Simulizi: Roho yake inadai

Simulizi: Roho yake inadai

*ROHO YAKE INADAI --- 06*

*Simulizi za Series za Steve*


ILIPOISHIA

.
.
Mrs Garett akamweleza dhamira yake kuwa anataka kutubu na kuomba msamaha. Padri akampeleka kwenye chumba maalum, Mrs Garett akaketi kitako upande wa pili akitenganishwa na Padri kwa ukuta mwepesi wa mbao wenye matundutundu.

.
.
Kabla hajaanza kusema kitu, akajikuta anaanza kumimina machozi.

ENDELEA
.
.

“Padri Alfonso,” Mrs Garett akaita. “Mimi ni mkosefu sana, naona hata sistahili kuwapo mbele ya madhabahu ya Mungu. Nimemwendea kombo. Nimemtendea ndivyo sivyo.”
.
.
“Na hao ndiyo wakaribishwao hapa,” akasema Padri Alfonso kwa sauti yake nzito. “Usijali maana umejua uliikengeuka. Wewe ni bora kuliko wale wanaojihisi wako safi. Mkombozi wetu alikuja kwa ajili yetu waongofu na tulipotoka apate kutukomboa.”
.
.
Mrs Garett akavuta kwanza makamasi, alafu akamtazama Olivia. Alikuwa amesimama mbali akiwa katika hali ya upweke na woga.
.
.
“Padri Alfonso,” Mrs Garett akaita na kusema, “Nimekuja hapa kinyume kabisa na maagizo ya mume wangu. Hataki kabisa mimi kuja kanisani, hata akigundua anaweza kunikatakata vipande na kuwatupia nguruwe wanile. Lakini …”
.
.
Akabanwa na kwikwi. Akajipangusa na leso yake kisha akaendelea kunena, “ … nimeshindwa kuvumilia hili. Limekuwa mzigo sana kifuani mwangu, siwezi tena kuhimili. Limenitesa miaka kumi sasa na naona inatosha.”
.
.
“Ni nini hiko?” Padri akauliza.
.
.
Mrs Garett akanyamaza kwa muda akijaribu kuremba dhambi yake, akashindwa kabisa kuifanya isionekane kali masikioni, akaamua tu kusema vivyo hivyo, “Nilimuua mwanangu.”
.
.
Padri Alfonso akatulia kidogo kisha akamuuliza, “Una maanisha Kecie?”
.
.
“Ndio. Nilimuua Kecie,” akajibu Mrs Garett akitazama chini na macho yake mekundu.
.
.
“Kwanini ulimuua?” Akauliza Padri.
.
.
“Ni simulizi pana kidogo,” akasema Mrs Garett. Akajipangusa machozi kisha akaendelea kuongea …
.
.
Miaka kumi na mbili iliyopita …
.
.
Ulikuwa ni mchana wa saa saba wakati mume wangu aliporejea nyumbani toka kazini. Anafanya kazi kwenye kiwanda hivyo nilistaajabu kwake kuwahi kurudi siku hiyo tofauti na ilivyo kawaida yake. Alikuwa amenuna sana kiasi cha kuogopa hata kuongea naye, ila baadae alipotulia akaniambia nini kinamtatiza.
.
.
Hakuwa anamtaka Kecie pale nyumbani. Nilishangazwa sana na neno lake hilo. Sikuona mahusiano ya yeye kurudi kazini mapema na uwepo wa Kecie.
.
.
Akiwa amefura kwa hasira, akanambia kuwa Kecie ni gundu kubwa ndani ya nyumba. Amekuwa ni mtoto wa mikosi na laana. Amekuwa ni mtoto anayemsababishia matatizo sana kazini kwake.
.
.
Nilibaki naduwaa. Nilitaka kujua ni kwanini anasema hivyo lakini hakuniambia abadani. Kitu pekee alichoniambia ni kwamba amefukuzwa kazi. Aliponiambia hivyo akaenda zake ndani, na tangu hapo hatukuwa na mahusiano mazuri baina yangu na yeye.
.
.
Basi siku zikapita. Mahusiano baina yake na Kecie yakawa mabaya sana sana. Hakuwa anataka kumwona kabisa. Na muda mwingine angempiga nusura kumuua. Alikuwa na chuki kubwa sana juu yake.
.
.
Na kwakuwa hakuwa na kazi, tukawa tunaishi kwenye umasikini mkubwa sana. Nakumbuka siku nne zilipita tukiwa hatuna kitu mfukoni, tukiomba tu kwa majirani. Mume alikuwa anatafuta kazi, akizunguka huko viwandani na hata kuomba vibarua, akawa hapati ata cha ndani ya masaa.
.
.
Siku moja, tukiwa chumbani, akiwa ametulia kabisa, akaniita, “Mke wangu, kuna kitu nataka kukwambia.” Nilikuwa nimechoka kwa njaa, tulikuwa tumepata chakula kidogo sana, hata majirani walikuwa wametuchoka.
.
.
“Unataka sema nini?” nikamuuliza. Akaniambia, “Tumuue Kecie.” Nikashtuka sana. Nikamtazama na kumuuliza, “kwanini tumuue mtoto wetu wa pekee?”
.
.
Aliposhusha pumzi ndefu, akasema ya kwamba tangu Kecie azaliwe amekuwa akiandamwa na mabalaa, tabu na mikosi. Amekuwa akipatwa na wakati mgumu sana hajapata kuona. Na kama Kecie akiendelea kuwapo hai, basi hali itakuwa mbaya zaidi na wote tutakufa kwa njaa, ikiwemo na huyo mtoto.
.
.
Jambo hili likawa gumu sana kwangu. Kumuua mtoto niliyemzaa kwa uchungu si jambo jepesi hata kidogo. Nilikataa katakata, nikamfokea na kumtahadharisha asiwaze hilo kabisa maana halitakuja kuwahi kutokea. Haikuwa inaniingia akilini kuwa Kecie anaweza akawa sababu ya ufukara wetu.
.
.
Basi siku zikasogea. Ikafikia kipindi mpaka tukaanza kuuza vitu vyetu vya ndani tupate chakula. Navyo vikakwisha. Hapa sasa Kecie naye akaanza kudhoofu sana. Mume wangu akanikumbusha lile jambo tena na tena.
.
.
Siku moja, ikiwa ni majira ya usiku mwepesi, mume wangu akaja na babu mmoja ambaye alinitambulisha kuwa aitwa Tomas Fringe. Mwanaume huyo alikuwa mfupi na mwenye kubebelea briefcase rangi ya kahawia. Mume wangu alisema kuwa mwanaume huyo ni ‘mtaalamu’ na yupo pale kutusaidia.
.
.
Akatuagiza tuzime taa nyumba nzima. Tukafanya vivyo. Tufunge madirisha na kila mlango, na Kecie awepo chumbani kwake. Tukafanya vivyo. Akatoa chupa fulani ya duaria yenye vitu vya kung’aa ndani yake. Na kwasababu giza lilikuwa limetawala ndani, mwanga wa chupa ile ndiyo ukawa umeng’aza.
.
.
Ulikuwa ni mwanga wa kijani hafifu.
.
.
Aliweka chupa hiyo mezani, akaisugua kwa viganja vyake akisema maneno ambayo sikuwa nayaelewa. Katika namna ya ajabu, chupa ile ikaanza kubadilika rangi kuwa nyekundu. Yule mzee, bwana Tomas Fringe, akamtazama mume wangu, kisha mimi. Akasema. “Kuna tatizo ndani ya nyumba yenu.”
.
.
Hatukusema kitu, akaendelea kuongea baadhi ya maneno yake, taa ikazidi kukolea wekundu kuelekea damu ya mzee. Hapo akakoma na kutuuliza, “Tukiondoe kitu hiko?”
.
.
“Ndio,” Mume wangu akawahi kujibu. Lakini Thomas akan’tazama na kuniuliza, “Upo tayari?” Nikamtazama mume wangu. Akan’tikisa kichwa kunishawishi nikubali, basi nami nikaridhia.
.
.
Bwana yule akatutaka tuweke mikono yetu juu ya ile chupa na kufuatisha maneno kadhaa aliyokuwa anatamka. Tukiwa tunatamka maneno hayo, tukawa tunasikia mlango unagongwa kwanguvu! Mlango wa Kecie. Kama haitoshi akawa anatuita, analia kuomba msaada!
.
.
Nilitaka kuacha, nilipatwa na shauku ya kwenda kumwona, lakini mzee yule akanikazia macho na kunipa ishara ya kuendelea kuteta aliyokuwa anasema. Tukaendelea.
.
.
Kadiri tulivyokuwa tunasema, basi na makelele yale ya Kecie yakawa yanapungua, na ile taa inageuka rangi kuwa ya kijani. Tulipomaliza, taa ile ilikuwa kijani kilichokolea. Na katika namna ya kustaajabisha, nikaona kivuli cha mwanamke kikiwa ukutani kinatambaa kana kwamba mende!
.
.
Kivuli hicho kikasimama sebuleni na kuangaza, kisha kikaambalia nje.
.
.
“Vizuri!” akasema yule bwana Fringe akitutaka sasa tuache kushika chupa yake. “Sasa kazi imekwisha hatua ya kwanza, imebakia hatua ya mwisho.”
.
.
Akaweka chupa yake ndani ya briefcase na kumuagiza mume wangu akamzike Kecie kule misituni. Akifanya vivyo atasema maneno kadhaa aliyomtajia na kila kitu kitakuwa kimekwisha. Ataona faida yake.
.
.
Kwasababu za woga, Mume wangu akataka kwenda na mimi kule msituni. Bwana Fringe akamruhusu na alipoenda zake, sisi tukangoja usiku uwe mkubwa tukatimize kazi hiyo.
.
.
Basi baada ya masaa kadhaa, tukabeba mwili wa Kecie na kwenda nao msituni, tukafukua shimo na kuutumbukiza humo. Mume wangu akawa anafukia wakati mimi nikiwa natazama huku na kule kuangazia usalama.
.
.
Nikiwa naangaza, nikahisi kumwona mtu anatutazama! Alikuwa ni mwanaume mrefu mwenye mwili mpana. Tulikuwa katikati ya msitu. Nilihofia sana kumwona mtu huyo, niliona sasa habari yetu itajulikana Boston nzima, basi nikamshtua mume wangu na kumwambia kuna mtu kule. Upesi mtu yule akaanza kukimbia.
.
.
Mume wangu akamkimbiza sana na hatimaye akampata. Alimrukia na kumdondosha chini. Akamtwanga na chepeo kichwani. Na kwasababu za kuondosha ushahidi tukamzika kisha tukarudi nyumbani upesi.
.
.
Usiku huo sikulala kabisa. Nilitekwa na mawazo mabaya kabisa. Hata nilipopata lepe la usingizi, nikaota ndoto za ajabu ajabu. Nikawa macho mpaka jua linakucha.
.
.
Lakini asubuhi hiyo, tukiwa bado hatujatoka kitandani, nikakumbuka jambo ambalo lilintia hofu. Nikamwamsha na kumwamba mume wangu ya kwamba usiku ule baada ya kumzika Kecie, hatukutamka yale maneno ambayo mtaalamu alituagiza.
.
.
Mume wangu akashtuka sana. Ilikuwa ni kwasababu ya yule mtu aliyemkimbiza ndiyo maana akasahau. Tukapata sana maswali itakuaje, lakini mwishowe tukapuuzia, akinipa moyo kuwa kwasababu Kecie hayupo, basi mambo yatakuwa tu shwari.
.
.
Kumbe tulikuwa tumekosea kabisa kabisa, Alfonso …
.
.
.
***
.
.
.
Nini mama anataka kusema? Kama Kecie aliuawa na kuzikwa, vipi zile habari zake za kuonekana mara ya mwisho msituni akiwa na Faris aliyekuwa bubu na kuchora michoro ya ajabu?”
.
 
*ROHO YAKE INADAI --- 07*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA
.
.
Mume wangu akashtuka sana. Ilikuwa ni kwasababu ya yule mtu aliyemkimbiza ndiyo maana akasahau. Tukapata sana maswali itakuaje, lakini mwishowe tukapuuzia, akinipa moyo kuwa kwasababu Kecie hayupo, basi mambo yatakuwa tu shwari.
.
.
Kumbe tulikuwa tumekosea kabisa kabisa, Alfonso …
.
.
ENDELEA
.
.
Mrs Garett akaweka kituo na kufuata machozi kwanza. Akameza mate na kutazama pembeni akiendelea kusema.
.
.
Basi kwakuwa tulikuwa tumekiuka kile tulichoambiwa na bwana Fringe, tukawa tunaishi kwa hofu kidogo labda pengine mambo yanaweza kukiuka, ila zikapita masiku pasipo jambo lolote kutukia. Tatizo lilikuwa tu kwamba, bado kwa upande wa mume wangu mambo yalikuwa yaleyale.
.
.
Hakuwa anapata kazi popote pale, maisha yalikuwa magumu magumu magumu. Ikafikia kipindi mume wangu akaniambia, mke wangu kwakuwa tulikosea yale masharti, basi tumfuate tena bwana yule tumweleze, labda anaweza kutusaidia. Sikuwa na lingine zaidi ya kumkubalia, akafunga safari na kesho yake akaja naye nyumbani.
.
.
Bwana yule akalalama sana kwa kufanyia uzembe jambo alilotuambia. Akasema kuwa yale yote tuliyoyafanya yalikuw bure, na basi kukata mzizi wa fitna, basi inabidi turudie tena lile swala upya. Lakini tutalirudiaje na wakati Kecie ameshakufa? Nikauliza.
.
.
Yule bwana, Fringe kwa jina, akatuambia ataongozana na sisi kwenda huko msituni, tumfukue Kecie na turejelee zoezi. Niliogopa sana, mosi kwenda msituni, pili kwenda kuona maiti. Nilihisi mwili umekuwa wa baridi, natetemeka kila kiungo, lakini … lakini sikuwa na machaguzi. Ilibidi nifanye tulichokubaliana.
.
.
Tukatoka majira ya saa tisa usiku tukiwa watatu. Nakumbuka siku hiyo mvua ilikuwa inanyesha sana. Baridi lilikuwa kali pia kiasi kwamba barafu zilikuwa zimejaa njiani.
.
.
Nikiwa nimejikunyata, tukaelekea huko msituni, siku hiyo hatukuwa tumebeba taa, wanaume wakachimba shimo na kumfukua Kecie. Mwili wake ulikuwa umejawa na udongo mweusi. Ulikuwa wa baridi mno kama barafu!
.
.
Yule bwana, Fringe, akaniambia niushike mwili huo, nami nikafanya vivyo. Akafungua mkoba wake na kutoa ile chupa yake ya kioo cha duara. Akaipangusa akisema maneno kadha wa kadha, mara ikaanza kuwaka ikiwa ya kijani! Akatutaka tuiwekee viganja chupa yake ile na kusema maneno aliyokuwa anayatamka.
.
.
Basi tukafanya vivyo, mwili wa Kecie ukazamishwa tena ndani ya shimo na mume wangu pamoja na bwana Fringe wakatenda kazi ya kuufukia. Walipomaliza, mume wangu akasema yale maneno ambayo bwana Fringe alimtaka ayatamke kisha kazi ikawa imeishia apo.
.
.
Ila kabla hatujaondoka, Bwana Fringe alituuliza, “Kuna yeyote aliyewaona wakati mnamzika Kecie mara ya kwanza?” mimi na mume wangu tukatazamana, akawahi kujibu, “Hapana. Hamna aliyetuona.”
.
.
Bwana Fringe akatabasamu, ila tabasamu lake lilinitisha zaidi. Mtu yule hakuwa wa kawaida. Kila nilipomtazama nilijikuta natetemeka kwa hofu. Na kila macho yangu yalipokutana na yake, nilihisi moyo wangu umesimama kwa muda. Sikuwa najua kwanini.
.
.
Alitutazama na kutuambia, kwa ajili ya usalama wetu, tutangaze kuwa Kecie amepotelea msituni. Haitakuwa hoja sana kwani watoto kadhaa huwa wanapotelea huko misituni. Lakini nilipata swali, watu wataaminije hilo kwa wepesi?
.
.
Bwana yule, Fringe, katika hali ya kustaajabisha akajua swali langu hilo kichwani, akanitazama na kunambia, “Usijali, Kecie atapotelea msituni na kila mtu ataamini hilo.”
.
.
Sikujua amemaanisha nini, ila jua lilipokucha, nikastaajabu asubuhi ya mapema mlango ukigongwa. Nilipoenda kufungua nikakutana na Kecie mlangoni. Moyo wangu ulishtuka mno. Kwa muda nilijihisi nimepoteza nguvu. Sikuwa najua nini cha kufanya!
.
.
Kecie akazama ndani na kwenda kuketi kitini. Nikiwa katika hali ya bumbuwazi, mara mume wangu naye akaja. Naye akashangazwa sana kumwona Kecie, ila Kecie hakuonyesha muitikio wowote ule. Alikaa pale kitini kana kwamba mdoli.
.
.
Ni baada ya muda kidogo ndipo alinitazama na kuniomba nimletee mdoli wake aupendao. Nikampatia. Na asikae sana, akaenda zake nje. Sikuwa najua anaelekea wapi, nilitaka kumfuata lakini mume wangu akanikataza.
.
.
“Mwache aende. Huwezi jua anaelekea wapi.”
.
.
Ni siku hiyo ndiyo nikaja kuambiwa kuwa Kecie alipotelea kule msituni watu wakiwa wana ushahidi wa kuwa na Faris huko kama mtu wa mwisho.
.
.
Tukiwa na mashaka, tukaenda kutazama lile shimo lake. Ajabu tukalikuta halijafukuliwa, lipo vilevile kama ambavyo tulikuwa tumeliacha. Tukastaajabu alitokaje humo. Lakini pia tukapata shaka sana kuhusu yule mtoto ambaye alikuwa naye kwa mara ya mwisho, yaani Faris.
.
.
Tulijiuliza je atakuwa ameona chochote? Ajabu baadae tukaja sikia taarifa kuwa mtoto huyo amekuwa bubu tangu hapo. Hakuwa anaweza kuongea kabisa isipokuwa kubwatuka vitu ambavyo havieleweki, vitu ambavyo havina maana.
.
.
Ila …
.
.
Mrs Garett akanyamaza kidogo. Akashusha pumzi ndefu kwa pua yake ndefu alafu akajifuta mdomo wake na leso.
.
.
Yule mtoto, Mrs Garett akaendelea kuteta, atakuwa ameona kitu. Ni wazi kuna kitu alikiona. Anataka kusema lakini hawezi. Amekuwa wa ajabu tangu hapo. Amekuwa wa kufungiwa hata leo hii.
.
.
Tulitoa taarifa ya upoteaji wa Kecie. Matangazo yakawa yanabandikwa mara kwa mara lakini tukiwa tunajua kuwa ni bure, lengo lilikuwa ni kulaghai watu tu.
.
.
Lakini mbali na hayo, tangu Kecie alipopotelea, hatukumwona tena. Japo nilisumbuliwa na ndoto za ajabu mara kwa mara hapo karibuni, sikumwona tena mwanangu huyo. Alikuwa ameenda zake.
.
.
Mume wangu akaanza kupata kazi, tena akitafutwa. Ajabu ni kwamba kazi zote alizokuwa anapata zilikuwa ni za kufanya kazi kwenye viwanda vya mbao. Kila alipofanya kazi kwa muda mfupi, akawa anapandishwa nafasi na hata mshahara.
.
.
Maisha yakawa mazuri haswa. Hata hapa katikati tukawa tumemsahau kabisa Kecie, japo kila tulipokuwa tunafanya jitihada za kupata mtoto zikawa zinagonga mwamba. Mpaka leo hii hatujabahatika kupata mtoto, wala dalili. Ndipo tukaona ni vema kutafuta mtoto yeyote wa kukaa naye nyumbani.
.
.
Mrs Garett akamtazama Olivia.
.
.
Ndipo tukampata yule binti yatima, aitwa Oliva.
.
.
Padri Alfonso akasafisha koo lake na kuuliza, “Ina maana matendo uliyoyafanya ndiyo yanakusuta kuja kutubu?”
.
.
Mrs Garett akatikisa kichwa na kusema, “Huenda matendo hayo ningelikuwa nimeyasahau. Ila nilichokujia hapa, ni kikubwa zaidi ya kutubu, kikubwa zaidi ya matendo hayo…”
.
.
“Ni nini hicho?” Padri Alfonso akauliza.
.
.
“Padri,” akaita Mrs Garett. “Nahitaji msamaha kwa Muumba wangu. Lakini pia nahitaji msaada …”
.
.
“Sema nakuskiza,” Padri Alfonso akanguruma.
.
.
.
**
.
.
.
Saa mbili usiku …
.
.
Watu kadhaa walikuwa barabarani. Nyumba ziizokuwa zimepakana na barabara zilikuwa zimewashwa taa kuangazia nuru.
.
.
Wakiwa njiani kutoka kanisani, walikuta gari nje ya nyumba yao. Mrs Garett akasimama ghafla na kumtazama Olivia. “Usiongee kitu chochote, sawa?” akamwonya. Olivia akaitikia kwa kichwa kisha wakaendelea na safari yao iliyokomea mlangoni.
.
.
Walimkuta Mr Garett akiwa ameketi sebuleni, anavuta sigara. Mwanaume huyo alitulia sana kana kwamba hakuna watu walioingia. Kiti alichokuwa amekalia kilikuwa chaenda mbele na kurudi nyuma. Uso wake ulikuwa hauonekani kwa wepesi kwa kujaliwa na moshi wa sigara.
.
.
Mrs Garett akamsalimu, hakuitika. Mwanamke huyo akamtaka Olivia aende chumbani, Olivia akatii. Mrs Garett akaketi na kumtazama mumewe kwa sekunde kadhaa. Mr Garett akasimamisha kiti chake na kuzima sigara akiuliza, “Umetoka wapi?”
.
.
Uso wake haukuwa na lepe la masikhara. Macho yake yalikuwa mekundu, na mdomo wake uliotoka kunyonya sigara ulikuwa mkavu na mweusi.
.
.
“Nimetoka kanisani,” akasema Mrs Garett. Ghafla mumewe akanyanyua kisosi alimokuwa anakung’utia majivu ya sigara, akamrushia mkewe ghafula. Kama si Mrs Garett kukwepa, kisosi hicho kilikuwa kinapasua uso wake. Kilienda kwa kasi na kujibamiza ukutani. Kikapasuka kwenye vipandevipande milioni!
.
.
.
.
***
.
.
.
LAKO JICHO.
 
Duuhhh stori matata sana!kama naangalia series flani lakini sio zilizotafsiriwa
 
Steve tafadhali hii hadithi ni based on true story au ya kutunga.maana imekaa km true stori kabisa.
Leo hadi nimekumbuka kuna jamaa zamani tukiwa tunaangalia nae muvi anapata hisia akiamini kwamba yale ni maukweli kabisa!sasa na leo mi hii stori nataka nijue
 
*ROHO YAKE INADAI --- 07*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA
.
.
Mume wangu akashtuka sana. Ilikuwa ni kwasababu ya yule mtu aliyemkimbiza ndiyo maana akasahau. Tukapata sana maswali itakuaje, lakini mwishowe tukapuuzia, akinipa moyo kuwa kwasababu Kecie hayupo, basi mambo yatakuwa tu shwari.
.
.
Kumbe tulikuwa tumekosea kabisa kabisa, Alfonso …
.
.
ENDELEA
.
.
Mrs Garett akaweka kituo na kufuata machozi kwanza. Akameza mate na kutazama pembeni akiendelea kusema.
.
.
Basi kwakuwa tulikuwa tumekiuka kile tulichoambiwa na bwana Fringe, tukawa tunaishi kwa hofu kidogo labda pengine mambo yanaweza kukiuka, ila zikapita masiku pasipo jambo lolote kutukia. Tatizo lilikuwa tu kwamba, bado kwa upande wa mume wangu mambo yalikuwa yaleyale.
.
.
Hakuwa anapata kazi popote pale, maisha yalikuwa magumu magumu magumu. Ikafikia kipindi mume wangu akaniambia, mke wangu kwakuwa tulikosea yale masharti, basi tumfuate tena bwana yule tumweleze, labda anaweza kutusaidia. Sikuwa na lingine zaidi ya kumkubalia, akafunga safari na kesho yake akaja naye nyumbani.
.
.
Bwana yule akalalama sana kwa kufanyia uzembe jambo alilotuambia. Akasema kuwa yale yote tuliyoyafanya yalikuw bure, na basi kukata mzizi wa fitna, basi inabidi turudie tena lile swala upya. Lakini tutalirudiaje na wakati Kecie ameshakufa? Nikauliza.
.
.
Yule bwana, Fringe kwa jina, akatuambia ataongozana na sisi kwenda huko msituni, tumfukue Kecie na turejelee zoezi. Niliogopa sana, mosi kwenda msituni, pili kwenda kuona maiti. Nilihisi mwili umekuwa wa baridi, natetemeka kila kiungo, lakini … lakini sikuwa na machaguzi. Ilibidi nifanye tulichokubaliana.
.
.
Tukatoka majira ya saa tisa usiku tukiwa watatu. Nakumbuka siku hiyo mvua ilikuwa inanyesha sana. Baridi lilikuwa kali pia kiasi kwamba barafu zilikuwa zimejaa njiani.
.
.
Nikiwa nimejikunyata, tukaelekea huko msituni, siku hiyo hatukuwa tumebeba taa, wanaume wakachimba shimo na kumfukua Kecie. Mwili wake ulikuwa umejawa na udongo mweusi. Ulikuwa wa baridi mno kama barafu!
.
.
Yule bwana, Fringe, akaniambia niushike mwili huo, nami nikafanya vivyo. Akafungua mkoba wake na kutoa ile chupa yake ya kioo cha duara. Akaipangusa akisema maneno kadha wa kadha, mara ikaanza kuwaka ikiwa ya kijani! Akatutaka tuiwekee viganja chupa yake ile na kusema maneno aliyokuwa anayatamka.
.
.
Basi tukafanya vivyo, mwili wa Kecie ukazamishwa tena ndani ya shimo na mume wangu pamoja na bwana Fringe wakatenda kazi ya kuufukia. Walipomaliza, mume wangu akasema yale maneno ambayo bwana Fringe alimtaka ayatamke kisha kazi ikawa imeishia apo.
.
.
Ila kabla hatujaondoka, Bwana Fringe alituuliza, “Kuna yeyote aliyewaona wakati mnamzika Kecie mara ya kwanza?” mimi na mume wangu tukatazamana, akawahi kujibu, “Hapana. Hamna aliyetuona.”
.
.
Bwana Fringe akatabasamu, ila tabasamu lake lilinitisha zaidi. Mtu yule hakuwa wa kawaida. Kila nilipomtazama nilijikuta natetemeka kwa hofu. Na kila macho yangu yalipokutana na yake, nilihisi moyo wangu umesimama kwa muda. Sikuwa najua kwanini.
.
.
Alitutazama na kutuambia, kwa ajili ya usalama wetu, tutangaze kuwa Kecie amepotelea msituni. Haitakuwa hoja sana kwani watoto kadhaa huwa wanapotelea huko misituni. Lakini nilipata swali, watu wataaminije hilo kwa wepesi?
.
.
Bwana yule, Fringe, katika hali ya kustaajabisha akajua swali langu hilo kichwani, akanitazama na kunambia, “Usijali, Kecie atapotelea msituni na kila mtu ataamini hilo.”
.
.
Sikujua amemaanisha nini, ila jua lilipokucha, nikastaajabu asubuhi ya mapema mlango ukigongwa. Nilipoenda kufungua nikakutana na Kecie mlangoni. Moyo wangu ulishtuka mno. Kwa muda nilijihisi nimepoteza nguvu. Sikuwa najua nini cha kufanya!
.
.
Kecie akazama ndani na kwenda kuketi kitini. Nikiwa katika hali ya bumbuwazi, mara mume wangu naye akaja. Naye akashangazwa sana kumwona Kecie, ila Kecie hakuonyesha muitikio wowote ule. Alikaa pale kitini kana kwamba mdoli.
.
.
Ni baada ya muda kidogo ndipo alinitazama na kuniomba nimletee mdoli wake aupendao. Nikampatia. Na asikae sana, akaenda zake nje. Sikuwa najua anaelekea wapi, nilitaka kumfuata lakini mume wangu akanikataza.
.
.
“Mwache aende. Huwezi jua anaelekea wapi.”
.
.
Ni siku hiyo ndiyo nikaja kuambiwa kuwa Kecie alipotelea kule msituni watu wakiwa wana ushahidi wa kuwa na Faris huko kama mtu wa mwisho.
.
.
Tukiwa na mashaka, tukaenda kutazama lile shimo lake. Ajabu tukalikuta halijafukuliwa, lipo vilevile kama ambavyo tulikuwa tumeliacha. Tukastaajabu alitokaje humo. Lakini pia tukapata shaka sana kuhusu yule mtoto ambaye alikuwa naye kwa mara ya mwisho, yaani Faris.
.
.
Tulijiuliza je atakuwa ameona chochote? Ajabu baadae tukaja sikia taarifa kuwa mtoto huyo amekuwa bubu tangu hapo. Hakuwa anaweza kuongea kabisa isipokuwa kubwatuka vitu ambavyo havieleweki, vitu ambavyo havina maana.
.
.
Ila …
.
.
Mrs Garett akanyamaza kidogo. Akashusha pumzi ndefu kwa pua yake ndefu alafu akajifuta mdomo wake na leso.
.
.
Yule mtoto, Mrs Garett akaendelea kuteta, atakuwa ameona kitu. Ni wazi kuna kitu alikiona. Anataka kusema lakini hawezi. Amekuwa wa ajabu tangu hapo. Amekuwa wa kufungiwa hata leo hii.
.
.
Tulitoa taarifa ya upoteaji wa Kecie. Matangazo yakawa yanabandikwa mara kwa mara lakini tukiwa tunajua kuwa ni bure, lengo lilikuwa ni kulaghai watu tu.
.
.
Lakini mbali na hayo, tangu Kecie alipopotelea, hatukumwona tena. Japo nilisumbuliwa na ndoto za ajabu mara kwa mara hapo karibuni, sikumwona tena mwanangu huyo. Alikuwa ameenda zake.
.
.
Mume wangu akaanza kupata kazi, tena akitafutwa. Ajabu ni kwamba kazi zote alizokuwa anapata zilikuwa ni za kufanya kazi kwenye viwanda vya mbao. Kila alipofanya kazi kwa muda mfupi, akawa anapandishwa nafasi na hata mshahara.
.
.
Maisha yakawa mazuri haswa. Hata hapa katikati tukawa tumemsahau kabisa Kecie, japo kila tulipokuwa tunafanya jitihada za kupata mtoto zikawa zinagonga mwamba. Mpaka leo hii hatujabahatika kupata mtoto, wala dalili. Ndipo tukaona ni vema kutafuta mtoto yeyote wa kukaa naye nyumbani.
.
.
Mrs Garett akamtazama Olivia.
.
.
Ndipo tukampata yule binti yatima, aitwa Oliva.
.
.
Padri Alfonso akasafisha koo lake na kuuliza, “Ina maana matendo uliyoyafanya ndiyo yanakusuta kuja kutubu?”
.
.
Mrs Garett akatikisa kichwa na kusema, “Huenda matendo hayo ningelikuwa nimeyasahau. Ila nilichokujia hapa, ni kikubwa zaidi ya kutubu, kikubwa zaidi ya matendo hayo…”
.
.
“Ni nini hicho?” Padri Alfonso akauliza.
.
.
“Padri,” akaita Mrs Garett. “Nahitaji msamaha kwa Muumba wangu. Lakini pia nahitaji msaada …”
.
.
“Sema nakuskiza,” Padri Alfonso akanguruma.
.
.
.
**
.
.
.
Saa mbili usiku …
.
.
Watu kadhaa walikuwa barabarani. Nyumba ziizokuwa zimepakana na barabara zilikuwa zimewashwa taa kuangazia nuru.
.
.
Wakiwa njiani kutoka kanisani, walikuta gari nje ya nyumba yao. Mrs Garett akasimama ghafla na kumtazama Olivia. “Usiongee kitu chochote, sawa?” akamwonya. Olivia akaitikia kwa kichwa kisha wakaendelea na safari yao iliyokomea mlangoni.
.
.
Walimkuta Mr Garett akiwa ameketi sebuleni, anavuta sigara. Mwanaume huyo alitulia sana kana kwamba hakuna watu walioingia. Kiti alichokuwa amekalia kilikuwa chaenda mbele na kurudi nyuma. Uso wake ulikuwa hauonekani kwa wepesi kwa kujaliwa na moshi wa sigara.
.
.
Mrs Garett akamsalimu, hakuitika. Mwanamke huyo akamtaka Olivia aende chumbani, Olivia akatii. Mrs Garett akaketi na kumtazama mumewe kwa sekunde kadhaa. Mr Garett akasimamisha kiti chake na kuzima sigara akiuliza, “Umetoka wapi?”
.
.
Uso wake haukuwa na lepe la masikhara. Macho yake yalikuwa mekundu, na mdomo wake uliotoka kunyonya sigara ulikuwa mkavu na mweusi.
.
.
“Nimetoka kanisani,” akasema Mrs Garett. Ghafla mumewe akanyanyua kisosi alimokuwa anakung’utia majivu ya sigara, akamrushia mkewe ghafula. Kama si Mrs Garett kukwepa, kisosi hicho kilikuwa kinapasua uso wake. Kilienda kwa kasi na kujibamiza ukutani. Kikapasuka kwenye vipandevipande milioni!
.
.
.
.
***
.
.
.
LAKO JICHO.

Kecie anatia simanzi sana...

Roho yake imedhulumiwa ndiyo maana bado inatanga tanga...


Cc: mahondaw
 
Steve tafadhali hii hadithi ni based on true story au ya kutunga.maana imekaa km true stori kabisa.
Leo hadi nimekumbuka kuna jamaa zamani tukiwa tunaangalia nae muvi anapata hisia akiamini kwamba yale ni maukweli kabisa!sasa na leo mi hii stori nataka nijue
Nimeandika tu mkuu, ila kama utangulizi ulivyosema, haya hutukia pia.
 
Ila halahala, pengine story hii si kama uwazavyo kuwa.
 
*ROHO YAKE INADAI --- 08*

*Simulizi za Series za Steve*


ILIPOISHIA
.
.
“Nimetoka kanisani,” akasema Mrs Garett. Ghafla mumewe akanyanyua kisosi alimokuwa anakung’utia majivu ya sigara, akamrushia mkewe ghafula. Kama si Mrs Garett kukwepa, kisosi hicho kilikuwa kinapasua uso wake. Kilienda kwa kasi na kujibamiza ukutani. Kikapasuka kwenye vipandevipande milioni!
.
.
ENDELEA
.
.
“Nilikwambiaje kuhusu kwenda kanisani?” akafoka Mr Garett akinyanyuka. “Nakuuliza wewe mwanamke, nilikuambiaje kuhusu kwenda kanisani!”
.
.
Akamnyaka mkewe na kumtikisa kana kwamba dawa. Alimfokea na kumchapa makofi akimuuliza sababu ya yeye kwenda kanisani. Ilifikia kipindi Mrs Garett akajawa na damu usoni kwasababu ya kipigo, lakini bado hakusema kitu.
.
.
Mumewe akaendelea kumpiga mpaka pale alipoanza kupoteza fahamu, akamwacha hapo sebuleni kitini na kwenda zake chumbani. Mrs Garett akawa anaona hafifu kwa mbali. Macho yake yalijawa na kitu kama vile ukungu na masikio yake yalikuwa ni kana kwamba yametoka kupuliziwa sauti kali, akawa anasikia kwa mbali sauti ya kitu kama kucha kikikwaruza bati.
.
.
Akalia sana. Alisikia maumivu makali kichwani. Hakuweza hata kunyanyuka kwenda chumbani ikamlazimu alale papo hapo sebuleni akiwa amejikunyata kwa baridi.
.
.
Baada ya dakikaa kadhaa kupita, Olivia akaja kumjulia hali.
.
.
“Mama,” Olivia akaita. “Mama, upo sawa?”
.
.
Aliona uso wa mama yake ukiwa umezibwa na damu. Alikuwa anaogopa sana. Alimtazama kwa huruma na woga pia ndaniye.
.
.
“Mama, mama, mama,” akaendelea kuita akimsukumasukuma Mrs Garett. Alihofia huenda akawa amekufa basi machozi yakatawala macho yake.
.
.
“Mama, amka,” akalia. “Mama, mama!”
.
.
Mrs Garett akaitikia kwa mbali akiguna. Alimsikia Olivia kwa mbali sana. Alijaribu kufungua macho yake kumtazama mtoto huyo. Hakumwona vema. Alinyanyua mkono wake wa kuume na kuuweka shingoni mwa Olivia, akasema, “Usijali, Olivia. Niko sawa.”
.
.
Sauti yake ilikuwa ni ya kunong’ona, ila angalau ilimfariji Olivia. Hakurudi tena chumbani, akaamua kulala na mama yake palepale sebuleni mpaka asubuhi.
.
.
.
**
.
.
.
Saa nne asubuhi …
.
.
“Naweza kuingia ndani?” sauti iliulizia mlangoni. Ndani Dkt Hamill aliyekuwa anasoma kitabu akatazama mlango kwa jicho la nje ya vioo vya miwani kisha akairuhusu hodi hiyo kwa sauti yake ya kizee.
.
.
Mlango ukafunguka na Brian akaingia ndani.
.
.
“Brian!” Dkt Hamill akamkarimu kijana huyo. Akaweka kitabu chake pembeni na kumwelekezea kiti cha kuketi. Wakasalimiana.
.
.
“Samahani, Dkt Hamill. Nisingeweza kuja jana maana sikuwapo shule, nilipata udhuru nyumbani.”
.
.
“Ni sawa,” akasema Dkt Hamill kisha akavuta kitabu chake na kuendelea kusoma kana kwamba hamna mtu.
.
.
“Dokta,” akaita Brian. “Nimekuja …”
.
.
“Sawa,” akasema Dkt akiwa amegandisha macho yake kwenye kitabu.
.
.
“Ulikuwa na ahadi na mimi,” Brian akasema. “Unakumbuka?”
.
.
“Ndio, Brian,” akajibu Dkt Hamill. “Ila si leo, ilikuwa jana. Leo sina ratiba ya kuonana na mtu yeyote bali kusoma kitabu changu tu, Brian.”
.
.
“Tafadhali, Dkt. Sitakaa sana kukuibia muda wako. Naomba tu unisaidie kuniambia maana ya maneno yale niliyokuambia nami ntaondoka zangu.”
.
.
Dkt Hamill akamtazama Brian kwa macho ya nje ya kitabu, alafu akashusha pumzi ndefu na kuweka kitabu pembeni.
.
.
“Brian, najua uliniongopea siku ile juu ya wapi uliyatoa hayo maneno,” akasema akiwa amekumbatisha mikono yake. “Pengine hutaki kunambia, natumai hata na haya ntakayokwambia utayafanya kuwa siri. Au si hivyo, Brian?”
.
.
Brian akasita kidogo na kisha akasema, “Ndio, nitayafanya kuwa siri.”
.
.
Basi Dkt Hamill akatabasamu na kisha akalaza mgongo wake kwenye kiti. Akamtazama Brian kwa sekunde kadhaa na kumwambia, “Kwasababu umetaka kuyafahamu, basi n’takujuza … Ila, ni kheri ukachunga sana mdomo wako. Najua kwenu vijana ni ajabu na ni ngumu sana kufanya hilo. Punde mjuapo jambo, basi mwataka mji mzima ufahamu. Lah!
.
.
Si kila kitu ni cha kuwa bayana, Brian. Na naomba sana ushike hilo neno. Nimesemaje? …”
.
.
“Si kila kitu cha kuwa bayana, Dokta.”
.
.
“Sawasawa. Basi nami nitakueleza mambo hayo ya kale na ya kutisha. Na nitakueleza hayo kwa siku na siku, siwezi kuyamaliza yote kwa siku moja. Huenda si simulizi ndefu sana, ila ni kwasababu ya muda wangu. Sina muda wa kutosha. Hata haya nafanya kwakuwa wataka sana kufahamu.”
.
.
Aliposema hayo, akanyamaza kwa sekunde kadhaa. Akasafisha koo lake na kisha akatazama chini.
.
.
“Ni zamani sana ndani ya Boston. Bila shaka ni watu wachache sana walioshuhudia hayo wapo hai mpaka sasa. Hapa hakukuwa na watu wengi kiasi hiki cha leo. Kulikuwa na watu wachache hapa na pale na pia makazi.
.
.
Basi miongoni mwa familia hizo zilizokuwapo hapa, kulikuwa kuna familia moja ya kilatini ya bwana maarufu aliyekuwa anaitwa Hernandez Lorenzo, ama wengi wakimwita Helo kwa ufupi.
.
.
Bwana huyo alikuwa maarufu kwa michezo yake ya mazingaombwe katika eneo hili zima la Boston na hata Massachusetts nzima. Kila mtu alikuwa anampenda na kumtukuza. Banda lake lilikuwa linajaa kila mwisho wa wiki wa ajili ya kutumbuiza kiasi kwamba lilikuwa linatanuliwa kila mwisho wa mwezi kukidhi idadi ya watu.
.
.
Mitaani na hata huko barabarani watu wakawa wanaita jina lake. Helo! - Mtu wa maajabu!! Helo - Mtu wa maajabu!! Mtu huyo akavutia watu wengi sana kuja Boston, kumjua na hata kumfurahia. Familia yake ikawa maarufu sana, na si tu hivyo, wakawa matajiri sana.
.
.
Ila mambo yakaja kukengeuka punde baada ya jimbo hili kupata kiongozi mpya, Bwana Ralph Blacksmith. Mwanaume huyo aliyekuwa na kariba ya ukali na mpenda mabadiliko ya haraka, alitangaza ya kwamba hakuna mambo yoyote ya kiudanganyifu na kiutapeli yatakayofanyika ndani ya jimbo lake hili. Na swala hilo halikuishia hapo tu, bali likawekwa na kuidhinishwa mpaka kwenye mfumo wa sheria.
.
.
Jambo si kwamba watu walikuwa wanapenda udanganyifu na kutapeliwa, lah! Ila vipi kuhusu mazingaombwe ya Bwana Helo? Wakajiuliza. Je yale nayo yalikuwa udanganyifu na utapeli?
.
.
Kujibiwa hilo, katika hali ya kustaajabisha, siku moja maafisa wa serikali wakajaa wengi kwenye nyumba ya Bwana Helo. Wakaangusha banda lake pasipo huruma, na Helo akapewa onyo kali kuwa inambidi afanye kazi halali kujiingizia kipato na si utapeli na udanganyifu!
.
.
Akasononeka sana. Haikujalisha aliomba namna gani, hakusikika na hakuna mtu aliyemjali. Lakini kama kuna kitu ambacho watu walikuwa hawakijui, Helo hakuwa tapeli wala mdanganyifu. Yote aliyokuwa anayafanya kwenye banda lake, hayakuwa udanganyifu hata kidogo, bali uchawi!
.
.
Familia ya wakina Helo ilikuwa ya kichawi kutokea huko Amerika ya kusini. Hakuna aliyekuwa anajua hilo kipindi hicho. Ulozi ulikuwa umekatazwa kabisa ndani ya jimbo na kwa mtu yeyote aliyekuwa amebainika kujihusisha nao, adhabu yake ilikuwa ni kukamatwa na kuchomwa mbele ya kadamnasi ya watu!
.
.
Basi kwasababu ya kukatazwa kwa mambo ya mazingaombwe, familia ya bwana Helo ikafilisika sana. Wakawa mafukara na kituko ndani ya jij. Kila walipopita wakanyooshewa kidole, wengine wakisanifu na wengine wakihuzunika.
.
.
Maisha yalibadilika ghafla! Kutoka kwenye shujaa mpaka tapeli wa Massachusetts. Kutoka kwenye umaarufu mpaka kujificha kwenye miti na ndani vyumbani.
.
.
Hali hii ikadumu kwa mwaka mmoja tu. Fedheha, lawama, dharau zikachosha familia hii. Walitaraji mambo yangekuwa sawa, lakini pengine ilionekana ingechukua muda mrefu kuwa vivyo. Sasa Helo na familia yake wakaanza kuonyesha kucha na rangi zao halisi.
.
.
Wakaapia kuwavuta kwenye fedheha na aibu wale wote waliokuwa wanawataka wao waishi kwenye shimo hilo. Basi mmoja mmoja akawa anakufa kila uchwao. Hali hii ikatisha sana Boston na hata Massachusetts nzima. Walipokuja kugundua ni Halo na familia yake wafanya vivyo, wakachoma nyumba yao. Wakawakamata na kuwachoma moto mbele ya hadhira.
.
.
Huo ukawa mwisho wa Halo na familia yake. Nyumba yake, iliyokuwa imebakia kuwa ghofu, ikatengwa na hata mpaka sasa imebakia huko ndani ya misitu ikiwa pweke.
.
.
Lakini kabla Helo hajafa, wakati moto wamuunguza kula mwili wake, alilia sana na kusema kuwa atarudi kulipiza kisasi. Alikuwa anaamini hakuwa na makosa, aliishi kwa upendo wote na wakazi wa Boston na Massachusetts nzima kabla ya wao kukengeuka.
.
.
Neno lake la mwisho alilitamka kwa kilatini akisema wote mtakuwa wangu. Wote mtasujudia miguuni mwangu. Majivu yake yalienda kutupwa huko msituni na toka siku hiyo mpaka leo hii Helo akageuka kuwa historia ya kuwasimulia watu.
.
.
Ni wachache sana waliojali yale maneno yake aliyoyasema wakati anakufa. Ila Helo alisema ukweli. Atarudi tena kwenye mji huu na atafanya kila mtu awe wake.”
.
.
Brian alikuwa ameachama mdomo wake wazi akiskiza mpaka hapo mwisho. Alipoufumba akauliza, “Ina maana yale maneno maana yake ni ‘Helo, kuwa wangu!’ kwa kilatini?”
.
.
“Ndio,” akajibu Dokta, “Hiyo ndiyo maana yake, ndiyo maana nikashangazwa sana na mahali ulipoyatolea hayo maneno. Ebu niambie uliyasikia wapi? Kuwa mkweli, pengine naweza kukusadia.”
.
.
Dkt Hamill alimtazama Brian kwa macho ya kidadisi na hamu. Kabla Brian hajatia neno, akamuuliza, “Umeyasikia maneno hayo ndotoni au msituni?”
.
.
.
.
****
.
.
LAKO JICHO.
 
*ROHO YAKE INADAI ---- 09*

*Simulizi za Series*


ILIPOISHIA
.
.
“Ndio,” akajibu Dokta, “Hiyo ndiyo maana yake, ndiyo maana nikashangazwa sana na mahali ulipoyatolea hayo maneno. Ebu niambie uliyasikia wapi? Kuwa mkweli, pengine naweza kukusadia.”
.
.
Dkt Hamill alimtazama Brian kwa macho ya kidadisi na hamu. Kabla Brian hajatia neno, akamuuliza, “Umeyasikia maneno hayo ndotoni au msituni?”
.
.
ENDELEA
.
.
“Sijayasikia huko,” Brian akatikisa kichwa chake. “Ni kutoka kwa rafiSki yangu anaitwa Faris. Yeye amekuwa mgonjwa hivi sasa, hawezi kusema jambo lolote akaeleweka. Niliona akiwa ameandika maneno hayo kwenye kingo yake ya kitanda!”
.
.
Dkt akanyamaza asitie neno. Aliminya tu lips zake na kuendelea kumtazama Brian.
.
.
“Dokta,” Brian akaita. “Waweza kunambia maana yake ni nini? Kwanini ameandika maneno hayo?”
.
.
Dokta akameza kwanza mate, kisha akamwambia Brian, “Muda wangu umekwisha. Sina muda tena wa kuongea na wewe. Tuonane kesho majira haya, sawa?”
.
.
“Lakini Dokta,” Brian akataka kuongea. Dkt Hamill akamzuia na kumkumbusha makubaliano yao ya mwanzoni kuwa maongezi hayo ni marefu na vivyo hatoyamaliza yote kwa siku moja. Basi Brian, kishingo upande, akanyanyuka na kuuendea mlango. Dokta akamkumbusha, “Usisahau kuja kesho. Uwe ndani ya muda.”
.
.
Akatikisa kichwa chake kuitikia na kisha akaenda zake. Siku hiyo alikuwa amegundua kitu kikubwa lakini kilichompa hofu zaidi. Alijikuta akitaka kufahamu zaidi kuhusu Halo, na je kuna mahusiano gani kati ya Halo na Faris? Na labda kupotea kwa Kecie msituni?
.
.
Wakati anajiuliza hayo akaona ni vema kama asipomficha kitu Dkt Hamill. Inabidi amweke wazi, labda atakuwa anfahamu kila shaka alilo nalo kichwani. Basi akaapa kesho yake atakapopata fursa ya kuonana na Dkt Hamill atahakikisha analifanyia kazi shauri lake.
.
.
Alipofika nyumbani, baada ya kula na kupumzika kidogo, akatoka pasipo kuaga. Akaenda nyumbani kwa Brewster, mwanaume mzee ambaye alimweleza mama yake juu ya safari yake ya kwenda nyumbani kwa wakina Faris, na pia kumtahadharisha asifanye tena hilo jambo.
.
.
Alitumai atapata mawili matatu kwa mzee huyo. Alikuwa na maswali kadhaa ya kumuuliza.
.
.
Basi kwa mwendo wa robo saa, akawa amefika nyumbani kwa mzee huyo. Ilikuwa ni nyumba ndogo iliyojitenga. Kulikuwa ni kimya sana. Nje ya nyumba kulikuwa kumejawa na majani makavu ya miti. Kibaraza hakikuwa kisafi, pia na vioo vilikuwa vimebadilisha rangi.
.
.
Juu ya paa kulikuwa na kunguru wawili wakimtazama Brian kwa macho ya pembeni kabla hawajalia mara mbili na kupeperusbha mbawa zao.
.
.
“... kuna yeyote ndani?” Brian aliita baada ya kugonga mara tano pasipo majibu. Aliacha kugonga akazunguka nyuma ya nyumba. Huko akakuta banda la nguruwe wawili wadogo. Akapumbazwa kuwatazama rangi zao na namna wanavyokula kwa kufakamia. Ila ghafla akasikia sauti kavu nyuma yake.
.
.
“Hey! We mvulana.”
.
.
Alipogeuka akamwona Brewster. Alikuwa amevalia shati refu na suruali pana. Uso wake ulikuwa mtulivu ila macho yake ya kizee ameyakodoa. Mashavu yake yaliyoanza kudondoka yalikuwa yamemezwa na vinyweleo vya ndevu vilivyosimama. Mdomo wake mwembamba ulikuwa unaonekana kwa hafifu kwasababu ya mustachi.
.
.
“We ni nani na unafanya nini hapo kwa nguruwe wangu?” akauliza Brewster. Brian akamsogelea na kujitambulisha, akamwambia ya kwamba amekuja kumtembelea kwani kuna maneno mawili matatu anataka kuyaongea naye.
.
.
“Ni wewe, Brian!” akastaajabu Brewster. Alikuwa ana tatizo la kuona mbali hivyo Brian alivyosogea karibu na kuongea ndipo akamtambua.
.
.
“Ila sina miadi na wewe,” akasema Brewster. “Pia sina cha kuteta na wewe. Nadhani mama yako alikuambia kila unachostahili kujua, mvulana.”
.
.
“Hapana,” akasema Brian. “Hakuniambia kila ninachokitaka zaidi ya kunipa vitisho. Nataka kujua kwanini? … ulinionaje?”
.
.
Brewster akanyamaza kwa muda. Akamtazama Brian kwa sekunde kadhaa kisha akamsogelea karibu na kuinamisha kichwa chake amtazame machoni. Brewster alikuwa mrefu kuliko Brian, kwahivyo alipofanya vivyo wakawa sawa. Uso wake wa kizee haukuwa unavutia. Macho yake yaliyoanza kufifia kiini yalitazama macho ya Brian na kisha akasema, “Kuna ambacho haukuelewa? … si kila kitu kimejawa na maswali, Brian. Muda mwingine kuwa mwerevu ni kufanya unachoambiwa pasipo kutia mashaka. Ni faida kwako … lakini tu kama unahitaji roho yako.”
.
.
“Kwanini unasema hivyo?” Brian akauliza. “Kwani kuna nini?”
.
.
“Kuna kifo,” akajibu Brewster. “Huko nyuma ya maswali na kutaka kwako kutafutia majibu … kuna kifo. Ni juu yako kuchagua, aidha maisha ama kifo.”
.
.
Brewster aliposema hayo, akaenda zake Brian akimtazama. Alipopiga hatua nane, akageuka na kumtazama Brian. Akamwambia, “Nenda nyumbani. Usifanye jambo lolote la kijinga.”
.
.
Mzee huyo akaenda zake asigeuke tena. Brian akabakia akisimama, akitazama huku na kule, na hatimaye akaenda zake. Alipitia kwa rafiki yake fulani kisha ndiyo akaenda nyumbani. Ilikuwa ni majira ya jioni ya saa moja sasa. Akamkuta mamaye akiandaa chakula cha usiku.
.
.
Akaketi sebuleni na kulaza kichwa chake kwenye kiti akitafakari siku yake nzima. Alitamani kumshirikisha mama yake lakini alihofia. Alishamkataza kuhangaika na mambo hayo, basi akawa anahangaika mwenyewe akipanga na kupangua vipande vya ‘pazo’.
.
.
“Amekuambia chochote?” sauti ya mama yake ikamshtua.
.
.
“Nani?” akauliza.
.
.
“Kwani umetoka wapi? Si kwa Brewster?”
.
.
“Umejuaje kama nimetoka huko?” Brian akauliza akiketi vema kitini kumtazama mama yake aliyekuwa amesimama hatua kadhaa toka kwake.
.
.
“Amekuja hapa kunambia.”
.
.
“Nani? Brewster?”
.
.
“Ndio. Amekuja hapa akaniambia ulienda kumwona.”
.
.
“Saa ngapi?”
.
.
“Si muda mrefu tangu uondoke. Vipi amekuambia kitu?”
.
.
Kabla Brian hajajibu, alikabwa na mawazo. Brewster amewezaje kufika hapo muda mfupi baada ya yeye kuondoka. Amefanya hilo kwa kasi gani? Mama yake alimshtua kwa kurejea kumuuliza, “Amekuambia nini?”
.
.
“Hajaniambia kitu … hamna kitu alichoniambia,” alimalizia akitikisa kichwa. “Wewe amekuambia nini?” akauliza.
.
.
Mama akaketi na kumtazama Brian, akasema, “Amenisisitizia uache kuyafuatilia hayo mambo.”
.
.
Brian akasonya na kunyanyuka. “Kuna siku utaniambia mambo mengine zaidi ya hilo?” akaenda zake chumbani na kubamiza mlango.
.
.
.
**
.
.
.
“Karibu,” alisema Mrs Garett akiufungua mlango kumkaribisha Padri Alfonso. Padri huyo alikuwa amevalia shati jeusi alilolichomekea vema, shingoni lilikuwa na doa jeupe. Mkono wake wa kuume alikuwa amebebelea Biblia ya zamani.
.
.
“Ahsante,” akasema kwa tabasamu, akazama ndani na kuketi kwenye kiti. Naye Mrs Garett akaketi akimwita Olivia ambaye alimwagiza alete chai kwa ajili ya mgeni.
.
.
Padri akautazama uso wa Mrs Garett uliokuwa umeharibika kwa majeraha, akamuuliza mwanamke huyo, “Ni mume wako?”
.
.
Mrs Garett akatikisa kichwa pasipo kutia neno. Macho yake yalikuwa mekundu, mdomo wake ulikuwa umevimba na upande wa juu wa shavu lake la kushoto kulikuwa kumevilia damu.
.
.
“Pole sana.”
.
.
“Nashukuru, usijali,” Mrs Garett akasema akijitahidi kutabasamu.
.
.
“Yupo wapi sasa?”
.
.
“Ameondoka. Alisema anasafiri hivyo atarejea kesho asubuhi.”
.
.
Padri akatikisa kichwa. Baada ya muda mfupi mlango ukagongwa, akaingia mwanadada aliyekuwa amevalia sare ya mtawa wa kike rangi nyeusi na nyeupe. Mwanamke huyo mrefu mwembamba alikuwa amebebelea chupa mkononi mwake na sanamu ya msalaba yenye ukubwa wa wastani.
.
.
“Anaitwa dada Magdalena. Tutakuwa naye kwa ajili ya sala,” alisema Padri. Mrs Garett akaagiza chai kwa ajili ya dada huyo.
.
.
“Karibu sana, dada.”
.
.
“Ahsante, nimekaribia.”
.
.
“Nimefurahi sana kuja kunitembelea, natumai tatizo langu litakoma.”
.
.
“Kwa uweza wa Mungu, litawezekana,” akasema Padri Alfonso. “Natumai tukitoka hapa, roho hiyo haitarudi tena kwenye makazi haya. Itakuwa mwanzo na mwisho!”
.
.
Basi baada ya maongezi hayo mafupi, mazingira yakaanza kuandaliwa kwa ajili ya sala. Olivia alikuja sebuleni, taa zikazimwa na mishumaa ikawasha na ile sanamu ya msalaba ikasimamishwa mezani.
.
.
Dada Magdalena akachovya mkono kwenye maji yaliyokuwa ndani ya chupa na kukung’utia kwenye kila kona ya sebule akiteta maneno kadha wa kadha ya sala. Baada ya hapo akaungana na Padri Alfonso kuanza kusali, Mrs Garett pamoja na Olivia wakifuatisha yale yaliyokuwa yanatamkwa.
.
.
Wakasali kwa takribani nusu saa. Wakiwa wanaendelea kufanya vivyo, Olivia akafungua macho yake na kuangaza. Akatupa macho yake huku na kule kana kwamba mtu anayehisi kitu.
.
.
Mbali na sauti ya sala, kuna sauti nyingine alikuwa anaisikia kwa mbali sikioni mwake ikinong’oneza. Sauti ya mtoto wa kike. Sauti ikimwita jina lake.
.
.
“Oliiviaaaa … Oliiviaaaa … njoo kwangu. Oliviaaaa … Oliviaaaa …. Njoo kwa …”
.
.
Mara akamwona binti mdogo mlangoni! Binti huyo alikuwa ameshikilia mdoli mkono wake wa kuume. Alikuwa anamtazama Olivia kwa macho makali na kinywa chake amekiachama.
.
.
Akaanza kupiga hatua kumsogelea Olivia. Hatua zake zilikuwa nzito kinyume kabisa na mwili wake. Kila alipokanyaga chini ilisikika tih! Tih! Tih!
.
.
Olivia akajawa na woga mkubwa, akapiga kelele kali sana na kumshtua kila mtu!
.
.
.
**
.
.
.
LAKO JICHO.
 
*ROHO YAKE INADAI ---- 09*

*Simulizi za Series*


ILIPOISHIA
.
.
“Ndio,” akajibu Dokta, “Hiyo ndiyo maana yake, ndiyo maana nikashangazwa sana na mahali ulipoyatolea hayo maneno. Ebu niambie uliyasikia wapi? Kuwa mkweli, pengine naweza kukusadia.”
.
.
Dkt Hamill alimtazama Brian kwa macho ya kidadisi na hamu. Kabla Brian hajatia neno, akamuuliza, “Umeyasikia maneno hayo ndotoni au msituni?”
.
.
ENDELEA
.
.
“Sijayasikia huko,” Brian akatikisa kichwa chake. “Ni kutoka kwa rafiSki yangu anaitwa Faris. Yeye amekuwa mgonjwa hivi sasa, hawezi kusema jambo lolote akaeleweka. Niliona akiwa ameandika maneno hayo kwenye kingo yake ya kitanda!”
.
.
Dkt akanyamaza asitie neno. Aliminya tu lips zake na kuendelea kumtazama Brian.
.
.
“Dokta,” Brian akaita. “Waweza kunambia maana yake ni nini? Kwanini ameandika maneno hayo?”
.
.
Dokta akameza kwanza mate, kisha akamwambia Brian, “Muda wangu umekwisha. Sina muda tena wa kuongea na wewe. Tuonane kesho majira haya, sawa?”
.
.
“Lakini Dokta,” Brian akataka kuongea. Dkt Hamill akamzuia na kumkumbusha makubaliano yao ya mwanzoni kuwa maongezi hayo ni marefu na vivyo hatoyamaliza yote kwa siku moja. Basi Brian, kishingo upande, akanyanyuka na kuuendea mlango. Dokta akamkumbusha, “Usisahau kuja kesho. Uwe ndani ya muda.”
.
.
Akatikisa kichwa chake kuitikia na kisha akaenda zake. Siku hiyo alikuwa amegundua kitu kikubwa lakini kilichompa hofu zaidi. Alijikuta akitaka kufahamu zaidi kuhusu Halo, na je kuna mahusiano gani kati ya Halo na Faris? Na labda kupotea kwa Kecie msituni?
.
.
Wakati anajiuliza hayo akaona ni vema kama asipomficha kitu Dkt Hamill. Inabidi amweke wazi, labda atakuwa anfahamu kila shaka alilo nalo kichwani. Basi akaapa kesho yake atakapopata fursa ya kuonana na Dkt Hamill atahakikisha analifanyia kazi shauri lake.
.
.
Alipofika nyumbani, baada ya kula na kupumzika kidogo, akatoka pasipo kuaga. Akaenda nyumbani kwa Brewster, mwanaume mzee ambaye alimweleza mama yake juu ya safari yake ya kwenda nyumbani kwa wakina Faris, na pia kumtahadharisha asifanye tena hilo jambo.
.
.
Alitumai atapata mawili matatu kwa mzee huyo. Alikuwa na maswali kadhaa ya kumuuliza.
.
.
Basi kwa mwendo wa robo saa, akawa amefika nyumbani kwa mzee huyo. Ilikuwa ni nyumba ndogo iliyojitenga. Kulikuwa ni kimya sana. Nje ya nyumba kulikuwa kumejawa na majani makavu ya miti. Kibaraza hakikuwa kisafi, pia na vioo vilikuwa vimebadilisha rangi.
.
.
Juu ya paa kulikuwa na kunguru wawili wakimtazama Brian kwa macho ya pembeni kabla hawajalia mara mbili na kupeperusbha mbawa zao.
.
.
“... kuna yeyote ndani?” Brian aliita baada ya kugonga mara tano pasipo majibu. Aliacha kugonga akazunguka nyuma ya nyumba. Huko akakuta banda la nguruwe wawili wadogo. Akapumbazwa kuwatazama rangi zao na namna wanavyokula kwa kufakamia. Ila ghafla akasikia sauti kavu nyuma yake.
.
.
“Hey! We mvulana.”
.
.
Alipogeuka akamwona Brewster. Alikuwa amevalia shati refu na suruali pana. Uso wake ulikuwa mtulivu ila macho yake ya kizee ameyakodoa. Mashavu yake yaliyoanza kudondoka yalikuwa yamemezwa na vinyweleo vya ndevu vilivyosimama. Mdomo wake mwembamba ulikuwa unaonekana kwa hafifu kwasababu ya mustachi.
.
.
“We ni nani na unafanya nini hapo kwa nguruwe wangu?” akauliza Brewster. Brian akamsogelea na kujitambulisha, akamwambia ya kwamba amekuja kumtembelea kwani kuna maneno mawili matatu anataka kuyaongea naye.
.
.
“Ni wewe, Brian!” akastaajabu Brewster. Alikuwa ana tatizo la kuona mbali hivyo Brian alivyosogea karibu na kuongea ndipo akamtambua.
.
.
“Ila sina miadi na wewe,” akasema Brewster. “Pia sina cha kuteta na wewe. Nadhani mama yako alikuambia kila unachostahili kujua, mvulana.”
.
.
“Hapana,” akasema Brian. “Hakuniambia kila ninachokitaka zaidi ya kunipa vitisho. Nataka kujua kwanini? … ulinionaje?”
.
.
Brewster akanyamaza kwa muda. Akamtazama Brian kwa sekunde kadhaa kisha akamsogelea karibu na kuinamisha kichwa chake amtazame machoni. Brewster alikuwa mrefu kuliko Brian, kwahivyo alipofanya vivyo wakawa sawa. Uso wake wa kizee haukuwa unavutia. Macho yake yaliyoanza kufifia kiini yalitazama macho ya Brian na kisha akasema, “Kuna ambacho haukuelewa? … si kila kitu kimejawa na maswali, Brian. Muda mwingine kuwa mwerevu ni kufanya unachoambiwa pasipo kutia mashaka. Ni faida kwako … lakini tu kama unahitaji roho yako.”
.
.
“Kwanini unasema hivyo?” Brian akauliza. “Kwani kuna nini?”
.
.
“Kuna kifo,” akajibu Brewster. “Huko nyuma ya maswali na kutaka kwako kutafutia majibu … kuna kifo. Ni juu yako kuchagua, aidha maisha ama kifo.”
.
.
Brewster aliposema hayo, akaenda zake Brian akimtazama. Alipopiga hatua nane, akageuka na kumtazama Brian. Akamwambia, “Nenda nyumbani. Usifanye jambo lolote la kijinga.”
.
.
Mzee huyo akaenda zake asigeuke tena. Brian akabakia akisimama, akitazama huku na kule, na hatimaye akaenda zake. Alipitia kwa rafiki yake fulani kisha ndiyo akaenda nyumbani. Ilikuwa ni majira ya jioni ya saa moja sasa. Akamkuta mamaye akiandaa chakula cha usiku.
.
.
Akaketi sebuleni na kulaza kichwa chake kwenye kiti akitafakari siku yake nzima. Alitamani kumshirikisha mama yake lakini alihofia. Alishamkataza kuhangaika na mambo hayo, basi akawa anahangaika mwenyewe akipanga na kupangua vipande vya ‘pazo’.
.
.
“Amekuambia chochote?” sauti ya mama yake ikamshtua.
.
.
“Nani?” akauliza.
.
.
“Kwani umetoka wapi? Si kwa Brewster?”
.
.
“Umejuaje kama nimetoka huko?” Brian akauliza akiketi vema kitini kumtazama mama yake aliyekuwa amesimama hatua kadhaa toka kwake.
.
.
“Amekuja hapa kunambia.”
.
.
“Nani? Brewster?”
.
.
“Ndio. Amekuja hapa akaniambia ulienda kumwona.”
.
.
“Saa ngapi?”
.
.
“Si muda mrefu tangu uondoke. Vipi amekuambia kitu?”
.
.
Kabla Brian hajajibu, alikabwa na mawazo. Brewster amewezaje kufika hapo muda mfupi baada ya yeye kuondoka. Amefanya hilo kwa kasi gani? Mama yake alimshtua kwa kurejea kumuuliza, “Amekuambia nini?”
.
.
“Hajaniambia kitu … hamna kitu alichoniambia,” alimalizia akitikisa kichwa. “Wewe amekuambia nini?” akauliza.
.
.
Mama akaketi na kumtazama Brian, akasema, “Amenisisitizia uache kuyafuatilia hayo mambo.”
.
.
Brian akasonya na kunyanyuka. “Kuna siku utaniambia mambo mengine zaidi ya hilo?” akaenda zake chumbani na kubamiza mlango.
.
.
.
**
.
.
.
“Karibu,” alisema Mrs Garett akiufungua mlango kumkaribisha Padri Alfonso. Padri huyo alikuwa amevalia shati jeusi alilolichomekea vema, shingoni lilikuwa na doa jeupe. Mkono wake wa kuume alikuwa amebebelea Biblia ya zamani.
.
.
“Ahsante,” akasema kwa tabasamu, akazama ndani na kuketi kwenye kiti. Naye Mrs Garett akaketi akimwita Olivia ambaye alimwagiza alete chai kwa ajili ya mgeni.
.
.
Padri akautazama uso wa Mrs Garett uliokuwa umeharibika kwa majeraha, akamuuliza mwanamke huyo, “Ni mume wako?”
.
.
Mrs Garett akatikisa kichwa pasipo kutia neno. Macho yake yalikuwa mekundu, mdomo wake ulikuwa umevimba na upande wa juu wa shavu lake la kushoto kulikuwa kumevilia damu.
.
.
“Pole sana.”
.
.
“Nashukuru, usijali,” Mrs Garett akasema akijitahidi kutabasamu.
.
.
“Yupo wapi sasa?”
.
.
“Ameondoka. Alisema anasafiri hivyo atarejea kesho asubuhi.”
.
.
Padri akatikisa kichwa. Baada ya muda mfupi mlango ukagongwa, akaingia mwanadada aliyekuwa amevalia sare ya mtawa wa kike rangi nyeusi na nyeupe. Mwanamke huyo mrefu mwembamba alikuwa amebebelea chupa mkononi mwake na sanamu ya msalaba yenye ukubwa wa wastani.
.
.
“Anaitwa dada Magdalena. Tutakuwa naye kwa ajili ya sala,” alisema Padri. Mrs Garett akaagiza chai kwa ajili ya dada huyo.
.
.
“Karibu sana, dada.”
.
.
“Ahsante, nimekaribia.”
.
.
“Nimefurahi sana kuja kunitembelea, natumai tatizo langu litakoma.”
.
.
“Kwa uweza wa Mungu, litawezekana,” akasema Padri Alfonso. “Natumai tukitoka hapa, roho hiyo haitarudi tena kwenye makazi haya. Itakuwa mwanzo na mwisho!”
.
.
Basi baada ya maongezi hayo mafupi, mazingira yakaanza kuandaliwa kwa ajili ya sala. Olivia alikuja sebuleni, taa zikazimwa na mishumaa ikawasha na ile sanamu ya msalaba ikasimamishwa mezani.
.
.
Dada Magdalena akachovya mkono kwenye maji yaliyokuwa ndani ya chupa na kukung’utia kwenye kila kona ya sebule akiteta maneno kadha wa kadha ya sala. Baada ya hapo akaungana na Padri Alfonso kuanza kusali, Mrs Garett pamoja na Olivia wakifuatisha yale yaliyokuwa yanatamkwa.
.
.
Wakasali kwa takribani nusu saa. Wakiwa wanaendelea kufanya vivyo, Olivia akafungua macho yake na kuangaza. Akatupa macho yake huku na kule kana kwamba mtu anayehisi kitu.
.
.
Mbali na sauti ya sala, kuna sauti nyingine alikuwa anaisikia kwa mbali sikioni mwake ikinong’oneza. Sauti ya mtoto wa kike. Sauti ikimwita jina lake.
.
.
“Oliiviaaaa … Oliiviaaaa … njoo kwangu. Oliviaaaa … Oliviaaaa …. Njoo kwa …”
.
.
Mara akamwona binti mdogo mlangoni! Binti huyo alikuwa ameshikilia mdoli mkono wake wa kuume. Alikuwa anamtazama Olivia kwa macho makali na kinywa chake amekiachama.
.
.
Akaanza kupiga hatua kumsogelea Olivia. Hatua zake zilikuwa nzito kinyume kabisa na mwili wake. Kila alipokanyaga chini ilisikika tih! Tih! Tih!
.
.
Olivia akajawa na woga mkubwa, akapiga kelele kali sana na kumshtua kila mtu!
.
.
.
**
.
.
.
LAKO JICHO.

Mara nyingi sana penye sala au maombi, roho zinazotanga tanga hukimbia mahali hapo...

Ila huyu mtoto ni roho inayotanga ila bado haina wasi wasi na maombi yanaoyendelea hapo...

Kazi ipo...

Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom