Mnachihanguuu
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 6,111
- 9,360
Shusha vitu mkuu
PamojaKaribu.
Nicheki kwa ile namba utanipata.
Shukrani sana mwandishi [emoji1363][emoji1363]STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA THEMANINI NA TATU
SONGA NAYO................
Baada ya kumkuta kwenye hali ile iliniuma sana, nilimpatia kila kitu kwenye maisha yake, nilimpatia mali nyingi sana ambazo zote ziliandikwa kwa jina la binti yake. Nilimtaka ataje vitu vyote ambavyo alikuwa anatamani kuvifanya kwenye maisha yake na mimi ningevifanya kwa naiba yake. Yule ndiye mtu wa kwanza kwenye maisha yangu mimi kumuamini na kumpatia siri zangu zote, yule alikuwa anajua kila kitu kuhusu mimi, hakuna taarifa yangu hata moja ambayo hakuwa nayo ila alikuwa na ombi moja kwangu baada ya kugundua ile mipango yangu ambayo ilikuwa mezani.
Haizulu hakutaka kufa bila kuwa msaada kwangu, aliomba angalau angepumzika kwa amani kama angekufa akiwa anarudisha asante kwangu ndipo yeye akaja na lile wazo la mimi kwenda huko Kenya ndani ya ule msitu wa Mau. Sasa kwanini nilitakiwa kwenda mimi lakini ambaye amekufa kule ni yeye? Kipindi kile kuna baadhi ya watu walianza kusambaza taarifa maeneo mbali mbali wakieleza kwamba sisi tulizaliwa wawili hivyo aliyekufa hakuwa mimi, habari hizo wengi walizupuuzia lakini zilikuwa za kweli na mpango wake ndio ambao umenifanya nikapiga hatua kubwa sana.
Kuna watu ambao mimi nawatafuta lakini kwa miaka yangu yote ambayo niliwatafuta sikuwahi kuwapata mpaka nilipo ikamilisha ile adhma yake ya yeye kujiua kwa ajili yangu, sasa ilikuaje? Mpango ulikuwa ni kwamba tuvujishe siri kwa baadhi ya watu kwamba mimi Gavin Luca nipo hai, tulijua kabisa kwamba zile habari zingewagawa kwenye makundi mawili, kundi moja lingekuwa ni lile kundi ambalo lingeamini moja kwa moja lakini kundi la pili ni lile kundi ambalo lisingeamini kuhusu taarifa hizo, sasa hesabu zetu zilikuwa kwenye hilo kundi ambalo lingeamini habari hizo na kama lisingeamini basi tulihitaji tu wachukue tahadhari maana yake wasingeacha jambo hilo lipite na bila shaka nyie kama jeshi mliingia kwenye kundi ambalo sisi tulikuwa tumelilenga.
Tulielewa kabisa kwamba kama kundi hilo moja lingeamini basi mara moja ungeanza msako ili kuhakikisha hakuna makosa yanafanyika huku nikiwa naonekana mara moja moja baadhi ya maeneo ili kuwahakikishia kwamba BADO NINAISHI mkaingia kwenye huo mtego. Lengo lilikuwa kwamba wakati ambao mngekuwa mnanitafuta mimi mngeanza kujiaminisha kwamba mimi nipo hai hivyo mngepambana muweze kunipata lakini baada ya kunipata ni lazima watu kadhaa watake kuniua ili kumaliza utata huo hivyo baada ya mimi kufa mngehisi yale yote yameisha tayari. Mimi nilinufauika vipi na hilo?
Siku zote adui yako akishajua amekumaliza huwa anaanza kutamba, atataka mitaa iitambue furaha yake kwa sababu ile hatari yake haipo tena na hapo niliamini kwamba lazima kuna makosa wangeyafanya ningeanza kuwapata watu wangu ambao walijificha kwa miaka yote ambayo niliwasaka bila mafanikio yoyote yale. Nilikuwa na uhakika taarifa za kifo changu zingewaibua wengi kwenye maficho na hao wangenisaidia mimi kufika na kumpata yule ambaye najua ndiye alikaa chini akauandaa huu mchezo mzima.
Na ndio ule wakati ambao kijana Michael alikabidhiwa kile kikosi wewe mwenyewe ukiwemo kuanza kunitafuta mpaka mlipo fanikiwa kumpata Haizulu mkidhani ni mimi. Wakati tumeuandaa ule mchezo ilinilazimu nimfue kwanza ili asiwe lege lege, angekuwa legelege lazima mngeshtuka kirahisi ndiyo maana hata siku mnampata mliwapoteza watu wenu kadhaa, hakuwa mtu dhaifu kwa sababu nilimtengeneza kwa mikono yangu mwenyewe. Baada ya kukamilika kwake ndipo tukamfanyia oparesheni ya kumbambikia sura yangu, tulihakikisha kunakuwa na mfanano mkubwa kwenye kila kitu ili asije kushtuka mtu yeyote yule. Huo ndio ulikuwa mpango wake yeye kutoa asante kwangu kwa sababu alijua amebakisha miaka michache ya kuishi hivyo aliitafuta furaha ya kufa nayo na hilo kwake akaona kabisa kwamba linamfaa.
Hilo ni jambo ambalo binafsi nililipinga sana ila alisisitiza kufanya hivyo, kwake aliona kama ni neema na bahati ya pekee kufanya na kulitimiza hilo kwa sababu hisia za moyo wake zilikuwa zinamtuma kufanya kitu kama hicho. Nadhani kwa sasa utakuwa umepata jibu kuhusu mkanganyiko wako wa kujua kwamba mlimuua nani badala yangu mimi”
Mwanaume aliidadavua historia na fumbo zito ambalo lilikuwa linawaumiza watu kwamba ni kwanini mtu huyo walimuua halafu bado akaonekana akiwa hai tena, kiukweli hakuna mtu ambaye alikuwa anaamini kwamba ni sayansi watu walihisi ni mzimu wake labda lakini hapo alifunguka akili na kuelewa mchezo mzima ulisukwa vipi na watu hao wenye akili zao ambao waliuandaa nao ukakubali kama walivyokuwa wameutaka uwe.
“Hii ndiyo stori ya kutisha zaidi kuwahi kuisikia kwenye maisha yangu, moyoni nazidi kujawa na hofu, mlifanya jambo la hatari sana kwa mwanadamu wa kawaida hakuna ambaye anaweza kuja na mpango kama huo”
“Mhhhh bibie kwenye kuzunguka kwangu dunia nimegundua kwamba matukio makubwa ya kutisha watu wengi hawayajui kwa sababu mnasubiri yaripotiwe kwenye vyombo vya habari ndipo myasome. Huu ulimwengu una sehemu za kutisha na binadamu ambao ni hatari hata kuongea nao tu, nimeishi China kwa miaka kadhaa, kuna mambo nimeyashuhudia kule sikuwahi kuhisi kwamba yanawezekaan hapa duniani. Siku zote mwanadamu huwa anapenda kukiamini kitu mpaka akili yake inapo ishia, eneo ambalo akili yake haiwezi kufika hata akiambiwa vipi huwa hawezi kukubali kwa sababu anahisi ni zile nomino za dhahania na watu wa hivyo wengi huwa wanajifanya wajuaji na wabishi sana”
“Bado haiifanyi stori kama hii kuwa ya kawaida, kila mtu mpaka sasa huwa anajiuliza lile jambo linawezekana vipi, ndiyo maana licha ya kuonekana maeneo kadhaa ukiwa unaua watu, kuna watu bado wanaamini kwamba wewe umekufa na hawakubali kabisa kama upo hai, kwa sasa naanza kuwaelewa ni kwanini wanafikiria hivyo”
“Na hilo ndilo nilikuwa nalitaka tangu mwanzo kwa sababu limenifanya nimewapata watu wangu wengi sana na hivi sasa natarajia kumaliza kazi hii sitaki kuja kuanza kuua watu tena ndiyo maana sitaki kuacha mtu hata mmoja nyuma kwa sababu najua haya mambo yatakuja kurudi upya tena. Nataka nihakikishe nawamaliza wote ndipo naenda kupumzika jumla na sitakuja kuonekana sehemu yoyote ile duniani”
“Unampango wa kufanya jambo gani mpaka usije kuonekana tena?”
“Hilo haupaswi kulijua kwa sababu halina faida yoyote kwako”
“Naweza kujua kwamba yule binti aliishia wapi, kwa sababu kama baba yake alijitoa kifo lazima alikuwa na imani kwamba anamuacha binti yake kwenye mazingira mazuri na ya kueleweka ili asije kuteseka”
“Yule ni binti ambaye ataishi maisha mazuri na kizazi chake chote, ana bima ya maisha na nimempeleka mbali sana kiasi kwama hakuna mtu atakuja kujua kama aliwahi kuwepo labda kama atakuja kuamua kurudi mwenyewe tena Tanzania kipindi akiwa mtu mzima ila kwa sasa hakuna mtu anaweza kumpata. Nilifanya kama namsaidia ni binti yangu”
“Nashukuru sana kwa kuniamini na kuwa muwazi kwangu mpaka umenipa taarifa kama hizi ambazo huenda sikustahili kabisa kuzipata ama kuwa nazo ila jambo kubwa zaidi ambalo huwa linanifanya nikilala niwe na mawazo mengi ni lile la wewe kunipa nafasi ya kuishi wakati ulikuwa na uwezo mkubwa tu wa kuweza kuyabeba maisha yangu. Nimejiuliza sana hili swali kiasi kwamba nilitamani siku moja niweze kuonana na wewe ili nikuulize moja kwa moja huenda kama ukinijibu moyo wangu unaweza kutulia kwa sababu nitaijua sababu ya mimi kupata nafasi nyingine ya kuishi ukiacha lile la kunipa pesa nyingi ambazo zijawahi kuzishika kwa pamoja mimi kama mimi tangu nizaliwe. Begi lilikuwa na zaidi ya pesa za kitanzania milioni mia tano, hili nalo lilinitisha sana” Sarah bado alionekana kuwa na mengi ya kuzungumza na mtu huyo hivyo nafasi hiyo hakutaka kuweza kuichezea vibaya, alihitaji kuitumia vyema kumaliza dukuduku lake ambalo alikuwa nalo moyoni.
“Moja ya vitu amnavyo nimewalisha hata vijana wangu ni kufanya maamuzi ukiwa na uhakika na taarifa sahihi za unacho kiamualia hayo maamuzi yako. Hautakiwi kufanya maamuzi kwa sababu tu umejisikia kufanya hivyo, hilo ni jambo la hatari na unaweza kuja kujuta ukiwa umechelewa hivyo binafsi huwa sishauri kabisa mtu kufanya hilo kosa. Mimi mpaka nafikia uamuzi wa kufanya yale maamuzi tayari nilikuwa najua aina ya watu ambao nilikuwa nawaua, nilikuwa nina taarifa zao wote ndiyo maana hata taarifa za kujua wapi nilipo kule msituni ni mimi nilizivujisha nikaamua hata kufanya jukumu la kuhifadhi silaha na kuacha ujumbe kule kwa sababu nilijua kuna watu wataupata ili uendelee kuwachanganya zaidi.
Niliisoma historia nzima ya maisha yako, niliona jinsi ambavyo umeteseka kufika pale ulipo, hakika kwa mtoto wa kike ulikuwa unastahili pongezi zisizo na mipaka, ni mabinti wachache wana huo uthubutu. Lakini hilo pekee halikuwa jibu la kukupa nafasi nyingine ya kuishi kwa sababu kuna watu wamekua kama wewe lakini baadae wakaja kuwa washenzi hawa huwa siizingatii sana historia zao, kama anastahili kufa basi ni lazima tu afe. Jambo la msingi zaidi ambalo lilinivutia kwako ni uzalendo wako kwa taifa lako, jinsi ulivyo mwema na mpenda kusaidia watu. Huwa unajitoa hata kwa kidogo ulicho nacho. Huna kikubwa ila umekuwa msaada kwa watu wengi, hupendi kuona mtu anaonewa kwenye haki yake, hupendi kuwa sababu ya matatizo kwa watu.
83 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
RespectHii kitu ina mafunzo mengi sana hata kwenye maisha yetu ya kawaida kabisaa ya kila siku.
Kazi safi sana mkuu
Karibu sanaKiukweli hii story ina mafunzo mno
Hahahaha narudi leo mkuuStori tamu sana
Umeniacha na arosto mkuu ifanye kuisogeza kidogo wikiendi hii mkuu
🔥ina fundisha sana-----------
Leo saa ngapi mkuuHahahaha narudi leo mkuu