SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,442
- Thread starter
- #61
*ROHO YAKE INADAI --- 10*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Akaanza kupiga hatua kumsogelea Olivia. Hatua zake zilikuwa nzito kinyume kabisa na mwili wake. Kila alipokanyaga chini ilisikika tih! Tih! Tih!
Olivia akajawa na woga mkubwa, akapiga kelele kali sana na kumshtua kila mtu!
.
.
ENDELEA
.
.
Kila mtu akaangaza. Hawakuona jambo. Wakamtazama Olivia na kumuuliza nini kimemsibu. Olivia akanyooshea mkono wake mlangoni.
.
.
“Ni nini, Olivia?” mama akauliza kwa ukali kidogo.
.
.
“Nimemwona mtu, mama. Nimemwona mtu mama!” akalia Olivia.
.
.
“Umemwona wapi?” akauliza mama akiangaza macho yake. Olivia akaendelea kunyooshea mkono wake mlangoni. Macho yake yalikuwa yanatema machozi. Uso wake umejawa na mashaka tele.
.
.
“Nimemwona pale mlangoni. Mtoto mdogo mwenye mdoli mkononi!”
.
.
Mama akashika mdomo wake. Akamtazama Padri Alfonso na dada Magdalena.
.
.
“Usijali, Mrs Garett,” akasema Padri. Akainama na kumshika mikono Olivia. Akamtazama kwa macho ya upole na tabasamu kwa mbali. “Mtoto mzuri Olivia, usiogope. Sawa? Sasa hivi tukienda kusali, usifumbue macho yako mpaka tutakapomaliza. Umesikia?”
.
.
Olivia akatikisa kichwa kukubali aliachoambiwa. Bado macho yake yalikuwa yanatoa machozi na uso wake ukisema hofu. Padri akamfuta machozi kwa vidole vyake kisha akambusu kwenye paji lake la uso. Akamkumbusha tena, “usifungue macho yako.”
.
.
Basi baada ya kumwambia hivyo, Padri akamtazama Dada Magdalena na kumpatia ishara ya kichwa. Dada huyo akachovya mkono wake kwenye maji na kukung’utia kule ambapo Olivia alisema amemwona mtu. Alipomaliza akajumuika na wenzake na kuanza kusali upya.
.
.
Zikapita dakika nne za sala. Watu wote walikuwa wamefumba macho yao. Ni sauti tu ya padri ndiyo ilikuwa inasikika hapa. Na mbali na mishumaa ile iliyokuwa imewekwa pale mezani, hakukuwa na chanzo kingine cha mwanga humu ndani.
.
.
Katika dakika hiyo nne ya sala, Olivia ambaye alikuwa ameyafumba macho yake kwanguvu akaanza kuhisi kitu. Alihisi kuna mtu anatembea akitokea kule koridoni kuja sebuleni. Akaogopa sana. Alinyamaza kimya na akijitahidi kutoyafungua macho yake kama alivyoelekezwa, lakini sikio lake la kushoto bado likaendelea kumfanya ahofie zaidi na zaidi.
.
.
Vishindo vya mtu vilikuwa vinasikika vikifika sebuleni, na kisha vinafifia kwenda koridoni. Vinakuja tena na tena vinarudi kwenda koridoni. Zoezi hili lilijirdia mara tatu. Mara ya nne, vishindo vya miguu vilipokuja sebuleni havikurudi tena koridoni. Vikabakia palepale sebuleni!
.
.
Hapa Olivia akahisi kubanwa na mkojo. Mwili wake ulisisimkwa sana. Alihisi baridi la ajabu linampitia na kila kinyweleo kilichopo kwenye mwili wake kimemsimama! Alitamani kukimbia. Alitamani kukaa. Alitamani kulia, alitamani kunyamaza. Alijikuta anatamani kila kitu!
.
.
Ila kwa muda kidogo akahisi kimya. Hakusikia tena vishindo vya mtu na basi akapata angalau ahueni. Huenda mtu huyo atakuwa ameondoshwa na maombi. Akatamani kufungua macho yake atazame, ila akaogopa. Aliona ni kheri asifumbue macho hayo kama alivyoelekezwa kwani anaweza kuona mambo atayoshindwa kuyastahimili.
.
.
Akaendelea na zoezi lake. Ila baada ya dakika moja, akaanza kusikia tena vishindo vile vya binadamu! Moyo wake ukaanza kupiga makasi. Ubaya ni kwamba vishindo hivyo vilikuwa vinamjongea! Na vilipomfikia karibu kabisa vikasimama. Kwa mbali sauti ya kike ikaita,
.
.
“Oliviiaaa …”
.
.
Sauti hii ilikuwa mithili ya upepo. Ilikuwa ni ya baridi sana. Ilipofika kwenye sikio la Olivia ilimfanya mtoto huyo ahisi baridi kali sikioni na shingoni. Alitamani kupiga kelele, lakini akajizuia. Ilihitaji moyo mkubwa sana kuvumilia haya.
.
.
“Oliviaaaa … amka, amka! … Oliviaaaa … amka! Njoo uone mchezo mzuri kule msituni, kweli utafurahia! …” sauti ya baridi ilipulizia sikioni mwa Olivia.
.
.
“Najua unataka kuuona … njoo, twende Oliviaa … twende upesi!”
.
.
Olivia akajitahidi sana kujikaza. Hakufungua macho yake kumwona mtu huyo anayemwongelesha, wala hakumjibu. Alikuwa amefunga tu macho na kinywa chake japo anahofia sana.
.
.
Basi baada ya mtu huyo kuona Olivia hasikii, akamsogelea karibu zaidi na kuanza kumshika! Kiganja chake cha baridi kilipapasa mkono wa Olivia, ukapandisha mpaka shingoni mwake. Ukapapasapapasa shingo ya Olivia, na kisha ukadumbukia mgongoni mwa mtoto huyo na kuendelea kumpapasapapasa!
.
.
Hapa Olivia akashindwa kubana mkojo, akajikuta analowanisha mapaja yake kwa woga. Akatetemeka kwa hofu kupita kiasi, na kama zoezi hili lingeendelea kama kwa dakika mbili mbele, Olivia angepiga kelele na kufumbua macho, ila bahati likakoma na akabaki salama!
.
.
Akahema kwanguvu. Akatazama kushoto na kulia, hakuhisi kitu. Akaendelea kuhema kwanguvu moyo wake nao ukipiga kwanguvu kwenda pole. Ikapita dakika moja kukiwa kimya.
.
.
Ikapita dakika ya pili kukiwa kimya.
.
.
Ikapita dakika ya tatu kukiwa kimya.
.
.
Kwenye dakika ya nne Olivia akaanza kusikia kitu ambacho kilimshangaza. Si vishindo vya mtu wala kiganja kikimpapasa, bali sauti ya Padri Alfonso na Dada Magdalena. Watu hao walikuwa wanateta na kucheka. Wanagonga mikono yao na pia kulia!
.
.
Olivia akaachama mdomo wake kwa kustaajabu. Hakuwa anaamini alichokuwa anasikia. Padri Alfonso na Dada Magdalena! Haiwezekani! Akatikisa kichwa chake. Hapana. Akatikisa kichwa chake. Hapana. Alikuwa haamini kitu alichokuwa anasikia. Alfonso na Magdalena walikuwa wanasali, ndivyo alivyokuwa anaamini na si vinginevyo.
.
.
Lakini masikio yake yalikuwa yanamwambia tofauti. Padri Alfonso na Dada Magdalena walikuwa wakipanga kuwamaliza. Alfonso na Magdalena walikuwa wanapanga kuwatupia kule msituni! Na walipoelezana hayo wakawa wanacheka kwanguvu. Wanacheka kishetani!
.
.
Olivia akafungua macho yake kwa mbali apate kutazama kama ni kweli alichokuwa anasikia. Alishindwa kuvumilia. Alitaka kushushudia namna ambavyo Padri na Dada walivyokuwa wanapanga madhalimu juu yao.
.
.
Alichokiona kikamtisha, na kikamfanya afungue macho kwa nguvu kukodoa asiamini. Alimwona Padri Alfonso akiwa na uso mweusi, macho mekundu yenye mboni mithili ya mbuzi, meno makali yaliyochongoka, masikio marefu na ulimi mrefu mwembamba.
.
.
Dada Magdalena alikuwa na uso mweupe pe wenye michirizi meusi. Macho yake yalikuwa mekundu na makubwa. Mdomo wake ulikuwa mweusi kana kwamba kunguru. Meno yake yalikuwa yamekaa hovyo na yenye rangi ya kuoza.
.
.
Punde Olivia alipokodoa macho yake, Padri Alfonso na Dada Magdalena wakamtazama wakiwa wamekodoa. Nyuso zao zilikuwa zimesimama tuli kana kwamba zimegandishwa. Mara ghafla shingo zao zikaanza kupinda na kupeleka vichwa vyao kushoto, kulia, juu na chini! Kushoto, kulia, juu na chini!
.
.
Olivia akamtazama mama yake kwa hofu. Mama alikuwa amefumba macho hajui kinachoendelea. Olivia akamwita na kumwita. Akamvuta mkono na kumtikisatikisa ila wapi! Mama hakufungua macho wala kumtazama.
.
.
Basi padri Alfonso na Dada Magdalena wakaanza kumjongea. Olivia akamvuta mamaye kwanguvu sana kumwamsha aone, ila jitihada zake hazikuzaa matunda. Mama alikuwa kwenye usingizi mzito sana. Ni kana kwamba ametiliwa kiasi kingi cha madawa ya kulevya!
.
.
Padri Alfonso na Dada Magdalena wakazidi kumsogelea Olivia wakitembea kama watu wasiokuwa na mifupa, wakijikunjakunja , wakijipindapinda, wakijikunjakunja na wakijipindapinda. Wakitazama kana kwamba watu wasiokuwa na kope.
.
.
Mdomo wa Padri Alfonso ukaanza kuchuruza damu iliyofika kidevuni mwake na kudondokea chini. Macho ya Dada Magdalena nayo yakaanza kuvuja damu, ikipita mashavuni mwake na kudondokea chini.
.
.
Walipomkaribia Olivia wakakunjua mikono yao yenye vidole vyembamba na kucha ndefu wakitaka kumyaka binti huyo. Olivia akapiga kelele kali sana akimkumbatia mama yake kwanguvu. Mara mama akafungua macho na kumtazama, “Una nini Olivia?”
.
.
Olivia akamtazama mama yake akiwa anahema kwa hofu, akamnyooshea kidole upande wa Padri Alfonso na Dada Magdalena.
.
.
“Kuna nini?” mama akauliza. Hakuwa anaona kitu. Hakukuwa na kitu. Padri Alfonso na Dada Magdalena nao wakaduwaa wakimtazama. Wote walikuwa kwenye hali yao ya kawaida.
.
.
“Nini, Olivia?” Padri Alfonso akauliza akimjongea mtoto huyo. Olivia akapiga kelele kali na kukimbilia nyuma ya mgongo wa mama yake kujificha. Akalia sana.
.
.
“Olivia,” Padri akaita. “Olivia, ulifungua macho?” akauliza kwa sauti ya chini akijaribu kumtazama binti huyo, ila Olivia hakutaka kabisa kumtazama Padri. Kadiri Padri alivyokua anasogea, ndivyo naye akawa anasonga mbali naye. Ila upande wa pili alipokuwa anaelekea akakutana na Dada Magdalena, naye akamuuliza, “Ulifungua macho?”
.
.
Olivia akapiga tena kelele kali. Mama akamnyanyua na kumbeba.
.
.
“Olivia, una nini?”
.
.
.
**
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Akaanza kupiga hatua kumsogelea Olivia. Hatua zake zilikuwa nzito kinyume kabisa na mwili wake. Kila alipokanyaga chini ilisikika tih! Tih! Tih!
Olivia akajawa na woga mkubwa, akapiga kelele kali sana na kumshtua kila mtu!
.
.
ENDELEA
.
.
Kila mtu akaangaza. Hawakuona jambo. Wakamtazama Olivia na kumuuliza nini kimemsibu. Olivia akanyooshea mkono wake mlangoni.
.
.
“Ni nini, Olivia?” mama akauliza kwa ukali kidogo.
.
.
“Nimemwona mtu, mama. Nimemwona mtu mama!” akalia Olivia.
.
.
“Umemwona wapi?” akauliza mama akiangaza macho yake. Olivia akaendelea kunyooshea mkono wake mlangoni. Macho yake yalikuwa yanatema machozi. Uso wake umejawa na mashaka tele.
.
.
“Nimemwona pale mlangoni. Mtoto mdogo mwenye mdoli mkononi!”
.
.
Mama akashika mdomo wake. Akamtazama Padri Alfonso na dada Magdalena.
.
.
“Usijali, Mrs Garett,” akasema Padri. Akainama na kumshika mikono Olivia. Akamtazama kwa macho ya upole na tabasamu kwa mbali. “Mtoto mzuri Olivia, usiogope. Sawa? Sasa hivi tukienda kusali, usifumbue macho yako mpaka tutakapomaliza. Umesikia?”
.
.
Olivia akatikisa kichwa kukubali aliachoambiwa. Bado macho yake yalikuwa yanatoa machozi na uso wake ukisema hofu. Padri akamfuta machozi kwa vidole vyake kisha akambusu kwenye paji lake la uso. Akamkumbusha tena, “usifungue macho yako.”
.
.
Basi baada ya kumwambia hivyo, Padri akamtazama Dada Magdalena na kumpatia ishara ya kichwa. Dada huyo akachovya mkono wake kwenye maji na kukung’utia kule ambapo Olivia alisema amemwona mtu. Alipomaliza akajumuika na wenzake na kuanza kusali upya.
.
.
Zikapita dakika nne za sala. Watu wote walikuwa wamefumba macho yao. Ni sauti tu ya padri ndiyo ilikuwa inasikika hapa. Na mbali na mishumaa ile iliyokuwa imewekwa pale mezani, hakukuwa na chanzo kingine cha mwanga humu ndani.
.
.
Katika dakika hiyo nne ya sala, Olivia ambaye alikuwa ameyafumba macho yake kwanguvu akaanza kuhisi kitu. Alihisi kuna mtu anatembea akitokea kule koridoni kuja sebuleni. Akaogopa sana. Alinyamaza kimya na akijitahidi kutoyafungua macho yake kama alivyoelekezwa, lakini sikio lake la kushoto bado likaendelea kumfanya ahofie zaidi na zaidi.
.
.
Vishindo vya mtu vilikuwa vinasikika vikifika sebuleni, na kisha vinafifia kwenda koridoni. Vinakuja tena na tena vinarudi kwenda koridoni. Zoezi hili lilijirdia mara tatu. Mara ya nne, vishindo vya miguu vilipokuja sebuleni havikurudi tena koridoni. Vikabakia palepale sebuleni!
.
.
Hapa Olivia akahisi kubanwa na mkojo. Mwili wake ulisisimkwa sana. Alihisi baridi la ajabu linampitia na kila kinyweleo kilichopo kwenye mwili wake kimemsimama! Alitamani kukimbia. Alitamani kukaa. Alitamani kulia, alitamani kunyamaza. Alijikuta anatamani kila kitu!
.
.
Ila kwa muda kidogo akahisi kimya. Hakusikia tena vishindo vya mtu na basi akapata angalau ahueni. Huenda mtu huyo atakuwa ameondoshwa na maombi. Akatamani kufungua macho yake atazame, ila akaogopa. Aliona ni kheri asifumbue macho hayo kama alivyoelekezwa kwani anaweza kuona mambo atayoshindwa kuyastahimili.
.
.
Akaendelea na zoezi lake. Ila baada ya dakika moja, akaanza kusikia tena vishindo vile vya binadamu! Moyo wake ukaanza kupiga makasi. Ubaya ni kwamba vishindo hivyo vilikuwa vinamjongea! Na vilipomfikia karibu kabisa vikasimama. Kwa mbali sauti ya kike ikaita,
.
.
“Oliviiaaa …”
.
.
Sauti hii ilikuwa mithili ya upepo. Ilikuwa ni ya baridi sana. Ilipofika kwenye sikio la Olivia ilimfanya mtoto huyo ahisi baridi kali sikioni na shingoni. Alitamani kupiga kelele, lakini akajizuia. Ilihitaji moyo mkubwa sana kuvumilia haya.
.
.
“Oliviaaaa … amka, amka! … Oliviaaaa … amka! Njoo uone mchezo mzuri kule msituni, kweli utafurahia! …” sauti ya baridi ilipulizia sikioni mwa Olivia.
.
.
“Najua unataka kuuona … njoo, twende Oliviaa … twende upesi!”
.
.
Olivia akajitahidi sana kujikaza. Hakufungua macho yake kumwona mtu huyo anayemwongelesha, wala hakumjibu. Alikuwa amefunga tu macho na kinywa chake japo anahofia sana.
.
.
Basi baada ya mtu huyo kuona Olivia hasikii, akamsogelea karibu zaidi na kuanza kumshika! Kiganja chake cha baridi kilipapasa mkono wa Olivia, ukapandisha mpaka shingoni mwake. Ukapapasapapasa shingo ya Olivia, na kisha ukadumbukia mgongoni mwa mtoto huyo na kuendelea kumpapasapapasa!
.
.
Hapa Olivia akashindwa kubana mkojo, akajikuta analowanisha mapaja yake kwa woga. Akatetemeka kwa hofu kupita kiasi, na kama zoezi hili lingeendelea kama kwa dakika mbili mbele, Olivia angepiga kelele na kufumbua macho, ila bahati likakoma na akabaki salama!
.
.
Akahema kwanguvu. Akatazama kushoto na kulia, hakuhisi kitu. Akaendelea kuhema kwanguvu moyo wake nao ukipiga kwanguvu kwenda pole. Ikapita dakika moja kukiwa kimya.
.
.
Ikapita dakika ya pili kukiwa kimya.
.
.
Ikapita dakika ya tatu kukiwa kimya.
.
.
Kwenye dakika ya nne Olivia akaanza kusikia kitu ambacho kilimshangaza. Si vishindo vya mtu wala kiganja kikimpapasa, bali sauti ya Padri Alfonso na Dada Magdalena. Watu hao walikuwa wanateta na kucheka. Wanagonga mikono yao na pia kulia!
.
.
Olivia akaachama mdomo wake kwa kustaajabu. Hakuwa anaamini alichokuwa anasikia. Padri Alfonso na Dada Magdalena! Haiwezekani! Akatikisa kichwa chake. Hapana. Akatikisa kichwa chake. Hapana. Alikuwa haamini kitu alichokuwa anasikia. Alfonso na Magdalena walikuwa wanasali, ndivyo alivyokuwa anaamini na si vinginevyo.
.
.
Lakini masikio yake yalikuwa yanamwambia tofauti. Padri Alfonso na Dada Magdalena walikuwa wakipanga kuwamaliza. Alfonso na Magdalena walikuwa wanapanga kuwatupia kule msituni! Na walipoelezana hayo wakawa wanacheka kwanguvu. Wanacheka kishetani!
.
.
Olivia akafungua macho yake kwa mbali apate kutazama kama ni kweli alichokuwa anasikia. Alishindwa kuvumilia. Alitaka kushushudia namna ambavyo Padri na Dada walivyokuwa wanapanga madhalimu juu yao.
.
.
Alichokiona kikamtisha, na kikamfanya afungue macho kwa nguvu kukodoa asiamini. Alimwona Padri Alfonso akiwa na uso mweusi, macho mekundu yenye mboni mithili ya mbuzi, meno makali yaliyochongoka, masikio marefu na ulimi mrefu mwembamba.
.
.
Dada Magdalena alikuwa na uso mweupe pe wenye michirizi meusi. Macho yake yalikuwa mekundu na makubwa. Mdomo wake ulikuwa mweusi kana kwamba kunguru. Meno yake yalikuwa yamekaa hovyo na yenye rangi ya kuoza.
.
.
Punde Olivia alipokodoa macho yake, Padri Alfonso na Dada Magdalena wakamtazama wakiwa wamekodoa. Nyuso zao zilikuwa zimesimama tuli kana kwamba zimegandishwa. Mara ghafla shingo zao zikaanza kupinda na kupeleka vichwa vyao kushoto, kulia, juu na chini! Kushoto, kulia, juu na chini!
.
.
Olivia akamtazama mama yake kwa hofu. Mama alikuwa amefumba macho hajui kinachoendelea. Olivia akamwita na kumwita. Akamvuta mkono na kumtikisatikisa ila wapi! Mama hakufungua macho wala kumtazama.
.
.
Basi padri Alfonso na Dada Magdalena wakaanza kumjongea. Olivia akamvuta mamaye kwanguvu sana kumwamsha aone, ila jitihada zake hazikuzaa matunda. Mama alikuwa kwenye usingizi mzito sana. Ni kana kwamba ametiliwa kiasi kingi cha madawa ya kulevya!
.
.
Padri Alfonso na Dada Magdalena wakazidi kumsogelea Olivia wakitembea kama watu wasiokuwa na mifupa, wakijikunjakunja , wakijipindapinda, wakijikunjakunja na wakijipindapinda. Wakitazama kana kwamba watu wasiokuwa na kope.
.
.
Mdomo wa Padri Alfonso ukaanza kuchuruza damu iliyofika kidevuni mwake na kudondokea chini. Macho ya Dada Magdalena nayo yakaanza kuvuja damu, ikipita mashavuni mwake na kudondokea chini.
.
.
Walipomkaribia Olivia wakakunjua mikono yao yenye vidole vyembamba na kucha ndefu wakitaka kumyaka binti huyo. Olivia akapiga kelele kali sana akimkumbatia mama yake kwanguvu. Mara mama akafungua macho na kumtazama, “Una nini Olivia?”
.
.
Olivia akamtazama mama yake akiwa anahema kwa hofu, akamnyooshea kidole upande wa Padri Alfonso na Dada Magdalena.
.
.
“Kuna nini?” mama akauliza. Hakuwa anaona kitu. Hakukuwa na kitu. Padri Alfonso na Dada Magdalena nao wakaduwaa wakimtazama. Wote walikuwa kwenye hali yao ya kawaida.
.
.
“Nini, Olivia?” Padri Alfonso akauliza akimjongea mtoto huyo. Olivia akapiga kelele kali na kukimbilia nyuma ya mgongo wa mama yake kujificha. Akalia sana.
.
.
“Olivia,” Padri akaita. “Olivia, ulifungua macho?” akauliza kwa sauti ya chini akijaribu kumtazama binti huyo, ila Olivia hakutaka kabisa kumtazama Padri. Kadiri Padri alivyokua anasogea, ndivyo naye akawa anasonga mbali naye. Ila upande wa pili alipokuwa anaelekea akakutana na Dada Magdalena, naye akamuuliza, “Ulifungua macho?”
.
.
Olivia akapiga tena kelele kali. Mama akamnyanyua na kumbeba.
.
.
“Olivia, una nini?”
.
.
.
**