyewe kama mkuu wa majeshi nitalazimika kutumia nguvu kukutoa. Hilo nimezungumzia kwenye uvunjifu wa katiba ya nchi, sasa umepiga mahesabu itakuwaje kama hii video ikifika kwa wakubwa? Kaulimbiu ya mhimu ni kwamba hautakiwi kuua watu wako, wewe umemuua mlinzi wako tena kwa kumdhalilisha, unahisi watakuacha? Jibu baki nalo mwenyewe.
Upumbavu wako mwenyewe ni kwamba nilikuingiza mkenge nawe ukaingia kwenye suala la kumuua mkurugenzi wa shirika la kijasusi la taifa na mpaka sasa wananchi hata hawajui, unajua hizi habari zikisambaa utakuwa kwenye hali gani wewe? Haya yote nayaongea kwa sababu nina ushahidi wake hivyo angalia kauli ambazo unaniambia mimi, nimeishika hatima nzima ya maisha yako hivyo kwa sasa utafanya kile ambacho nakitaka mimi na hii itabaki kuwa siri ya watu wawili baina yangu mimi na wewe na kama ukienda kinyume basi nitaachia ushahidi wote halafu nione utaishia wapi na hizo harakati zako za kipuuzi”

Raisi alitulia, raisi alinywea, angeongea nini tena mbele ya mtu huyo? Angefanya nini raisi wa Tanzania? Alibanwa kila kona, mwanaume huyo alimtafutia sanduku kwa akili ya muda mrefu naye akajiingiza humo. Mpaka wakati huo alikuwa chini ya mikono ya mkuu wa majeshi. Alichoka mheshimiwa.

93 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA SABINI NA NNE
SONGA NAYO................

“Mheshimiwa!”
“Unaweza ukanipa sababu ya kwanini ulirudi pale wakati ulijua kabisa mimi na wewe tulitoka pale pale?”
“Kwa sababu nilitaka kuwa na uhakika zaidi juu ya jambo lile, pia nilijua kama mwanamke yule angehisiwa kuwa mhusika wa jambo lile basi huenda kuna watu wangekuwa na sababu kubwa ya kuweza kumvamia hivyo nilihitaji nipate majibu ya uhakika hivyo nilienda pale kwa ajili yako”
“Kwa ajili yangu?”
“Ndiyo”
“Kuna kazi ambazo huwa unazifanya kwa siri kwa ajili yangu mimi?”
“Hapana mheshimiwa, kwa wakati ule nilijua haupo sawa, ulitoka kumpoteza mkeo hivyo kama mkuu wa majeshi niliona kabisa kwamba kuna umuhimu wa kuwajibika kwa ajili ya raisi wangu”

“Okay, uliishia wapi baada hapo?”
“Nilichelewa kufika eneo la tukio kwa sababu ilikuwa imeshatokea tayari”
“Kwahiyo unataka upewe medali kwa hilo?”
“Hapana”
“Ila?”
“Nahitaji umjue muuaji wa mkeo”
“Nakusikiliza”
“Sarah Martin ndiye binti aliye husika kwenye mauaji ya mkeo mheshimiwa”
“Mhhhhh! una ushahidi upi juu ya hili?”
“Kwa sababu eneo la tukio lilikutwa ganda la risasi. Kuna kosa moja ambalo mhusika nadhani alilifanya kwenye kazi yake huenda kwa bahati mbaya ama kwa kuto kujua. Alishika risasi kwa mkono wake hivyo baada ya kupima finger prints na DNA zimekutwa zake moja kwa moja na taarifa za awali ni kwamba ile risasi ilikuwa inatumika kwenye silaha ya mdunguaji wa ngazi za juu na binti yule ni mmoja wao”
“Kumbukumbu zangu zinaniambia kwamba lile ganda lipo kwa mkemia mkuu na hakuna mtu mwingine ambaye nilitoa ruhusa ya kuweza kulipata, inamaanisha ulienda nyuma ya mgongo wangu na kufanya hili?”
“Nisamahe mheshimiwa ila ni sehemu ya jukumu langu”
“Mke wangu ni jukumu lako kwa namna ipi labda?”
“Kwa sababu wadunguaji wote ambao wamewahi kuwa na uwezo mkubwa hili taifa wanatokea jeshini, mimi ndiye mkuu wa majeshi na jambo hili nahesabia kwamba limetokea kwa uzembe wangu wa kushindwa kuwaweka vijana wangu kwenye mstari hivyo nilijiona kuwa mwenye hatia ndiyo maana nikaamua kulifuatilia mwenyewe hili suala”
“Una muda gani tangu ulifahamu hili?”
“Nilikuwa nina hisia tu na uvumi ila sikuwa na uhakika bado leo hii ndipo nimepata uhakika kwa asilimia zote”
“Huyu binti sina kumbukumbu sahihi kama namfahamu ila ni wewe ambaye uliniambia kwamba ndiye pekee ambaye alipona kule Kenya, au sio huyu?”
“Ni yeye mheshimiwa”
“Kwahiyo ni jambo gani linaendelea hapa?”
“Ndiyo maana imekuwa sahihi yeye kuhusika na mauaji haya kwa sababu kuna uhusiano wa haya matukio”
“Kivipi?”
“Huyu binti siku ile alidaiwa kwamba ndiye pekee alikutana na Gavin Luca na kuachwa hai. Swali la msingi ni kwamba kwanini iwe yeye pekee ndiye aweze kuishi kwenye hilo? Maana yake watu hawa huenda walikuwa wanafahamiana kabla ya siku hiyo. Wenzake wote waliuawa isipokuwa yeye, kulikuwa na kitu nyuma ya pazia ambacho alituficha yule binti”
“Enhe! nakusikiliza”
“Kwahiyo baada ya lile kuisha inaonekana kuna makubaliano waliyaingia na baadae ndipo alikuja kuyafanyia kazi”
“Makubaliano yapi hayo?”
“Ya kumuua mkeo”
“Huyu binti kuna sababu gani ambayo imefanya mpaka aweze kumuua mke wangu”
“Inasemekana kwamba hii amri imetoka kwa yule mama Aurelia, na imekuwa rahisi kwa sababu ndiye mama wa Gavin hivyo Sarah hakuwa na namna zaidi ya kukubali kuifanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa”
“Aurelia?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Kuna sababu gani mpaka yule mwanamke akubali kifanya hii kazi? Mimi kumhoji sikuwa na maana kwamba nina uhakika kahusika”
“Kwa habari chache nilizokuwa nazo ni kwamba wawili hawa waliwahi kuwa na ugomvi huko nyuma kwa sababu hawa wamezaliwa sehemu moja. Pole sana kama nitakuwa naongea jambo ambalo halipo kwenye matarajio yako kwa sasa ila nadhani unastahili kujua hili mheshimiwa”
“Nakusikiliza”
“Nmepitia historia yao hawa wawili inaonekana kabisa waliwahi kusoma shule moja, hawakuwahi kuwa vizuri tangu wakiwa wanasoma na baadae mkeo akaja kukutana na wewe wakati huo Aurelia aliingia jeshini ambako alifanikiwa mpaka kuwa kanali wa jeshi, ilikuwa ni moja ya hatua kubwa kwake.
Kumbuka kwamba hawakuwa sawa hivyo kila mmoja hakuwa anataka kuona mwenzake akifanikiwa kuliko yeye, wakatengeneza uhasama mkubwa baina yao. Jambo hilo likapelekea mkeo kuanza kumletea visa Aurelia ili afukuzwe jeshini ila alikuwa makini sana, hakuwahi kufanya kosa hata moja ila jambo hilo lilizidi kumletea kisasi kizito kweye moyo wake. Baadae sana nadhani ulizisikia zile taarifa za mwanamke huyu kuipoteza familia yake kabla hajaanza kusumbuliwa na lile tatizo la akili ambalo aliamua kutuigizia”
“Nakuelewa, endelea”
“Sasa kwenye lile tukio mtu ambaye yeye anaamini kwamba ndiye aliruhusu zile risasi kwenda kwa familia yake ambapo alimpoteza mumewe na mtoto ni mkeo. Kwahiyo alikuwa anatafuta sababu ya kulipa kwa namna yoyote ile kuhakikisha anamuua siku moja mpaka sasa ambapo aliona ni muda wake sahihi wa kufanya hivyo”
“Umesema mke wangu ndiye aliua familia yake?”
“Kwa jinsia ambavyo yeye anaamini, ndiyo”
“Ile kazi walitumwa vijana kuifanya, sasa mke wangu aliingia vipi hapa?”
“Huenda ni kweli endapo kama aliwazuia vijana kwenye hatua za mwisho na kufanya lile, kumbuka alikuwa anajua kila kitu mheshimiwa na alikuwa karibu yako na kwa wakati ule ulikuwa moja ya wanasiasa wenye nguvu kubwa nani angemzuia kama angetaka kulifanya hilo kwa amri yako?”
“Hizi habari wewe umezitolea wapi?”
“Kuna msamaria mmoja ambaye amenipatia taarifa hizi kwenye simu muda ule ambao nimekupigia simu kwamba nahitaji kuonana na wewe ndiyo maana nilivyo zipata tu nikaona kuna umuhimu wa kuonana na wewe ili ujue mheshimiwa”
“Msamaria huyo ni yupi?”
“Bado sijajua kwa sababu amegoma kutaja jina lake japo amedai kwamba kama mimi na wewe tunahitaji kupona kwenye hili hatuna budi kukubali masharti yake ili aweze kutusaidia”
“Kutusaidia mimi na wewe?”
“Ndiyo”
“Kwenye nini?”
“Anaamini kwamba huyu mtu ambaye sisi tunatafutana naye, hakuna namna tunaweza kuishi mbele yake”

74 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
Respect bro
 
Duuh mbn kama story ndo inachanganya zaid
Congratulations author [emoji120]
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA NNE
SONGA NAYO................

Bashir ni kweli alikuwa karibu na kwa mheshimiwa, nyumbani kwake kabisa Bunju na ndiko ambako walikuwa wamepanga kukutania, alikuwa amenyoosha barabara kuu lakini alichepuka kuanza kuifuata njia ambayo ilikuwa inaenda moja kwa moja kwa mkuu wa majeshi, alikuwa amebakiza mita elfu moja kuweza kufika nyumbani kwa mheshimiwa ndipo aligundua kwamba kuna mtu alisimama barabarani akiwa amempa mgongo.
Mtu huyo hakujali honi ya gari ambayo alikuwa anaipiga bwana huyo, huenda alimsikia ila akamdharau, hapendi dharau bwana huyo, kwanini adharauliwe kirahisi namna hiyo? Alighafilika Bashir kiasi kwamba alishuka ndani ya hiyo gari akiwa na hasira mno baada ya kubakisha hatua kadhaa ili aweze kumfikia mtu wake huyo.

Taratibu alianza kupunguza mwendo wake, ni baada ya viashiria kadhaa ambavyo vilimpa uhakika kwamba hakuwa salama ama mazingira yote kwa ujumla hayakuwa salama kabisa hilo eneo. Namna mtu huyo alivyokuwa amesimama hakuonekana kuwa mtu wa kawaida, hakuwa akiyumba wala kutikisika, alisimama kama mti ambao ulikuwa umekufa. Bashir aliangaza kila pembe lakini hakuona jambo lolote la maana wala dalili za uwepo wa watu wengine jambo ambalo kidogo lilimpa amani.
“Wewe ni nan….” ile kasi ambayo aligeuka nayo Gavin hata yeye hakutegemea, aliona kitu kinakuja upande wake jambo ambalo lilimfanya arudi nyuma kwa nguvu ili kujihami. Alifanikiwa kukipangua akagundua kwamba ni upanga ulikuwa unakuja kwenye kifundo maana yake mhusika hakuwa anahitaji kumuua haraka. Licha ya kufanikiwa kupangua lakini bastola haikuwa kwenye mkono wake, mkono ambao ulikuwa na bastola ndio ambao aliutumia kuweza kupangua upanga huo hivyo hata bastola yenyewe ilidondokea mbali.
Alimwangangalia mwanaume huyo lakini kwa bahati iliyokuwa mbaya hakufanikiwa kabisa kuweza kuiona sura yake, ilikuwa imefunikwa na kitambaa usoni. Spidi ambayo alikuwa anatembea nayo mwanaume huyo haikuwa ya kawaida wala hakuwa na uwezo wa kwenda nayo sawa, alirudi nyuma baada ya kuona bwana huyo anakuja kwa spidi ya kimbunga, ngumi zilikuwa zinakuja nzito mno upande wake.
Alikoswa na mguu ambao ulikita kwenye gari mpaka sehemu hiyo ikabonyea na kuweza kuharibika vibaya mno. Alirudi nyuma akiwa anaipimia bastola yake lakini ilikuwa mbali, alistaajabu aliyokuwa anayaona, hali iliyo mfanya kutamka kwa sauti kubwa
“GAVIN LucA” alikuwa sahihi kabisa, bwana huyo ndiye mwenyewe kabisa ambaye alikuwa hapo muda huo. Ni mtu ambaye walikuwa wakimtafuta sana ila siku hiyo tena akiwa mwenyewe alipata bahati ya kukutana naye ana kwa ana, alikuwa anazijua vizuri sifa za bwana huyo walikufa makomando kadhaa msituni tena kama watoto wadogo, hata yeye alikuwa na hayo mafunzo lakini hakuwa na imani kama atafanikiwa kupona, jambo la mhimu kwake ilikuwa ni kupata msaada ambao hakuujua unakuja muda gani.
Alikuwa akizielewa sheria za mapigano, ukikubali kushambuliwa basi mara zote lazima itakula kwako hivyo alitakiwa yeye ndiye ashambulie zaidi ya anavyo shambulia na hapo ndipo alifanya maamuzi ya kumfuta bwana huyo kwa spidi na nguvu zote. Alitoa visu kwenye buti zake, hakuwa anaviacha mahali hivyo vilikuwa ni mhimu kwake, alimkosa bwana huyo kwenye mguu wake wa kulia, aliinuka na kuzamisha kisu lakini hakikuingia, kilidakwa kabla hakijafika mbali kikaishia kwenye nguo.
Gavin alijizungusha kwa nguvu kubwa akiwa anarusha ngumi nzito ambapo nne zilitua kwenye taya ya Bashir, alitoa muungurumo akiwa anamwaga meno. Alirudi nyuma ila alihisi kama anaona kivuli, hakikuwa kivuli bali sarakasi za Gavin na zile nguo nyeusi ambapo aliishia kwenye kifua cha Bashir, alipigwa mateke matano akatua chini akiwa anavuja damu ambayo aliitema.
Akiwa pale chini alizunguka kwenda upande upande, alipishana na goti ambalo lilitua chini kiasi kwamba mpaka ardhi ilitikisika kabisa akawa anahema kwa nguvu akiwa mwingi wa wasiwasi. Aliinuka kuhitaji kuirukia bastola, alikutana na teke la uso ambalo liliirarua vibaya sura yake akarudi nyuma akiwa anagalagala huku uso wake ameufumba kwa sababu alikuwa anaona kiza mbele. Alijikaza kusimama ila aliinama tena, teke lilitua kwenye goti, mlio wa kuvunjika kwa goti ilikuwa ni kama kelele za mtu akiwa anavunja kuni.
Gavin aliiokota bastola ambayo ilikuwa imedondokea pembeni ambayo alikuwa nayo Bashir kwa mara ya kwanza. Alimsogelea bwana huyo taratibu na kumwangalia akiwa analalamika kwa maumivu ambayo alikuwa anayapitia. Kwa namna ambavyo alikuwa anajifanya hana hatia basi usinge amini kabisa kwamba ndiye yule ambaye alikuwa anaua wenzake kama kuku bila kujali hali ambayo walikuwa wanaipitia.
“Haukupaswa kuwa miongoni mwa hawa watu Bashir”
“Naiomba nafasi nyingine tafadhali mimi kuanzia sasa nitakuwa mtu mwema na nitafanya kila ambalo ni jema mbele ya jamii, nakuomba” Bashir siku hiyo alikuwa anaomba nafasi ya kuweza kuishi kwa mara nyingine, nafasi ambayo hata yeye hakuwahi kumpatia mtu yeyote yule, kifo kilimtia mbavuni bwana huyo akawa hana namna nyingine zaidi ya kufanya hivyo ili aweze kuishi kwa mara nyingine tena.

“Kuna kosa ambalo mpaka sasa najiuliza nilikosea wapi ila nahisi limekuja kuleta matatizo makubwa kwangu na kwa watu wangu wa karibu. Sina kumbukumbu kwamba ni nani ila nahisi miaka kadhaa ambayo imepita kuna mtu niliwahi kumsamehe hivi hivi kama unavyo omba wewe japo yeye aliomba kwa kumaanisha akiwa anatia sana huruma, nahisi kumpa nafasi nyingine ni moja kati ya makosa makubwa zaidi mimi kuwahi kuyafanya kwenye maisha yangu mpaka leo kwa sababu bila kufanya vile nahisi mpaka sasa kuna matatizo yasingetokea hivyo kukusamehe wewe ni sawa na kurudia ko……” Gavin kabla hajamalizia taarifa hiyo simu yake ilianza kuita mfukoni, aliitoa na kuipokea.
Haikuonekana kuwa simu nzuri kwa sababu ilimbadilisha, bila shaka alipokea tarifa mbaya wakati huo ndiyo maana sura yake ilikuwa tofauti ghafla. Simu hiyo ilibadilisha upepo wake na kumfanya aruhusu risasi zote ambazo zilikuwa kwenye bastola kwenda kwenye kichwa cha Bashir. Mwanaume huyo alikufa vibaya sana akiwa anaendelea kuomba msamaha ili aweze kuachwa.


Ulipita muda kidogo tu ndipo msafara wa mkuu wa majeshi ukawa unakuja kupitia eneo hilo. Msafara huo ulikuwa kwenye mwendo wa kawaida lakini wenye tahadhari kwa sababu mheshimiwa huyo alikuwa ameitangaza vita mpaka na raisi wa nchi hivyo alitakiwa kuwa makini kwa masaa yote ishirini na manne. Msafara huo uliweza kusimama hususani baada ya kugundua kwamba kwa mbele kulikuwa na gari ambayo ilisimama barabarani.
Alishuka akiwa na tahadhari kali, makomando wake walikuwa makini kuhakikisha kwamba mheshimiwa anakuwa salama muda wote. Gari ambayo aliiona mbele haikuwa mpya kwake, alikuwa akiijua vyema kabisa kwa sababu ilikuwa ni ya kijana wake Bashir hapo akahisi hali ya hatari mbele yake. Haikuwa kawaida kabisa kwa kijana wake kuweza kufanya makosa ya namna hiyo na hata siku moja asingeweza kufanya jambo la namna hiyo hivyo ikamlazimu kusogea zaidi ili aweze kuona kilichokuwa kimetokea ndipo akahamaki aliyokuwa anayaona. Kijana wake huyo alikuwa amekufa na sio kufa tu alikuwa amekufa kikatili isivyokuwa kawaida. Alionekana kabisa kwamba aliteseka kabla hajafa, mwanaume mmoja aliinama na kuugusa mwili wake;
“Bado ni wa moto sana, kwa maana hiyo huyu amekufa sio zaidi ya dakika kumi ambazo zimepita. Maana yake muuaji bado yupo karibu na eneo hili” walishtukia jambo hilo lakini walikuwa wamepoteza muda mwingi kufikiria, ni wakati ambao walihisi mmoja wao anashuka taratibu kuelekea chini.
Komando huyo alishuka taratibu baada ya upanga ambao ulikuwa na makali ya kutisha kutoboa vibaya shingo yake ukatokezea mpaka mbele. Alibaki amelishika koo lake wakati wenzake wanahamaki akiwemo mkuu wa majeshi kwani lilikuwa tukio la ghafla ambalo hawakujiandaa nalo kwa muda huo. Wakiwa wanaangaza huku na huko waliona kivuli juu, nguvu ambayo mtu aliyekuwa juu alikuwa anakuja nayo ilikuwa ni kubwa mno, mtu huyo alitua kwenye kifua cha mkuu wa majeshi ambaye alibebwa mpaka kwenye gari, alijibamiza vibaya mgongoni kiasi kwamba hakuwa na uwezo wa kusimama tena. Alibaki anahema kwa maumivu akiwa analalamika na kutukana ila muda haukuwa muda rafiki kwa ajili ya kufanya jambo hilo.
Gavin aligeuka kwa sarakasi zingine akiwa anamkimbia bwana ambaye alikuwa ametoa bastola na kuanza kupiga risasi ovyo.

94 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA TANO
SONGA NAYO................

“Don’t shoot, tutauana wenyewe hapa. Tunatakiwa kumkamata akiwa hai huyu, hatakiwi kufia kwenye mikono yenu nadhani unalijua hilo?” aliongea mwanaume mmoja kwa sauti kubwa, wakati wanafanya hayo makubaliano yao, Gavin alikuwa ametua karibu na yule komando mmoja ambaye alimuua mara ya kwanza kabisa akiwa anafika hilo eneo. Aliuvuta ule upanga wake ambao ulikuwa na mng’ao usiokuwa wa kawaida.
Akiwa anafanya hilo makomando wawili walitembea kwa nguvu kwa pamoja wakiwa wanabaraza ardhini, wote wawili walimjia kwa kasi ya ajabu, alizunguka mguu wake mmoja ukasimama kwenye gari kisha alijigeuza kwa nguvu akatua nyuma yao. Wakati anatua alikuwa amepita na sikio la mwanaume mmoja lakini mmoja alifanikiwa kumpiga na buti zito kwenye ubavu wake. Lilikuwa ni kosa la jinai analifanya, hiyo ndiyo ile sehemu ambayo alikatazwa kwamba hakutakiwa kuja kupigwa vibaya kwa sababu nguvu ambazo zilikuwa kwenye mwili wake zilihifadhiwa eneo hilo.
Mwanaume huyo alipiga makelele kama vile anataka kupata ukichaa, makelele hayo yaliambatana kwa ukaribu na yeye kupiga magoti huku akiwa anatoa machozi mpaka wote wakabaki wanamshangaa tu, ni kwa sababu hawakuwa wakijua lolote kuhusu nguvu hizo ambazo alikuwa nazo kwenye mwili wake. Haikuwa bahati kwao.
Gavina alipiga goti moja huku akiwa ameusimamia upanga ambao ulikuwa umechomekwa na kushikiliwa kwa mkono mmoja. Alipo yainua macho yake wote walirudi nyuma hata mboni zake zilibadilika kabisa. Hakuwa yule binadamu ambaye anakuwa na uelewa kwa asilimia zote, hapo hakuwa yeye tena bali ni kitu kingine kilikuwa kwenye mwili wake na ndicho kilikuwa kinamuendesha wakati huo.
“Kimbieeeeni?” ndiyo kauli ambayo aliiongea wakati ananyanyuka huku akiunguruma kama simba. Hakusimama kawaida bali aliuzungusha upanga wake na kudunda kidogo akajigeuza mithili ya mtu anayepaa, alikuwa na nguvu za ajabu mno. Aliuachia ule upanga kwa nguvu ambayo hakuna binadamu alikuwa anaweza kuihimili, kuna makomando wawili walikuwa wamepangana vibaya, upanga ule ulizama kwa mmoja ukatokezea kwa mingine ambapo yeye haukupitiliza bali ulitokezea tu nyuma. Walikuwa wanakufa wakiwa wanajiona, yule wa kwanza ambaye ule upanga ulitoboa na kupita kwenye tumbo lake alibaki amesimama yeye mwenyewe akiwa haelewi jambo ambalo lilikuwa linawatokea hapo hata angeulizwa hakuwa na majibu.
Aligeuka na kuanza kumwangalia mwenzake kwa masikitiko akiwa anahangaika ndipo na yeye alipo jishangaa alipo gundua kwamba alikuwa natokwa na damu kwenye mdomo wake. Alishuka taratibu kwa sababu utumbo ulikuwa umegawanywa, hakuna mahali angeenda, makomando watatu walikuwa wamekufa kama utani. Yule ambaye alikuwa anahangaika na ule upanga alihisi anaona kivuli tu ila alikuwa ni mtu, alikutana na kifuti cha kichwa, ngumi ambayo ilifuatia hapo iliifanya sehemu hiyo kupasuka kabisa ule upanga ukavutwa, hakustahili kuwa nao kwenye mwili wake.

Walibakia sita, waliamua kujipanga kwa tahadhari kwa sababu hawakuwa wakipambana na mwanadamu kwa wakati huo bali kiumbe. Mmoja alijazia kuliko wenzake wote, ndiye alitolewa sadaka akiwa anaikoki bastola yake, alirusha ngumi zikakutana katikati. Mifupa ilijitokeza nje baada ya ngumi hizo kukutana ile bastola ambayo alihitaji kuitumia ikatua kwenye mkono wa Gavin alimimina risasi zote kwenda kwenye moyo wa bwana huyo kisha akazungusha ule upanga wake ukakita kwenye kiganja cha mguu cha mmoja kiasi kwamba mguu ukachimbiwa chini na upanga huo.
Alitembea juu ya vichwa vyao wakiwa wanahangaika kurusha ngumi na mateke kwa ujumla. Risasi hazikufaa kwa sababu mtu huyo hakuwa akisimama eneo moja wangejikuta wanauana wenyewe. Aligeuka na koromeo la mmoja ambalo alilinyofoa na kumshindilia ngumi nyingi mno mpaka kifua kikavunjika vibaya. Alizunguka kwa spidi ya ajabu na kuuvuta ule upanga kwa nguvu akauzamisha kwenye moyo wa yule bwana ambaye alikuwa anahangaika kuweza kuutoa mguuni.

Alikuwa amefumba macho yake, kuna nguvu ambayo alionekana kuwa anashindana nayo kwa wakati huo na ilikuwa ni wazi kwamba ilikuwa inamuelemea. Walikuwa wamebaki makomando watatu tu kwa muda mfupi, mmoja wao alirusha risasi nyingi mno lakini ziliishia kwa mwenzao ambaye bwana huyo aliuzamisha upanga kwenye moyo wake, alimsukuma kwa nguvu akatua kwa wenzake wawili.
Mmoja alikuwa amebaki amesimama Gavin alimjia yeye, alitaka kuzipangua ngumi za mtu huyo alifanikiwa kuzuia lakini mkono wake haukuwa wake tena, akiwa anataka kujiogeza nyuma alipishana na Gavin, shingo yake haikuwa ikifaa tena, ilikuwa imegawanyishwa na kiwili wili hivyo kichwa kilidondokea upande wake na mwili ulidondokea upande wake. Mmoja ambaye alikuwa pale chini alianza kukimbia, asingeweza kuivumilia hiyo hali lakini hakufika hatua hata tano alisimama mwenyewe akaanza kutembea kwa kujivuta, yaani alikuwa anatamani kuweza kuendelea na safari yake lakini hakuweza.
Upanga ulitumwa kwa nyuma, ulizama kwenye shingo nyuma ukatokezea mbele, ulikuwa unamletea maumivu makali na wakati huo Gavin alikuwa amemfikia. Mmoja pekee aliyekuwa chini alikuwa ameivuta bastola yake na Gavin aliliona hilo hivyo wakati anauvuta upanga wake aliurudisha kwa yule bwana ambao ulitua kwenye kiuno kilicho mpatia maumivu makali mno. Mwanaume huyo alijipiga risasi mwenyewe Gavin akiwa anamjia kwa kasi huku akiwa ameushika mwili wa mwenzake kama ngao. Hakupenda kufanya hivyo bali ni hofu ambayo alikuwa nayo moyoni.

Mambo ambayo aliyaona bwana huyo anawafanyia wenzake, hakutamani kabisa yaweze kumkuta na yeye. Gavin alipiga goti akiwa amefumba macho yake, alitumia kama dakika mbili mpaka kurudi kwneye hali yake ya kawaida, alikuwa ametumia nguvu nyingi sana. Baada ya kuwa sawa alinyanyuka na kumsogelea mheshimiwa ambaye alikuwa anahema na kulia kama mtoto mdogo. Alikuwa amejibamiza vibaya kiasi kwamba kiuno hakikuwa sawa ndiyo maana alikuwa kwenye ile hali pale chini, hakuwa na uwezo wa kutembea zaidi ya kutambaa kwa wakati huo.
“Mke wangu na mama yangu wametekwa muda mfupi uliopita bila shaka mimi na wewe tutakuwa na mazungumzo marefu sana” aliongea akiwa anamgonga bwana huyo na kitako cha upanga akapoteza fahamu, alimbeba na kupotea naye hilo eneo ili wakaeleweshane wakiwa ndani ya eneo tulivu.



********
Kiyoyozi kilikuwa kinapiga vizuri, mwanga ulikuwa wa kutosha, mwanaume mmoja alikurupuka kutoka kwenye usingizi wa pono ambao alikuwa nao baada ya kumwagiwa maji ya baridi, maji yale yaliusisimua mno mwili wake kiasi kwamba hakuwa na uwezo wa kuendelea kulala tena.
Baridi lilikuwa ni kali mno kwenye mwili wake wakati huo alikuwa ameinama asijue alikuwa wapi, aliuinua uso wake na kuangalia mbele ili kuona kilichokuwepo, ndipo sura yake ikapiga kite, kwa sababu alimuona mtu ambaye hakutarajia kuweza kumuona kwenye hilo eneo. Mwanaume ambaye alikuwa amekumbata na hiyo dhahama alikuwa ni mkuu wa majeshi bwana Medrick Savato akiwa kwenye nguo ya ndani tu pekee. Hakuwa amevaa kitu kingine chochote, yaani nguo zote zilitolewa.
Alijaribu kutaka kujiinua pale ambapo alikuwa amekalishwa lakini aligundua kwamba hawezi kufanya jambo lolote ni kwa vile aliegeshwa kwenye kiti ndiyo maana kwa mara ya kwanza alijihisi kuwa na balansi ila ukweli ni kwamba hakuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote. Maumivu makali ambayo yalipiga kama shoti kwenye mwili wake ndiyo ambayo yalimkumbushia kile kilichokuwa kimemtokea kule, kiuno kiliteguliwa.
Alijikuta anatukana kimoyo moyo hasa baada ya kumuona Gavin mbele yake, mwanaume huyo moyo wake ulikuwa unaenda kwa nguvu na wasiwasi mwingi mno. Gavin alivuta kiti akiwa na bastola nne ambazo aliziweka kwenye bakuli moja yenye rangi ya dhahabu, aliketi mbele hatua moja kutoka alipokuwepo mkuu wa majeshi.
Aliikoki bunduki moja na kumpiga risasi kiongozi huyo wa jeshi kwenye goti bila kuongea jambo lolote lile. Alilia mno kwa sababu alikuwa anaongezewa maumivu juu ya maumivu, yale tu ambayo alikuwa nayo mwilini yalikuwa yanampeleka puta sasa kuongezewa risasi zingine mwilini lilikuwa tatizo lingine la kiufundi hilo.
“Kabla hujanieleza jambo lolote lile nataka unitajie kiongozi wako ni nani?”
“Simjui” baada ya kujibu hivyo ulisikika mlio mwingine a risasi eneo lile lile ambalo alikuwa amepigwa risasi mara ya kwanza
“Davoc Mavambo”
95 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA SITA
SONGA NAYO................

“Hilo jina ninalo ila sina taarifa zake kwa sababu inaonyesha kwamba duniani hakuna mtu wa namna hiyo”
“Ndiyo, ndiyo, ni mtu wa kujificha sana ndiyo maana hakuna sehemu kuna taarifa zake”
“Ni nani huyu mtu?”
“Yeye anadai kwamba wewe na yeye mnajuana kwenye maisha ya huko nyuma. Ana alama nyingi kwenye mwili wake na nyingi ni makovu ambayo anadai kwamba ni wewe ulimpatia. Anadai kwamba ulikuwa na nafasi ya kuweza kumuua lakini alikuomba msamaha uweze kumuacha na wewe ukakubali kufanya hivyo lakini ukampatia majeraha hayo. Anadai kwamba ameishi maisha yake yote akiwa anakutafuta wewe ili akuue, ana jina lako kabisa kwenye kifua chake”
“Umenipa kumbukumbu nzuri lakini hilo halijibu swali langu, huyo mtu ambaye unamsema wewe, nilikutana naye kipindi mzee wangu amekufa, mimi ninaye mtaka ni yule ambaye aliusuka huo mpango mapaka huyo kijana akaingizwa kwenye hilo kundi”
“Huyo hata mimi sijawahi kukutana naye hata siku moja, ni mtu ambaye anaishi nje ya mfumo wa ulimwengu kabisa hata kwenye vikao huwa tunaishia kuisikia sauti yake tu”
“Kama humjui maana yake unamjua ambae anamfahamu huyu”
“Sina uhakika ila huenda raisi anamjua”
“Kwanini ulijiingiza kwenye hii vita ambayo haikuwa ikikuhusu kabisa halafu ukajifanya kuwa mtu mwema sana, ukajifanya huelewi linalo endelea upo kwa ajili ya kulipambania taifa lako?”
“Nilifanya vile ili niweze kuishi”
“Kuishi kwa kuua watu wengine?”
“Sikuwa na chaguo kwa sababu wakati napewa nafasi hii sikuwa mtu ambaye najulikana, sikuwa lolote kwenye taifa hili na kama ningegoma kabisa basi mimi ningekufa kipindi kile”
“Unajua kazi yako imesababisha hatari kwa watu wangapi?”
“Sina idadi kamili”
“Nimempoteza kaka yangu, baba, yangu na mama yangu kwa sababu ya ujinga wenu wa kudandia vitu ambavyo haviwahusu. Hivi ninavyo ongea na wewe mke wangu na mama yangu wametekwa, unaweza ukanipa sababu ya msingi ya kwanini natakiwa kukupa nafasi nyingine ya kuishi?”
“Ndiyo sababu ipo”
“Nakusikiliza”
“Mimi nitakusaidia kuwateketeza hao watu”
“Una kipi?”
“Nina frash yenye ushahidi wote”
“wa nini?”
“Raisi na mambo ambayo anayafanya nyuma ya pazi hususani baada ya kumuua mlinzi wake na kijana wake kumbaka mke wa mlinzi huyo”
“Sivutiwi na habari kama hizo sidhani kama kuna jambo la maana kwenye hiyo taarifa yako”
“Hilo ni jambo kubwa kwa sababu lina ushahidi wote wa uchafu wa raisi ambao kama ukienda kwa watu utamuondoa Ikulu kwa dakika moja na ushahidi huo kwa sasa unaweza kuutumia kumfanya afanye jambo lolote lile ambalo wewe unalitaka”
“Endelea”
“Raisi nina uhakika anamjua huyu kiongozi hivyo kupitia yeye utampata kirahisi tu kwa sababu anaweza kuwasiliana nae. Ukiwa na huo ushahidi utamwambia raisi mkutane lakini aje na simu yake ya siri ambayo huwa anaitumia kuwasiliana na kiongozi wake huyo vinginavyo kesho utausambaza ushahidi huo. Hawezi kuruka kwenye hilo jambo kwa sababu namjua vizuri namna alivyo ni mtu ambaye ni muoga sana nje ya kamera, lakini pia kwenye hiyo frash kuna ushahidi wote juu ya hao watu, kuna kila kitu ambacho uwezo wangu uliishia kukipata hivyo nafasi ambayo inapelea ni ya kiongozi mkuu ambaye simfahamu basi”

“Inaonekana wewe ni msaliti kwa wenzako sasa kwanini nikuamini kirahisi namna hii?”
“Kwa sababu mimi nafanya haya mambo ili niishi hivyo hata hapa nataka kuishi lakini watu hawa nilianza kuukusanya ushahidi kuhusu wao hasa baada ya kugundua kwamba ni kama walianza kunitupa taratibu, hakuna aliye nitamkia kwa mdomo ila niliwaona kama wanaandaa mazingira ya kunipoteza hivyo nikaanza kujihami mapema kwamba kama kuna siku wangekuja na kutaka kuniua ama kubeba kila kitu kwangu basi ningeutumia ushahidi huo kwa ajili ya kuwaangusha ama kuwatisha”
“Kuna lingine ambalo unalifahamu?”
“Mengi yapo kwenye hiyo frash”
“Mavambo anaishi wapi?”
“Mlandizi”
“Ndio nyumbani kwake?”
“Ana eneo kubwa amelinunua huko wengi wanajua kwamba ni mtu ambaye anafuga samaki na biashara hiyo huwa inafanyika sana lakini ndani yake kuna biashara ya madawa ya kulevya na viungo vya wanadamu. Chini ya hilo eneo ndiko yaliko makazi ya mtu huyo.
“Bila shaka ndiye amewabeba mama na mke wangu si ndiyo?”
“Lazima ni yeye kwa sababu ana kisasi kizito kwako”
“Hilo ni jambo zuri lakini nina swali lingine la msingi hapa ambalo unatakiwa unyooshe maelezo kwa sababu ukishindwa kunipa taarifa sahihi, nina uhakika unajua jambo ambalo linaenda kukutokea bwana mkubwa”
“Ndiyo ndiyo”
“Unafahamiana vipi na mama?”
“Samahani umesema?” ile anauliza alilimwa risasi mbili kwenye paja lake akaanza kulia mkuu wa majeshi, ilikuwa ni rahisi sana kutoa amri kwa wenzake lakini kwake kupokea amri ikawa mtihani, hakuna mtu ambaye alikuwa anamchekea hapo.

“Mimi na mama yako tumejuana jeshini kabla hata hajawa kanali, mimi na yeye tulikuwa watu wa karibu sana kiasi kwamba zilizaliwa zile hisia za kweli kabisa za mapenzi baina yetu. Hisia zile zilizalisha penzi la kweli ambalo tuliamini tungefika nalo mbali lakini yeye alionekana kuwa na mipango tofauti kidogo.
Ukweli ni kwamba ni yeye ambaye nyota yake ilianza kung’aa hata kabla yangu jambo hilo lilimfanya yeye kupanda vyeo kila leo. Ukuaji wa kwenye kazi yake aliona kabisa kama mimi sikuwa sawa naye kama ilivyo kawaida kwa maskini akipata, anaweza hata kuwasahau wale ambao alikuwa anatafuta nao na ndilo jambo ambalo lilitokea kwake pia.
Jambo lile mimi liliniumiza sana tena sana kwa sababu nilikuwa nimempenda mno na aliniaminisha kwamba angekuwa nami maisha yake yote. Kuniacha ingali bado nikiwa namhitaji, kulizalisha wivu ambao baadae haukuishia hapo tu bali ikawa chuki, hakuonekana kujali kabisa kama aliwahi kuwa na mtu kama mimi.
Aliishi maisha yake na mara moja moja nilipokuwa namuona akiwa na furaha, mimi nilikuwa naumia sana, nilikuwa natamani kumuona mwanamke huyo akiwa anateseka siku zote, nilitamani mabaya yaweze kumfika asifurahi abadani lakini maombi yangu hayakuwahi kutimia nikaishia kuumia zaidi baada ya yeye kupata mwanaume ambaye ndiye alikuja kumuoa, moja ya wafanya biashara wakubwa ambao walikuwa na ukaribu na baba yako mzazi enzi za uhai wao.
Jambo lile lilinifanya niwe na hasira zaidi, niliamua kupambana na kujikutanisha na watu wengi ili niweze kufika hatua kubwa kimaisha aje kujua kwamba alifanya kosa kubwa kuweza kumuacha mtu kama mimi. Nilikuwa namfuatilia kila nilipopata muda mpaka wakati anakuja kupata familia nilikuwa namfuatilia kiundani, ukweli ni kwamba sikuwahi kuipenda furaha yake, nilitamani apate donda la maisha ambalo litamfanya kila siku aweze kujutia mpaka ile siku anaenda kaburini baada ya kufa.
96 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA SABA
SONGA NAYO................

Maisha yalienda hivyo mpaka ilipo tokea ile nafasi, ukweli ni kwamba sikuwahi kufikiria kumuua, lengo langu nilitaka apitie kipindi kigumu kwenye maisha yake mpaka ajute yaani. Hivyo ilipotokea ile fursa ya kuweza kuteketeza familia ya baba yako mimi nilishiriki kikamilifu ila sikuwa na shida kabisa na baba yako mzazi, sababu kubwa ilikuwa ni yule mwanamke ukiacha sababu ya kutaka kuwaaminisha mabosi zangu kwamba nipo pamoja nao siku zote.
Hivyo mimi ndiye ambaye nilitoa taarifa za mahali ambapo ilikuwepo familia yake Valeria akahusika kwa sehemu kubwa kuwaua kwa sababu ya visasi vyao vya kutopendana tangu wakiwa wanasoma shuleni huko ambako walisoma pamoja. Mimi binafsi sikuwahi kujua kama Valeria alikuwa sehemu ya ule mpango ila nimekuja kujua hilo baadae sana”
“Hiyo ndiyo sababu alikutaka wewe umuue mke wa raisi?”
“Ndiyo”
“Ilikuwaje watu ambao unadai hamkuwa mkielewana akakupa kazi ya hatari kama hiyo na wewe ukakubali kuifanya?”
“Kwa sababu baadae alikuja kugundua kwamba nilihusika kwenye lile suala, alikuja kuniambia kabisa hadharani ila akadai kwamba angekuja kunitafuta ili nimfanyie kazi yake na huenda angenisamehe juu ya hilo. Alinihakikishia kwamba asingekwambia kwa ajili ya usalama wangu, wakati ananipa kazi ya kumuua mke wa raisi alinipa onyo kwamba kama ningegoma basi taarifa zingekufikia”
“Kama ni hivyo, kwanini ulimtumia Sarah, binti ambaye hakuwa na hatia yoyote ile?”
“Kwa sababu yeye ndiye pekee ambaye ulimuacha kule msituni, mimi nilielewa kwamba haikuwa bure, lazima kungekuwa na sababu ya msingi ya wewe kufanya hivyo kwa hiyo nikaona kama yule binti ni hatari hususani baada ya kuhisi kwamba kuna taarifa ambazo alikuwa ananificha hivyo mpango ukawa ni kumuua
Nikiwa napanga kufanya hilo ndipo mama yako alipo nifuata, kunifauata kwake ulikuwa ni muda mwafaka kwahiyo badala ya kuweza kumuua binti huyo bila faida yoyote ile nikaona ndiyo sehemu sahihi ya kufanyia tukio hilo la kumuua mke wa raisi.
Kama ningefanya mwenyewe bila kuwa na sababu kungekuwa na ugumu sana hususani wakati wa uchunguzi lakini nilijua kabisa kwamba kama nikimtumia binti huyo kukamilisha hilo zoezi basi kwangu itakuwa rahisi kwani atamaliza kazi kisha nitamuua na kumpatia hiyo kesi. Kesi isingekuwa ndefu kwa sababu wangejua mhusika amekufa”
“Unajiskiaje kumsingizia binti wa watu ambaye alikuamini kesi kama hiyo?”
“Hakuna kitu naweza kukibadilisha kwahiyo binafsi naona sawa tu”
“Frash iko wapi?”
“Kwenye mfuko wa koti langu”
“Simu yako”
“Nina uhakika mpaka umenivua nguo basi unayo”
“Namaanisha ya siri”
“Ile ambayo nilikuwa nayo muda ule ina kila kitu”
“Nahitaji unaindikie address ya mahali ambako anapatikana Mavambo” aliongea huku akimpa karatasi mtu huyo ambaye aliiandika kwa shida mno akiwa anatetemeka.
“Mimi sina shida na wewe kwa sasa ila kuna mtu ambaye yeye ndiye ataamua kama aweze kukua ama kukupa hiyo nafasi ya pili ambayo unaitaka. Kumbuka tu kwamba kwenye kifua changu niliweka kamera hivyo kila ulilo liongea hapa limerekodiwa” Gavin alianza kutoka humo ndani lakini kabla hajatoka kabisa kuna mtu mwingine aliingia.

Alikuwa ni Sarah Martin, mkuu wa majeshi hakuweza kabisa kuamini kama angemuona mwanamke huyo hilo eneo. Ni huyo ambaye aliiteka familia yake akatishia kuiua lakini akapewa nafasi ya kumuua mke wa raisi ili familia iwe salama, akafanya hivyo. Ni huyo ambaye yeye alimtangaza hadharani kwamba ndiye muuaji wa mke wa raisi na wanajeshi wenzake, ndiye huyo ambaye yeye alitaka kumuua ila wakati huo alikuwa anategemea kumuomba mwanamke huyo nafasi ya pili ya kuishi. Zilisikika risasi tu kwa muda mrefu mpaka zilipokata Sarah alitoka akiwa amechakaa damu iliyo mrukia, mkuu wa majeshi alikuwa amewahi mahali ambako alitakiwa kuwepo. Aliuwa amekufa tayari kiongozi huyo mkubwa kabisa wa jeshi.


*********
Ilikuwa inasoma saa tisa na nusu usiku, ndio muda ambao mheshimiwa raisi wa Tanzania alipokea simu kkwenye namba yake binafsi. Simu hiyo ilikuwa ya mashaka usiku huo ukizingatia mapema ya siku hiyo wawili hao walikuwa wametoka kuongea na mazungumzo yao hayakuweza kuishia sehemu nzuri hivyo alikuwa na mashaka nayo lakini kwa usiku kama huo aliamini ni lazima kulikuwa na dharura ambayo hakutakiwa kuipuuzia hivyo akaamua kuipokea.
“Sidhani kama haya ni makubaliano yetu mimi na wewe kuweza kusumbuana muda kama huu” raisi alifoka kwa sauti ya juu ambayo ilionyesha kutopendezwa na hali ile kabisa.
“Habari yako mheshimiwa raisi!” sauti ambayo aliisikia ilimshtua, hakuwa na matarajio nayo, haikuwa ile ambayo ailiikusudia kuweza kuisikia.
“Ni nani ambaye unaongea?”
“Gavin Luca” alicho kisikia kilimfanya aidondoshe simu na kuketi chini, aliiokota akiwa mwingi wa wasiwasi jasho likiwa limavuja kila sehemu. Hakuwa na matarajio wala hakuelewa bwana huyo aliipataje simu ya mkuu wa majeshi.
“Hii haiwezi kuwa kweli, hii simu ni ya Medrick Savato ambaye leo hii nimeongea naye, kama wewe ndiye imefikaje kwako?”
“Kwa sababu tayari amekufa”
“Whaaaat! Umemuua mkuu wa majeshi?”
“Sijali kuhusu hilo, nina taarifa zako zote na ushahidi wako wote ambao kama nikiuweka hadharani basi historia yako yote itapotea hapa duniani, utakuwa mtu ambaye jina lako na familia yako itakuja kuchukiwa mpaka dunia inafika mwisho. Unajua kabisa mkuu wa majeshi alikuwa na video zako za hovyo juu ya ushenzi wote ambao umekuwa ukiufanya kwa muda mrefu, nina imani hata wewe hautaki kabisa hizi video ziufikie ulimwengu hivyo nahitaji unisikilize kwa umakini sana George” raisi huyo alionekana akimeza mate kwa taabu akiwa anamsikiliza mtu wake.
“Nakusikiliza”
“Nina mazungumzo binafsi na wewe kwa sababu kuna taarifa ambazo nazihitaji kwako hivyo nataka nikutane mimi na wewe tukiwa wawili tu. Yaani usije na mtu mwingine yeyote, kama utavunja haya makubaliano basi mpaka asubuhi utajikuta maarufu kila kona ya ulimwengu huu kisha wananchi waje wakutoe hapo Ikulu kwa lazima uharibu jina zima la familia yako ambalo umelitengeneza kwa miaka mingi iliyo pita. Lakini nahitaji uje na simu ambayo huwa unaitumia kufanyia mazungumzo na bosi wako”

“Haiwezi kuwa hivyo, unajua kabisa itifaki haiwezi kuruhusu jambo kama hilo kufanyika. Uliwahi kusikia wapi raisi anatoka pekeyake? Lazima kutakuwa na namna nyingine, nipo tayari kukusikiliza ili usiachie hizo video lakini sio kwa kukutana kama ambavyo unataka wewe”
“Nina uwezo wa kukuua popote ulipo, shida yangu nataka tufikie makubalino kisha maamuzi ya mwisho utayafanya mwenyewe na binafsi sitaki kukuua kwa mkono wangu”
“Nitaaminije kuhusu usalama wangu?”
“Sio kama nakuomba George, nakupa dakika tano fanya maamuzi tukutane muda huu au uwe maarufu baada ya hapo” simu ilikatwa, raisi alibaki anahaha akiwa haelewi afanye nini na hatima yake ingekuaje huko mbele. Siku zote ubaya huwa ni mzuri unapokuwa unaufanya lakini matokeo yake huwa ni mabaya sana.
Muda ambao alikuwa amepewa kwa ajili ya kufanya maamuzi hakuona kama unatosha, ulikuwa ni mdogo mno kwani dakika zilikuwa inakimbia kama sekunde moja. Mwili ulikuwa umeloa kwa jasho, yaani ajipeleke kwa Gavin kirahisi hivi tena mwenyewe? Jambo hilo aliona kabisa haliwezekani! Lakini je, alikuwa na chaguo lingine? Hapana, hakuwa nalo. Sasa alipaswa kufanya nini? Alichanganyikiwa lakini ulikuwa ni wakati wa kuweza kufanya maamuzi.
97 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

********************
SEHEMU YA TISINI NA NANE
SONGA NAYO................

Dakika zilikuwa zimeisha akiwa anazunguka kila sehemu, aliibeba simu na kupiga;
“Naomba usiziachie hizo video tafadhali, nakuja lakini naomba unihakikishie usalama wangu nikifika huko” hakupewa jibu, simu ilikatwa na haukupita muda akatumiwa location ya mahali ambako walitakiwa kufanyia mkutano wao huo.

Ulikuwa usiku sana, mheshimiwa aliwataarifu walinzi wake kwamba anatakiwa kutoka wakati huo, walinzi walimgomea mheshimiwa kwa sababu itifaki za kazi yao zilikuwa zinakinzana na jambo hilo lakini yeye ndiye alikuwa bosi mwenyewe hivyo alitoa kama amri sio kama ombi. Hawakuwa na namna yeye ndiye ambaye alikuwa akiwalipa na kuwapa huo ujiko hivyo walipaswa kumtii. Alihitaji kuondoka na gari moja tu Ikulu tena kwa siri kubwa akiwa na walinzi wake wawili pekee.
Alikuwa anaikata mitaa ya jiji la Dar es salaam akiwa anawaangalia wapambanaji ambao walikuwa wamewahi wakati huo kusaka Jala lakini yeye akili yake haikuwa huko kabisa. Alikuwa anauwazia muda, muda haukuwa rafiki kwake kwa sababu dakika kadhaa mbele angekutana na binadamu ambaye hakuwa akieleweka kama ni mzimu ama ni mtu ambaye yu hai. Moyo ulikuwa unamuenda mbio isivyokuwa kawaida mheshimiwa raisi.

Safari yake iliishia mpaka ilipo karakana ya TAZARA, aliingia eneo hilo ambalo lilionekana kutokuwa na ulinzi majira hayo, alielewa Gavin alikuwepo hapo na huenda alikuwa amewaua walinzi wote wa eneo hilo. Alimeza mate kwa taabu akiwa anailegeza tai yake mheshimiwa, mpaka muda huo walinzi wake hawakuwa wamemuelewa kabisa mheshimiwa, walikuwa makini mno kwa sababu ilikuwa ni hatari kubwa raisi kutembea usiku kama huo halafu akiwa hana ulinzi wa kutosha namna hiyo.
Aliangalia kwenye simu yake sehemu ambayo ilikuwa inamuelekeza aweze kwenda, ilikuwa ni kwenye behewa la treni moja ambalo lilionekana kutokamilika kutengenezwa kwake. Aliwataka walinzi wake wamsubiri hapo, walipigwa na butwaa kwani ni kama raisi alikuwa amechanganyikiwa, vipi kama angepata tatizo si na wao wangeuliwa? Walimpinga ila hawakuwa na nguvu hiyo wakabaki wakiwa na mashaka wamesimama kwenye gari huku akiwataka wasimsumbue mpaka pale atakaporudi mwenyewe.

Alirusha hatua zake kuelekea eneo lile akiwa na mawazo mengi sana kwenye kichwa chake, alifika mpaka nje ya lile behewa akasimama. Aliwaza mambo mengi mno, aliwaza vitu vingi na madhambi ambayo alikuwa ameyafanya kwenye maisha yake. Mpaka anaenda eneo hilo alikuwa anajua kabisa kwamba nafasi ya yeye kuweza kuishi ilikuwa ni ndogo hivyo alijiandaa kwa lolote lakini hakuwa tayari kuona zile video zinaachiwa, ilikuwa ni heri afe yeye sio kuharibu jina la kizazi chote kwa makosa yake binafsi, asingeruhusu hilo lifanyike kwa sababu alielewa ilivyokuwa kazi ngumu kuweza kutengeneza jina. Hatimaye aliingia ndani ya behewa hilo.
Aliangaza kila upande ila hapakuwa na mtu, alisogea kwenye siti moja ambayo ilikuwa na simu juu yake na aligundua kabisa kwamba ndiyo simu ambayo alikuwa anawasiliana nayo. Aliangaza kila kona ndipo akashtuliwa na sauti ya mtu kwa nyuma.
“Za siku nyingi mheshimiwa?” almanusura aweze kudondokea kichwa kwa namna alivyo shtuka. Gavin alikuwa anaonekana kawaida kwenye simulizi ila hakuna mtu alikuwa anatamani kukutana naye ana kwa ana tena akiwa mwenyewe, lilikuwa jambo la hatari ambalo halikuwa rafiki kwa mtu yeyote. Ni Gavin ambaye alimshtua mzee huyo na bila shaka alitokea kwenye behewa lingine huku akimtaka mzee huyo aketi waweze kuzungumza kwa mapana. Aliiweka bastola juu ya meza katikati ya sehemu ambayo walikaa, raisi alikuwa anaitazama kwa mashaka mno huku akiwa anatetemeka.
“Nina imani ulikuwa unatamani kukutana na mimi siku moja mheshimiwa hivyo nina uhakika kabisa kwamba ndoto yako itakuwa imetimia”
“Sio kukutana kwa namna kama hii”
“Nalielewa hilo lakini sipo hapa kuanza kukuhubiria propaganda ambazo nyie huwa mnazisambaza huko kwenye mitandao”
“Unataka nini Gavin!”
“Nahitaji jina la bosi wako”
“Ni jambo ambalo haliwezekani”
“Hiyo ina maana kwamba unamjua”
“Hata kama namjua nisingeweza kukutajia kwamba ni nani”
“Ni jambo zuri kutamka hivyo lakini unajua kabisa kwamba upo kwenye mazingira ambayo hauna namna ya kufanya”
“Nikimtaja lazima ataua kila mtu ambaye anahusika na mimi hivyo siwezi”
“Mhhhhhhhhh unajua kabisa kwangu ni sehemu mbaya zaidi ya huyo bosi wako, bila shaka mimi na wewe tuna historia ndefu kwa sababu wewe hapo ulishiriki kuipoteza familia yangu hivyo usitake kunilazimisha niifanyie familia yako jambo ambalo sikuwa nimelipanga nadhani unajua yaliyo wakuta wenzako ambao walikuwa wabishi kama wewe”
“Kama nikikutajia unanihakikishia usalama wangu?”
“Ukinipa maelezo ambayo nayataka mimi binafsi sitakuua ila sina uhakika pia kama utabaki hai kwahiyo siwezi kukuahidi kwa hilo”
“Jina lake halisi anaitwa Rabinus Mtatiro, mkurya wa kwanza kuliongoza hili taifa lakini jina lake ambalo amejipatia kwa maisha ya sasa ni Natron Vinza”
“Subiri kwanza, unamaanisha yule raisi ambaye aliziuzulu miaka hiyo?”
“Ndiyo”
“Historia imeandika kwamba alikufa kwa kujiua baada ya mzee wangu kumtaka aondoke Ikulu ili alisaidie taifa. Kwa kuogopa aibu na sononeko aliamua kuyabeba maisha yake mwenyewe”
“Hilo ndilo jambo ambalo yeye aliutaka ulimwengu uamini kwamba ipo hivyo”
“Kwahiyo yule ndiye alikuwa nyuma ya mambo yote haya?”
“Ndiyo, ule udhalilishaji ambao alifanyiwa na baba yako ulimtengenezea kisasi kibaya kwenye moyo wake. Huenda alikosea kuhitaji mali za baba yako kwa nguvu lakini kama raisi aliona kabisa hakutakiwa kufanyiwa vile hivyo kwake aliona kama ni kudhalilishwa ndiyo maana akaamua kuigiza kama amekufa kwa sababu alijua kabisa kwamba kushindana na mtu ambaye humjui ni jambo gumu kwani unakuwa hujui anashambulia kutoka wapi na kupitia hilo alijua angetekeleza mambo yake bila baba yako kujua

Alihitaji kumuua kila mtu ambaye alikuwa kwenye familia yenu kisha ajimilikishie mali zote. Bwana huyu hakuwahi kujulikana hata kwetu sisi, ni mtu ambaye alikuwa anaishi gizani muda wote ila ndiye ambaye ametutengeneza sisi wote tunafanya kazi chini yake.
Lilikuwa ni zoezi la miaka mingi hata mimi hapa nimefanikiwa kukutana naye saivi, sikuwa namjua kabla. Akiwa anaishi gizani alihakikisha anatawala kila kona, alihakikisha anakuwa na watu kila sehemu, alitengeneza watu wenye nguvu na hata yeye mwenyewe anadaiwa kuwa na nguvu za ajabu, lengo tu lilikuwa ni kutobakiza mtu hata mmoja kwenye familia yenu. Baadae baada ya kuanza kutekeleza jambo hili hakuwahi kujua kama nyie mpo wawili hivyo alimuua mwenzako akiwa na uhakika kama amemaliza kazi ndipo akaamua kurudi nyuma kuandaa mpango mpya ambapo kwa mahesabu ya haraka haraka kuna sehemu ambapo kete moja ilikuwa inapelea”
“Wapi?”
“Baada ya kuteketeza familia nzima alisahau jambo moja, alijua itakuwa rahisi ila baadae ilimuwia ugumu. Alihitaji kumiliki mali zote za baba yako ziwe zake na baada ya hapo angejitokeza hadharani kuuambia ulimwengu kwamba yeye alikuwa hai. Kwa nguvu ambazo alikuwa nazo, watu ambao alikuwa nao alijua akizipata pesa za baba yako hakuna binadamu ambaye angethubutu kufanya jambo lolote lile mbele yake.
Zoezi hilo lilikuja kuwa gumu kwake nje na matarajio aliyokuwa amejiwekea na hapo ndipo akaanza kufanya utafiti wa ndani. Yule mwanamke kanali wa jeshi kwa taarifa yake ni kwamba hakumuacha hai kwa bahati mbaya ndiyo maana alizuia mtu yeyote asije akamgusa kwa sababu yule ndiye alikuwa anamtumia kufanyia uchunguzi ili ajue pesa zipo kwenye mkono wa nani wakati huo wewe mwenyewe ulikuwa unamtumia yule mama ili kuweza kumjua mhusika wa mauaji ya familia yako hivyo kiufupi mlikuwa mnaviziana mpaka ambapo jina lako lilianza kurudi tena kwenye masikio yetu.
98 inafika mwisho.

FEBIANI BABUYA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom