Simulizi: Roho yake inadai

Simulizi: Roho yake inadai

Hii stori na za shigongo ni kama baskeli ya chuma na baskeli yA miti.steve uko vizuri
Stori za Shigongo zinatusaidia sana kipindi tukiwa na arosto Kali.Hata wale jamaa zetu wa imani nyingine ,wakizidiwa na nja wanaruhusiwa kula kitimoto Ila wasishibe.
 
*ROHO YAKE INADAI --- 04*

*Simulizi za Series za Steve*


ILIPOISHIA

“Lipi hilo?” Dkt akauliza. Brian akamtajia yale maneno aliyoyasoma toka kwenye kingo ya kitanda cha Faris. Dkt akamuuliza akimkazia macho, “Umeyaona wapi hayo maneno?”

ENDELEA

Brian akafikiria kidogo. Pengine hakuona tabu yoyote kuhusu hayo maneno lakini muitikio wa Dkt Hamill ukamfanya apate mashaka. Dkt aliyekuwa katika mpango wa kuondoka, akarejea na kusimama mbele ya Brian kungoja majibu.

“Niliona tu mahali,” akajibu Brian. Hakutaka kusema uhalisia kwa kuhofia pengine anaweza kujikuta amemwingiza Faris na familia yake kwenye matatizo.

Dkt akaketi juu ya meza, kisha akauliza kwa sauti ya upole, “Unaitwa nani kijana?”

“Brian Woodgate.”

“Brian,” Dkt akaita. Alikuwa anamtazama Brian kwa macho ya umakini. “Kuwa muwazi, sawa? Sina mpango wa kukudhuru bali kukusaidia … umeyaona wapi hayo maneno?”

“Kwenye kitabu,” Brian akajibu.
“Hakuna maneno hayo kwenye kitabu changu,” akasema Dkt Hamill.

“Si kwenye kitabu chako,” Brian akajitetea. “Ni kitabu kingine kabisa nilichokutana nacho kule maktaba.”

“Una uhakika?” Dkt akauliza akifinya ndita.

“Ndio,” Brian akajibu akitazama chini. Dkt akatazama saa yake ya mkononi kisha akanyanyuka na kusema, “Muda wangu wa kuwapo hapa umekwisha. Nina kazi nyingi za kufanya nyumbani kwangu. Kama hutojali, kesho majira ya saa tano asubuhi, ufike ofisini, tutaongea mambo kadhaa.”

Dkt akaondoka zake na kumwacha Brian akiwa mpweke darasani. Akiwa na mawazo kadhaa juu ya maneno yale ya Faris na namna ambavyo Dkt alivyoyapokea. Naye hakudumu muda, akaweka begi lake mgongoni na kwenda zake nyumbani.


**

Saa mbili usiku …

Brian alikuwa na mama yake sebuleni mahali pa kupatia chakula. Mbali na sauti ndogo ya redio iliyokuwa inasikika kwa mbali, hakukuwa na sauti nyingine kubwa zaidi ya midomo inayotafuna.

Walipomaliza kula, mama alitoa vyombo, na kabla Brian hajaondoka mama akamweleza kuwa kuna jambo anataka kuongea naye, basi akangoja kitini wakati mama anamalizia kazi kadhaa jikoni. Kichwani mwake akijaribu kubashiri ni kitu gani ambacho mama anataka kumweleza.

Hapa akajikuta akili yake yote inakimbilia kwa Wayde. Pengine baba wa binti huyo atakuwa amekuja kumweleza mama yake kuhusu mahusiano yao. Kidogo akapata shaka, akapanga namna ya kulikabili hilo endapo mama yake atakapomhabarisha.

Ni hivi, yeye hajui lolote kuhusiana na hilo jambo, anasingiziwa tu, akapanga vivyo.

“Brian,” mama akaita akiketi. Alimtazama Brian katika namna ambayo ilimfanya ajue kuna mushkeli kwenye kauli ijayo.

“Jana usiku ulikwenda wapi?” mama akauliza, na kabla Brian hajajibu akatahadharisha, “Usijaribu kuniongopea chochote, Brian. Ni kwa ajili yako.”

Brian akapatishwa shaka na kauli ya mama yake. Hapa akawa njia panda kujua ni kipi haswa mama yake anakiongelea, kwenda kule kwa wakina Faris ama kwenye tafrija pamoja na wakina Wayde? Kutaka kujua hilo, akauliza, “Kwani kuna nini, mama?”

“Brian, nimekuuliza,” mama akapandisha sauti. “Nahitaji majibu na si maswali.”

“Nilienda kutembelea familia ya Garett!”

“Alafu?”

“Nikaenda kwenye tafrija ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya mwanafunzi mwenzetu.”

“Ukiwa na nani?”

Hapa Brian akaanza kuhakikisha kuwa mawazo yake ya awali yalikuwa sahihi. Wanaenda kujadili lile swala la Wayde, mtoto wa seneta.

“Nikiwa na marafiki zangu … watu ninaosoma nao darasa moja! Kuna ubaya kwenye hilo?”

“Alafu ulipotoka hapo ukaenda wapi?”

Hapa Brian akapata shaka, pengine alivyokuwa anawaza sivyo. Akajiuliza zaidi ni nini mama yake anajua kabla hajafungua mdomo wake aidha kuongopa ama kusema ukweli.

“Tulipotoka hapo tukarudi nyumbani,” akajibu. “Hivyo ndivyo ilivyokuwa, hamna cha ziada.”

Mama akanyamaza akimtazama kwa sekunde kadhaa kisha akamuuliza, “Haukwenda kwa wakina Faris?”

Moyo wa Faris ukaruka pigo. Akahisi mstari wa baridi umempitia mwilini kwa wepesi. Mama amejuaje hilo?

“Brian,” mama akaita. Akashusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa chake taratibu. “Wewe ni mwanangu wa pekee, sina mtoto mwingine yeyote yule. Tangu baba yako alipofariki, wewe ndiye familia pekee niliyobaki nayo. Sitaki kukupoteza.”

“Kivipi?” Brian akauliza.

“Sitaki maswali, Brian!” mama akafoka. “Kuanzia leo hii sitaki kukusikia wala kukuona ukienda kwa Garett tena. Sitaki kusikia ukienda kwa wakina Faris pia. Tumeelewana?”
Mama alikuwa amebadilika rangi. Uso wake ulikuwa unatisha. Macho yake yalikuwa mekundu yamekodoa.

“Sawa, mama,” Brian akajibu kwa hofu. Mama akanyanyuka na kwenda zake chumbani akitembea upesi na kwa hasira. Alimwacha Brian akiwa na maswali, mama amejuaje kama alienda kwa wakina Faris?

Aliwaza sana lakini hakupata jibu. Alijaribu kutengeneza kichwani namna ambavyo mama yake aling’amua safari hiyo, akashindwa. Akaona ni stara, siku ambapo mama yake atakuwa amepungukiwa na hasira, amuulize apate kujua.

Basi akaendaze kulala.

Baadae katikati ya usiku, kwenye majira ya saa nane ya saa yako, akasikia mlango wa chumba chake ukigongwa. Akafungua macho na kuweka shuka kando, akajiuliza kwa muda mfupi kabla hajapaza sauti,

“Nani? - mama?” Hakukuwa na majibu. Hodi ikagongwa tena. Basi akanyanyuka na kwenda mlangoni kufungua. Hakuona mtu. Alitazama kushoto na kulia, patupu! Kabla hajatoka hapo mlangoni, akasikia tena hodi nyingine. Akashangaa!

Alitega sikio lake kwa umakini, akagundua hodi hiyo ilikuwa inatokea kwenye mlango wa sebule. Akakunja ndita za mashaka, lakini akapata hamu ya kujua. Akanyanyua nyayo zake kuuendea mlango … alitembea taratibu, hakukuwa na vishindo vyovyote … sakafu yao ya mbao ilikuwa ya baridi … aliufungua mlango kwa upole na kutupa macho nje.

Hakukuwa na mtu. Akaufungua mlango zaidi kutazama. Alitupa macho yake upande wa maghariki. Barabara ilikuwa pweke na upepo wa baridi ulikuwa unapuliza. Nyumba zote zilikuwa kimya. Hakukuwa na sauti ya kitu chochote isipokuwa ya matawi ya miti punde yakipulizwa na pepo.

Alipotazama upande wa mashariki, moyo wake ukapiga fundo kubwa. Kwa mbali alimwona mtoto mdogo wa kike akiwa amesimama katikati ya barabara. Mtoto huyu alikuwa kwa umbali wa hatua thelathini toka kwenye nyumba yao. Alikuwa amevalia gauni jeupe linalokomea juu ya magoti, mkononi akiwa amebebelea mdoli.

Moyo wa Brian ukaanza kwenda upesi.

“Kecie! …” akajikuta anatamka. “Kecie, ni wewe?” alikuwa anauliza kwa sauti ya chini kana kwamba mtoto yule yupo kando yake. Bado kichwa chake hakikuwa sawa. Alikuwa anawaza ni nini anachokiona mbele yake. Ni jinamizi ama mzimu?

“Kecie!” akaendelea kuteta, sasa akitoka nje ya mlango. “Ni wewe, Kecie? … ni wewe kweli?”

Akapiga hatua mbili kuuacha mlango, macho yake yakimtazama yule mtoto amwonaye. Kwakuwa alikuwa mbali na kulikuwa kiza barabarani, hakupata kumwona uso wake vema. Ila yule mdoli, lile gauni, lilikuwa kweli ni la Kecie.

Brian hakuwa na kumbukumbu kiasi hicho cha kuweza kukumbuka sawasawa kitu kilichopita miaka kumi, ila ndani ya chumba chake kuna matangazo yote ya kutafutwa kwa Kecie. Matangazo yaliyokuwa yanaelezea ni nini Kecie alivaa siku anapotea.

Basi akaendelea kupiga hatua kumfuata yule mtoto, sasa hatua tano toka mlangoni. Ila mara, kwa mbali, akasikia sauti ya kike inamwita. … Briaaan! … Briaaan! … kana kwamba mtu yupo ndani ya chungu.

Lakini kabla hajaitikia sauti hiyo, kwa macho yake, akashuhudia yule mtoto akigeuka na kuanza kwenda zake. Akapaza sauti kumwita. Mtoto hakusikia, akaendelea kwenda zake. Mara mtoto huyo akaanza kukimbia. Brian akiwa anashuhudia, japo kwa uhafifu wa uwezo wake wa macho, akamwona yule mtoto amesimama ghafla, na alipofinya macho yake kumtazama kwa umakini, akagundua kuna mtu pembezoni yake. Na mara mtu huyo akaanza kuondoka naye wakitokomea gizani!

Alijitahidi kumtazama mtu huyo, hakubahatika kabisa kumwona. Alikuwa mweusi kufanana na giza. Akataka kuwafuata, ila aliponyanyua mguu, akahisi amedakwa mkono wake wa kuume, akavutwa kwanguvu!

“Brian!” Kutazama alikuwa ni mama yake. Akatazama kule alipomwona mtoto, hakukuwa na kitu. Taa zilikuwa zinamulika barabara iliyokuwa nyeupe pe.

“Brian, nini shida?” Mama akauliza. Bado Brian alikuwa haelewi kinachoendelea. Hakuwa anajua hata cha kusema. Basi mama akamrejesha ndani na kisha akaufunga mlango.

“Brian!” mama akaita, na kuuliza, “Umeanza lini kuota ukiwa unatembea?”

Kumbe yale yote ambayo Brian alikuwa anayafanya alikuwa usingizini. Lakini akiwa katika hali hiyo, akafungua mlango na kwenda mpaka nje ya nyumba.

Akamweleza mama yake kilichojiri, nini aliona na kusikia.

“Unafikiri mno kuhusu Kecie … Kalale, Brian. Tutaongea kesho.” mama yake akambusu kwenye paji la uso na kisha akaenda zake chumbani kulala. Brian naye akanyanyuka na kwenda kujitupia kitandani mwake bado akiwa na hofu. Aliwaza sana juu ya kile alichokiona. Kilimnyima raha na kumpatia maswali mengi ambayo hakuona dalili ya kupatia ufumbuzi.

Ila akiwa hapo, anajibuabidua kutafuta usingizi, akatazama dirishani na kuona kitu. Kulikuwa kuna maandishi kwenye kioo cha dirisha. Alisonga kwa ukaribu na kutazama vema. Ni kweli alichokiona. Kulikuwa na maandishi yaloandikwa kwa herufi kwa kutumia kidole dhidi ya unyevu uliojishika kiooni.

‘NIOKOE, BRIAN’

Maandishi yalisomeka vivyo.


***
 
Sijapendezwa na swala la moderators, nilipoandika kichwa cha habari simulizi by Steve ni kwakuwa nililenga wateja wangu wote wa simulizi kwa kujua itakuwa rahisi kwao kuaccess. Ila wakaamua kutengua title yangu na kuweka yao kana kwamba wamechangia kilichotumwa humu. Basi tuwe tunawapa content watutafutie vichwa wao kama ni hivyo
 
Anyway, tuonane keshokutwa kwa mwendelezo. Kwa wanaohitaji, simulizi ipo whatsapp. Karibu kwa kuniungisha alfu tatu tu kama ni mhusika wa JF. Ahsante.
 
Sijapendezwa na swala la moderators, nilipoandika kichwa cha habari simulizi by Steve ni kwakuwa nililenga wateja wangu wote wa simulizi kwa kujua itakuwa rahisi kwao kuaccess. Ila wakaamua kutengua title yangu na kuweka yao kana kwamba wamechangia kilichotumwa humu. Basi tuwe tunawapa content watutafutie vichwa wao kama ni hivyo
Pole tivu
 
*ROHO YAKE INADAI --- 05*

*Simulizi za series za Steve*


ILIPOISHIA

Ila akiwa hapo, anajibuabidua kutafuta usingizi, akatazama dirishani na kuona kitu. Kulikuwa kuna maandishi kwenye kioo cha dirisha. Alisonga kwa ukaribu na kutazama vema. Ni kweli alichokiona. Kulikuwa na maandishi yaloandikwa kwa herufi kwa kutumia kidole dhidi ya unyevu uliojishika kiooni.

‘NIOKOE, BRIAN’

Maandishi yalisomeka vivyo.

ENDELEA

Brian akafikicha macho kwa kutoamini. Alipotazama tena hakuona kitu kiooni. Kioo kilikuwa kimefutwa seemu ile ya maneno na kubakia kisafi kabisa king’aacho. Akajiuliza ni macho yake, ni akili yake ama uhalisia? Alihisi kuchanganyikiwa!

Alishindwa kabisa kujua mambo haya yanavyomtukia. Hakulala tena akabaki anawaza sana usiku mzima. Akawaza sana na kujikuta akianza kuunganisha matukio kadha wa kadha. Mosi, ule mchoro aliouona kwenye kingo ya kitanda cha Faris, na pili ile ndoto yake ya wima.

Ina maana yule mtoto ambaye Faris alikuwa amemchora akiwa amesimama na mtu nyuma yake ndiyo wale ambao aliwaona kwenye ndoto? Yule mtoto aweza kuwa Kecie lakini yule mtu aliyekuwa amesimama naye ni nani? Ndiye aliyemteka Kecie? Na yeye ndiye aliyesema maneno yale ambayo bado hajayapatia ufumbuzi? Alichanganyikiwa kwa maswali. Alihisi kichwa kinamuuma.

Jua lilipochomoza, mama yake alimgongea mlango kumuuliza hali yake. Aliamka toka kitandani kichwa kikiwa kizito. Akajikongoja mpaka sebuleni na kuketi kwenye kochi. Hakuonekana kama mtu mwenye dhamira ya kwenda shuleni siku hiyo. Macho yake yalikuwa mekundu na uso wake mzito.

“Unajisikiaje, Brian?” mama yake akamuuliza. “Uko sawa?”

“Siko sawa,” akajibu akitazama kando.

“Nini shida?” Mama akauliza akimshika mkono.

“Naota na kuona mambo ya ajabu,” Brian akajibu, kisha akakunja ndita zake kama mtu anayetaka kulia.

“Ni sawa, Brian. Mara nyingiine hutokea mambo kama hayo. Usijali, utakuwa sawa,” Mama akampoza. Ila Brian akapata na mashaka. Mama yake alikuwa mtulivu sana kwenye mambo haya. Tangu jana usiku alipomkomboa toka kwenye ndoto mpaka leo hii anapomweleza mengine. Hali hii haikuwa ya kawaida.

“Mama,” Brian akaita. “Kuna lolote unalolijua kuhusiana na hivi vitu? … tafadhali, kama kuna unalolijua niambie.”

Mama akabinua mdomo wake na kupandisha mabega. “Sijui kitu, Brian. Naamini ni kwasababu ya wewe kumfikiria sana, Kecie. Nadhani inabidi upunguze sasa.”

Ila Brian aliona kitu kwenye macho ya mamaye. Hakuwa anazungumza kwa mwili wake wote.

“Mama, tafadhali naomba uniambie,” akasisitizia. “Najua kuna kitu unafahamu.”

Mama akashusha pumzi ndefu. Akajitengenezea kwenye kiti na kumtazama Brian, kisha akatulia kwa kama sekunde sita pasipo kunena jambo.

“Brian,” Mama akaita kwa sauti ya chini. “Nadhani unamfahamu Brewster”

“Brewster!” Brian akalipuka. “Yule mzee anay…”

“Ndiye huyo huyo!” mama akadakia. “Pengine ana mambo anayoyajua kuhusu wewe.”

“Mambo gani hayo?”

“Sijui. Ila anajua ….”

Mama akashusha tena pumzi. Kwa muda kidogo kukawa kimya katikati yao.

“Sikutaka kukuambia kabisa haya mambo lakini naona yanaweza yasikome. Jana wakati wa jioni, Brewster alikuja hapa kunigongea mlango. Nilishangazwa na ujio wake maana hajawahi kuwa mgeni wangu tangu nimjue miaka kenda iliyopita. Nilimkaribisha na akanieleza mambo ya ajabu…”

Brian alikuwa makini akisikiliza, macho yake mekundu yalikuwa tenge na kwa muda mfupi, usingizi ulimtoweka kichwani japo kichwa chake bado kilimgonga kwa mbali.

“… swali lake la kwanza kuniuliza ni wapi alipo mtoto wako? Nikamwambia sifahamu, ametoka muda mrefu. Akaniambia ulipo na mwishowe akanipa onyo pasipo kunielezea mambo mengi. Kama nataka uwe hai, basi nikusihi uache mambo unayoyafanya na uishi maisha yako.”

“Kwanini alisema hivyo?” Brian akauliza.

“Sijui!” Mama akajibu. “Hakunieleza mambo mambo mengi zaidi ya hayo, na hakukaa muda mrefu akaenda zake … sikufahamu alijuaje ulipo, na sijui ana nini kichwani kuhusu wewe.”

“Alikueleza nitakuwa naota na kuona mambo ya ajabu?”

“Alichoniambia ni kwamba, endapo usipofuata anachokisema basi maisha yako yatakuwa ya taabu sana. Utaishi kwa masumbuko, hofu na woga … Brian, sijui kama anachokisema ni kweli au lah! Ila nahisi kuna kitu hakipo sawa. Naomba uachane na mambo ya Kecie. Sawa?”

Brian akatazama chini. Hakujibu, ikabidi mama yake arudie kuuliza.

“Sawa, Brian?”

“Sawa, mama … nitafanya hivyo.”

“Nenda kapumzike sasa. Najua usiku haukulala.”

Brian akanyanyuka na kwenda zake chumbani. Kulikuwa na mambo kadhaa yanampitia kichwani ila alipojitupia kitandani hakupata wasaa wa kuyafikiria, usingizi ulimnyaka na kumpoteza.


***


Saa kumi jioni …


“Oliviiia!” Sauti ya Mrs Garett ilitikisa nyumba. Alikuwa amekunja sura, ametoka chumbani anaelekea sebuleni akiwa ameweka mkono wake kiunoni.

Akaendelea kuita na kuita, hakusikia wala kuona kitu. Alikasirika sana, akaketi kitini akiwaza Olivia atakuwa wapi. Alimkataza asiende kucheza pasipo kumwomba ruhusa. Alimkataza kwenda popote pale. Ina maana amekaidi agizo lake.

Akiwa ametulia hapo kwa sekunde kadhaa, akasikia sauti ya kike ikiita, “Moooom! … moooom!” akashtuka.

Sauti hiyo ilikuwa ni kana kwamba inatoka chini ya mto. Ilikuwa ni kana kwamba mtu anakabwa na sasa anajitahidi kuzungumza. Basi Mrs Garett akasimama na kuanza kuita tena kama mtu aliyekabwa na hofu.

“Oliviaa! Oliviiiaa!”

Sauti ile ya kike ikawa inamjibu, ikisikika kwa mbali. Haraka Mrs Garett akarudi tena chumbani akiita. Mara akamwona Olivia akiwa juu ya paa. Uso wake ulikuwa umetapakawa na woga. Macho yake yalikuwa yanatiririsha machozi.

“Olivia!” Mrs Garett akatahamaki. Akafanya jitihada za kumshusha kisha akaenda naye sebuleni. Ila Olivia alikuwa mwoga sana, alikuwa anatazama nyuma kila mara kana kwamba kuna kitu kinamfuata.

“Nini Oliva! Kuna shida gani?” Mrs Garett akamuuliza akimlazimisha amtazame usoni. “Niambie kuna nini? … Olivia, nambie!”

Olivia alitazama koridoni. Macho yake yalikuwa mekundu mno, pua yake ilikuwa inachuruza kamasi jepesi. Akasema kwa sauti ya kilio, “Sitaki kucheza naye.”

“Nani? Nani hutaki kucheza naye, Olivia?” Mrs Garett akauliza. Alikuwa anamtazama Olivia kwa macho na sura ya huruma.

“Yule mtoto,” Olivia akaropoka. “Ananifuata chumbani, anataka kucheza na mimi. Analazimisha kwenda na mimi tukacheze.”

“Mtoto gani? Niambie ni nani huyo?”

Olivia akanyooshea kidole chake kwenye picha iliyopo ukutani. Mrs Garett kutazama, akaona ni picha ya Kecie. Akaachama mdomo wazi kwa kuduwaa.

“Una uhakika ni yeye?” akamuuliza Olivia.

“Ndio, ni yeye! Hunifuata kila siku usiku … mchana na jioni. Anataka twende tukacheze kule msituni!”

Mrs Garett akashusha pumzi akikosa la kusema. Macho yake yakageuka kuwa mekundu. Alitazama chini akihangaika kutafuta neno la kuongea.

Baada ya mfupi, akiwa ameongozana na Olivia, akatoka nyumbani akitembea kwa kasi. Alikuwa amevalia gauni jeusi na mtandio mweupe, Olivia, gauni rangi ya pinki lenye mauamaua shingoni.

Moja kwa moja wakaelekea kanisani. Lilikuwa ni kanisa kubwa linalosimama upande wa kaskazini mwa mji wa Boston. Hapo Mrs Garett akaonana na padri Alfonso, mwanaume mrefu aliyevalia joho refu jeusi kasoro ya shingoni kuna doa jeupe. Alikuwa mtu wa makadirio ya miaka arobaini na tano.

Mrs Garett akamweleza dhamira yake kuwa anataka kutubu na kuomba msamaha. Padri akampeleka kwenye chumba maalum, Mrs Garett akaketi kitako upande wa pili akitenganishwa na Padri kwa ukuta mwepesi wa mbao wenye matundutundu.

Kabla hajaanza kusema kitu, akajikuta anaanza kumimina machozi.



****
 
Daah kumbe kumekucha sijatembelea jukwaa hili muda sasa.heko kwako steve maana nasoma kama nacheki movie flani hivi ya kutishatisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom