FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 2,232
- 4,389
- Thread starter
- #401
STORY: IDAIWE MAITI YANGU
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA THEMANINI NA SABA
SONGA NAYO................
Wenzake waligeuka kumwangalia kwa muda, hali yake haikuwa njema japo alijikaza kusimama, zile hasira zake ndizo ambazo zilimfanya awe kwa kwanza tena kurudi kwa mwanaume yule, kurudi kwake ikawa safari yake ya mapema kwenda kuzimu. Alienda bila balansi ya kueleweka, aligeuka na mateke mawili mfululizo, aliishia kupiga hewa, aliinama na kujigeuza kwa kujiviringisha lakini alikuta kapiga hewa, hakumuona mhusika, kasi ambayo Gavin alikuwa anatembea nayo haikuwa inaendana naye, alibaki ameduwa mpaka alipohisi kuna mtu nyuma yake.
Aligeuka kwa pupa, bahati ikawa mbaya zaidi kwake, alikamatwa kwenye eneo lake la koromeo ambalo lilinyofolewa kikatili kiasi kwamba hata wenzake walianza kuingiwa na woga. Slyvanos alikufa akiwa hana msaada wowote ule, Dayana aliitoa bastola yake na kuruhusu risasi nyingi sana kuweza kupiga lakini alifanya kosa kwa sababu ziliishia kwa mwenzo na kummalizia kabisa. Jambo hilo liliwafanya wapaniki, siku zote vitani ukipaniki basi umeshapoteza, risasi hazikufaa kwa sababu waliona wangezidi kuuana wenyewe hivyo njia bora zaidi kwa hapo ikawa ni kutumia mikono tu kuweza kupambana na huyo bwana mbele yao japo ilionekana kuwa zoezi lenye utata mkubwa.
Dayana alitangulia mbele, alirusha ngumi yake ilitua kwenye tumbo la Gavin wala hakumkwepa, alirusha nyingine ilidakwa akavutwa kwa nguvu na kupigwa kichwa ambacho alihisi kwamba kinapasuka. Alirudishwa nyuma kidogo, ngumi ambayo ilizama kwenye eneo lake la moyo ilimfanya kushindwa kupumua vizuri, alikuwa anahema juu juu tena kwa nguvu kubwa kiasi kwamba alishindwa kuhimili kuendelea kusimama ikamlazimu aweze kukaa.
Jaden alikuwa anaichanganya miguu yake kwa kasi ila kwa bahati mbaya hakufanikiwa hata kumfikia bwana huyo, alisimama akiwa anakakamaa. Upanga ulizama kwenye shingo yake vibaya kiasi kwamba ulitokezea mpaka nyuma, ulipokuja kuvutwa, hakuwa hai tena, hayo yote Dayana alikuwa anayashuhudia kwa macho yake akiwa amekaa hana jambo anaweza kulifanya. Tigan aliichomoa bastola yake ili ashambulie kwa risasi, Tigana alijirusha juu na kurudi chini kwa kasi ya ajabu, risasi zilipiga hewa.
Mkono wake wenye bastola ulikutanishwa na mguu bastola ilimponyoka, Gavin aliurusha upanga wake juu kwa nguvu kubwa huku macho yake yakiwa makali isivyokuwa kawaida. Tigan alikuwa ameurusha mguu wake, mguu ulikutanishwa na ngumi nzito na kuufanya kupinda kiasi, alipiga kelele ambazo hazikudumu zikabadilika baada ya mkono kuzama kwenye mbavu yake ambayo ilivunjwa wakati anashtuka alikuwa anaelekea chini. Gavin alizunguka kwa sarakasi na kutua juu ya Tigan kwenye kifua, alitapika damu nyingi akiwa anahema kwa mbali mno lakini wakati huo ule upanga ulikuwa unatua kwenye mikono ya mwanaume huyo.
Aliudaka na kuuzamisha kwenye moyo wa Tigan, wanaume hao walikuwa wanakufa kama utani ila ndio ulikuwa uhalisia wa mambo hayo. Wanaume watatu mpaka wakati huo walikuwa kwenye hali mbaya, ni Crepin na Bariki Dumba ambao walikuwa wamesimama japo nao walikuwa hawako sawa kwani alikuwa amewapitia mara ya kwanza. Bariki alikuwa na uchungu ambao alitakiwa kuulipa, Tigan kwake alikuwa zaidi ya kaka.
Alipiga makelele akiwa anatukana na kumfuata Gavin kwani hakuwa mbali, kisu kilirushwa huku naye akiwa anakuja, lakini wakati anafanya hayo Gavin naye alikuwa ameutuma upanga wake ambao uliikatisha safari ya Bariki. Ulizama kwenye paja lake, mwanaume huyo alitua karibu na alipokuwa Bariki, alimtisha, hakuwa anaweza kwenda popote pale, aliutua mguu wake kwenye goti likapinda, aliuvuta upanga wake kwa nguvu na kuitua ngumi yake kwenye shingo. Bariki alishuka chini akiwa anagugumia lakini muda huo huo alikaa kimya, ni Crepin ambaye alikuwa anajishauri kama ashambulie au aondoke eneo hilo kwani alikuwa amebaki mwenyewe lakini misingi ya kazi yake haikuwa ikimtaka kabisa yeye kuweza kukimbia kwenye eneo la tukio.
Akiwa anajishauri alishangaa upanga unakuja upande wake, ulitua kwenye kifua bahati nzuri ulikuja kwenye kishikio, alipata maumivu makali kwani upanga huo ulikuwa mzito. Mwanaume huyo mbele yake Gavin alimfikia mara moja, wakati anarusha ngumi yake alipigwa na kitu kizito kwenye tumbo, ulikuwa mkono. Zilifuata ngumi tatu kwenye kifua akadondoka na kupoteza fahamu muda huo huo. Dayana alikuwa anajivuta chini alipokuwa akiwa hana hata ujasiri wa kuweza kunyanyuka ili apambane na bwana huyo ambaye alikuwa mbele yake.
Alikuwa amepoa tayari lakini hiyo nguvu ya kusimama ndiyo haikuwepo, alikuwa anahema na kumeza mate kama kibaka ambaye amefikishwa jela kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake. Mambo ambayo aliyaona hapo kwa muda mfupi yalikuwa yanataka sana moyo kuweza kuyavumilia na kujifanya haujaona halafu usimame kupambana na bwana huyo. Alikuwa anajivuta kwenda nyuma mpaka pale ambapo alikita kwenye jiwe kubwa, alijua kabisa hana sehemu nyingine ya kuweza kwenda.
Ujivuni wake na maamuzi yake ya kujigamba ndiyo ambayo yalimfanya wakati huo kuishia sehemu mbaya kama hiyo, maamuzi yake yalikuwa ya kipuuzi na kwa wakati huo yalikuwa yanamtokea puani. Angefuata ule ushauri ambao alipewa mara ya kwanza asingekuwa kwenye majuto, mpaka wakati huo alikuwa mewapoteza vijana wake watatu na wawili hali zao hazikuwa zikieleweka vizuri huku yeye pekee ndiye ambaye alionekana kuwa mzima wa afya kabisa kiasi kwamba alikuwa anaweza hata kusimama na kuondoka eneo hilo. Gavin alimsogelea pale alipokuwepo.
“Nimekwambia mapema kuhusu hili bibie, haya maisha muda mwingine huwa yanawapa watu somo muda ukiwa umeenda ndiyo kama hivi. Ni dakika kadhaa tu nyuma nimetoka kukupa ushauri wa jambo gani la mhimu wewe kuweza kulifanya ila umedharau na kuleta ujuaji, maamuzi yako ya kipumbavu kama kiongozi yameyaponza maisha ya vijana wako. Sijui utakuwa na lipi la kujitetea kuhusu hilo.
Ukiwa na uwezo wa kufanya jambo fulani ogopa sana kutangaza hadharani kwa sababu kuna watu huwa wanamchukulia kila mtu kama mshindani kwao hivyo kama wakikujua wewe basi watakutafuta wakumalize. Ndilo kosa ambalo umelifanya kuanza kunitambia. Nikiwa China, kuna jamaa niliwahi kukutana naye, yeye alikuwa anajiamini kwamba anaweza kupiga mtu yeyote yule duniani hivyo alikuwa anazunguka kila sehemu akimkuta mtu mwenye uwezo wa mapigano basi anamhesabia kama ni mshindani ambaye ni hatari kwake hivyo akawa anawaua mpaka siku alipokuja kukutana na mimi.
Nilimuua kizembe tu kwa sababu alinidharau, lile ni kosa ambalo mpaka sasa nina uhakika huko aliko huwa analijutia. Ile dharau yake ndiyo ambayo iliondoka na maisha yake kama wewe ambavyo umewafanyia vijana wako. Haya mauaji hapa ni wewe ndiye sababu, wewe ndiye umewaua vijana wako kwa sababu ya ujuaji wako”
Ile ni shule zaidi ya kitabu alipewa lakini alianza kuielewa vizuri muda ukiwa umeenda. Alikuwa na nafasi ya kufanya hivyo mapema lakini alidharau, muda haukuwa rafiki kwake ndipo alilikumbuka hilo. Gavin alitoweka eneo hilo akimuacha Dayana mzima wa afya kabisa, alijua ile hatia ambayo angejikuta nayo ndiyo ilikuwa adhabu ya ubishi wake, jambo lile lingemtafuta maisha yake yote.
Dayana aliibeba miili ya wenzake na wale majeruhi na kuondoka nao huku akiwa anawaza sababu ya msingi ya kumjibu bosi wake. Kwa kosa ambalo alikuwa amelifanya, hasara ya kuliteketeza kundi lake kwa mkono wake mwenyewe? Hakuwa na uhakika kama kiongozi wake angemuacha hai hivyo hakupata hata tone la usingizi, alijitahidi tu kuihifadhi miili ya wenzake na kuwatibia wale ambao hawakuwa kwenye hali mbaya kisha akawa amezongwa na mawazo ya sababu za kumpa bosi wake.
Akiwa kwenye hayo mawazo ndipo alipokea ujumbe mwingine mzito na wa kutisha, alihisi huo ulikuwa mbaya kuliko hata ambalo lilimkuta na wenzake. Mkurugenzi Othman Micho alikutwa ameuawa na mwili wake ulipatikana kwenye bwana lake la kuogelea nyumbani, habari hiyo iliupasua moyo wake, alihisi jambo hilo haliwezekani alikuwa anaota ila hakuwa na uwezo wa kubadilisha lolote lile kwa sababu kama picha alitumiwa. Nani alikuwa amemuua mkurugenzi? Ni swali ambalo hata yeye hakuwa na uwezo wa kulijibu, alijihisi kuchanganyikiwa, kichwa kilikuwa kizito akakaa sehemu na kuanza kushusha kilio kwa hisia na uchungu mkubwa.
Ndiyo maana wakati huo alikuwa amekaa na kuujutia uamuzi wake, kushindwa kwake kuweza kufanya mahesabu na maamuzi sahihi. Dayana alijiona kwamba hana maana tena, alijiona kuwa yeye ndiye sababu ya yote hayo kutokea. Angeweza vipi kupambana na ulimwengu mwanamke huyo na kuibeba hatia ya hayo yote ambayo aliyasababisha? Moyo wake ulikuwa mdogo, mambo hayo yalikuwa makubwa asingewezekana nayo. Dayana alitoa bastola ambayo ilikuwa kwenye droo ya meza ambayo alikuwa ameegamia, alitazama kwenye simu yake ambako kulikuwa na picha za familia yake pamoja na hao wenzake wa THE INVISIBLE, kisha akajipiga risasi. Dayana aliamua kuyabeba maisha yake mwenyewe kwa kujiua kwa sababu ya hatia moyoni.
87 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
STORYTELLER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
********************
SEHEMU YA THEMANINI NA SABA
SONGA NAYO................
Wenzake waligeuka kumwangalia kwa muda, hali yake haikuwa njema japo alijikaza kusimama, zile hasira zake ndizo ambazo zilimfanya awe kwa kwanza tena kurudi kwa mwanaume yule, kurudi kwake ikawa safari yake ya mapema kwenda kuzimu. Alienda bila balansi ya kueleweka, aligeuka na mateke mawili mfululizo, aliishia kupiga hewa, aliinama na kujigeuza kwa kujiviringisha lakini alikuta kapiga hewa, hakumuona mhusika, kasi ambayo Gavin alikuwa anatembea nayo haikuwa inaendana naye, alibaki ameduwa mpaka alipohisi kuna mtu nyuma yake.
Aligeuka kwa pupa, bahati ikawa mbaya zaidi kwake, alikamatwa kwenye eneo lake la koromeo ambalo lilinyofolewa kikatili kiasi kwamba hata wenzake walianza kuingiwa na woga. Slyvanos alikufa akiwa hana msaada wowote ule, Dayana aliitoa bastola yake na kuruhusu risasi nyingi sana kuweza kupiga lakini alifanya kosa kwa sababu ziliishia kwa mwenzo na kummalizia kabisa. Jambo hilo liliwafanya wapaniki, siku zote vitani ukipaniki basi umeshapoteza, risasi hazikufaa kwa sababu waliona wangezidi kuuana wenyewe hivyo njia bora zaidi kwa hapo ikawa ni kutumia mikono tu kuweza kupambana na huyo bwana mbele yao japo ilionekana kuwa zoezi lenye utata mkubwa.
Dayana alitangulia mbele, alirusha ngumi yake ilitua kwenye tumbo la Gavin wala hakumkwepa, alirusha nyingine ilidakwa akavutwa kwa nguvu na kupigwa kichwa ambacho alihisi kwamba kinapasuka. Alirudishwa nyuma kidogo, ngumi ambayo ilizama kwenye eneo lake la moyo ilimfanya kushindwa kupumua vizuri, alikuwa anahema juu juu tena kwa nguvu kubwa kiasi kwamba alishindwa kuhimili kuendelea kusimama ikamlazimu aweze kukaa.
Jaden alikuwa anaichanganya miguu yake kwa kasi ila kwa bahati mbaya hakufanikiwa hata kumfikia bwana huyo, alisimama akiwa anakakamaa. Upanga ulizama kwenye shingo yake vibaya kiasi kwamba ulitokezea mpaka nyuma, ulipokuja kuvutwa, hakuwa hai tena, hayo yote Dayana alikuwa anayashuhudia kwa macho yake akiwa amekaa hana jambo anaweza kulifanya. Tigan aliichomoa bastola yake ili ashambulie kwa risasi, Tigana alijirusha juu na kurudi chini kwa kasi ya ajabu, risasi zilipiga hewa.
Mkono wake wenye bastola ulikutanishwa na mguu bastola ilimponyoka, Gavin aliurusha upanga wake juu kwa nguvu kubwa huku macho yake yakiwa makali isivyokuwa kawaida. Tigan alikuwa ameurusha mguu wake, mguu ulikutanishwa na ngumi nzito na kuufanya kupinda kiasi, alipiga kelele ambazo hazikudumu zikabadilika baada ya mkono kuzama kwenye mbavu yake ambayo ilivunjwa wakati anashtuka alikuwa anaelekea chini. Gavin alizunguka kwa sarakasi na kutua juu ya Tigan kwenye kifua, alitapika damu nyingi akiwa anahema kwa mbali mno lakini wakati huo ule upanga ulikuwa unatua kwenye mikono ya mwanaume huyo.
Aliudaka na kuuzamisha kwenye moyo wa Tigan, wanaume hao walikuwa wanakufa kama utani ila ndio ulikuwa uhalisia wa mambo hayo. Wanaume watatu mpaka wakati huo walikuwa kwenye hali mbaya, ni Crepin na Bariki Dumba ambao walikuwa wamesimama japo nao walikuwa hawako sawa kwani alikuwa amewapitia mara ya kwanza. Bariki alikuwa na uchungu ambao alitakiwa kuulipa, Tigan kwake alikuwa zaidi ya kaka.
Alipiga makelele akiwa anatukana na kumfuata Gavin kwani hakuwa mbali, kisu kilirushwa huku naye akiwa anakuja, lakini wakati anafanya hayo Gavin naye alikuwa ameutuma upanga wake ambao uliikatisha safari ya Bariki. Ulizama kwenye paja lake, mwanaume huyo alitua karibu na alipokuwa Bariki, alimtisha, hakuwa anaweza kwenda popote pale, aliutua mguu wake kwenye goti likapinda, aliuvuta upanga wake kwa nguvu na kuitua ngumi yake kwenye shingo. Bariki alishuka chini akiwa anagugumia lakini muda huo huo alikaa kimya, ni Crepin ambaye alikuwa anajishauri kama ashambulie au aondoke eneo hilo kwani alikuwa amebaki mwenyewe lakini misingi ya kazi yake haikuwa ikimtaka kabisa yeye kuweza kukimbia kwenye eneo la tukio.
Akiwa anajishauri alishangaa upanga unakuja upande wake, ulitua kwenye kifua bahati nzuri ulikuja kwenye kishikio, alipata maumivu makali kwani upanga huo ulikuwa mzito. Mwanaume huyo mbele yake Gavin alimfikia mara moja, wakati anarusha ngumi yake alipigwa na kitu kizito kwenye tumbo, ulikuwa mkono. Zilifuata ngumi tatu kwenye kifua akadondoka na kupoteza fahamu muda huo huo. Dayana alikuwa anajivuta chini alipokuwa akiwa hana hata ujasiri wa kuweza kunyanyuka ili apambane na bwana huyo ambaye alikuwa mbele yake.
Alikuwa amepoa tayari lakini hiyo nguvu ya kusimama ndiyo haikuwepo, alikuwa anahema na kumeza mate kama kibaka ambaye amefikishwa jela kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake. Mambo ambayo aliyaona hapo kwa muda mfupi yalikuwa yanataka sana moyo kuweza kuyavumilia na kujifanya haujaona halafu usimame kupambana na bwana huyo. Alikuwa anajivuta kwenda nyuma mpaka pale ambapo alikita kwenye jiwe kubwa, alijua kabisa hana sehemu nyingine ya kuweza kwenda.
Ujivuni wake na maamuzi yake ya kujigamba ndiyo ambayo yalimfanya wakati huo kuishia sehemu mbaya kama hiyo, maamuzi yake yalikuwa ya kipuuzi na kwa wakati huo yalikuwa yanamtokea puani. Angefuata ule ushauri ambao alipewa mara ya kwanza asingekuwa kwenye majuto, mpaka wakati huo alikuwa mewapoteza vijana wake watatu na wawili hali zao hazikuwa zikieleweka vizuri huku yeye pekee ndiye ambaye alionekana kuwa mzima wa afya kabisa kiasi kwamba alikuwa anaweza hata kusimama na kuondoka eneo hilo. Gavin alimsogelea pale alipokuwepo.
“Nimekwambia mapema kuhusu hili bibie, haya maisha muda mwingine huwa yanawapa watu somo muda ukiwa umeenda ndiyo kama hivi. Ni dakika kadhaa tu nyuma nimetoka kukupa ushauri wa jambo gani la mhimu wewe kuweza kulifanya ila umedharau na kuleta ujuaji, maamuzi yako ya kipumbavu kama kiongozi yameyaponza maisha ya vijana wako. Sijui utakuwa na lipi la kujitetea kuhusu hilo.
Ukiwa na uwezo wa kufanya jambo fulani ogopa sana kutangaza hadharani kwa sababu kuna watu huwa wanamchukulia kila mtu kama mshindani kwao hivyo kama wakikujua wewe basi watakutafuta wakumalize. Ndilo kosa ambalo umelifanya kuanza kunitambia. Nikiwa China, kuna jamaa niliwahi kukutana naye, yeye alikuwa anajiamini kwamba anaweza kupiga mtu yeyote yule duniani hivyo alikuwa anazunguka kila sehemu akimkuta mtu mwenye uwezo wa mapigano basi anamhesabia kama ni mshindani ambaye ni hatari kwake hivyo akawa anawaua mpaka siku alipokuja kukutana na mimi.
Nilimuua kizembe tu kwa sababu alinidharau, lile ni kosa ambalo mpaka sasa nina uhakika huko aliko huwa analijutia. Ile dharau yake ndiyo ambayo iliondoka na maisha yake kama wewe ambavyo umewafanyia vijana wako. Haya mauaji hapa ni wewe ndiye sababu, wewe ndiye umewaua vijana wako kwa sababu ya ujuaji wako”
Ile ni shule zaidi ya kitabu alipewa lakini alianza kuielewa vizuri muda ukiwa umeenda. Alikuwa na nafasi ya kufanya hivyo mapema lakini alidharau, muda haukuwa rafiki kwake ndipo alilikumbuka hilo. Gavin alitoweka eneo hilo akimuacha Dayana mzima wa afya kabisa, alijua ile hatia ambayo angejikuta nayo ndiyo ilikuwa adhabu ya ubishi wake, jambo lile lingemtafuta maisha yake yote.
Dayana aliibeba miili ya wenzake na wale majeruhi na kuondoka nao huku akiwa anawaza sababu ya msingi ya kumjibu bosi wake. Kwa kosa ambalo alikuwa amelifanya, hasara ya kuliteketeza kundi lake kwa mkono wake mwenyewe? Hakuwa na uhakika kama kiongozi wake angemuacha hai hivyo hakupata hata tone la usingizi, alijitahidi tu kuihifadhi miili ya wenzake na kuwatibia wale ambao hawakuwa kwenye hali mbaya kisha akawa amezongwa na mawazo ya sababu za kumpa bosi wake.
Akiwa kwenye hayo mawazo ndipo alipokea ujumbe mwingine mzito na wa kutisha, alihisi huo ulikuwa mbaya kuliko hata ambalo lilimkuta na wenzake. Mkurugenzi Othman Micho alikutwa ameuawa na mwili wake ulipatikana kwenye bwana lake la kuogelea nyumbani, habari hiyo iliupasua moyo wake, alihisi jambo hilo haliwezekani alikuwa anaota ila hakuwa na uwezo wa kubadilisha lolote lile kwa sababu kama picha alitumiwa. Nani alikuwa amemuua mkurugenzi? Ni swali ambalo hata yeye hakuwa na uwezo wa kulijibu, alijihisi kuchanganyikiwa, kichwa kilikuwa kizito akakaa sehemu na kuanza kushusha kilio kwa hisia na uchungu mkubwa.
Ndiyo maana wakati huo alikuwa amekaa na kuujutia uamuzi wake, kushindwa kwake kuweza kufanya mahesabu na maamuzi sahihi. Dayana alijiona kwamba hana maana tena, alijiona kuwa yeye ndiye sababu ya yote hayo kutokea. Angeweza vipi kupambana na ulimwengu mwanamke huyo na kuibeba hatia ya hayo yote ambayo aliyasababisha? Moyo wake ulikuwa mdogo, mambo hayo yalikuwa makubwa asingewezekana nayo. Dayana alitoa bastola ambayo ilikuwa kwenye droo ya meza ambayo alikuwa ameegamia, alitazama kwenye simu yake ambako kulikuwa na picha za familia yake pamoja na hao wenzake wa THE INVISIBLE, kisha akajipiga risasi. Dayana aliamua kuyabeba maisha yake mwenyewe kwa kujiua kwa sababu ya hatia moyoni.
87 inafika mwisho.
FEBIANI BABUYA.