Sehemu ya 33
“Mpenzi wangu nilikukumbuka mno,” alining’oneza sikioni, sauti yake ilijaa mahaba. Pumzi zake zilimtoka kwa nguvu.
Taratibu ule wahaka wa dhamira ya kumwambia ukweli ikaanza kuyeyuka. Nikajikuta nasombwa na misisimko ya huba, mapigo ya moyo yakaanza kunidunda kwa nguvu.
Sauti moja akilini ikawa inanikumbusha: Uhai wa mwanao upo mikononi mwako, fanya kilichokuleta. Mwambie ukweli kwamba una mke na mtoto, mweleze waziwazi kwamba uhai wa mwanao unamtegemea yeye. Lakini sauti hiyo ikazidiwa ushawishi na kila alichokianzisha Lawalawa.
Alisogeza mdomo wake karibu na wangu, papi zetu zikagusana, macho yake malegevu yakiniangalia kwa hisia kali. Tukaanza kunyonyana denda. Tukio hilo likachochea kuiendea hatua nyingine.
Niliingiza mkono ndani ya blauzi yake, nikawa napapasa mzunguko wa kiuno chake chembamba, mtoto wa watu akaanza kuweweseka. Kwa kweli Lawalawa alikuwa na hisia za karibu. Nilimweka kwenye kochi lililokuwa mule ndani akiwa hana nguvu.
“Tuongee kidogo.” Nilimwambia.
Hakujibu kitu, alibakia kama bubu huku macho yake yakiwa yamebadilika rangi.
“Habari za siku mpenzi?” nilimsalimu huku nikiketi kitandani.
“Ni nzuri mpenzi, nilikukumbuka tu hadi nikawa na wasiwasi Ajibu.”
“Pole sana Lawalawa, usiwe na wasiwasi tena.”
“Kuna wakati nilikuwa napata ndoto mbaya juu yako.”
“Ndoto gani tena?”
“Nilikuwa naona kama umepata manamke mwingine na umezaa naye mtoto,” alisema.
Ingawa mwanamke yule aliongea kwa hisia tu, lakini ndio hasa ulikuwa ukweli wenyewe, nilikuwa na mke na mtoto ambaye kwa wakati huo alikuwa hoi kitandani kwa ugonjwa wa saratani ya damu. Na yeye ndiye alitakiwa kumtolea uboho mwanangu ili upandikizwe kwenye mifupa yake.
“Ingetokea ndoto hiyo ikawa kweli ungeafanya nini Lawalawa mpenzi?”nilimuliza.
“Wallah ningekuacha upesi sana, katika maisha yangu huwa sipendi kusalitiwa,” alisem. Moyo wangu ulipiga kite, meneno ya mrembo huyo yalinitisha sana. Akaendelea kuniambia :
“Unajua kwa nini nataka uwe mume wangu mpenzi, Ajibu?”
“Sijui mpenzi.”
“Ni kwa kuwa wewe ni mwanaume mstarabu sana, ni mtu wa pekee, hujawahi kunichanganya na wanawake wengine, unanipenda na kuniheshimu, wewe ni tofuati na watu wengine maarufu.