SEHEMU YA 61
Siku hiyo niliamini, na nilipokumbuka jinsi alivyokuwa akikileta kifua chake juu na kushuka chini, niliamini kabisa ningeweza kumuua. Haijati akachanganyikiwa, aliniambia kabisa kwamba angemsaliti mume wake kwangu katika maisha yake yote, na hata kama ingetokea siku nimeoa, bado angehitaji kupata nafasi ya kuwa nami.
“Sawa. Wewe tu,” nilimwambia.
Baada ya dakika kadhaa tukatoka na kumsindikiza mpaka Tabata Bima na mimi kurudi zangu.
Nilifurahi sana, unajua unapokuwa na adui yako halafu unafanya kitu ambacho unaamini kabisa kwamba kama ingetokea siku akajua, ataumia sana, basi ungefurahi mno.
Niliporudi nyumbani, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwasiliana na Halima, nilihitaji kumseti kwanza kwa sababu ni zamu yake ndiyo iliyokuwa ikifuata.
Nikaanza kuchati naye mpaka majira ya saa tano usiku, alilegea kwa sababu alijua kwamba nina pesa, basi kila kitu nilichokuwa nikiongea, alikuwa akichekacheka tu.
“Ila nilikumisi,” aliniambia bila aibu, eti alinimisi, nilikuwa kapuku, alinimisi kwa lipi? Ila kwa sababu na mimi nilikuwa nahitaji kitu kutoka kwake, nikaunganisha.
“Hata mimi! Nimekuwa nikiota ila siku kuhisi wewe. U msichana wa ajabu sana,” nilimwambia.
“Kweli?”
“Yaah! Nikuulize swali?”
“Niulize!”
“Hivi umevaa ya rangi gani hapo?” nilimuuliza.
“Nini?”
“Acha utoto bwana!” nilisema na kuanza kucheka kile kicheko cha chini.
Alikuwa mtu mzima, alijua kabisa kile nilichomaanisha ila mwenyewe akaanza kujifanya kama mtu anayesikia aibu kubwa.
Akaanza kujiumauma ila mwisho wa siku akaniambia mwenyewe.
“Rangi ya pinki!” “Oh! Daah! Natamani sana siku nione jinsi inavyokupendeza. Unavaa kiuno namba ngapi?” nilimuuliza.
“Mh! Wala sijui! Mi nanunuaga tu! Kwa nini umeuliza?” aliniuliza.
“Nataka nikununulie kadhaa, tena nikuvalishe mimi mwenyewe,” nilimwambia kwa sauti fulani hivi ya kimitego.
“Mh! Utanichungulia!” aliniambia.
“Nitafumba macho! Kweli sitoona,” nilimwambia.
Kwenye maongezi kama haya ndipo unapogundua kuwa mwanaume raha sana. Yaani unaanza kuona mwili wako ukianza kupata hali fulani na sehemu moja kuanza kukakamaa.