Simulizi: Roho yake inadai

Simulizi: Roho yake inadai

Creep stories ni hatari kwa wapenzi wa horror movie mnaeza cheki movie hizi
1/ annabelle recreation
2/pay the ghost
3/ conjouring 1,2
4/the NUN
 
Naogoopa jamani hapaa
*ROHO YAKE INADAI -- 18*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA
.
.
Wasaa ulipowadia, nakumbuka ilikuwa ni kwenye majira ya jioni ya mapema, Jasmine akauteka mkono wangu na kutokomea nami msituni. Hakuna mtu aliyetuona. Hata watumwa wengine hawakuwa wanajua. Tukatembea upesi sana.
.
.
Njiani Jasmine akinieleza namna nitakavyofurahia mazingaombwe ninayoenda kuyaona!
.
.
ENDELEA
.
.
Basi kwasababu ya mwendo wetu huo, tukawasili eneoni mapema. Ilikuwa ni kama baada ya dakika sita tu! Tayari jengo ghofu lilikuwa mbele yetu. Lakini kabla hatujaingia humo, ajabu nikasikia sauti kali ya risasi! Nilishtuka mno!
.
.
Sikuwahi nimewahi kusikia sauti kali kama hiyo. Huwa nasikia risasi ila si kwa ukaribu kiasi kile. Nilipotazama kando, nikamwona Jasmine akiwa hatamaniki kwa damu! Uso wake wote ulikuwa umefumuliwa na risasi! Haki sikuwahi kuona picha ya kinyama kama ile.
.
.
Tundu kubwa lililopasua kichwa cha Jamsmine na kutapanya uso wake lilikuwa linachuruza damu kedekede. Nikatazama, kwa hofu, wapi ilipotokea risasi ile. Macho yalikua yamenitoka na moyo wanienda kwa pupa sana.
.
.
“Hey Hamill!” nikasikia sauti kavu ikiniita. Kutazama upande wangu wa kulia, nyuma, hatua kama arobaini na mbili, nikamwona baba yangu. Mkononi alikuwa amebebelea gobore kubwa alilokuwa amelitua. Kumbe ndi’ yeye aliyemuua Jasmine.
.
.
“Upo sawa?” akaniuliza akijongea. Nilikosa cha kumjibu. Nilipandwa na hasira mno. Nilimtazama kwa ghafira nikitamani kummaliza. Lakini yeye hakuwa anajali. Aliposonga karibu nami, akani ‘patipati’ kichwani na kumtazama Jasmine aliyekuwa maiti. Akamtemea mate.
.
.
“Kufa wewe malaya!”
.
.
Kwa hasira nikajikuta namshika baba yangu pindo lake la suruali na kumuuliza, “Kwanini umemuua Jasmine?” mara machozi yakaanza kunivuja. Nilishindwa kuuweka mdomo wangu sawa, ulipinda kana kwamba upinde wa mshale.
.
.
“Unasemaje?” baba yangu akafoka. “Alikuwa anakupeleka wapi huyu malaya?” akaniuliza. Asingoje hata jibu, akasema, “Nilimkanya mara kadhaa akae mbali na familia yangu, hakusikia! Kwa maana mgongo wake hausikii tena mijeledi, ngoja na tuone kama kichwa chake kinaweza kuwa sugu mbele ya risasi!” aliposema hivyo akaguna akibinua mdomo.
.
.
Akanyanyua mwili wa Jasmine na kuupeleka ndani ya ghofu. Akautupia humo na kukung’uta mikono yake kwa kumaliza kazi. “Twende!” akaniamuru.
.
.
“Siendi popote!” nikamwambia. Na nisimngoje aniambie kitu, nikakimbia nisijue wapi naelekea. Nikakimbia tu kwenda mbali na baba yangu. Nilimchukia sana. Nilimwona ni mtu asiyefaa kabisa.
.
.
Nikakimbia kadiri ya uwezo wa miguu yangu. Nilipochoka, nikalala chini na kulia sana. Pale nilipokuwa nimelaza kichwa changu pakalowana kwa machozi.

Nilikaa huko mpaka giza lilipoanza kumeza uso wa nchi. Niliogopa sana kuwa msituni nyakati za usiku ila niliona ni kheri kuliko kwenda nyumbani. Basi nikajikunyata kwa baridi na kulazimisha usingizi unitwae.
.
.
Ila kila mara nikawa nashtuka. Wanyama wakikatiza ama matunda yakidondoka ama miti ikisogezwa na upepo, nilikuwa nafungua macho na kuangaza. Nilikuwa naogopa. Sikuweza kudhani usiku ule ungekuwaje.
.
.
Nikiwa sijapata usingizi, nahangaika kufumba na kufumbua macho, nikasikia jina langu likiitwa kwenye miti! Nikanyanyua uso wangu haraka na kuangaza. Ilikuwa ni sauti ya kike. Punde kidogo nikaona mwanga wa taa kwa mbali. Haraka nikanyanyuka na kwenda kufichama nyuma ya mti kuchungulia.
.
.
Nikaendelea kuitwa. Mara ya tatu nikatambua kuwa sauti hiyo ni ya mama yangu, nikaguswa moyoni. Nikaitikia na kukimbia kwenda kumkuta mama. Alikuwa mwenyewe katikati ya msitu. Mkono wake wa kushoto ulikuwa umebebelea taa, na ule wa kulia ukiwa umebebelea gongo kubwa kumlinda.
.
.
Aliponiona akafurahi sana. Akanikumbatia kwanguvu akitupia taa kando. Akanibusu na kunikumbatia tena kwanguvu.
.
.
“Twende nyumbani!” Akasema akinishika mkono. Alikuwa ni jasiri wa namna gani. Alikuja mwenyewe msituni kunitafuta, akimwacha baba peke yake nyumbani akivuta tumbaku. Asingeweza kulala ndani mimi nikiwa nje. Kuna muda nilikuwa najiuliza, ilikuaje mama yangu akaolewa na mwanaume katili kama baba yangu? Ila niliamini watu wadhalimu huitaji zaidi malaika kama mama yangu kuliko wawahitajivyo wadhalimu wenzao.
.
.
Tukafika nyumbani salama, naye baba asiseme jambo, mdomo wake ulikuwa umetingwa na shughuli kubwa ya kunyonya tumbaku na kutemea moshi nje.
.
.
Siku hiyo nikalala kwa maruweruwe sana. Jua liliponyanyuka, nikashukuru. Nikaomboleza kifo cha Jasmine na hata ile safari yetu ya kwenda kwenye mazingaombwe. Ningeenda na nani na yeye ashakufa? Niliogopa kwenda mwenyewe ingawa eneo nalifahamu.
.
.
Basi nikaachana na mpango huo. Na sasa nikadhani ya kuwa Jasmine atakuwa ameenda milele. Nisingemwona wala kumsikia tena. Hakuna mtu anayemkumbuka mtumwa. Hakuna anayejali wala kutunza tarehe yake ya kifo, labda wenzake.
.
.
Ila nilikuwa mwongofu. Nilikosea kuwaza hivyo. Roho ya Jasmine haikwenda, ilirejea kudai haki yake ya uhai. Ilirejea ikiwa si ya yule Jasmine nimjuaye, mwenye upendo, mpole na mkarimu. Ilirejea ikiwa ya muuaji asiye na chembe ya huruma. Aliyejawa na kisasi kikubwa!”
.
.
Brian akaishia hapa kusoma. Macho yalikuwa yamechoka sasa na hakuweza kuendelea tena. Akaweka nyaraka ile kando na kuchukua muda kidogo kuyawaza yale aliyoyasoma, Hakuchukua muda, usingizi ukamkwapua asiamke mpaka asubuhi.
.
.
Hakukuwa na shule hivyo hakuwa na sababu ya kuwahi. Akajibandua kitandani majira ya saa tatu asubuhi, akaoga na kuosha uso alafu akajivuta sebuleni. Huko akamkuta mama yake, Mrs Garett na Olivia. Walikwishaamka na tayari wamejipatia kifungua kinywa.
.
.
“Brian, leo ndiyo siku ambayo Padri atakuja hapa. Naomba uwapo mapema nyumbani,” mama akakumbushia. Brian asionyeshe muitikio wowote, akaenda jikoni na kutwaa chakula cha asubuhi. Baada ya hapo, hakukaa sana nyumbani. Hakuona shughuli ya kufanya papo. Alipata wazo la kwenda kwa Brewster, kwakuwa ni asubuhi, aliamini atamkuta mzee huyo.
.
.
Aliamini ana mambo kadhaa ya kuteta naye ingawa mlengwa wake hakuwa mtu wa kuunga mkono. Mkimya. Na kwa namna moja ama nyingine, anatisha.
.
.
Kuna kitu alihisi hakipo sawa na mzee yule. Brian aliamini. Na pia alihisi kuna mambo ambayo mzee yule anayajua ila mdomowe kautia gundi.
.
.
Akaendea stoo na kuchukua baiskeli yake, akakwea na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Brewster. Kama ilivyo ada nyumba hii ilikuwa imetulia haswa. Ni kama vile hakukuwa na mtu aishiye hapa. Kunguru walikuwa wametandia kwenye paa, wakitazama huku na kule, huku na kule.
.
.
Brian akasonga karibu. Akaugonga mlango na kuita. Hakukuwa na majibu. Akachungulia ndani, hakumwona mtu. Sebuleni kulikuwa na kiti kimoja cha kucheza. Mbali na kiti hicho hakukuwa na samani nyingine. Sebule ilikuwa pweke, hodi ikibishwa inasikika na mwangwi.
.
.
Brian akashusha pumzi na kujiuliza kwa sekunde kadhaa. Akakata shauri la kwenda nyuma ya nyumba hiyo. Huenda Mr. Brewster akaja kumkutia huko kama ilivyokuwa siku ile.
.
.
Napo huko akakaa kwa muda mrefu akimtazama nguruwe wa Brewster. Mzee huyo hakutokea. Akawaza kuondoka, ila kabla hajafanya hilo, akapata wazo. Vipi akizama ndani ya nyumba ya mzee huyo na kutazama? Kupekua kidogo?
.
.
Huenda nikagundua mambo ambayo hataki kuniambia, akawaza. Akili yake ikatumikisha viungo vyake vya mwili kutenda wazo hilo la kidhalimu. Akauendea mlango wa nyuma na kufanya namna kwa kuufungua kwa ndani baada ya kusukuma dirisha.
.
.
Taratibu akaurudishia mlango huo na akarusha macho yake kukagua nyumba hiyo. Ilikuwa imejawa na tando za buibui kwenye kona zake. Kuta zilikuwa na ukungu. Harufu iliyokuwamo ndani haikuwa ya kuridhisha.
.
.
Brian aliwaza ni namna gani mzee huyo anaishi humo. Alifika sebuleni, akakagua. Uso wake ulikuwa umeumba ndita kwa kutopenda anachonusa. Alipomaliza kutazama sebuleni, akaendea korido kwenda kukuta vyumba viwili vya nyumba hii.
.
.
Ila kadiri alivyokuwa anapiga hatua kwenda huko, nayo harufu ikawa inazidi maradufu. Hakujua ni nini inanuka. Ilikuwa ni harufu kali ya kitu kilichooza.
.
.
Alijaribu kuusukuma mlango wa kwanza, ukafunguka. Akachungulia humo ndani. Kulikuwa na kitanda chakavu chenye godoro lililotobokatoboka. Akaangaza huku na huko. Hakuona kitu zaidi ya tando za buibui, nguo zikiwa zimezagaa huku na kule.
.
.
Akaachana nacho na kwenda kwenye chumba cha pili. Akajaribu kukifungua, mlango ukakubali. Harufu ile aliyokuwa anaisikia, sasa ikazidi mara tatu yake! Ilikuwa ni kali mno kiasi cha kuwa ngumu kuvumilika.
.
.
Brian akabana pua yake kwanguvu. Akaangaza huku na kule chumbani. Hakukuwa na kitu! Chumba kilikuwa kitupu. Kimejawa na nzi na kina kiza kiasi kutokana na kutofunguliwa kwa pazia.
.
.
Ila kabla Brian hajakiacha chumba hiki, akaona mlango mdogo kwa sakafuni. Kulikuwa na andaki kwenye chumba hiki. Na Brian akawaza kuwa huko ndipo kwenye kitu kitoacho harufu.
.
.
Akabaki njia panda, aende kutazama, ama ajiondokee upesi kabla hajakutwa?

.
.
**
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom